Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Bainisha matumizi ya viambishi vilivyopigiwa mistari katika sentensi

      

Bainisha matumizi ya viambishi vilivyopigiwa mistari katika sentensi

i)Yego ana ujuzi mwingi
ii) Yule mfanyibiashara aliyejidanganya amepata hasara

  

Answers


Wilfred
i)Yego ana ujuzi mwingi – hali

ii)Aliyejidanganya – nafsi rejeshi/mtu kujitendea kitendo mwenyewe
Wilfykil answered the question on October 2, 2019 at 10:55


Next: Describe five impacts of the First Lancaster House Conference of 1960.
Previous: Mention six extra ordinary things in the birth stories of Jesus.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Tunga sentensi sahihi kuonyesha wakati uliopo usiodhihirika(Solved)

    Tunga sentensi sahihi kuonyesha wakati uliopo usiodhihirika

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha sentensi: lo unaweza kuubeba mzigo huo pekeyo mzee alishangaa(Solved)

    Akifisha sentensi:
    lo unaweza kuubeba mzigo huo pekeyo mzee alishangaa

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli kwenye mabano(Solved)

    Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli kwenye mabano

    1. Oa (kufanyiza)
    2. -la- (kufanyana )
    3. Dhuru (fanyika)

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Andika upya sentensi zifuatazo kwa kutumia jina jingine lililo na maana sawa na lililopigiwa mstari(Solved)

    Andika upya sentensi zifuatazo kwa kutumia jina jingine lililo na maana sawa na lililopigiwa mstari

    i. Ni nadra sana kumpata msichana asiyetoga masikio siku hizi

    ii. Zahama ilizuka wafanyikazi walipogoma

    iii. Lengo la kila mwanafunzi ni kupasi mtihani

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Tumia neno vizuri kama:(Solved)

    Tumia neno vizuri kama:
    i) Kielezi

    ii)Kiwakilishi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Weka shadda kwa neno WALAKINI ili kuonyesha maana mbili(Solved)

    Weka shadda kwa neno WALAKINI ili kuonyesha maana mbili

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Tumia ‘po’ kutunga sentensi ya kuleta dhana ya wakati maalum(Solved)

    Tumia ‘po’ kutunga sentensi ya kuleta dhana ya wakati maalum

    i) Wakati maalum
    ii) Wakati usiodhihirika

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi yenye maneno N + V + E + E + T + N(Solved)

    Tunga sentensi yenye maneno N + V + E + E + T + N

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Toa mifano miwili ya aina za nomino zifuatazo(Solved)

    Toa mifano miwili ya aina za nomino zifuatazo
    i)nomino mseto
    ii) nomino za wingi
    iii) nomino za fikra

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Tumia kivumishi cha a- unganifu pamoja na nomino katika ngeli ya I-I kutunga sentensi(Solved)

    Tumia kivumishi cha a- unganifu pamoja na nomino katika ngeli ya I-I kutunga sentensi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa.(Solved)

    Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa.
    “Mimi nitawakaribisha wageni leo jioni. Kisha nitaondoka kwenda kwangu kesho.” Fatuma alimwambia juma.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha viambishi katika neno HAKUJULIKANA(Solved)

    Ainisha viambishi katika neno HAKUJULIKANA

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya kiambishi(Solved)

    Eleza maana ya kiambishi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Sisi vijana wa Kenya inatupasa tuwajibike kufanya kazi kwa bidii, na kwa dhati ya mioyo yetu tuweze kupata ufanisi, na uwezekano wa kuinua nchi yetu...(Solved)

    Sisi vijana wa Kenya inatupasa tuwajibike kufanya kazi kwa bidii, na kwa dhati ya mioyo yetu tuweze kupata ufanisi, na uwezekano wa kuinua nchi yetu changa katika kiwango cha juu. Tukumbuke, “Ajizi ni nyumba ya njaa” Kwa hivyo basi haifai kulaza damu ikiwa matatizo nchini mwetu yametuzonga. Lazima tufanye kazi kwa busara, adabu njema na jitihada kwa moyo mmoja. Sharti tutilie maanani zaidi elimu ya vijana na watu wazima,kilimo,uchumi na amani katika nchi yetu vigumu sana kuweza kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo. Tupende tusipende lazima tizidishe mazao kilimo, uchumi na amani katika nchi yetu. Tunahitaji taifa lenye watu walioelimika, kwani bila elimu itakuwa vigumu sana kuweza kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo. Tupende tusipende lazima tuzidishe mazao mashambani kwani kila kukicha idadi ya watu inaongezeka, Ni sharti tuweze kujitosheleza katika vyakula. Zaidi ya haya pia lazima tujishughulishe na biashara ambapo kwa sasa ni Wakenya wachache sana ambao wanatambua umuhimu wa biashara. Wengi ni wale wenye mawazo ya kwamba, lazima kila mmoja aajiriwe maishani. Yatupasa tujitahidi kuleta uchumi katika mikono ya wananchi wa Kenya badala ya kuwaachia wengine ambao hawahusiki.

    Mafunzo tunayopata majumbani, shuleni na hata katika jamii, lazima yatuwezeshe kutambua mbinu za kupitia. Tunahitaji elimu tambuzi ambayo itamfanya Mwanakena kujua wajibu wake katika jamii. Tumesinywa na elimu pumbao; inayotupumbaza na kutufanya tusione mbele. Sisi vijana tukiwa viongozi wa ‘utengano ni uvundo’, lugha ya taifa ndicho chombo cha pekee ambacho kinatuunganisha na kuweza kutuwasilishia mapendekeza, mawaidha ni hisia zetu. Kukosa ndiko binadamu, wakati tunapokosea, lazima tukubali tumekosea na kufanya masahihisho mara moja. “Kwani usipoziba ufa, utajenga ukuta”. Tusikasirike kwa sababu tumesahihishwa makosa yetu tukiwa wazalendo halisi.

    Sisi tukiwa vijana sharti tujishughukishe na kuyaangalia matatizo ya nchi, pia kutafuta njia za kutatua matatizo hayo. Siku zote tutekeleze nidhamu.Ni jambo la kusikitisha kwamba sisi vijana twashutumiwa mara kwa mara kwa kutokuwa na nidhamu shuileni na majumbani mwetu.Utamaduni wa assili unanakariri sana kuwa tuwe na nidhamu shuleni na majumbani mwetu.Ili watu waweze kuishi maisha bora na kuwa na maendeleo,amani na upendo lazima tuwe na bidii,ushirikiano mwema na kuchagua viongozi wenye mioyo ya maendeleo.Tukiwa viongozi ambao hawajishughulishi na maendeleo,basi tutabaki nyuma kama mkia kila siku zote.Bahati mbaya ni kwamba wananchi wengi siku hizi huchagua viongozi wao kwa kufuata ukoo ama kama kwa utajiri wake.Kwa hivyo basi tuchagueni viongozi ambao watatuletea ufanisi badala ya viongozi wanaotokana na sababu kubwa au ya utajiri.


    a) Ni nini dhamira ya mwandishi?
    b) Katika aya ya kwanza, mwandishi anawahimiza vijana kufanya nini ili kuleta maendeleo nchini?
    c) Ni mambo gani yaliyochangia, kuzorota kwa maendeleo nchini Kenya kwa mujibu wa taarifa?

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Siku ya kuzungumza gharama za serikali katika bunge hungojewa kwa pashau kubwa.(Solved)

    Siku ya kuzungumza gharama za serikali katika bunge hungojewa kwa pashau kubwa. Maana kwa hakika siku hiyo ndiyo inayomuathiri kila mtu kwani ndipo serikali inapomchakuria mifuko na vibindo vyake. Wiki nzima kabla ya hapo huwa Waziri wa Hazina na Maendeleo ya Uchumi amekwisha onyesha kiasi kadha wa kadha kitahitajiwa katika mwaka kuikuza elimu ya wananchi – kwa idadi ya skuli zilioko mpaka sasa, vifaa na ala zihitajiwazo, waalimu watakiwao, shule gani mpya za aina gani zataka kujengwa na zitagharimu Serikali kiasi gani, na kadhalika. Wizara ya Afya itahitajia milioni kadha wa kadha kuongeza mavuno ya konde na mazao ya nyanyangu. Basi hivyo Waziri anaendelea kudondoa makisio ya kila wizara kinaganaga na viwango vya fedha zinazodhamiriwa kutumiwa kutosheleza kila kinacholazimu.

    Basi juma hilo lote huwa wafanyibiashara wanavuna kwa wanunuzi; namna biashara inayokwenda ni ajabu maana wanunuzi huwa wananunua kila kitu ambacho wanachelea kitabandikwa ushuru. Wafanyi biashara ndio wanaowatia hofu kuwa bidhaa zitapanda bei.Wachuuzi wa magari huwa wanatangaza kuwa wamepata fununu ‘mwaka huu ushuru wa magari utapandishwa mpaka thalathini katika mia. Basi patilizeni kabla siku hiyo maana baada ya hapo bei itakuwa haishikiki.’

    Wauzaji mapombe nao huwa na vishindo vyao: “Kodi ya forodha ya kila aina ya mvinyo itokayo ugenini itaongezwa ishirini kila mia, na pombe za kienyeji zitapandishwa peni kila chupa.’ Sigara nazo pia zaambiwa zitapanda: Fulani amedokezwa kuwa kila pakiti itazidishwa bei kwa mapeni mawili.

    Mradi, mlolongo wa bidhaa hupandishwa ushuru mkubwa kabla ya siku yenyewe haijafika.Basi angalia kufundika huko! Kande za vyakula na vifaa aina aina hununuliwa vikawekwa kwa kuchelea kuwa vitaongezwa bei au pengine vitakuwa adimu. Wafanyi biashara nao huwa wamekwisha ‘piga pua’ kuwa vitu fulani vitaekewa ushuru. Basi huvinunua kwa wingi wakavitutiza maghalani mwao kwa bei ya tahafifu kabla ya kuongezwa ushuru na baada ya kupandishwa kodi, huviuza kwa bei mpya.

    Ikifikia hiyo siku kila mtu mwenye hamu ya mambo ya kilimwengu huwa amechachawa kukimbilia penye redio kusikiliza hotuba ya waziri wa Fedha.Ikishamalizika huwa kila mtu akishusha pumzi,maana huwa mbichi na mbivu ishajulikana na kwa upande wake anaona hakuelemewa sana.


    a) Toa anwani mwafaka kwa taarifa uliyoisoma
    b) Taja wizara ambazo zimetajwa kwenye taarifa
    c) Ni mambo gani huzingatiwa katika makisio ya masomo
    d) Unadhani ni sababu zipi zichangiazo mavuno ya wafanya biashara kabla ya kusomwa makadirio ya fedha
    e) Wafanyi biashara hutumia mbinu gani ili kujipa faida zaidi
    f) Kuvumbika bidhaa maghalani si ufanyaji biashara halali. Toa maoni yako
    g) Eleza maana ya vifungu hivi kama vilivyotumiwa katika muktadha wa habari hii
    i. Fununu
    ii. Siha
    iii. Mbichi na mbivu

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Uhifadhi wa mazingira una manufaa mengi kwa binadamu .Thibitisha(Solved)

    Uhifadhi wa mazingira una manufaa mengi kwa binadamu .Thibitisha

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Nchi nyingi duniani zimetia saini mkataba wa umoja wa mataifa kuhusu haki za watoto.(Solved)

    Soma taarifa ifatayo kwa makini kisha ujibu maswali yanayofuata.
    Nchi nyingi duniani zimetia saini mkataba wa umoja wa mataifa kuhusu haki za watoto.
    Haki ni mambo mema ambayo watoto wanastahili kutendewa. Kwa kutia saini, nchi hizizimetangaza kujitolea kwao kuzilinda na kuhahakikisha kuwa hakuna ukiukaji wake nakuwa watoto wote katika himaya zao wananufaika kutokana na haki hizi.
    Miongoni mwa haki hizi ni kuwa kila mtoto ana haki ya kuishi na kupata chakula cha kutosha na chenye viinilishe bora. Pili, kila mtoto ana haki ya kupata elimu. Elimu hii inafaa kutolewa bila ada na iwe inayofaa na inayopatikana kwa urahisi.Kisha kila mtoto ana haki ya kutopigwa na kutodunishwa kwa namna yoyote, iwe kitabaka, kirangi, kijinsia na vinginevyo. Mtoto ana haki pia kutolazimishwa kufanya kazi za kiutumwa, nzito na zakushurutishwa. Hali kadhalika, ana haki ya kuishi katika nyumba au makazi bora nasalama, kutunzwa na kulindwa dhidiya hali yoyote inayoweza kumhatarisha. Anatakiwa ashirikishwe katika kufanya maamuzi.Fauka ya haya, ana haki ya kupata huduma za afya,mahitaji maalum,michezo, upendo na habari. Isitoshe,anastahili kuheshimiwa kimawazo na kihisia. Haki hizi zinatakiwa kulindwa na kila mwanajamii, hivyo serikali za mataifa mengi zimeshirikisha haki hizi katika katiba za nchi zao na sheria zao.
    Walakini haki hizi bado zinakiukwa.Watoto wengi kote duniani bado wananyimwa haki zao. La kusikitisha na kukera ni kuwa wanaotarajiwa kuwa vigogo vya kuzilinda haki hizi, ndio wanaoongoza kuzikiuka. Kila siku tunasikia na kushuhudia visa vya watoto kupigwa, kunyimwa chakula, kufanyishwa kazi kipunda, kuteswa, kuishi katika mazingira hatari, na hata kuuawa. Kuna watoto wengi wanaolala nje, wengine hawapati chakula licha ya kuwa wanatakiwa kupata chenye lishe bora. Kwao kutarajiwa mlo awamu tatu kwa siku ni njozi kwani hata awamu moja ni adimu kupata.
    Watoto wengi katika mataifa yenye fujo na ghasia hutekwa na kutumikishwa vitani. Viongozi katika mataifa haya hawafanyi kitu ila kutazama tu wakati watoto wanaotakiwa kuwalinda wanageuzwa kuwa mibaba ya kuua na kuuana. Watoto hawa huvishwa magwanda ambayo miili yao minyonge haiwezi kuyahimili. Pia, huvalishwa mabuti ya kijeshi ambayo ni mizigo mizito ya kubeba mbali na bunduki zinazokaribia kuwazidi uzani wakati wanatakiwa kuwa wamelindwa majumbani, na shuleni na wazazi wao na serikali.
    Jukwaa la vijiji vya mataifa ya ulimwengu wa tatu limesheheni watoto wasioenda shule kwa sababu ya lindi la ufukara uliokithiri. Elimu ya bure inayogusiwa katika haki za watoto haipo. Wanaong‘ang‘ana iwepo ni kana kwamba ni waota ndotomchana. Jiulize watoto wangapi sasa hivi wamo majumbani bila kwenda shuleni kutokana na ukosefu wa karo? Wangapi wamo mitaani wakivuta na kunusa gundi huku wakiombaomba vishilingi?
    Hali ilivyo sasa hivi inadai kuwa mimi na wewe tufanye hima na kuungana mikono kutafuta suluhisho la kudumu kuhusu haki za watoto. Twapasa kuhimiza serikali zetu kufanya kila ziwezavyo kuhakikisha kuwa watoto wote wamo shuleni. Nasi tushirikiane kutoa huduma kwa watoto na kukomesha dhuluma, mateso na dhiki kwao. Haitoshi kupeleka miswada mbungeni kuhusu haki za watoto na kuipitisha kuwa sheria. Twastahili kubadilisha misimamo yetu kuhusu haki hizi na kuzilinda kwa dhati bali si kwa chati.
    Maswali
    a) Fupisha aya mbili za kwanza. ( maneno 65-70)
    b) Eleza ni vipi ukiukaji wa haki za watoto unaweza kuepukwa . ( maneno 30-35)

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Alipokuwa akiukemea utamaduni na dhana za kikabila katika nyimbo zake, marehemu Bob Marley aliufananisha ubepari na "wanyama wala watu."(Solved)

    Soma taarifa hii kisha ujibu maswali yanayofuata.

    Alipokuwa akiukemea utamaduni na dhana za kikabila katika nyimbo zake, marehemu Bob Marley aliufananisha ubepari na "wanyama wala watu." Katika wimbo "Babylon System" (yaani mfumo wa kibepari), Marley alisema kuwa utamaduni huo ndio mzawa wa matatizo yote ya kiutawala ambayo yalikuwa yakiyakumba mataifa ya Weusi katika karne ya 20, wakati nchi zao zilikuwa zikitawaliwa na nchi za mataifa ya Ulaya.
    Kwa mantiki hiyo, pengine Marley alikuwa na maono kuwa Afrika haingejikomboa kutoka kwa utumwa wa Kizungu, ikiwa ingeendelea kuziabudu na kuzishadidia tamaduni za Kimagharibi.
    Utabiri huo nauoanisha na yanayoendelea nchini, ambapo serikali ya Jubilee imeonekana kushindwa kabisa kuikabili saratani ya ufisadi, ambayo inahatarisha kuliangamiza taifa hili lenye uchumi dhalili.
    Donda hili linazidi kuyatandaza mabawa yake kutoka, tisho kuu likiwa ni uvamizi wa taasisi ―takatifu‖ ambazo tunazitegemea kulikabili donda hilo.
    Ni nani tutategemea kukabiliana na rushwa ikiwa taasisi kama Bunge, Tume ya Maadili na Kukabiliana na Ufisadi (EACC) kati ya zingine muhimu zimepakwa tope na saratani hiyo?
    Kimsingi yote tunayopitia ni matunda ya uasi wa tamaduni za Kiafrika na uegemezi wa mifumo ya Kizungu kama mihimili ya jamii na nchi zetu.
    Ndoto za watetezi wa Uafrika na nafasi ya Weusi kama marehemu Malcom X na Martin Luther King, zilikuwa ni kuona kuwa wameungana kabisa kukabiliana na matatizo yaliyowakabili bila kuzingatia mazingara waliyokuwemo.
    Pindi tu baada ya mataifa mengi ya Kiafrika kujinyakulia uhuru wao katika miaka ya hamsini na sitini, viongozi wakuu walioziongoza nchi hizo kama Kwame Nkrumah, Jomo Kenyatta, Mwalimu Julius Kibarage Nyerere kati ya wengine walianza harakati za kuliunganisha bara hili na kubuni Muungano wa Nchi za Kiafrika (OAU) japo ndoto hiyo haikufikia.
    Kwa msingi huo, mhimili mkuu wa kiutawala ungekuwa ni mfumo wa kisosholisti, ambao ungekuwa nguzo kuu ya kuyaunganisha mataifa hayo.
    Hata hivyo, migawanyiko mikubwa ilianza kushuhudiwa, huku baadhi ya mataifa yakianza kukabiliwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa kutaasisika kwa maovu yote tunayoshuhudia sasa: ufisadi na tamaa ya kuogofya kutoka kwa viongozi wetu.

    Maswali
    a. Ipe taarifa hii anwani mwafaka.
    b. Onyesha mambo mawili makuu ambayo msanii aliyapinga .
    c. Kwa nini ubepari umelinganishwa na "wanyama wala watu"?
    d. Kwa mujibu wa taarifa eleza sifa za Bob Marley.
    e. Swala linalozungumziwa limerejelewa kama "Donda".
    i) Eleza mbinu ya lugha iliyotumika..
    ii) Ni kweli kuwa donda hili laelekea kuwa gumu? Thibitisha.
    f. Tatizo hili la "donda" ni kama kujipalia makaa. Fafanua.
    g. Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa mujibu wa taarifa.
    i) Mhimili
    ii). Taasisi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • …ya leo ni kuwapa pole wanaofuata na kuenzi makala ya Burudani,toleo la kila Ijumaa.Mwanamziki huyu aliteka nyoyo za wapenzi wa mtindo huu wa mziki.Kwa kweli...(Solved)

    …ya leo ni kuwapa pole wanaofuata na kuenzi makala ya Burudani,toleo la kila Ijumaa.Mwanamziki huyu aliteka nyoyo za wapenzi wa mtindo huu wa mziki.Kwa kweli ya Muumba hufumbwa tu!Mnapoyasoma wakumbukeni jamaa na wapenzi wa nyimbo zake.
    (i) Tambua sajili hii na utoe Ushahidi.
    (ii) Fafanua sifa zozote za sajili hii.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Tambua na ueleze virai katika sentensi hii. Kisichana kile kimejirembesha kwa manukato mazuri ajabu(Solved)

    Tambua na ueleze virai katika sentensi hii.
    Kisichana kile kimejirembesha kwa manukato mazuri ajabu

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)