Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo

Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo

Answers


Kavungya
TUMBO LISILOSHIBA
• Eneo la Madongoporomoka ndiko wanamoishi watu wepesi wasio na mashiko
• Watu wa Madongoporomoka walikuwa maskini
• Katika eneo la Madongoporomoka kulikuwa na mkahawa mshenzi wa Mzee Mago
• Bi Suruti alishangaa kwa kuuliza kuhusu wanachojali matajiri kuhusu maskini kama wao
• Huko Madongoporomoka kuna mashonde ya vinyesi, vibwagizo wa choo, uchafu unaonekenya, vibanda uchwara na majichafu
• Tunaambiwa kuwa watu wengi waliokuwa wamelala waliamka na kutoka nje ya vibanda vyao haraka

MAPENZI YA KIFAURONGO
• Dennis Machora alisema kuwa umaskini uhostakimu kwao haukuwa na mfano
• Dennis Machora alisema kuwa wazazi wake hawakuwa na mali ya kuwarithisha
• Dennis Machora hana chakula, inabidi apike uji usiokuwa na sukari
• Dennis Machora alikuwa na kijiredio na ametandika kitandani shuka zilizozeeka na kuchanikachanika
• Penina alimwangalia msimulizi kwa huzuni yamkini alitelewa na hali yake duni
• Dennis Machora alimwambia Penina kuwa hawawezi kuwa na usuhuba kwa kuwa Dennis anatoka kutoka familia ya umaskini naye Penina anatoka kwenye familia yenye nafasi
• Kwa kuwa Penina alimshinda Dennis Machora kiuchumi angejidunisha na Penina angemwona kama kupe
• Penina alimwita Dennis Machora kama mkata
• Penina alimwambia Dennis kuwa Mungu angempa mpenzi mwingine aupakati ufukara wake aliouzoea
• Mwanafunzi aliyekuwa na pesa angelipa kujinasibisha na mwenzake maskini
Kavungya answered the question on May 6, 2019 at 05:31

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions