Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Maneno haya yamo katika ngeli gani? i) Fagio ii) Nyigu

Maneno haya yamo katika ngeli gani?
i) Fagio
ii) Nyigu

Answers


sharon
i) U-ZI ;
ii).A-WA
sharon kalunda answered the question on September 26, 2019 at 05:49

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Ngeli ni nini? (Solved)

    Ngeli ni nini?

    Date posted: September 26, 2019 .    Answers (1)

  • Kiswahili ni lugha ambayo inakua na kuenea kila uchao. Imeenea kwa kasi hivi kwamba waliokuwa wameitweza wamelazimika kujifunza, kuizungumza na hata kuitumia katika maandishiLugha hii... (Solved)

    Soma taarifa ifuatavo kisha uiibu maswali
    Kiswahili ni lugha ambayo inakua na kuenea kila uchao. Imeenea kwa kasi hivi kwamba waliokuwa wameitweza wamelazimika kujifunza, kuizungumza na hata kuitumia katika maandishiLugha hii imetambuliwa kama mojawapo ya lugha za mawasiliano katika muungano wa Afrika. Magwiji wa Kiswahili wamechaguliwa kuunda msamiati mwafaka kutegemea mabadiliko ulimwenguni na kuingiza katika matumizi kupitia tarakilishi.
    Mpango huu utakapo faulu, mtu ataweza kutumia tarakilishi akiwasiliana kwa Kiswahili. Juhudi hizi heri zizidi kupongezwa na nyingine kuimarishwa Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili barani ni mojawapo wa hatua za kufanikisha juhudi hizi. Taasisi kama hiyo itatafiti historia ya lugha, mabadiliko yake na maenezi, msamiati wake na kuleta usawa wa mazungumzo kwa Kiswahili miongoni mwa mambo mengine.Kuweka lugha hii katika maandishi ni jambo litakalochangia kuimarisha lugha ya Kiswahili. Vitabu ,magazeti, na majarida yatakayolenga kiwango cha wasomaji yaandikwe na bei yake isiwe ghali mno ili wengi waweze kugharamia. Tanzu zote za lugha zizingatiwe.Lugha hii ifunzwe na kutahiniwa katika daraja zote za elimu. Lifanyapo hili, bila shaka lugha ya Kiswahili itaimarika.Uajiri wa wafanyikazi ukitambua ujuzi katika lugha hii hadhi yake itaimarika.Tafsiri ya kazi zilizoandikwa katika lugha mbalimbali zikifanywa katika Kiswahili, lugha hii itakua na kukitamizizi kwingi ulimwenguni.Watu wengi watapata hamu ya kusoma kazi asilia na ile ya tafsiri yake.Redio na magazeti ni vyombo muhimu katika kuwasiliana na kundi kubwa la watu kote duniani. Vyombo hivi vya mawasiliano kwa umma vikihimiza matumizi ya Kiswahili, bila shaka mchango mkubwa utaonekana katika kustawisha lugha hii. Vipindi maalumu matangazo na burudani vizingatie matumizi ya Kiswahili.Mashindano kati ya shule na shule,nchi na nchi ya kianzishwa na kuzingatiwa yanaweza kuimarisha Kiswahili pakubwa. Mashairi, mijadala, matokeo ya utafiti fulani, nyimbo, ngano na hadithi za kufunza umma ni njia za kuwezesha kufanyiwa mashindano kama hayo.Mikakati hii na mingine ikizingatiwa itakuwa mbolea nzuri ya kukuza lugha ya Kiswahili.

    Maswali
    i) Bila kubadilisha maana iliyokusudiwa ,fupisha aya mbili za mwanzo. (maneno 35 - 40)
    ii) Andika kwa muhtasari juhudi zinazofaa katika uimarishaji wa lugha ya Kiswahili kwa mujibu wa Makala haya. (maneno 70 -80)

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Ulimwengu unapaswa kuzuka na mbinu za Kulitadarukia tatizo la umaskini ambalo una kwamiza juhudi za maendeleo. (Solved)

    Soma nakala yafuatayo kishaujibu maswali
    Ulimwengu unapaswa kuzuka na mbinu za Kulitadarukia tatizo la umaskini ambalo una kwamiza juhudi za maendeleo. Umaskini unaoukabili mataifa yanayoendelea. Unayatosa kwenye dhiki kubwa huku mataifa ya kimagharibi yakipiga hatua kubwa kimaendeleo. Ufa uliopo baina ya mataifa yanayoendelea na yaloyaliyoendelea kama vile Marekani, nchi za Ulaya na Ujapani unapanuka kila uchao.
    Vyanzo vya umaskini huu ni anuwai ; mathalan, ufisadi, uongozi mbaya, turathi za kikoloni, uchumi kuegemea mvua isiyotabirika,idadi ya watu inayoupiku uwezo wa uchumi wa taifa linalo husika na ukosefu wa nyenzo na amali za kuwakwamua raia kutoka lindi la umaskini. Ukosefu na adimu za ajira huchangia pia katika tatizo hili.
    Jamii ya xxxxxxx mpaswa kuelewa kuwa umaskini unaoathiri nchi fulani unaathari pana sana.Uvunigu unaotokana na umaskini unaweza kuwa msingi ambako matendo ya kihalifu ili kujinasua kutoka dhiki ile. Hii inaweza kuwa mbegu ya kuatika maovu kama ugaidi na uhalifu wa kila aina.
    Mataifa ya magharibi yanapaswa kuyaburai madeni mataifa yanayoendelea kama njia mojawapo ya kupambana na umaskini. Asilimia kubwa ya pato la kitaifa katika mataifa mengi hutumika kuyalipa madeni hayo. Katika hali hii inakuwamuhali kwa mataifa hayo kujikwamua kutokana na pingu za umaskini. Njia nyingine ni kustahabu kutoa ruzuku za kimaendeleo badala ya mikopo kwa nchi zinazoendelea.
    Kwa upande wake, mataifa yanayoendelea yanapaswa kuibuka na mikakati bora yakupambana na umaskini. Ni muhimu pawepo na sera zinazotambua ukweli kuwa asilimia kubwa ya raia wa mataifa hayo ni maskini. Pana dharura ya kuzalisha nafasi za ajira, kupanua viwanda hususan vinavyohusiana na zaraa ambayo ni tegemeo kuu la mataifa mengi, kuendeleza elimu na kuimarisha miundo msingi. Ipo haja pia ya mataifa haya kuhakikisha kuwa mfumo wa soko huru unaotawala ulimwengu sasa hauishii kuwa chanzo cha kufa kwa viwanda asilia na kuendeleza umasikini zaidi. Kwa ufupi, maamuzi yote ya sera za kiuchumi lazima ya zingatie uhalisi wa maisha ya raia wa mataifa hayo.

    a) Kwa nini umaskini umetamalaki katika mataifa yanayoendelea?
    b) Madeni yana athari gani kwa mataifa yanayoendelea?
    c) Ni mapendekezo yapi ambayo mwandishi anatoa kwa mataifa machanga kuhusu utatuzi wa tatizo la umaskini?
    d) Mfumo wa soko huru una mathara gani kwa mataifa machanga?
    e) Ukirejea kifungu, eleza maana ya:
    i) Kulitadarukia
    ii) Kuatika
    iii) Kuyaburai madeni

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • "Asanteni sana kwa kuja, sisi. . . hukabiliana na mengi." (Solved)

    Damu Nyeusi na Hadithi nyingine : Ken Walibora na Said A. Mohamed
    "Asanteni sana kwa kuja, sisi. . . hukabiliana na mengi."
    i) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    ii) Fafanua matukio yaliyosababisha mkutano huu. (alama 4)
    iii) Jadili changamoto sita zinazokumba jinsia ya kike katika hadithi hii.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Matatizo yanayowakumba wanacheneo ni kielelzo cha matatizo yanayowakumba wananchi wa mataifa mengi ya ulimwengu wa tatu. Thibitisha ukerejelea "Mstahiki Meya". (Solved)

    Matatizo yanayowakumba wanacheneo ni kielelzo cha matatizo yanayowakumba wananchi wa mataifa mengi ya ulimwengu wa tatu. Thibitisha ukerejelea "Mstahiki Meya".

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Huku ukirejelea riwaya ya Kidagaa Kimemwozea thibitisha kwamba vijana wana suluhu tosha kwa matatizo yanayoikumba jamii wanamoishi. (Solved)

    Huku ukirejelea riwaya ya Kidagaa Kimemwozea thibitisha kwamba vijana wana suluhu tosha kwa matatizo yanayoikumba jamii wanamoishi.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Andika kinyume. Sufuria iliyoinjikwa mekoni ni chafu. (Solved)

    Andika kinyume.
    Sufuria iliyoinjikwa mekoni ni chafu.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi kudhihirisha maana ya msemo ufuatao. enda benibeni. (Solved)

    Tunga sentensi kudhihirisha maana ya msemo ufuatao. enda benibeni.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Andika visawe vya maneno haya; i) Wajihi ii) Laazizi (Solved)

    Andika visawe vya maneno haya;
    i) Wajihi
    ii) Laazizi

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Sahihisha kwa kutumia kirejeshi cha mazoea. Kambarau ambao iliyoundwa vyema haitatizi. (Solved)

    Sahihisha kwa kutumia kirejeshi cha mazoea.
    Kambarau ambao iliyoundwa vyema haitatizi.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Tambua matumizi ya kiambishi -ji- katika sentensi ifuatayo. Jino la jitu hilo lililiwezesha kujilia chakula kingi kuliko mkimbiaji yule. (Solved)

    Tambua matumizi ya kiambishi -ji- katika sentensi ifuatayo.
    Jino la jitu hilo lililiwezesha kujilia chakula kingi kuliko mkimbiaji yule.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Andika upya sentensi ifuatayo ukianzia yambwa tendwa. Wakulima waliwakatia ngamia wote majani ya mti huo. (Solved)

    Andika upya sentensi ifuatayo ukianzia yambwa tendwa.
    Wakulima waliwakatia ngamia wote majani ya mti huo.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari, Wakazi waligawiwa vyandarua vya mbu lakini wanavitumai kujengea nyua. (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari,
    Wakazi waligawiwa vyandarua vya mbu lakini wanavitumia kujengea nyua.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Kanusha Ukiona vyaelea vimeundwa. (Solved)

    Kanusha
    Ukiona vyaelea vimeundwa.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi mbili tofauti kudhihirisha maana ya neno 'ilimradi' (Solved)

    Tunga sentensi mbili tofauti kudhihirisha maana ya neno 'ilimradi'

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi moja yenye viungo vya sarufi vifuatavyo; (Solved)

    Tunga sentensi moja yenye viungo vya sarufi vifuatavyo;
    i) Kikanushi
    ii) Kiima katika nafsi ya pili wingi.
    iii) Kiwakilishi cha wakati uliopita.
    iv) Mtendewa katika nafsi ya tatu wingi.
    v) Mzizi wa kitenzi cha silabi moja.
    vi) Mnyambuliko wa kitenzi kauli ya kutendea.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Taja sifa mbili bainifu za vokali /i/ (Solved)

    Taja sifa mbili bainifu za vokali /i/

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya sauti. (Solved)

    Eleza maana ya sauti.

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Ubinafsishaji wa mashirika ya umma ni nguzo kuu katika ulimwengu wa leo. (Solved)

    Soma kifungu kisha uiibu maswali
    Ubinafsishaji wa mashirika ya umma ni nguzo kuu katika ulimwengu wa leo. Kimsingi, ubinafsishaji ni hatua na harakati zinazochukuliwa kupunguza kushiriki kwa serikali katika uendeshaji wa mashirika na kuhimiza kupanuka kwa sekla ya kibinafsi.Serikali huweza kuhimiza, kutokana na uuzaji, uhawilishaji wa mali kutoka umiliki wa umma hadi kwenye umilikaji wa sekta ya kibinafsi. Aidha, serikali inaweza kuuza hisa zake kwenye mashirika ya umma. Njia nyingine ni kuchochea ugavi wa zabuni kupitia kwa mikataba ambayo inashindaniwa na mashirika au kampuni tofauti. Lengo kuu la ubinafsishaji ni kuigatuanafasi ya serikali katika utendakazi na uendeshaji wa mashirika.Uuzaji wamashirika ya kiserikali au hisa huwa chanzo cha mapato yanayoweza kutumiwa kuendesha miradi mingine, Hii ni njia ya kupunguza harija ya serikali inayotokana na uendeshaji wa mashirika yasiyoleta faida. Ubinafsishaji huzuia uwezekano wa kuingiliwa kwa mashirika na wanasiasa, huimarisha utamaduni mpya wa muundo wa mashirika na huvunja uhodhi wa kiserikali. Ubinafsishaji huweza kuatika mbegu za ujasiriamali wa raia kutamani kuanzisha amali tofauti.
    Ubinafsishaji huweza kuyaruhusu mashirika ya kimataifa kutwaa mashirika muhimu nchini, kufutwa kazi kwa wafanyikazi na kuongezeka kwa umaskini. Ubinafsishaji wa sekta zinazohusiana na elimu na afya huweza kuathiri vibaya wenye mapato ya chini.
    Ubinafsishaji haumaanishi ufanisi wa utendakazi wa makampuni na mashirika. Aidha, ikiwa haupo utaratibu mzuri wa kutathmini au kupima thamani za hisa pana uwezekano wa hisa zinazouzwa kupewa thamani ya juu au ya chini.
    Maswali
    a) Bila kupoteza maana iliyokusudiwa na mwandishi wa kifungu, andika muhtasari wa aya ya kwanza na ya pili. (Maneno 35 - 40).
    b) Dondoa hoja muhimu zinazojitokeza katika aya ya tatu na ya nne. (Maneno 45 - 50)

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)

  • Matumizi ya sheng' yameshamiri sana nchini Kenya hasa miongoni mwa vijana. (Solved)

    Soma taarifa inayofuata kisha uyajibu maswali
    Matumizi ya sheng' yameshamiri sana nchini Kenya hata miongoni mwa vijana. Ni kilugha ambacho kinakisiwa kuzuka katika miaka ya 60 na 70 katika makazi ya mashariki mwa jiji la Nairobi kama vile Kaloleni, Mbotela/ Bahati na kadhalika.Kwa sasa ni kilugha kilichoenea kwingi nchini Kenya na kuwa kitambulisho cha takriban vijana wengi. Wataalam mbalimbali wanabainisha nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha lugha hii. Kuna nadharia mbili kuu kuhusu asili ya lugha ya Sheng: kwamba kilugha hiki kiliibuka kutokana na wahuni na wakora jijini Nairobi ambao lengo lao Iilikuwa kuwasiliana kwa siri. Nadharia nyingine ni kuwa kilichipuka kutokana na vijana ambao walizua lugha ya kuwasiliana baada ya uhuru (kwa sababu walikichukia Kiswahili ambacho walikiona kama lugha ya uboi)
    Dhana hizi kwa muda mrefu, zimeathiri mitazamo kuhusiana na kilugha hiki. Kwa sasa ni kilugha ambacho ,yjiasambaa katika sehemu mbalimbali za Kenya na watu wa matabaka mbalimbali wanakitumia. Kilugha hiki kimeanza kuashiria uhalisia mkubwa wa maisha ya kisasa, zaidi katika jamii ya Wakenya. Aidha, sheng imejitanzua kutoka hali ya kuwa kilugha cha maongezi pekee na sasa kinatumiwa katika baadhi ya vitabu, hata waandishi wa vitabu wameanza kukitumia. Kwa mfano, katika miaka ya 80, David Mailu katika kitabu chake 'Without Kiinua Mgongo' alitumia Sheng. Katika siku za hivi karibuni, riwaya ya 'Kidagaa Kimemwozea' iliyoandikwa na Ken Walibora kilugha cha sheng kimepewa nafasi kama kitambulisho cha vijana kupitia kwa mhusika DJ Bob.
    Vilevile kumezuka vyombo vya habari kama redio, mfano idhaa ya Ghetto, redio ambayo inaendeleza mawasiliano kwa matumizi ya Sheng. Kuna vipindi vya matangazo ya kibiashara katika runinga ambayo yanaendelezwa kwa Sheng. Kwa mfano, katika 'gazeti la Taifa Leo, kuna ukumbi wa 'Mchongoano' ambao umekuwa ukiendelezwa kwa Sheng.
    Nchini Kenya ambapo asilimia 60% ya idadi ni vijana, Sheng imetokea kuwatambulisha vijana. Katika enzi hii ya Teknohama. wanaomiliki vyombo vya habari na sekta nyingine za biashara wamegundua kuwa matumizi ya Sheng ndiyo njia mwafaka zaidi ya kulifikia soko kubwa la vijana kwa ajili ya kueneza matangazo ya bidhaa na huduma za kibiashara. Kwa hivyo, Sheng imekuwa daraja la kuwafikia na kuwavutia vijana.
    Hata hivyo, kwa upande mwingine matumizi ya Sheng yamelaumiwa na walimu wengi katika shule za msingi na zile za upili kuwa ni sababu mojawapo kuu ya kushuka kwa matokeo ya lugha ya Kiswahili na Kiingereza miongoni mwa wanafunzi. Sheng imelaumiwa kwamba inasababisha wanafunzi kutozingatia mafunzo ya kanuni za sarufi na tahajia au maendelezo. Wataalam wanadai kuwa ni msimbo ambao hauzingatii sheria za sarufi na tahajia kwa sababu zisizofahamika, kwani ingawa muundo wake wa kisarufi hushahabiana na ule wa Kiswahili, Sheng hupuuza sarufi ya Kiswahili katika matumizi yake.
    Ingawa sheng imekuwa ikipigwa vita, kuna wataalam ambao wana mtazamo kwamba juhudi hizo haziwezi kufanikiwa kwani Sheng ni chombo cha mawasiliano miongoni mwa vijana na kwa hivyo ina umuhimu wake ambao hauwezi kufumbiwa macho. Wanasema kuwa ni chombo ambacho kinafumbata hisia na mshikamano wa kizazi kipya kama ilivyojitokeza katika kauli mbiu ya mgombeaji urais mwaka wa 2012,'Tunawesmake.
    Katika hali ambapo kiwango cha ubora wa matokeo ya Kiswahili yalidorora katika mtihani wa kidato cha nne (KCSE) mwaka wa 2012 na kuwa asilimia 35.81 pekee yakilinganishwa na asilimia 48.82 ya mwaka 2011, Sheng imekuwa ikilaumiwa kuwa ndicho chanzo cha kudorora kwa viwango vya ubora wa matokeo. Baadhi ya hao wataalamu wanasema kwamba Sheng haipaswi kuhujumiwa. kinachohitajika kufanywa ni kuwaelimisha vijana kuhusu mipaka ya matumizi yake.

    Maswali
    a) Taja mada ya kifungu hiki.
    b) Fafanua nadharia mbili zilizoeleza asili ya lugha ya sheng.
    c) Eleza matumizi bainifu ya kilugha cha Sheng katika jamii ya sasa.
    d) Taja matokeo hasi ya matumizi ya Sheng katika jamii.
    e) Ni kwa nini mwandishi Walibora ameshirikisha matumizi ya Sheng katika kazi yake ya Kidagaa Kimemwozea
    f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu hiki.
    i) Teknohama
    ii) kudorora
    iii) msimbo
    iv) Kuhujumiwa

    Date posted: September 25, 2019 .    Answers (1)