Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Kiswahili Darasa La Sita Question Paper

Kiswahili Darasa La Sita 

Course:Primary Level

Institution: Kcpe question papers

Exam Year:2005



DARASA LA SITA MUHULA WA III - 2005
KISWAHILI

Jaza nafasi zilizoachwa wazi.

Endapo ni ukweli kwamba binadamu ya 1. ______ aliishi Afrika basi 2. ______ kudai kuwa 3. ______ ya mwanzo aliianza 4. ______ humu. Binadamu 5. ______ alihitaji kuwinda na 6. ______ chakula chake na kwa hivyo, 7. ______ avumbue vyombo 8. ______ kufanya hivyo. Bara la Afrika lilikuwa 9. ______ hatua kimaendeleo 10. ______ usuli wa Wazungu.

1.
A. Hawali
B. Wali
C. Awali
D. Mbeleni

2.
A. Tunaeza
B. Tunaweza
C. Tunawaza
D. Tunaaweza

3.
A. Teknologia
B. Technologia
C. Teknolojia
D. Tekmolojia

4.
A. Barabarani
B. Baharini
C. Baharani
D. Barani

5.
A. Huyo
B. Huyu
C. Huo
D. Hao

6.
A. Kukula
B. Kupiga
C. Kupika
D. Kupikia

7.
A. Ilimbidi
B. Ilibidi
C. Alibidi
D. Ilimbidi

8.
A. Vitavyomsaidia
B. Vinayomsaidia
C. Vitakavyomsaidia
D. Visaidia

9.
A. Likipiga
B. Vinapiga
C. Inapiga
D. Linapiga

10.
A. Kabla
B. Kabla ya
C. Baada
D. Baada ya

Jaza nafasi iliyoachwa wazi ukitumia jibu sahihi lililopo kwenye mabano.

11. Vitu vimekuwa ______ sokoni.
(kali, ghali, gali)

12. Wageni kwa hivi sasa wame ______
(asili, wasiri, wasili)

13. Watu huoga kisha ______
(hukula, hukulanga, hula)

14. Sijamtembelea kaka kwa siku ______
(mingi, nyingi)

Kamilisha methali zifuatazo

15. Mtegemea nundu haachi
A. Kunona
B. Kuona
C. Kula
D. Kufa

16. Nyani haoni
A. Mkiawe
B. Kundule
C. Domole
D. Dondale

17. Baniani mbaya kiatu chake
A. Kizuri
B. Kibaya
C. Dawa
D. Sumu

Matumizi ya -ingine

18. Gari ______ jeupe limewasili leo
A. Lingine
B. Zingine
C. Mwingine
D. Jingine

19. Nguo ______ zote ni chafu isipokuwa hii.
A. Zingine
B. Nyingine
C. Zote
D. Lingine

20. Chakula ______ kinapikwa na nyoko
A. Kingine
B. Chengine
C. Lingine
D. Pengine

Kinyume: chagua jibu lifaalo zaidi

21. Fumba ______
(Vumbua, fumbua)

22. Anika ______
(Anikisha, anua)

Chora maumbo yafuatayo

23. Duara
24. Pia

Tegua vitendawili vifuatavyo

25. Hiwali amekonda lakini hana mganga
(mikia ya panya, mijusi, sindano)

26. Hata zangu ameshindwa
(njaa, mauti, nyuki)

27. Funga mizigo twende Zaire
(mtama, merikebu, mkia ya mbwa)

Andika tarakimu zifuatazo kwa nambari.

28. Milioni moja

29. Milioni nne, mia nane elfu

30. Milioni sita, elfu sita tisini na tisa, mia tisa na tisa

Andika majina ya wadudu katika sentensi zifuatazo

31. Mimi nina miguu mingi, nina sumu. Mimi ni
(nyoka, viroboto, tandu)

32. Ninapenda sana kuishi kwenye vichunguu walivyovijenga wao ni
(kunguni, viroboto, mchwa)

33. Mimi ni ndege ninapenda giza na ninapopumzika kichwa changu huangalia chini. Mimi ni
(kinyonga, popo, bundi)

Chagua mojawapo ya maneno haya kukamilisha sentensi.

Mtoro, mdadisi, mkalimani.

34. Mtu anayetafsiri lugha kwa ya pili ______

35. Mtu anayeondoka mahali bila ruhusa ______

36. Mtu mwenye hamu ya kujua ______

Tumia neno linalofaa kukamilisha sentensi hizi.

37. Ukisafiri ______ ndege utafika salama
(pamoja, kwa, na)

38. Tulilala ______ yeye
(kwa, na, katika)

39. Tuliandamana ______ hadi nyumbani
(naye, wao, wote)

40. Katika karamu niliyoandaliwa tulikula chakula chote ______ kijiko
(na, mwiko, kwa)

Soma ufahamu huu kisha ujibu maswali.

Kobe alitamani kubadili maskani yake. Basi akamwomba tai amchukue mpaka kwenye mastakimu yake mpaya. Akaahidi kumpa ujira wake. Tai akakubali. Akamkamata Kobe gamba lake akapaa naye juu sana. Njiani wakakutana na Kunguru, akamwambia Tai, "Bwana wee huna habari, huyo Kobe anafaa sana kwa chakula, dhihaka mbali."
Tai akamjibu akamwambia, "Ndiyo bwana, lakini gamba lake ni gumu mno."
Kunguru akamwambia "Ah! Hilo si neno. Mwamba waweza kulipasua mara moja wala siyo kazi kubwa."
Basi akakata shauri la Kunguru akamwaga Kobe kwenye mwamba mkali. Ndipo wale ndege wawili wakafaidi chakula chao, yaani Kobe.

Maswali

41. Kobe alitamani
A. Kuhamia maskani mapya
B. Kuhama maskani mapya
C. Kuchukuliwa na tai
D. Kubadili mastakini mapya

42. Tai angelipwa ujira wake
A. Kabla hajamchukua kobe
B. Baada ya kumfikisha kobe katika maskani yake
C. Punde tu angekubali kumbeba kobe
D. Angemfikisha kobe salama katika makao mapya

43. Tai alikubali kuchukua kobe kwa sababu
A. Alitaka kumla
B. Aliahidiwa malipo
C. Akijua ni chakula kinachofaa
D. Alitaka kumbwaga penye mwamba

44. Kunguru na Tai
A. Wote ni ndege
B. Wanaishi pamoja
C. Ni ndege walao mizoga
D. Ni ndege wanaozaa watoto

45. Neno lenye maana sawa na maskani ni?
A. Kiota
B. Chengo
C. Pango
D. Msalani

46. Dhihaka ni sawa na?
A. Mzaha
B. Haraka
C. Wahaka
D. Uongo

47. Gamba kwa kobe ni sawa na ______ kwa mti
A. Ganda
B. Gome
C. Ngozi
D. Utando

48. "Ah!" ni tamko la kishangao kinachotumiwa
A. Kuonyesha furaha
B. Kushangilia
C. Kuonyesha tukio la kukera
D. Kuitikia jambo

49. Kunguru alimaanisha nini aliposema "Hilo si neno"
A. Kobe hana la kufanya
B. Kobe hana taabu
C. Gamba la kobe si gumu
D. Ugumu wa gamba la kobe hauwezi kuzuia kumla

50. Habari hii inatufunza kwamba
A. Kobe ni mnyama mjinga
B. Tai ni ndege mwenye nguvu
C. Kunguru ana akili kuliko tai
D. Usimwamini adui wa jadi hata kama ana dhiki.






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers