Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."

      

Kidagaa kimemwozea
"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Ni nini sifa za mvuto zinazowaleta pamoja mzungumzaji na mzungumziwa.
c) Tambua na ufafanue mbinu inayotumika katika dondoo.
d) Kwa mifano mwafaka fafanua tanzia hiyo inayorejelewa katika dondoo.

  

Answers


sharon
a) i) Maneno ya Madhubuti kwa Amani
ii) Walikuwa katika kibanda cha Amani
iii) Wakati ambapo Madhubuti alipoamua kumtembelea Amani bila taarifa.
iv) ili kumuuliza iwapo alikuwa anavielewa vitabu alivyoviazima kutoka kwake na kumpata akitongoa kimombo kwa sauti.
b) i) Wote walikuwa vijana wa kiume.
ii) Walikuwa wasomi waliopendelea kusoma vitabu vya aina moja – vya mawazo ya uzalendo naukombozi.
iii) Walikuwa na falsafa sawa – kuwa shahada kutoka vyuo vya maisha vinavyofundisha watu kuwa binadamu na maadili ni
muhimu zaidi ya shahada ya vyuo vikuu.
iv) Waliamini katika kujitafutia kwa jasho lao bila kuegemea unasaba.
v) Walikuwa wasiri wakubwa walioelewana na kuelezana siri.
c) Jazanda: tanzia inayorejelea ukoloni mamboleo. Baada ya waafrika kupigania uhuru na kuwa na matumaini makubwa yanaishia kwenye mwisho mbaya wa viongozi ingawa ni weusi lakini wabaya zaidi. (zozote
d) i) Unyakuzi: Baada ya viongozi wa kiafrika kuwatimua wazungu, wao walianza kujinyukulia mali, kwa mfano, ardhi adal-basari za Mtemi Nasaba Bora.
ii) Udhalimu ulitekelezwa na askari kwa amri kwa mama yake Imani hadi akafa.
iii) Kutozwa kodi/ushuru kwa lazima. Mtemi Nasaba Bora alitumia mchango wa umma kumpeleka mwanawe Urusi.
iv) Kushurutishwa kuhudhuria mikutano , hata wale ambao hawakuelewa kimombo. Askariwalitembea wakiwatoa watu nyumbani mwao.
v) Matumizi mabaya ya asasi za serikali, ofisi, magereza na askari.
vi) Sheria dhalimu. Amani, Imani na Weye kutiwa ndani bila hatia na kuachiliwa bila kufikishwa mahakamani.
vii) Viongozi walitumia vibaya misaada iliyotumwa ili kujengea hospitali kuu zilifujwa na wasimamizi na badala yake wakajenga zahanati ndogo.
sharon kalunda answered the question on October 2, 2019 at 10:31


Next: Describe the way of life of human beings during the late stone age period.
Previous: Toa mifano miwili ya aina za nomino zifuatazo

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".(Solved)

    DAMU NYEUSI
    "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili
    (b) Fafanua sifa zozote nne za mrejelewa
    (c) Eleza fani uliotumiwa na mwandishi katika dondoo hili
    (d) Kwa kurejea hadithi zozote tatu,eleza namna wahusika wowote watatu walivyoathiriwa na kiu.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?(Solved)

    Mstahiki Meya
    Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja na ueleze mbinu za lugha zinazojitokeza katika dondoo hili.
    (c) Jadili umuhimu wa msemaji katika tamthilia hii.
    (d) Jadili njia za kuondoa uozo katika jamii ukijikita katika tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.(Solved)

    Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
    (a) Jazanda
    (b) Uzungumzi nafsia
    (c) Majazi
    (d) Methali
    (e) Taharuki

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.(Solved)

    Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine (Solved)

    Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine
    (i) Mke wangu
    (ii) Damu Nyeusi
    (iii) Tazamana na Mauti
    (iv) Mizizi na matawi

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Ulimwengu wake ulivurugika akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"(Solved)

    Kanda la usufi
    "Ulimwengu wake ulivurugika akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"
    (a) Eleza sifa zozote nne za mrejelewa
    (b) Kwa nini mrejelewa amelinganisha na tiara iliyopeperushwa na upepo

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Alipofikishwa kwenye zahanati hakushughulikiwa ipasavyo.Ubwete ni ugonjwa mmoja mbaya walioambukizwa madaktari na wauguzi wengi Tomoko"(Solved)

    "Alipofikishwa kwenye zahanati hakushughulikiwa ipasavyo.Ubwete ni ugonjwa mmoja mbaya walioambukizwa madaktari na wauguzi wengi Tomoko"
    a) Eleza Muktadha wa dondoo hili.
    b) Dhihirisha jinsi mtunzi alivyoitumia tamathali yoyote moja inayobainika kifunguni .
    c) Riwaya Ya Kidagaa Kimemwozea ni muhtasari wa maradhi yanayolihujumu Bara Afrika.Tetea rai hii kwa mifano faafu riwayani.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    "Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
    Jadili.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,(Solved)

    Soma mashairi yafuatayo kisha ujibu maswali.

    SIKUJUA!
    1. Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,
    Zisingenidhuru pembe, ngeu kuniandama,
    Samli ni lembelembe, na minofu ya minyama.

    2. Kama ningefuga mbuzi, na kondoo kundi zima,
    Ningewajengea zizi, na maziwa nikakama,
    Ningewachuna na ngozi, kutengenezea ngoma.

    3. Kama ningefuga bata, nao kuku kwa ujima,
    Chakula siyo matata, ni machicha na mtama,
    Mayai ningeyapata, na kitoweo kizima.

    4. Kumbe nimefuga punda, mashuzi ndio heshima,
    Ni ukaidi na inda, mateke kurusha nyuma,
    Nyama limekuwa nunda, mfugaji humuuma.

    Kiitikio
    Sikujua wa kufuga, mnyama mwenye faida

    SHAIRI B
    Afrika na Watu Wake

    Mimi ninaona mgonjwa
    Bado amelala kitandani.
    Kama hatutamtoa miiba iliyobaki
    Mgonjwa hataweka miguu yake chini
    Ili kutembea bila ya kujiegemeza.

    Miiba iliyomo ndani mwetu lazima
    Pia iondolewe upesi kabla haijaingia
    Kati ya mfupa na kufa pamoja nasi.
    Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma
    Halafu tucheze nao mchezo wa siasa na uchumi.

    Lakini kuitoa miiba hii
    Tunahitaji macho makali
    Mikono isiyotetemeka
    Moyo usio na huruma
    Na kuona miiba ilipoingilia.

    MASWALI
    (a) Onyesha jinsi ujumbe unaopatikana katika ubeti wa nne wa Shairi A na Shairi la B unavyokatisha tamaa.
    (b) Eleza maana ya mshororo huu kama unavyojitokeza kwenye ubeti wa pili wa shairi B.
    Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma.
    (c) Linganua sifa za kimuundo ukizingatia ubeti wa pili wa Shairi A na Shairi B.
    (d) Ukizingatia Mshororo wa kwanza kwenye ubeti wa pili wa Shairi A, onyesha jinsi Mshairi alivyotumia kibali chake.
    (e) Onyesha sifa moja ambayo inadhihirika kwenye shairi la B na ambayo hutawala tungo za aina hii.
    (f) Nafsi neni amedhihirisha toni gani kwenye shairi A?
    (g) Taja nafsi mbili nenwa kwenye shairi la B.
    (h) Andika ubeti wa mwisho wa shairi B kwa lugha ya nadhari.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Ewe tunu ya mtima, kwa nini wanikimbia?(Solved)

    SABUNI YA ROHO
    Ewe tunu ya mtima, kwa nini wanikimbia?
    Ndiwe suluhu za zama, waja wakukimbilia,
    Waja wanakutazama, madeni wakalipia,
    Ndiwa sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mafuta ya roho, walisema wa zamani,
    Utanunua majoho, majumba na nyumbani,
    Umezitakasa roho, umekuwa mhisani,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvinja mlima.
    Matajiri wanakujua, wema wako wameonja,
    Nguo zao umefua, wakupata kwa ujanja,
    Sura zao ‗mefufua, wanazuru kila njanja,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mvunja mlima, onana na maskini,
    Watazame mayatima, kwao kumekua duni,
    Webebe waliokuwa, wainue walio chini,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Ndiwe mvunja mlima, wapi kapata uwezo,
    Umezua uhasama, waja kupata mizozo,
    Ndiwe chanzo cha zahama, umewatia vikwazo,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Umevunja usuhuba, familia zazozana,
    Waliokuwa mahabuba, kila mara wagombana,
    Roho zao umekaba, majumbani wachinjana,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Nakutafuta kwa hamu, sabuni unirehemu,
    Sinilipue ja bomu, sije kawa marehemu,
    Niondoe jahanamu, ya ufukara wa simu,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
    Naondoka wangu moyo, nikuitapo itika,
    Fulusi wacha uchoyo, tatua yalonifika,
    Nichekeshe kibogoyo, nami nipate kuwika,
    Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Nitafukuzwa mbinguni Kwa ushairi wangu mbaya Lakini hata motoni nitaimba:(Solved)

    Nitafukuzwa mbinguni
    Kwa ushairi wangu mbaya
    Lakini hata motoni nitaimba:
    Wanasema
    Wanasiasa ni kama jizi
    Lililosukuma mtoto pembeni
    Na kunyonya ziwa la mama
    Wakati amelala usingizi usiku.
    Wanasema
    Mwanasiasa afapo
    Tumejikomboa na domo
    Moja pana lizibwalo na mchanga
    Na kilima cha simenti ngumu
    Lisikike tena hadharani.
    Wanasema pia
    Kusema haki
    Kwa kawaida
    Wanasiasa hatuwapendi.
    Kupiga kura ni hasira za mkizi
    Ni basi tu. Ni Ah!
    Ah!
    Wanamalizia
    Nchi mmefiilisi waacheni walimu
    Wakajenga taifa jipya.
    Top grade predictor publishers Page | 63
    Kama hamwezi kuona mbali
    Bure kuweka mkono usoni,
    Bure hakuna kichwa
    Kama hamwezi kufikiri.
    Ng‘ombe amekamuliwa na wazungu
    Waarabu, wahindi na wao
    Sasa anatoa damu
    Vilivyobaki ni chai ya rangi
    Na madomo mapana zaidi
    Yaliyo bado hai.
    Kuimba nimeimba

    Maswali
    (a) Mshairi ana dhamira gani?
    (b) Shairi hili ni la kukatisha tama, tetea rai hii.
    (c) Onyesha matumizi mawili ya mishata.
    (d) Eleza mbinu zozote nne za lugha zilizotumika katika shairi hili.
    (e) Andika ubeti wa mwisho katika lugha tutumbi.
    (f) Fafanua umbo la shairi hili.
    (g) Eleza maana ya mafungu ya maneno ya maneno yafuatayo:
    (i) kupiga kura ni hasira ya mkizi
    (ii) kuweka mkono usoni
    (iii) ng‘ombe amekamuliwa.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.(Solved)

    MSTAHIKI MEYA: Timothy Arege
    Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.
    Hayawezi kulinganishwa na tendo hili ndogo. Walifanya vizuri kuja.
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Fafanua nafasi ya wanaorejelewa kuwa ―"walifanya vizuri kuja" katika tamthilia hii.
    (c) Migogoro katika tamthilia hii hazikusuluhishwa vyema. Jadili.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.(Solved)

    Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • "Nyamaza boza wewe. Wadhani sisi kazi tunaanza leo? Tumekutana na wauaji wangapi?(Solved)

    Kidagaa Kimemwozea:
    "Nyamaza boza wewe. Wadhani sisi kazi tunaanza leo? Tumekutana na wauaji wangapi?
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Dondoo hili linadokeza maudhui gani? Kwa kutoa mifano saba kwenye riwaya, bainisha jinsi maudhui hayo yanavyojitokeza.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • "Hakujua maisha yake yangechukua mkondo upi. Mzo wa majuto ulimwandama. Ulimwengu wake ulivurugika, akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"(Solved)

    Kanda la Usufi
    "Hakujua maisha yake yangechukua mkondo upi. Mzo wa majuto ulimwandama. Ulimwengu wake ulivurugika, akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaenda arijojo"
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja na kueleza tamathali ya usemi kwenye dondoo hili.
    (c) Kwa kutolea mifano, onyesha jinsi anwani Kanda la Usufi inavyoafiki hadithi husika.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • "………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"(Solved)

    Damu Nveusi na Hadithi nyingine
    "………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Thibitisha ufaafu wa anwani ya hadithi hii.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Elimu imeshindwa kutimiza lengo la kuwapa vijana uwezo wa kukabiliana na maisha ya kisasa. Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hadithi zifuatazo.(Solved)

    Elimu imeshindwa kutimiza lengo la kuwapa vijana uwezo wa kukabiliana na maisha ya kisasa. Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
    (a) Mke wangu
    (b) Samaki wanchi zajoto
    (c) Damu nyeusi.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • "Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……."
    (a) Weka dondoo hili katika muktadha wake .
    (b) Eleza tamathali mbili zilizotumika katika dondoo hili.
    (c) Eleza aina za kiu na njaa zilizomkumba mrejelewa wa kwanza.
    (d) Mrejelewa wa pili alishindwa mtihani wa maisha. Jadili.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)

  • Kuvunjwa kwa haki na sheria lilikuwa jambo la kawaida chini ya uongozi wa Mtemi Nasaba bora. Thibitisha ukweli wa Kauli hii ukirejelea riwaya ya Kidagaa...(Solved)

    Kuvunjwa kwa haki na sheria lilikuwa jambo la kawaida chini ya uongozi wa Mtemi Nasaba bora. Thibitisha ukweli wa Kauli hii ukirejelea riwaya ya Kidagaa kimemwozea.

    Date posted: October 1, 2019.  Answers (1)