Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana, Nikaiga rika langu, kwa vileo, na mbio za wsichana, Kiwa ni riziki yangu,...

      

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana,
Nikaiga rika langu, kwa vileo, na mbio za wsichana,
Kiwa ni riziki yangu, mapokeo, kuoa na kuona,
Ni wakati utanena.

Nashukuru kwa ugumba, wenye ndimi, wanipazao nao,
Wapitao wakiimba, eti mimi, ningapenda hali zao,
Haupandiki mgomba, wana nyemi, fisadi wa hadhi zao,
Eti ni kwa raha zao.

Ni lipi lenye kukera, kwa Muumbi, marufuku kwenye misa,
Ni mtu kuwa hawara, wa vitimbi, ama alozawa tasa?
Ugumba na ukapera, sio dhambi, wala haujawa kosa,
Waama sina makosa

Bora tungeni vitabu, magazeti, mutangaze kwa rediyo,
Muwaite watribu, kina Siti, watuzwa ilimu hiyo,
Na zaidi muhutubu, kwa umati, muwambe ambayo siyo,
Kwalo sichafuki moyo

Hidhuru yote ni bure, sio kitu, kudhiki asodhikika,
Siwi nikaona ghere, lailatu, nyota njema itafika,
Kwa shangwe na njerejere, kila mtu, mdomo utafumuka,
Akiri amejibika.
(Mwalaa M. Nyanje)


(a) Eleza jambo ambalo mzungumzaji (nafsineni) katika shairi hili anasingiziwa.
(b) Fafanua mambo matano ambayo mzungumzaji (nafsineni) anapinga katika shairi hili.
(c) Eleza umuhimu wa viishio vya beti za shairi hili.
(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari.
(e) Eleza muundo wa shairi hili.
(f) Bainisha matumizi mawili ya tafsida katika shairi hili.

  

Answers


Francis
a) Mzungumzaji (nafsineni) anasingiziwa ugumba hasa kwa kutoshiriki mapenzi nje ya ndoa.

b)
? Kuiga rika; hususan kushiriki ulevi pamoja na kufukuza wasichana.
? Mzungumzaji kupakwa tope (kuaibishwa) kwa kuwa yeye ni gumba.
? Wamsemao kudai kwamba anatamani kuwa kama wao.
? Eti kuwa ugumba na ukapera ni kosa.
? Kuharibu maisha kwa ujana.
? Kusingiziwa atapenda (atatamani) hali za wamsemao.
? Watu kueneza uvumi kuwa yeye ni gumba.

c)
? Viishio hivi ni vifupi na hivyo vinatoa ujumbe kwa namna iliyo madhubuti.
? Viishio hivi vinaunga ujumbe wa kila ubeti/vinasisitiza ujumbe wa shairi.
? Viishiovinachimuza/kuonyesha/kubainisha dhamira au mwelekeo wa mshairi kuhusu hali ya vijana kujiingiza katika mahusiano yasiyofaa.

d) Ni jambo gani ambalo linamkasirisha Mungu ambalo halikubaliki kanisani? Je ni mtu kuwa kahaba na mwenye vioja ama mtu aliyezaliwa akiwa tasa? Kuwa gumba au kapera si kosa na wala haliwezi kuwa kosa. Kwa kweli mimi sina makosa.

e)
? Kila ubeti una mistari minne
? Mistari mitatu ya kwanza ina vipande vitatu ilhali wa nne una kipande kimoja.
? Vina katika kila kipande vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.
? Kiishio kimefupishwa.
? Kila mstari una mizani 20 isipokuwa kiishio chenye mizani 8
? Shairi lina beti 5

f)
? Mbio za wasichana- uasherati/uzinzi/uzinifu
? Haupandiki mgomba- hana uwezo wa kujamiana.
francis1897 answered the question on February 1, 2023 at 10:58


Next: Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Watafuta Riziki 1. Watafuta riziki, watatokwa jasho vijijini Wakulima shakiki, wakuza chai na mibuni Vyakula washakiki, visipungue vinyuani. 2. Watafuta riziki, wahaingaikao...
Previous: Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali 1. Huno wakati mufti, vijana nawausia, Msije juta laity, mkamba sikuwambia, Si hayatti si mamati, vijana hino dunia, Uonapo vyang’aria,...

View More Ushairi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Watafuta Riziki 1. Watafuta riziki, watatokwa jasho vijijini Wakulima shakiki, wakuza chai na mibuni Vyakula washakiki, visipungue vinyuani. 2. Watafuta riziki, wahaingaikao...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
    T. Arege: Watafuta Riziki
    1. Watafuta riziki, watatokwa jasho vijijini
    Wakulima shakiki, wakuza chai na mibuni
    Vyakula washakiki, visipungue vinyuani.

    2. Watafuta riziki, wahaingaikao mijini
    Kutwa kile na hiki, kama watanga na mipini
    Japo hawasikii, hawakosi kujiamini

    3. Watafuta riziki, wazalendo wa nchi hii
    Kamwe hawajidhiki, tama za moyo kutii
    Bali huafiki, kupingana na ulaghai

    4. Watafuta riziki, pato ambalo la halali
    Ndoto haizimiki, ya kesho kuwa njema hali
    Wiki baada wiki, la haramu jasho hawali


    (a) Fafanua sifa tano za watu wanaozungumziwa katika shairi hili.
    (b) Bainisha umuhimu wa tamathali tatu za usemi zilizotumiwa katika shairi hili.
    (c) Eleza kwa kutoa mifano, mbinu tatu ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi.
    (d) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo:
    (i) idadi ya mishororo katika beti.
    (ii) mpangilio wa vina
    (iii) mpangilio wa maneno

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Amiri A. S. Andanenga: Sauti ya Kiza 1 Ngakua na mato, ya kuonea Ngalisana kito,cha kuchezea Kilicho kizito, cha kuelea Kikamuenea,...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
    Amiri A. S. Andanenga: Sauti ya Kiza
    1 Ngakua na mato, ya kuonea
    Ngalisana kito,cha kuchezea
    Kilicho kizito, cha kuelea
    Kikamuenea, akivae.

    2 Makusudi yangu,ngaliandaa
    Ngafinyanga chungu, cha mduwaa
    Ngatia vitangu,vinavong’aa
    Ili ziwe taa, kwa apikae.

    3 Mkungu wa tano, wa mduwara
    Ulo bora mno, kisha imara
    Ulo na maono, kuwa ni dira
    Kwenye barabara, itindiae.

    4 Ngaomba Baraka, kwake Rabana
    Punje za nafaka, kila aina
    Chunguni kuweka, kwa kulingana
    Hajaangu suna, yule alae.

    5 Ngafanya bidii, kwenda mwituni
    Sio kutalii, kukata kuni
    Ya miti mitii, huko jikoni
    Isio na kani,ni iwakae.

    6 Kwa yangu mabega, nikathubutu
    Ngabeba mafiga, yalo matatu
    Bila hata woga, kwenye misitu
    Simba tembo chatu, sinitishie.

    7 Miti yenye pindi,na jema umbo
    Ngajenga ulindi, mwema wimbombo
    Fundi aso fundi, penye kiwambo
    Moyo wenye tambo, apekechae.

    8 Singaajiri, ngachimba mimi
    Kisima kizuri, cha chemchemi
    Maji ya fahari, ya uzizimi
    Jua la ukami, siyaishae

    9 Tamati nafunga, kwa kuishia
    Mato ndo malenga, kanikimbia
    Nahofu kutunga, mabeti mia
    Asije chukia, ayasomae.


    (a) Eleza ujumbe wa shairi hili.
    (b) Kwa kurejelea ubeti wa pili, eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa kishairi aliotumia mshairi.
    (c) Andika ubeti wa saba kwa lugha ya nathari.
    (d) Eleza toni ya shairi hili.
    (e) Fafanua aina tatu za urudiaji zilizotumiwa katika shairi hili.
    (f) Bainisha nafsi neni katika shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Mwili Leo kitaka nifike, natamani, ila wauma mwili Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili. Vitisho kamwe...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
    T. Arege: Mwili

    Leo kitaka nifike, natamani, ila wauma mwili
    Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili
    Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili.

    Vitisho kamwe kelele, ninavicha, kwa nafsi na mwili
    Ila ugonjwa utimile, umechacha, na kuudhili mwili
    Msikose simile, magalacha, si gurudumu mwili.

    Vingekuwepo viraka, kuutia, ngeushuruti mwili
    Kifundi kivipachika, kuingia, hata kuridhi mwili
    Upya ukaungilika, kuvutia, roho na wake mwili.

    Lakini kamwe haiwi, kuvipata, vipande vyake mwili
    Sihofu kupata mawi, sitajuta, kupigania mwili
    Hata kufutwa sikawi, nitakita, kidete nao mwili.

    Kazi ninaithamini, ni hakika, akilini na mwili
    Ila kamwe siamini, kusagika, damu, jasho na mwili
    Uwele hususani, kioneka, nguvu hitishi mwili.


    a) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili.
    b) Fafanua mbinu nne za lugha zilizotumiwa katika shairi hili.
    c) Eleza toni ya shairi hili.
    d) Ni nani anayezungumziwa na nafsineni katika shairi hili?
    e) Eleza bahari ya shairi hili kwa kurejelea vipande.
    f) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha ya nathari.

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Daima alfajiri na mapema Hunipitia na jembe na kotama Katika njia iendayo kondeni Kama walivyofanya babuze zamani; Nimuonapo huwa anatabasamu Kama mtu aliye na kubwa...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

    Daima alfajiri na mapema
    Hunipitia na jembe na kotama
    Katika njia iendayo kondeni
    Kama walivyofanya babuze zamani;
    Nimuonapo huwa anatabasamu
    Kama mtu aliye na kubwa hamu
    Kushika mpini na kutokwa jasho
    Ili kujikimu kupata malisho.

    Anapotembea anasikiliza
    Videge vya anga vinavyotumbuiza
    Utadhani huwa vimemngojea
    Kwa usiku kucha kuja kumwimbia;
    Pia pepo baridi kumpepea
    Rihi za maua zikimletea
    Nao umande kumbusu miguu;
    Na miti yote hujipinda migongo
    kumpapasa,kumtoa matongo;
    Na yeye kuendelea kwa furaha
    kuliko yeyote ninayemjua
    Akichekelea ha ha ha ha ha ha …

    Na mimi kubaki kujiuliza
    Kuna siri gani inayomliwaza?
    Au ni kujua au kutojua?
    Furaha ya mtu ni furaha gani
    katika dunia inayomhini?
    Ukali wa jua wamnyima zao
    Soko la dunia lamkaba koo;
    Dini za kudhani zamsonga roho
    Ayalimia matumbo ya waroho;
    Kuna jambo gani linamridhisha?
    Kama si kujua ni kutokujua
    Laiti angalijua, laiti angalijua!
    (T. Arege)

    Maswali
    a) Eleza hali ya mzungumziwa katika shairi hili.
    b) Huku ukitoa mifano, onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili.
    c) Fafanua aina tatu za taswira ukirejelea ubeti wa pili.
    d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili.
    e) Bainisha vipengele vifuatavyo vya kimtindo katika shairi hili:
    i. tashhisi
    ii. kinaya
    iii. tashbihi
    f) Eleza toni ya shairi hili.
    g) Bainisha nafsineni katika shairi hili.
    h) Changanua muundo wa shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali T. Arege: Barabara Barabara bado ni ndefu Nami tayari nimechoka tiki Natamani kuketi Ninyooshe misuli Nituliza akili Lakini Azma yanisukuma Mbele ikinihimiza kuendelea Baada ya miinuko na kuruba Sasa naona...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
    T. Arege: Barabara
    Barabara bado ni ndefu
    Nami tayari nimechoka tiki
    Natamani kuketi
    Ninyooshe misuli
    Nituliza akili

    Lakini

    Azma yanisukuma
    Mbele ikinihimiza kuendelea
    Baada ya miinuko na kuruba
    Sasa naona unyoofu wake
    Unyoofu ambao unatisha zaidi

    Punde natumbukia katika shimo
    Nahitaji siha zaidi ili kupanda tena
    Ghafla nakumbuka ilivyosema
    Ile sauti zamani kidogo
    “Kuwa tayari kupanda na kushuka.”

    Ingawa nimechoka
    Jambo moja li dhahiri
    Lazima nifuate barabara
    Ingawa machweo yaingia
    Nizame na kuibuka
    Nipande na kushuka

    Jambo moja nakukumbukia: Mungu
    Je, nimwombe tena? Hadi lini?
    Labda amechoshwa na ombaomba zangu
    Nashangaa tena!

    Kitu kimoja nakiamini
    Lazima niendelee kujitahidi kwa kila hatua mpya
    Nijikokote kuiandama hii barabara yenye ukungu
    Nikinaswa na kujinasua
    Yumkini nitafika mwisho wake
    Ingawa wangu mwisho haitauwahi kabla.


    (a) Eleza toni ya shairi hili.
    (b) Tambua nafsineni katika shairi hili.
    (c) Mshairi ana maana gani anaposema “Kuwa tayari kupanda na kushuka” katika ubeti wa tatu?
    (d) Fafanua tamathali tano za usemi zilizotumiwa katika shairi hili ukizitolea mifano mwafaka.
    (e) Eleza ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa tano wa shairi hili.
    (f) Eleza maana ya:
    (i) kuruba
    (ii) barabara yenye ukungu

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Kilio cha Lugha Ni wimbo najiimbia,nijiliwaze Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi Lugha ya mtu mweusi, Kiswahili chalilia Wataalamu ni nani, mulipo mwaninyanyasa Hamna nami...(Solved)

    Kilio cha Lugha
    Ni wimbo najiimbia,nijiliwaze
    Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi
    Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi
    Lugha ya mtu mweusi, Kiswahili chalilia

    Wataalamu ni nani, mulipo mwaninyanyasa
    Hamna nami imani, wala kupanga siasa
    Mwasema sayansini, siku ningalitosa
    Mwanambia nikotosa, kuiva sijafika

    Ela muelewe sana, Maamuma na Imamu
    Mulipokuwa vijana, kwenu nilikuwa timamu
    Sasa mumesoma sana, mwaniona ni haramu
    Mujue kuwa dawamu, utumwa mwauridhia.

    Mzaliwapo mwalia, ‘maa’, maneno ya kwanza
    Lugha munayokulia, ya mama zetu ya kwanza
    Wa lugha muwedoria, muweze na kuikuza
    Sio kujipendekeza, uzungu kuigiza.

    Majira ya ukoloni, ukombozi kusambaza
    Lugha mulithamini, Kiswahili kufukiza
    Hata kule risavuni, kizungu hanikuwaza
    Sasa mbona mwanibeza, mbali mwanitupilia?

    Sayansi sio asili, msamiatiwe sinao
    Sayansi yataka mbali, msamiati ni wa hao
    Nitakuwa Kiswahili, kiomba majina yao
    Lugha kujikuza kwao, huomba linalofaa.

    Enyi viongozi wetu, ipangeni nadharia
    Kujenga siasa yetu, tuzidi kuwa huria
    Lugha hata ‘mbusha watu, tuche kuriaria
    Sifa ni kwa chake mtu, cha mwenzi hutoringia

    Utajiri wangu hasa, nikiwatajia wote
    Msamiati huwa, ni wa Afrika yote
    Na methali za kuasa, nahau na ngeli zote
    Na nisemwapo popote, ujumbe hukamilika.

    Afrika ndipo petu, pa wabantu halisi
    Baba na mama ni Bantu, shina la wangu ukwasi
    Warabu na wengi wetu, sio wangu Adinasi
    Kwao ‘meomba kiasi, ili kujizidisha

    Mfumo mpya hongera, wa elimu humu Kenya
    Lugha takuwa imara, ukabila tutafinya
    Kiswahili ni ibara, kila mtu kiimanya
    Methali imetuonya, mtumwa si mwasilia.

    Tamati lugha yalia, yabaguliwa bayana
    Kukua imeridhia, msamiati kufana
    Wengine wataijulia, kwa marefu na mapana
    Lugha yetu ya maana, mwaipuuza yalia.


    Maswali
    (a) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu
    (b) Kwa kutoa hoja nne, eleza kwa nini shairi hililikaitwa kilio cha lugha.
    (c) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari.
    (d) Eleza toni ya shairi hili.
    (e) Tambua uhuru wa kishairi uliotumiwa kwa kurejelea mifano mitatu.
    (f) Bainisha nafsineni katika shairi.
    (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa mujibu wa shairi.
    i. nasongwa
    ii. kuriaria
    iii. adinasi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Lau dunia nanena, tuseme si ati ati, Mauti kawa hakuna, katika wote wakati, Vipi tungelisongana, tunaoishi tiati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Dunia ingetatana, na kizazi katikati, Huku kwazaliwa bwana,...(Solved)

    Lau dunia nanena, tuseme si ati ati,
    Mauti kawa hakuna, katika wote wakati,
    Vipi tungelisongana, tunaoishi tiati?
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Dunia ingetatana, na kizazi katikati,
    Huku kwazaliwa bwana, kule kwazawa binti,
    Vipi tungelioana, na kuzaa hatuwati?
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Lau mauti hakuna, tungesongana sharuti,
    Kwa viumbe kukazana, wanadamu na manyati,
    Vipi tungelijazana, kwa kusitawi umati?

    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?
    Walakini Subuhana, kapanga sisi na miti,
    Ili tusizidi sana, si wengi na si katiti
    Maisha ya kupishana, yule ende yule keti,
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Ndipo dunia kufana, ikawa kama yakuti,
    Kwa uwezowe Rabana, kaipanga madhubuti,
    Maisha kugawiana, kayagawa kwa mauti,
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Njia ingekuwa hapana, pembeni na katikati,
    Sote tungeambatana, kama ukosi na shati,
    Na njaa ingetutafuna, pa kulima hatupati,
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Peleleza utaona, hayataki utafiti,
    Kama tungelikongana, ingekuwa ni bahati,
    Vipi tungesukumana, katika hiyo hayati?
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?

    Mbele sitokwenda tena, hapa mwisho nasukuti,
    Yaoleni waungwana, shauri yake Jabaruti,
    Yote tuloelezana, katenda bila senti,
    Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana?
    (Abdalla Said Kizere)


    Maswali
    a) Pendekeza anwani mwafaka la shairi hili.
    b) Je, hili ni shairi la bahari gani? Eleza
    c) Eleza vile mwandishi alivyotumia uhuru wa kishairi.
    d) Eleza umbo la shairi hili.
    e) Fafanua ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa tano.
    f) Andika majina mawili ya Mungu kwa mujibu wa shairi.
    g) Kwa kutolea mifano, eleza mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi hili

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Eleza mambo yanayozingatiwa katika uhuru wa kishairi (Solved)

    Eleza mambo yanayozingatiwa katika uhuru wa kishairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja baadhi ya masuala muhimu katika uchambuzi wa mashairi(Solved)

    Taja baadhi ya masuala muhimu katika uchambuzi wa mashairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja aina mbalimbali za takriri katika ushairi(Solved)

    Taja aina mbalimbali za takriri katika ushairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Katika ikisiri yake, Joseph Nyehita anaangazia kuwa matumizi ya methali yanapozingatiwa, ushairi wa Kiswahili unaweza kuainishwa zaidi kwa kuzingatia kutumiwa au kutotumiwa kwa methali. Anasema...(Solved)

    Katika ikisiri yake, Joseph Nyehita anaangazia kuwa matumizi ya methali yanapozingatiwa, ushairi wa Kiswahili unaweza kuainishwa zaidi kwa kuzingatia kutumiwa au kutotumiwa kwa methali. Anasema kuwa kila kikundi cha ushairi kinaweza kupendekezewa jina mahususi kuwa kitambulisho chake. Taja majina yanayopendekezwa

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja huku ukitoa mfano, aina kadha za taswira katika ushairi(Solved)

    Taja huku ukitoa mfano, aina kadha za taswira katika ushairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja na ueleze tamathali tofauti za usemi(Solved)

    Taja na ueleze tamathali tofauti za usemi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja mambo ya kuzingatia katika kueleza muundo wa shairi(Solved)

    Taja mambo ya kuzingatia katika kueleza muundo wa shairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja na ueleze mambo muhimu yanayozingatiwa katika uchambuzi wa mashairi(Solved)

    Taja na ueleze mambo muhimu yanayozingatiwa katika uchambuzi wa mashairi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Eleza aina za bahari za ushairi zifuatazo: a) Sakarani b) Ngonjera c) Malumbano d) Masivina e) Taabili f) Mandhuma g) Kisarambe h) Mavue i) Sabilia j) Togoo k) Kumbukizi(Solved)

    Eleza aina za bahari za ushairi zifuatazo:
    a) Sakarani
    b) Ngonjera
    c) Malumbano
    d) Masivina
    e) Taabili
    f) Mandhuma
    g) Kisarambe
    h) Mavue
    i) Sabilia
    j) Togoo
    k) Kumbukizi

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Taja na ueleze aina za mashairi kulingana na mizani(Solved)

    Taja na ueleze aina za mashairi kulingana na mizani

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Eleza aina ya mashairi kulingana na mpangilio wa maneno(Solved)

    Eleza aina ya mashairi kulingana na mpangilio wa maneno

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Eleza aina za mashairi kulingana na vina(Solved)

    Eleza aina za mashairi kulingana na vina

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)

  • Eleza aina za mashairi kulingana na idadi ya vipande katika mshororo(Solved)

    Eleza aina za mashairi kulingana na idadi ya vipande katika mshororo

    Date posted: February 1, 2023.  Answers (1)