Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

"Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."

      

Mstahiki Meya.
"Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Eleza sifa zozote nne za msemaji.
c) Fafanua maudhui ya ufisadi kama yalivyoangaziwa na mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya.

  

Answers


sharon
(a) Msemaji ni Bili
- Anayeambiwa ni Meya
- Wako katika ofisi ya Meya
- Wanazungumza kuhusu mwanakandarasi wa awali ambaye kulingana na Meya hafai kuendelea na kazi. (zozote
(b) Sifa za mzungumzaji
Bili
Fisadi – anapendekeza njia nyingi za kifisadi kama vile kumplia mwanakandarasi.
Mbinafsi – anajidai tu maslahi yake mwenyewe na Meya – wanaiba fimbo ya Meya kwa manufaa yao wenyewe.
Mshaurimbaya – anapendkeza mambo maovu kama vile kuiba fimbo ya Meya na kutojali maslahi ya wafanyikazi wengine.
(c) Maudhui ya ufisadi kama yanavyoangaziwa na mwandishi.
- Meya anatumia fedha za umma kupeleka mkewe kuzalia ng‘ambo pamoja na kumstarehesha Bili na familia yake.
- Meya anagawa ardhi ya umma kwa njia isiyo halali. Anajigawia viwanja vinane na kungawia Bili vinne.
- Meya anatumia hazina ya Baraza kumlipa mhubiri.
- Meya anatumia gharama kubwa katika mapokezi ya mameya.
- Zahanatini ungonjwa wanaibiwa (kulipia huduma).
- Utoaji ajira kwa misingi ya undugu (uhaziti)
- Bili kulipwa marupurupu kwa ushauri wake ni ufisadi.
sharon kalunda answered the question on October 2, 2019 at 11:29


Next: Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,
Previous: State six instances, when the unity of believers becomes threatened in Kenya today.

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

    1) Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,
    Mpateni mweleweni, mchekeni, mlieni,
    Funzo lake mpateni, uamuzi mfanyeni,
    Kisa hiki asilani, sisahau maishani.

    2) Cha nne niliingiya, mtoto kafurahiya,
    Malkia ungedhaniya, duniani meingiya,
    Mapambo lijipambiya, kung‘ara kikang‘ariya,
    Kisa change chatokeya, mwanzowe nafunguliya.

    3) Darasani lizembea, bidii sikutilia,
    Starehe nakwambia, nilipenda najutia,
    Kimadaha litembea, tausi nilitulia,
    Kisa kilinigonjea, mtume! Ningalijua.

    4) Muhula kutamatika, dafu sikufua, kaka,
    Enda, Ewe, Embe, fika, alama duni, viraka,
    Nilipokea waraka, mzazi kahitajika,
    Kisa kijatambulika, nakuomba makinika.

    5) Muhula wa pili sasa, nikarudia makosa,
    Sikupigeni msasa, makali nikayakosa,
    Kisu sikunoa hasa, sikukata cha darasa,
    Kisa ndicho hicho sasa, ninakupa pasi pesa.

    6) Sasa muhula wa tatu, umetimia wanetu,
    Mtihani kama chatu, nimeuogopa, mtu,
    Sijausomea katu, ningalilindaje utu?
    Kisa mkasa wa chatu, kilinipata wa kwetu.

    7) Mbwa katu hafi maji, kiona ufuko, maji,
    Tajaribu sife maji, hata akiyanywa maji,
    Ilibidi twende jiji, kuwasaka wajuaji,
    Kisa change mfumbaji, sasa dawa lihitaji.

    8) Mpango ulitolewa, mchango ulipangiwa,
    Pesa tele litolewa, na simu kununuliwa,
    Mtandao liwekewa, ‗kunani‘ kupakuliwa,
    Kisa cha simu kujuwa, linifanya kupagawa.

    9) Tulikata dari ona, simu yetu kufichana,
    Usiku tulikutana, maswali kurushiana,
    Majibu tulipeana, "panga‘ kabadilishana,
    Kisa kinajulikana, vile nilivyokazana.

    10) Niliyangoja majibu, nikiwa na hamu, babu,
    Nilikimya kama bubu, nisije toa aibu,
    Nilivichoma vitabu, bila kuwa na sababu.
    Kisa kawa masaibu, kashindwa kuyaharibu.

    11) Kutangazwa matokeo, nakumbuka hadi leo,
    Lilishangaza toleo, sikuamini redio,
    Lipokea matokea, yalinitia kimbio,
    Kisa change mchocheo, haya yangu mapokeo.

    12) Nilifeli mtihani, sababu simu juweni,
    Najuta nisameheni, nijilaumu moyoni,
    Ningalijua mbeleni, ningalisoma jamani,
    Kisa nimemalizeli, wenzangu mzindukeni.

    13) Watahiniwa mlipo, msiwe mithili popo,
    Skuli kwenu kuwepo, nia mpate malipo,
    Bidii hapo mlipo, toa uzembe pasipo,
    Kisa change kingalipo, simu daima siwepo!

    MASWALI
    a) Taja anwani mwafaka ya shairi hili.
    b) Fafanua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi hili.
    c) Bainisha nafsi lengwa katika shairi hili.
    d) Changanua arudhi zilizotumiwa na mtunzi wa shairi hili.
    e) Andika ubeti wa kumi katika lugha nathari.
    f) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    g) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    (i) Sikukata cha darasa
    (ii) Yalinitia kimbio
    (iii) Kupagawa

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"(Solved)

    Damu nyeusi na hadithi zingine
    "Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili.
    c) Huku ukitoa mifano, thibitisha maudhui sita ambayo yamejitokeza katika hadithi ya Damu Nyeusi na wanayoyaendeleza.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kutoa mifano kumi,eleza vizingiti walivyokumbana navyo wanacheneo wakati wa kupigania mageuzi.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Kwa kutoa mifano kumi,eleza vizingiti walivyokumbana navyo wanacheneo wakati wa kupigania mageuzi.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Iwapo umefanya, yapo mengi ambayo hayakunyoka."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Iwapo umefanya, yapo mengi ambayo hayakunyoka."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Tambua mbinu moja iliyotumika katika muktadha wa dondoo.
    c) Fafanua kauli kwamba"yapo mengi ambayo hayakunyoka".
    d) Eleza jinsi baadhi ya wahusika walivyojaribu kuyanyoosha.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Ni nini sifa za mvuto zinazowaleta pamoja mzungumzaji na mzungumziwa.
    c) Tambua na ufafanue mbinu inayotumika katika dondoo.
    d) Kwa mifano mwafaka fafanua tanzia hiyo inayorejelewa katika dondoo.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".(Solved)

    DAMU NYEUSI
    "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili
    (b) Fafanua sifa zozote nne za mrejelewa
    (c) Eleza fani uliotumiwa na mwandishi katika dondoo hili
    (d) Kwa kurejea hadithi zozote tatu,eleza namna wahusika wowote watatu walivyoathiriwa na kiu.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?(Solved)

    Mstahiki Meya
    Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja na ueleze mbinu za lugha zinazojitokeza katika dondoo hili.
    (c) Jadili umuhimu wa msemaji katika tamthilia hii.
    (d) Jadili njia za kuondoa uozo katika jamii ukijikita katika tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.(Solved)

    Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
    (a) Jazanda
    (b) Uzungumzi nafsia
    (c) Majazi
    (d) Methali
    (e) Taharuki

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.(Solved)

    Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine (Solved)

    Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine
    (i) Mke wangu
    (ii) Damu Nyeusi
    (iii) Tazamana na Mauti
    (iv) Mizizi na matawi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Ulimwengu wake ulivurugika akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"(Solved)

    Kanda la usufi
    "Ulimwengu wake ulivurugika akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"
    (a) Eleza sifa zozote nne za mrejelewa
    (b) Kwa nini mrejelewa amelinganisha na tiara iliyopeperushwa na upepo

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Alipofikishwa kwenye zahanati hakushughulikiwa ipasavyo.Ubwete ni ugonjwa mmoja mbaya walioambukizwa madaktari na wauguzi wengi Tomoko"(Solved)

    "Alipofikishwa kwenye zahanati hakushughulikiwa ipasavyo.Ubwete ni ugonjwa mmoja mbaya walioambukizwa madaktari na wauguzi wengi Tomoko"
    a) Eleza Muktadha wa dondoo hili.
    b) Dhihirisha jinsi mtunzi alivyoitumia tamathali yoyote moja inayobainika kifunguni .
    c) Riwaya Ya Kidagaa Kimemwozea ni muhtasari wa maradhi yanayolihujumu Bara Afrika.Tetea rai hii kwa mifano faafu riwayani.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    "Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
    Jadili.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,(Solved)

    Soma mashairi yafuatayo kisha ujibu maswali.

    SIKUJUA!
    1. Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,
    Zisingenidhuru pembe, ngeu kuniandama,
    Samli ni lembelembe, na minofu ya minyama.

    2. Kama ningefuga mbuzi, na kondoo kundi zima,
    Ningewajengea zizi, na maziwa nikakama,
    Ningewachuna na ngozi, kutengenezea ngoma.

    3. Kama ningefuga bata, nao kuku kwa ujima,
    Chakula siyo matata, ni machicha na mtama,
    Mayai ningeyapata, na kitoweo kizima.

    4. Kumbe nimefuga punda, mashuzi ndio heshima,
    Ni ukaidi na inda, mateke kurusha nyuma,
    Nyama limekuwa nunda, mfugaji humuuma.

    Kiitikio
    Sikujua wa kufuga, mnyama mwenye faida

    SHAIRI B
    Afrika na Watu Wake

    Mimi ninaona mgonjwa
    Bado amelala kitandani.
    Kama hatutamtoa miiba iliyobaki
    Mgonjwa hataweka miguu yake chini
    Ili kutembea bila ya kujiegemeza.

    Miiba iliyomo ndani mwetu lazima
    Pia iondolewe upesi kabla haijaingia
    Kati ya mfupa na kufa pamoja nasi.
    Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma
    Halafu tucheze nao mchezo wa siasa na uchumi.

    Lakini kuitoa miiba hii
    Tunahitaji macho makali
    Mikono isiyotetemeka
    Moyo usio na huruma
    Na kuona miiba ilipoingilia.

    MASWALI
    (a) Onyesha jinsi ujumbe unaopatikana katika ubeti wa nne wa Shairi A na Shairi la B unavyokatisha tamaa.
    (b) Eleza maana ya mshororo huu kama unavyojitokeza kwenye ubeti wa pili wa shairi B.
    Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma.
    (c) Linganua sifa za kimuundo ukizingatia ubeti wa pili wa Shairi A na Shairi B.
    (d) Ukizingatia Mshororo wa kwanza kwenye ubeti wa pili wa Shairi A, onyesha jinsi Mshairi alivyotumia kibali chake.
    (e) Onyesha sifa moja ambayo inadhihirika kwenye shairi la B na ambayo hutawala tungo za aina hii.
    (f) Nafsi neni amedhihirisha toni gani kwenye shairi A?
    (g) Taja nafsi mbili nenwa kwenye shairi la B.
    (h) Andika ubeti wa mwisho wa shairi B kwa lugha ya nadhari.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Ewe tunu ya mtima, kwa nini wanikimbia?(Solved)

    SABUNI YA ROHO
    Ewe tunu ya mtima, kwa nini wanikimbia?
    Ndiwe suluhu za zama, waja wakukimbilia,
    Waja wanakutazama, madeni wakalipia,
    Ndiwa sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mafuta ya roho, walisema wa zamani,
    Utanunua majoho, majumba na nyumbani,
    Umezitakasa roho, umekuwa mhisani,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvinja mlima.
    Matajiri wanakujua, wema wako wameonja,
    Nguo zao umefua, wakupata kwa ujanja,
    Sura zao ‗mefufua, wanazuru kila njanja,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mvunja mlima, onana na maskini,
    Watazame mayatima, kwao kumekua duni,
    Webebe waliokuwa, wainue walio chini,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mvunja mlima, wapi kapata uwezo,
    Umezua uhasama, waja kupata mizozo,
    Ndiwe chanzo cha zahama, umewatia vikwazo,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Umevunja usuhuba, familia zazozana,
    Waliokuwa mahabuba, kila mara wagombana,
    Roho zao umekaba, majumbani wachinjana,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Nakutafuta kwa hamu, sabuni unirehemu,
    Sinilipue ja bomu, sije kawa marehemu,
    Niondoe jahanamu, ya ufukara wa simu,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Naondoka wangu moyo, nikuitapo itika,
    Fulusi wacha uchoyo, tatua yalonifika,
    Nichekeshe kibogoyo, nami nipate kuwika,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Nitafukuzwa mbinguni Kwa ushairi wangu mbaya Lakini hata motoni nitaimba:(Solved)

    Nitafukuzwa mbinguni
    Kwa ushairi wangu mbaya
    Lakini hata motoni nitaimba:
    Wanasema
    Wanasiasa ni kama jizi
    Lililosukuma mtoto pembeni
    Na kunyonya ziwa la mama
    Wakati amelala usingizi usiku.
    Wanasema
    Mwanasiasa afapo
    Tumejikomboa na domo
    Moja pana lizibwalo na mchanga
    Na kilima cha simenti ngumu
    Lisikike tena hadharani.
    Wanasema pia
    Kusema haki
    Kwa kawaida
    Wanasiasa hatuwapendi.
    Kupiga kura ni hasira za mkizi
    Ni basi tu. Ni Ah!
    Ah!
    Wanamalizia
    Nchi mmefiilisi waacheni walimu
    Wakajenga taifa jipya.
    Top grade predictor publishers Page | 63
    Kama hamwezi kuona mbali
    Bure kuweka mkono usoni,
    Bure hakuna kichwa
    Kama hamwezi kufikiri.
    Ng‘ombe amekamuliwa na wazungu
    Waarabu, wahindi na wao
    Sasa anatoa damu
    Vilivyobaki ni chai ya rangi
    Na madomo mapana zaidi
    Yaliyo bado hai.
    Kuimba nimeimba

    Maswali
    (a) Mshairi ana dhamira gani?
    (b) Shairi hili ni la kukatisha tama, tetea rai hii.
    (c) Onyesha matumizi mawili ya mishata.
    (d) Eleza mbinu zozote nne za lugha zilizotumika katika shairi hili.
    (e) Andika ubeti wa mwisho katika lugha tutumbi.
    (f) Fafanua umbo la shairi hili.
    (g) Eleza maana ya mafungu ya maneno ya maneno yafuatayo:
    (i) kupiga kura ni hasira ya mkizi
    (ii) kuweka mkono usoni
    (iii) ng‘ombe amekamuliwa.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.(Solved)

    MSTAHIKI MEYA: Timothy Arege
    Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.
    Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Fafanua nafasi ya wanaorejelewa kuwa ―"walifanya vizuri kuja" katika tamthilia hii.
    (c) Migogoro katika tamthilia hii hazikusuluhishwa vyema. Jadili.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.(Solved)

    Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • "Nyamaza boza wewe. Wadhani sisi kazi tunaanza leo? Tumekutana na wauaji wangapi?(Solved)

    Kidagaa Kimemwozea:
    "Nyamaza boza wewe. Wadhani sisi kazi tunaanza leo? Tumekutana na wauaji wangapi?
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Dondoo hili linadokeza maudhui gani? Kwa kutoa mifano saba kwenye riwaya, bainisha jinsi maudhui hayo yanavyojitokeza.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)