Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Sahihisha sentensi ifuatayo. Mtu ambaye aliyechukua kitabu chenye kilikuwa hapa arudishe.

      

Sahihisha sentensi ifuatayo.
Mtu ambaye aliyechukua kitabu chenye kilikuwa hapa arudishe.

  

Answers


Kavungya
Mtu aliyechukua kitabu kilichokuwa hapa arudishe.
au
mtu ambaye alichukua kitabu kilichokuwa hapa arudishe.
Kavungya answered the question on October 18, 2019 at 14:15


Next: Onyesha vishazi katika sentensi ifuatayo kisha uelezee ni vya aina gani. Ajapo tutamlaki kwa shangwe.
Previous: Tumia mzizi –w- katika sentensi kama: (i)Kitenzi kisaidizi. (ii)Kitenzi Kishirikishi.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Onyesha vishazi katika sentensi ifuatayo kisha uelezee ni vya aina gani. Ajapo tutamlaki kwa shangwe.(Solved)

    Onyesha vishazi katika sentensi ifuatayo kisha uelezee ni vya aina gani.
    Ajapo tutamlaki kwa shangwe.

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Andika kwa msemo wa taarifa: Askari: Ulikuwa unaelekea wapi uliposhambuliwa? Jirani: Nilikuwa nikienda sokoni jana. (Solved)

    Andika kwa msemo wa taarifa:
    Askari: Ulikuwa unaelekea wapi uliposhambuliwa?
    Jirani: Nilikuwa nikienda sokoni jana.

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Neno lifuatalo liko katika ngeli gani? Matukio (Solved)

    Neno lifuatalo liko katika ngeli gani?
    Matukio

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Viambishi vilivyopigiwa mstari vinawakilisha dhana zipi za kisarufi? i)Udhaifu ii)Walani? (Solved)

    Viambishi vilivyopigiwa mstari vinawakilisha dhana zipi za kisarufi?
    i)Udhaifu
    ii)Walani?

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Eleza ni kwa nini neno umma ni la asili ya kigeni.(Solved)

    Eleza ni kwa nini neno umma ni la asili ya kigeni.

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Taja maneno yenye miundo ifuatayo ya silabi. (i)KKKI (ii)Irabu pekee (II) (Solved)

    Taja maneno yenye miundo ifuatayo ya silabi.
    (i)KKKI
    (ii)Irabu pekee (II)

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata: Katika safu yangu hii sina lengo la kuzishambulia dini zetu na namuomba Mungu sana asiniandikie dhambi kutokana na ninayotaka...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata:

    Katika safu yangu hii sina lengo la kuzishambulia dini zetu na namuomba
    Mungu sana asiniandikie dhambi kutokana na ninayotaka kuyaandika. Lakini nashawishika kuikumbusha jamii yangu ambayo inatufanya watu tuzione dini zetu zinamkandamiza mwanamke. Dini zetu kubwa kama Uislamu na Ukristo zinatuelekeza mwanamke kumheshimu mumewe na kumsikiliza anachosema, lakini kwa yeye
    kufuata maadili ya dini na si kukuambia uue ukakubali.
    Wakati dini inasema utekeleze amri ya mumeo na wao wameelezwa mambo
    ya kuwafanyia wanawake, ikiwa ni pamoja na kuwaheshima na kuwaridhisha kadri
    ya uwezo wao.
    Kutokana na hilo la amri, wanaume wengi ndio wamechukua kama tiketi ya kunyanyasa mwanamke na hata kumnyima fursa ya kujiendeleza kielimu na hata kufanya shughuli za kuongeza kipato. Unakuta familia ni ya kimaskini, baba hana fedha za kutosha kuihudumia familia yake, lakini baba huyo anataka kujishughulisha
    na shughuli yoyote ya kumuingizia kipato kinachoweza kuwasaidia wote na matokeo yake kuendelea kuwepo, kwenye dimbwi la umasikini. Wengine kwa hofu ya kupata changamoto kutoka kwa wake zao wanawakatalia wanawake walio wao kujiendeleza kielimu au kutafuta mwanamke asiyeelimika ili asiweze kuhoji mambo kadhaa ndani
    ya nyumba.
    Hili limebainishwa hivi karibuni na shirika moja lisilo la kiserikali huko
    kigoma ambapo katika utafiti wao asilimia 90% ya wanawake wa vijijini wanashindwa kutoa hoja kutokana na uelewa wao duni na kutoa sababu ya kuwa hiyo ni kutokana
    na ukosefu wa elimu, masuala ya kidini yanayomwelekeza mwanamke kufuata amri
    za mumewe, mila na desturi kadhaa.
    Dini zote zinaeleza wazi umuhimu wa mtu kupata elimu bila kubagua kama
    ya kiislamu inavyosema; mtu anapata thawabu anapotafuta elimu na anatakiwa
    aitafute popote bila kujali umbali na hata ikiwezekana kufika China ambapo
    inaaminika ni mbali.
    Sijawahi kuona wala kusikia dini ikisema mwanamke asipate elimu lakini
    baba zangu na kaka zangu wanaume wanalipotosha hili kutaka kuendelea kumkandamiza mwanamke bila kufikiri kuwa mwanamke ni msaada mkubwa
    kwao na kwa maendeleo ya taifa lote; ikiwa leo tupo katika harakati za kupata maendeleo na nchi hii hivi kweli tutafanikiwa?
    Mapambano ya kuleta maendeleo yaanze katika ngazi ya familia kwa
    kuondoka kwa ujinga wa kumkandamiza mwanamke ili naye aelimike, aweze
    kujenga hoja, aweze kujitafutia kipato na mwisho kusaidia katika maendeleo ya
    familia ambayo kwa njia nyingine ndiyo maendeleo yenyewe ya taifa hili.

    (a)Fupisha aya tano za kwanza. (Maneno 70).
    Matayarisho
    Jibu.
    (b)Mwanamke anaweza kuendelezwa vipi. Rejelea aya mbili za mwisho. (Maneno 50).
    Matayarisho
    Jibu.

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata. Ni fedheha kuona taifa ambalo halijakuwa likitambua msamiati wa shibe kwa zaidi ya miongo miwili sasa limeacha chakula kiharibike...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.

    Ni fedheha kuona taifa ambalo halijakuwa likitambua msamiati wa shibe kwa zaidi
    ya miongo miwili sasa limeacha chakula kiharibike mashambani kutokana na ukosefu wa soko. Taarifa kuwa ni zamu ya wakulima wa mahindi kukadiria hasara baada
    ya wenzao wa maziwa ni za kuhuzunisha. Inasemekana wakulima wa zao la mahindi katika mikoa ya pwani, mashariki, kati na Bonde la ufa wanendelea kuhesabu hasara kutokana na ukosefu wa soko la mahindi kutoka kwa serikali.

    Hii ni hata baada ya serikali kuwapatia na kuwauzia pembejeo kwa bei nafuu kama
    njia mojawapo ya kuimarisha uzalishaji wa chakula nchini. Kinachovunja moyo
    zaidi ni habari kuwa serikali iyo hiyo ilitoa ahadi ya kununua mazao yote ya
    wakulima hao kama njia mojawapo ya kuwatia moyo katika kazi yao.

    Kando na wakulima wa kibinafsi, ilitumia mamilioni ya pesa za umma kuzindua
    miradi ya kilimo cha mahindi kwa kunyunyizia mashamba maji na mazao yake
    pia yanaharibikia. Wakulima wa mradi wa kilimo cha kunyunyizia mashamba wa
    Hola, kwa mfano, wameathirika pakubwa kutokana na ukosefu wa soko la mazao
    yao. Imekuwa ikijikokota kutokana na sababu kadhaa ikiwemo ukosefu wa fedha
    za kununua mahindi.

    Hii ni hata baada ya uchunguzi kuonyesha kuwa usalama wa chakula nchini
    umedorora kutokana na kiangazi cha muda mrefu. Mbali na kutokuwepo kwa
    utaratibu wa kununua mahindi kutoka kwa wakulima hao halmashauri ya nafaka
    haina uwezo wa kuwashughulikia wakulima wote nchini.

    Hii ni kwa sababu wakulima wengi hawapati huduma za halmashauri hiyo ambayo imejikita katika maeneo yaliyokuwa yakizalisha chakula kwa wingi miaka iliyopita. Eneo la Hola, kwa mfano, liko mbali kutoka kwa kituo cha halmashauri hiyo kwa sababu eneo hilo ni kame.

    Ni kutokana na muktadha huu serikali inapaswa ichukue hatua za haraka kuepusha
    kuharibika kwa zao la mahindi nchini. Serikali inapaswa kutenga fedha zaidi za kununua mahindi kutoka kwa wakulima. Inakisiwa kuwa hasara zaidi inatarajiwa kutokea ikiwa pesa zaidi hazitatengwa kwa sababu idadi ya wakulima wanaovuna mahindi inatarajiwa kuongezeka.

    Maswali
    (a)Kwa nini chakula kinaharibikia mashambani?
    (b)Serikali ilichangia vipi katika kuimarisha uzalishaji wa chakula?
    (c)Eleza vile halmashari ya nafaka haijaweza kuepushia wakulima wa mahindi hasara.
    (d)Kwa nini wakulima wa maeneo kame hawajashughulikiwa na halmashuri ya nafaka?
    (e)Kutokana na taarifa hii serikali inaweza kutatua tatizo la wakulima kwa njia gani?
    (f)Pendekeza namna taifa linaweza kuepuka na kupambana na uharibifu wa chakula mashambani.
    (g)Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika taarifa.
    (i)Miongo
    (ii)Pembejeo
    (iii)Umedorora

    Date posted: October 18, 2019.  Answers (1)

  • Taja mambo yoyote manne yanayofanywa na serikali yetu kuimarisha lugha ya Kiswahili (Solved)

    Taja mambo yoyote manne yanayofanywa na serikali yetu kuimarisha lugha ya Kiswahili

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Kanusha katika ukubwa Mwizi huyu aliiba kisu na ng’ombe wa mwanamke yule. (Solved)

    Kanusha katika ukubwa
    Mwizi huyu aliiba kisu na ng’ombe wa mwanamke yule.

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Eleza tofauti iliyopo kati ya sentensi hiziTulipofika hotelini tulipewa soda na chupaTulipofika hotelini tulipewa soda kwa chupa(Solved)

    Eleza tofauti iliyopo kati ya sentensi hizi
    Tulipofika hotelini tulipewa soda na chupa
    Tulipofika hotelini tulipewa soda kwa chupa

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya sentensi hii Ningalikuwa na pesa ningalinunua gari na ningalistarehe. (Solved)

    Eleza maana ya sentensi hii
    Ningalikuwa na pesa ningalinunua gari na ningalistarehe.

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Andika neno lenye maana sawa na Hawala Katani(Solved)

    Andika neno lenye maana sawa na
    Hawala
    Katani

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha matumizi ya kiimbo katika sentensi hii Ondoka hapa! (Solved)

    Onyesha matumizi ya kiimbo katika sentensi hii
    Ondoka hapa!

    Date posted: October 17, 2019.  Answers (1)

  • Eleza sifa mbili za vishazi tegemezi.(Solved)

    Eleza sifa mbili za vishazi tegemezi.

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)

  • Bainisha aina za vitenzi katika sentensi ifuatayo. Walimu ni watu wasiopendwa wanaposema ukweli kuhusu wanafunzi (Solved)

    Bainisha aina za vitenzi katika sentensi ifuatayo.
    Walimu ni watu wasiopendwa wanaposema ukweli kuhusu wanafunzi

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha virai katika sentensi zifuatazo na ueleze ni vya aina gani. i) Anachukia kusoma riwaya yenye masuala ya kisiasa. ii) Watoto wa kike hudunishwa katika jamii...(Solved)

    Onyesha virai katika sentensi zifuatazo na ueleze ni vya aina gani.
    i) Anachukia kusoma riwaya yenye masuala ya kisiasa.
    ii) Watoto wa kike hudunishwa katika jamii nyingi

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)

  • Yakinisha katika nafsi ya tatu wingi Sijasafiri kwenda marekani (Solved)

    Yakinisha katika nafsi ya tatu wingi
    Sijasafiri kwenda marekani

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)

  • Changamua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha jedwali Omondi anaazimia kuwa mhasibu Lakini hatii bidii masomoni (Solved)

    Changamua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha jedwali
    Omondi anaazimia kuwa mhasibu Lakini hatii bidii masomoni

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo kwa wingi, wakati uliopita hali ya kuendelea Mwalimu humuadhibu mwanafunzi mwenye hatia. (Solved)

    Andika sentensi ifuatayo kwa wingi, wakati uliopita hali ya kuendelea
    Mwalimu humuadhibu mwanafunzi mwenye hatia.

    Date posted: October 16, 2019.  Answers (1)