Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza dhima ya sentensi hii. Rudi ulikotoka.

      

Eleza dhima ya sentensi hii.
Rudi ulikotoka.

  

Answers


Kavungya
Kuamrisha.
Kavungya answered the question on October 31, 2019 at 08:42


Next: Kanusha. Mwanafunzi alikuwa akilia alipojikwaa.
Previous: Halleluyah… Mungu asifiwe sana… shetani ashindwe… Tambua na utoe sifa za sajili hii.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Kanusha. Mwanafunzi alikuwa akilia alipojikwaa.(Solved)

    Kanusha.
    Mwanafunzi alikuwa akilia alipojikwaa.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha aina ya vishazi katika sentensi hii. Isipokuwa ni kulewa kwake angeenda Kitui.(Solved)

    Onyesha aina ya vishazi katika sentensi hii.
    Isipokuwa ni kulewa kwake angeenda Kitui.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Kosoa sentensi ifuatayo kwa njia mbili tofauti. Ningelima shamba langu kwa wakati ufaao ningalivuna sawasawa.(Solved)

    Kosoa sentensi ifuatayo kwa njia mbili tofauti.
    Ningelima shamba langu kwa wakati ufaao ningalivuna sawasawa.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi kutofautisha maana ya majina haya. Nadhari Nathari(Solved)

    Tunga sentensi kutofautisha maana ya majina haya.
    Nadhari
    Nathari

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha shamirisho katika sentensi ifuatayo. Kakubwa alimjengea mama yake nyumba kwa mawe.(Solved)

    Onyesha shamirisho katika sentensi ifuatayo.
    Kakubwa alimjengea mama yake nyumba kwa mawe.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Badilisha sentensi ifuatayo iwe katika kauli ya kutendwa. Simba mwenda pole alimla swara mnono sana.(Solved)

    Badilisha sentensi ifuatayo iwe katika kauli ya kutendwa.
    Simba mwenda pole alimla swara mnono sana.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi. Anampenda wake sana lakini alimpiga sana(Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi.
    Anampenda wake sana lakini alimpiga sana

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Tumia neno msomi kama nomino na kama kivumishi katika sentensi.(Solved)

    Tumia neno msomi kama nomino na kama kivumishi katika sentensi.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Andika kinyume cha sentensi hii. Mama alienda sokoni jana asubuhi.(Solved)

    Andika kinyume cha sentensi hii.
    Mama alienda sokoni jana asubuhi.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi hii kwa udogo wingi. Mti ulikatwa ukatengeneze kiti.(Solved)

    Andika sentensi hii kwa udogo wingi.
    Mti ulikatwa ukatengeneze kiti.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja ukitumia kiunganishi cha kuongeza.(Solved)

    Tunga sentensi moja ukitumia kiunganishi cha kuongeza.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Tumia kiambishi ndi- pamoja na kiwakilishi huru cha nafsi ya kwanza wingi.(Solved)

    Tumia kiambishi ndi- pamoja na kiwakilishi huru cha nafsi ya kwanza wingi.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Thibitisha kuwa neno moja linaweza kuwa katika ngeli mbili tofauti.(Solved)

    Thibitisha kuwa neno moja linaweza kuwa katika ngeli mbili tofauti.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha mofimu mbalimbali katika neno kikikipikia.(Solved)

    Onyesha mofimu mbalimbali katika neno kikikipikia.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Eleza kanuni ya kutia shadda katika lugha ya Kiswahili.(Solved)

    Eleza kanuni ya kutia shadda katika lugha ya Kiswahili.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Toa mfano wa maneno mawili ambayo yana sauti mwambatano mbili.(Solved)

    Toa mfano wa maneno mawili ambayo yana sauti mwambatano mbili.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Taja sifa mbili za irabu /e/ na /i/ ambazo zinafanana.(Solved)

    Taja sifa mbili za irabu /e/ na /i/ ambazo zinafanana.

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Historia na fasihi zina uhusiano wa karibu sana hasa fasihi ya kihistoria. Hata hivyo fasihi siohistoria na historia si fasihi kwa...(Solved)

    UHUSIANO WA FASIHI NA HISTORIA

    Historia na fasihi zina uhusiano wa karibu sana hasa fasihi ya kihistoria. Hata hivyo fasihi sio
    historia na historia si fasihi kwa sababu hizi ni taaluma mbili ambazo zina uhusiano tu. Hata hivyo, fasihi
    na historia zina mambo ambayo yanafana na yale ambayo hayafanani.
    Kati ya mambo ambayo yanafanana ni kwamba fasihi na historia wakati mwingine huweza kuwa
    na wahusika ambao wanafanana kitabia, kimaumbile na hata wakati mwingine matendo ya kukumbukwa
    waliyofanywa. Mfano ni katika shairi la “Hongera Rais Moi” katika diwani ya ' Malenga wa ziwa kuu'
    ambapo mhusika ni rais Moi na mhusika kama yule pia aliishi katika kipindi Fulani katika nchi ya Kenya.
    Jambo jingine ambalo linapatikana katika fasihi na pia kinaoana na historia ni mandhari. Wakati
    mwingine, mandhari ambayo ni ya kihistoria yanakaribiana sana na ya kifasihi na hata wakati mwingine
    kufanana. Mandhari ya shamba la bwana Delamon katika 'kilio cha haki' yanaweza kuwa shamba lolote na
    mabwanyenye kama hata ni ya Bwana Dalamere.
    Wakati mwingine matukio katika fasihi huwa karibu sawa na yale ambayo yanapatikana katika
    historia ya kawaida. Mfano katika shairi la ' wasifu wa baba Kenyatta', mhusika mkuu yasemekana
    alipigania uhuru wa nchi ambayo aliiongoza. Matukio kama kufungwa jela ambayo mhusika huyu
    anapitia katika kujaribu kukomboa nchi ni sawa na yale ambayo mhusika wa kihistoria ambaye ni rais wa
    kwanza wa nchi ya Kenya.
    Pia, wakati mwingi historia na fasihi huwa na maudhui na dhamira sawa. Tamthilia kama 'Mstahiki
    Meya' ambayo nia yake ni kuonyesha jinsi waafrika ambao walichuukua uongozi baada ya ukoloni
    walivyowanyanyasa waafrika wenzao yaweza kuwa sawa na historia ambapo waafrika ambao
    walichukua uongozi waliwanyanyasa waafrika wenzao.
    Uhusiano mwingine wa karibu ni kwamba wakati mwingine fasihi huchota kutoka kwa historia na
    inapofanya hivyo fasihi hiyo inakuwa ya kufanana sana na historia yenyewe.Mfano ni kitabu cha
    mzalendo kimathi ambapo matukio mengi katika kitabu hicho kinadhihirisha kwamba kimechota kutoka
    kwa historia. Pia baada ya kipindi Fulani, fasihi husika inakuwa historia.
    Uhusiano mwingine ni kwamba zote huandikwa kwa lugha na zinapoandikwa fasihi hufufua majina
    ya wale ambao majina yao hayakuweza kuingia katika vitabu vya historia.
    Mwisho, historia na fasihi hufanya jukumu la kumjuza mwanadamu kuhusu mazingira yake hasa
    yale ya zamani na kumuwezesha kuweza aidha kuyarekebisha au kuyakubali. Mfano ni katika tamthilia ya
    kidagaa, Mtemi Nasaba Bora anawapokonya waafrika wezake mashamba kwa kutumia nguvu. Fasihi hii
    pia inaoana na jinsi ambavyo historia inafunza ambavyo viongozi wa kwanza walivyojipatia vipande
    vikubwa vikubwa vya ardhi.Fasihi na historia pia zinakaribiana sana kutokana kwamba mwanahistoria na
    mwanafasihi ni wanajamii wote. Wale ambao huchunguza matukio ya kihistoria na wale ambao huandika
    fasihi pia ni wanajamii.
    Mojawapo wa tofauti ya historia na fasihi ni tofauti ya kiwakati. Historia imefungika kiwakati hivi
    kwamba upeo wake ni sasa. Mwanahistoria akitaka kujuza kuhusu nchi Fulani anaeleza ilikoanza hadi
    ilikofika lakini mwanafasihi anaweza kueleza mahali nchi fulani ilikoanza, iliko sasa na itakavyokuwa
    baada ya miaka mingi baada ya sasa. Mwanafasihi anaweza kuandika kuhusu nchi ya kesho peke yake na
    fasihi iwe imekamilika. Mfano mwema ni George Orwell ambaye alikiandika kitabu mwaka wa 1978 na
    akakiita 1984. Pia Riwaya ya 'Walenisi' ni riwaya ambayo inazungumza kuhusu dunia ambayo ni ya kesho
    jambo ambalo historia haiwezi.
    Tofauti nyingine ni kwamba historia hutegemea ithibati ili iweze kufahamisha. Kama
    inazungumzia kuhusu tukio Fulani, lazima iwe na dhibitisho sahihi na hamna nafasi ya ubunifu. Kwa
    upande mwingine, fasihi ina nafasi ya ubunifu na sio lazima mwanafasihi adhibitishe yale ambayo
    ameandikia yalifanyika. Hata kama Mstahiki Meya ni jina ambalo ni la kihalisia katika masikio ya
    Wakenya, mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki hana jukumu la kutoa idhibati za kuonyesha kwamba aliishi
    na pia cheneo ni mojawapo wa miji ya nchi fulani.
    Tofauti nyingine ni kwamba kila mwanafasihi huwa na itikadi yake lakini mwanahistoria huweka
    mambo jinsi yalivyo na kumwachia msomaji awe wa kuamua. Mwandishi kama wa tamthilia ya 'Mstahiki
    Meya' ana itikadi kwamba viongozi dhalimu wanastahili kuondolewa mamlakani kwa nguvu lakini
    mwanahistoria hawezi kuwa na msimamo kama huo.
    Tofauti nyingine ni kwamba fasihi hujikita sana kwa wahusika na maisha yao lakini jambo kuu na
    ambalo historia huzingatia sana ni matukio na wakati ambao matukio hayo yalitokea. Hili hufanya takriban
    fasihi zote kuwa na mhusika mkuu lakini kipindi fulani cha historia chaweza kosa hata mhusika mmoja
    mkuu.
    Jambo jingine ni kwamba historia na fasihi hutofautiana kiwakati, mahali na mandhari ambamo
    matukio fulani yanatokea. Tamthilia kama ya ‘Mstahiki Meya’ ina uwezakano kwamba inazungumza
    kuhusu Kenya na viongozi wa baada ya uhuru lakini mahali ambapo matukio ya tamthilia yanafanyikia ni
    cheneo ala sio wa mji kama Nakuru au Nairobi.
    Tofauti nyingine ni kwamba hamna nafasi ya ubunifu katika historia lakini fasihi huwa ni zao la
    ubunifu. Mambo ambayo wanahistoria huwa wamekosa katika historia yanaweza yakawa wazi kupitia
    ubunifu wa mwandishi. Fasihi pia inaweza ikaumba wahusika au hata dunia ambayo haiwezi ikapatikana
    katika ulimwengu wa kawaida.

    Maswali.
    a. Fupisha aya tatu za kwanza kwa maneno 20-30.
    Nakala safi
    b. Fupisha aya tano za mwisho kwa maneno kati ya 60-70
    Matayarisho

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Siku ya Alhamisi tarehe 4 Disemba 2014 Umoja wa Mataifa ulitoa ripoti ukitahadharisha juu yakuongezeka vitendo vya ghasia na mauaji...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali

    Siku ya Alhamisi tarehe 4 Disemba 2014 Umoja wa Mataifa ulitoa ripoti ukitahadharisha juu ya
    kuongezeka vitendo vya ghasia na mauaji nchini Kenya. Ripoti hiyo inasema kuwa katika kipindi cha
    miaka miwili iliyopita watu zaidi ya 300 wameuawa na wengine takribani 220,000 kulazimika kuishi kama
    wakimbizi kutokana na ghasia hizo. Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja huo amesema kuwa
    ukame mkubwa na mivutano inayotokana na siasa za kuhamishia madaraka mashinani ni baadhi ya
    mambo yanayochangia kuongezeka vitendo vya ghasia na mapigano katika maeneo ya kaskazini na ya
    mbali nchini Kenya. Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wizi wa mifugo na mauaji ya kulipiza
    kisasi kati ya jamii hasimu za wafugaji katika maeneo hayo ni jambo la kawaida na kwamba silaha
    ndogondogo zinapatikana kwa wingi kati ya jamii hizo. Ugomvi wa kuwania ardhi, malisho, vyanzo vya
    maji na madaraka ya kisiasa mwaka huu umewafanya raia wengi katika maeneo ya kaskazini mwa Kenya
    kuwa wakimbizi katika nchi yao wenyewe. Kwa kadiri kwamba idadi ya wakimbizi hao imeongezeka
    mara nne zaidi ikilinganishwa na ya mwaka uliopita wa 2013.
    Mbali na matatizo ya ndani yanayotokana na ukame na ugomvi wa kikabila, mashambulio ya kundi
    la kigaidi la al- Shabaab ni jambo jingine ambalo linahatarisha usalama wa Kenya. Kundi hilo Jumapili
    iliyopita lilitangaza kuhusika na bomu lililolipuka katika soko moja huko mjini Garissa, mashariki mwa
    Kenya karibu na mpaka wa nchi hiyo na Somalia. Kundi hilohilo lilihusika na mauaji ya abiria 28
    waliokuwa kwenye basi moja la shirika la usafiri la Makka lililokuwa njiani kutoka mjini Mandera
    kaskazini mwa nchi kuelekea mji mkuu Nairobi. Siku 10 baadaye kundi hilo hilo la kigaidi lilivamia na
    kuwafyatulia risasi kinyama wafanyakazi 36 wa machimbo ya mawe katika kijiji cha Koromey kilicho nje
    kidogo ya mji huo wa Mandera.
    Katika tukio jingine la mashambulio ya kundi la al- Shabaab katika maeneo yanayopakana na
    Somalia, siku ya Jumatatu iliyopita kundi hilo lilishambulia klabu ya Ngamia mjini Wajir na kuwafatulia
    risasi kiholela watu waliokuwa katika klabu hiyo ambapo waliua mmoja kati yao na kuwajeruhi wengine
    13. Visa hivyo vya machafuko na ukosefu wa usalama vilimpelekea Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
    Jumanne iliyopita kuwafuta kazi Waziri wa Mambo ya Usalama wa Ndani pamoja na Inspekta Mkuu wa
    polisi ya nchi hiyo. Kufuatia matukio hayo, vyombo vya usalama vya Kenya vimezidisha hatua za
    kiusalama nchini ili kuzuia kukaririwa kwa matukio kama hayo ya utovu wa nidhamu na usalama. Mbali na
    hayo mwaka uliopita kundi la al- Shabaab lilishambulia na kusababisha maafa na hasara kubwa katika
    jengo la maduka ya kibiashara la West Gate mjini Nairobi. Al- Shabaab linapigana na kikosi cha askari wa
    kulinda amani cha Umoja wa Afrika kinachohudumu huko Somalia AMISOM na limekuwa likitekeleza
    mashambulio ya kigaidi nchini Kenya kama alama ya kulalamikia ushiriki wa nchi hiyo katika kikosi
    hicho, ili hatimaye liilazimishe iondoe askari wake katika radhi ya nchi hiyo.

    1. Yape makala haya kichwa mwafaka.
    2. Taja matatizo manne ya ndani kwa ndani ambayo yanahatarisha usalama wa Kenya.(alama 2)
    3. Taja matukio matatu yaliyomfanya rais awapige kalamu waziri na inspekta mkuu wa polisi (alama 3)
    4. Eleza sababu wanayotoa wana al-Shabaab ya kutekeleza ukatili dhidi ya Wakenya. (Alama 2)
    5. Eleza dhamira ya kikundi cha al-Shabaab
    6. Kwa maoni yako mwenyewe, Eleza mambo matatu ambayo anayevamiwa na kundi la al-shabaab
    anaweza kufanya ili kujiokoa na kuokoa wengine.
    7. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kufungu.
    a) Radhi
    b) Wakimbizi

    Date posted: October 31, 2019.  Answers (1)

  • Fafanua sababu tatu zilizochochea usanifishaji wa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru .(Solved)

    Fafanua sababu tatu zilizochochea usanifishaji wa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru .

    Date posted: October 29, 2019.  Answers (1)