Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Mwanafunzi aliadhibiwa kwa uongo wake. (Anza kwa .......Uongo)

      

Mwanafunzi aliadhibiwa kwa uongo wake.
(Anza kwa .......Uongo)

  

Answers


sharon
Uongo wa mwanafunzi ulisababisha kuadhibiwa kwake.
sharon kalunda answered the question on October 4, 2019 at 08:27


Next: Form one students from Inungo school arranged their apparatus as shown below, to investigate a certain phenomenon. The set up was placed in light.
Previous: Andika kinyume. Ukipitia kwao utalaaniwa.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Tambua kinai kilichopigwa mstari katika senensi hii; Watu wenye woga mwingi hukimbia ovyo.(Solved)

    Tambua kinai kilichopigwa mstari katika senensi hii;
    Watu wenye woga mwingi hukimbia ovyo.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Andika maana mbili za neno "mlango".(Solved)

    Andika maana mbili za neno "mlango".

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Jibu kulingana na maagizo. (i) Ufisadi (unda kitenzi) (ii) - pya (unda nomino)(Solved)

    Jibu kulingana na maagizo.
    (i) Ufisadi (unda kitenzi)
    (ii) - pya (unda nomino)

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi hii katika hali ya "a" Kibofu hupaa angani.(Solved)

    Kanusha sentensi hii katika hali ya "a"
    Kibofu hupaa angani.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • CHIMBUKO LA USHAIRI Ushairi ni fani kongwe kama mwanadamu mwenyewe alivyo mkongwe duniani. Na mashairi yamekuwepo kitambo sana hata kabla ya lugha...(Solved)

    CHIMBUKO LA USHAIRI
    Ushairi ni fani kongwe kama mwanadamu mwenyewe alivyo mkongwe duniani. Na mashairi yamekuwepo kitambo sana hata kabla ya lugha ya Kiswahili bado haijanawiri na kushamiri kama ilivyo hivi leo. Ndipo tunasikia kuna mashiri ya kipemba, mashairi ya kimvita, mashairi ya kivumba, mashairi ya kipate, mashairi ya kiyunani, ya kirumi na kadhalika,. Almradi kila jamii na kila kabila lilikuwa na mashairi yake.
    Katika utafiti na kongomano zao, wataalam wa arudhi za Kiswahili asili wamechambua na kufafanua kwamba mashairi ya Kiswahili asili yake ni nyimbo za jadi zilizokuwa zikiimbwa na manju, wangoi au waimbaji stadi wa tangu na tangu walipojumuika katika matukio na hafla mbalimbali kama za jando, arusi, matanga, ngoma na shangwe zao za maishani.
    Nyimbo hizi zilitumiwa na watangulizi wetu, kidhamira hazikuhitalafiana hata kidogo na mashairi ya Kiswahili tunayohimiza wakati huu. Farka iko katika lugha na umbo kwani kila jamii ilitumia lugha yake na lahaja ya mazingira yake. Na kwa upande wa umbo, tungo hizo za awali kabisa hazikuwa na sanaa kwa maana ya ushauri tunauona leo. Bali tungo hizo zilijengeka katika nguzo mbili kuu. Kwanza ni uzito wa mawazo maadilifu ambayo yalitaamaniwa sana. Na pili ni mizani ya sauti ya manju kulingana na lahani, pumzi zake pamoja na madoido katika uimbaji ambao ulikuwa burudani naathari katika noyo za wasikilizaji wake.
    Kwa kifupi ni kwamba, nyimbo hizo ziliuhifaid umma kwa njia mbili, mawaidha kwa mapana na taathira au jadhba kutokana na sauti tamu ya manju.
    Kama utakubalika, basi huo ndio ushairi wa awali kabisa ullioambatana na nyimbo zetu za kienyeji. Kila kabila katika nchi zetu lilikuwa na ushauri wake au nyimbo zake zenye undani uliolenga sababu maalum na tukio maalum katika jamii.
    Nyimbo kama hizo kwa jina la sasa tunaweza kuita mashairi ndizo zile zilizoitwa ‘mwali’ na wakamba; gichandi kwa ‘wakikuyu’; ‘gigia gi sigele’ kwa waluo na ‘wagashe’ kwa wasukuma zilikuwa na undani wa kipekee tena uliodidimia ambao si bure kutolewa hadharani.
    Aina za mashairi ya watu wa mwambao ni kama lelemama, misemele, gungu, nyiso, kongozi n.k.
    (Walla Bin Walla – Malenga wa Ziwa Kuu , E.A.E.P)



    1. Ni nini haswa chimbuko la ushairi?
    2. Kulingana na kifungu hiki, ni nini umuhimu wa ushairi ?
    3. Ni maswala gani yaliyowapendeza wasikilizaji wa tungo hizo za zama ?
    4. Tofauti kati ya nyimbo za zama na ushairi wa leo upo kwenye vipengele gani viwili ?
    5. Kifungu : ‘haijanawiri na kushamiri’ ina maana gani katika lugha nyepesi ?
    6. Eleza maana ya :
    (a) Kongamano …
    (b) Jadhiba
    (c) Farka
    (d) Awali..

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo halisi. Mwalimu alishangaa ni kwa nini Juma hakuwa amebeba mkoba wake siku hiyo.(Solved)

    Andika katika msemo halisi.
    Mwalimu alishangaa ni kwa nini Juma hakuwa amebeba mkoba wake siku hiyo.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo kwa udogo wingi. Mtu yule haachi kuandamana na mbwa wake aliyedhoofika kiafya.(Solved)

    Andika sentensi ifuatayo kwa udogo wingi.
    Mtu yule haachi kuandamana na mbwa wake aliyedhoofika kiafya.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja yenye kishazi huru na kishazi kitegemezi ukitumia "O" rejeshi tamati.(Solved)

    Tunga sentensi moja yenye kishazi huru na kishazi kitegemezi ukitumia "O" rejeshi tamati.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Changanua sentensi hii kwa kutumia jedwali. Mama alilima kwa bidii ingawa hakupata faida.(Solved)

    Changanua sentensi hii kwa kutumia jedwali.
    Mama alilima kwa bidii ingawa hakupata faida.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia kitenzi cha katika hali ya kutendwa.(Solved)

    Tunga sentensi ukitumia kitenzi cha katika hali ya kutendwa.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Bainisha shamirisho na chagizo katika sentensi ifuatayo. Kimathi alimwandikia babake barua kwa kalamu jana jioni.(Solved)

    Bainisha shamirisho na chagizo katika sentensi ifuatayo.
    Kimathi alimwandikia babake barua kwa kalamu jana jioni.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Asifuye mvua imemnyea. Huu ni msemo wenye hakika isiopingika, na kutilia shaka ni sawa na kudai jua linaweza kubadilika na kuchomozea upande...(Solved)

    Soma taarifa hii kisha ujibu maswali

    Asifuye mvua imemnyea. Huu ni msemo wenye hakika isiopingika, na kutilia shaka ni sawa na kudai jua linaweza kubadilika na kuchomozea upande wa magharibi badala ya mashariki. Huu ndio ukweli uliodhihirika juzi katika vyombo vyetu vya magazeti.
    Lisemwalo lipo, na kama halipo li njiani. Waama, pafukapo moshi pana moto. Mwanafunzi mmoja wa kike kwa jina P.N. katika chuo kikuu kimojawapo nchini alishangaza umma wa Kenya na ulimwengu kwa jumla alipodai kuwaambukiza wanafunzi wenzake wa kiume mia moja na ishirini na wanne virusi vya Ukimwi.
    Kisa na maana? Aliambukizwa Ukimwi na mwanafunzi mwenzake aliyekuwa akifanya majaribio ya ualimu katika shule yao ya upili. Baada ya kushawishika sana alijuana naye kimwili, na matokeo yakawa kifo ambacho sasa alikuwa anawagawia wenzake.
    Kisa kama hiki kinachangia kueleza kina kirefu cha kutamauka na upweke ambao maisha ya waja wengi yameingia kiasi cha kuwaacha wanyama ijapo wanaenda kwa miguu miwili bado. Katika mojawapo ya mafunzo ya kidini ambayo Padre alinifunza mimi na wanafunzi wenzangu, tuliambiwa kisasi ni chake Mola, sisi waja wetu ni kushukuru tu. Mbona basi mwanafunzi kama huyu kutaka kulipiza?
    Ima fa ima, na waswahili husema, “mlaumu nunda na kuku pia”. Huyu mwanafunzi hawezi kuachiwa atende alivyotenda. Aliyekula naye raha alikuwa mtu aliyefahamika vizuri sana kwake. Isitoshe, huenda wakati huo alikosana na mama na baba kulala nje. Huenda alikosana na ndugu zake kwa kuepa nyumbani usiku wa manane kwenda kumwona huyu kalameni. Huenda alikosana na mwalimu wake kwa sababu kiburi kilianza kuingia. Kwa vyovyote vile, alikula raha na hastahili kuwaadhibu watu wasio na hatia kufidia makosa yake. Je, kama yeye na huyo jamaa wasingekuwa na Ukimwi, raha kiasi gani wangezila hadi leo?
    Jamii na watu wote kwa jumla hawana budi basi kulaani vitendo vya P.N. vya kuambukiza wanafunzi wenzake virusi huku akijua. Hili ni kosa ambalo linastahili adhabu ya kifo. Dawa ya moto ni moto ni adhabu inastahili kuchukuliwa haraka ili P.N. ambaye tayari amekiri hatia, atiwe nguvuni na adhabu itolewe.
    Barua ya P.N. inafafanua jambo jingine sugu. Kwamba kiwango cha maadili katika vyuo vyetu kimezorota kiasi cha kufanyiana unyama usiosemeka. Vijana wengi siku hizi wanashiriki tendo la ndoa bila haya. Huu upotofu wa maadili katika jamii wapaswa kushutumiwa na wote. P.N. hana sababu yoyote ya kibinadamu, kidini au kitu chochote kile kudai haki kwa uovu huo wake.


    1.Taja kichwa kwa makala haya
    2. Katika aya mbili za kwanza, mwandishi anamlaumu mwanafunzi kwa kosa gani? Eleza chanzo cha tabia za P.N
    4. Mwandishi wa taarifa hii anataka P.N achukuliwe hatua gani? Kwa nini?
    5. Barua ya P.N. bila shaka imeonyesha uvumbuzi mpya. Utaje
    6. Eleza maana ya vifungu hivi kama vilivyotumiwa katika taarifa:
    (a) Kina kirefu cha kutamauka
    (b) Ima fa ima
    (c) Kufidia makosa yake

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi kwa kutumia. (i) Kivumishi cha "ki" ya mfanano. (ii) Kielezi cha kiasi cha jumla.(Solved)

    Tunga sentensi kwa kutumia.
    (i) Kivumishi cha "ki" ya mfanano.
    (ii) Kielezi cha kiasi cha jumla.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha matumizi ya "kwa" katika sentensi hii. Kwa kuwa alikuwa amechelewa kwenda kwa nyanyake alisafiri kwa baiskeli.(Solved)

    Onyesha matumizi ya "kwa" katika sentensi hii.
    Kwa kuwa alikuwa amechelewa kwenda kwa nyanyake alisafiri kwa baiskeli.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Kiswahili lugha yenye asili yake katika ukanda wa Afrika Mashariki imeenea duniani ambako inafundishwa katika uyuo vikuu saba vya umma na vyuo vikuu viwili visivyo vya...(Solved)

    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali.
    Kiswahili lugha yenye asili yake katika ukanda wa Afrika Mashariki imeenea duniani ambako inafundishwa
    katika uyuo vikuu saba vya umma na vyuo vikuu viwili visivyo vya umma. Hivi ni Baratoni na Chuo kikuu ch aKikatoliki. Katika kiwango hiki, watu wanafunzwa isimu na fasihi mafunzo haya yanatolewa kuanzia shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na shahada ya uzamifu.Elimu ya juu ya Kiswahili inatiliwa mkazo katika vyuo vikuu nchini Tanzania na hasa Dar-es-Salaam. Chuo hiki ndicho mlezi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI). Kwa muda mrefu, TUKI imechapisha mararida, kuzua istilahi na kuandaa kamusi. Vyuo vikuu nchini Uganda vikiongozwa na Makerere vimeanzisha mikakati kabambe ya kufunza Kiswahili. Kwingineko barani Afrika, Kiswahili kinafunzwa nchini Msumbiji, Sudan, Misri, Lesotho, Ghana, Nigeria n.k lugha hii imepewa msisimko mkubwa katika mitaala kuambatana na sera ya Afrika Kusini kutukuza lugha za Kiafrika. Ikumbukwe kuwa lugha hii ilichangia pakubwa ukombozi wa Afrika Kusini.Ukitembelea baadhi ya vyuo vikuu katika nchi za mashariki ya mbali kama Japani, Kora Kusini na Uchina, utapata Kiswahili kwenye orodha ya masomo. Maandishi mengi yanatafsiriwa kwa Kiswahili katika vyuo hivi. Takribani nchi zote ulaya zina vyuo vikuu vinavyofunza Kiswahili. Lakini Uingereza, Ujeremani na nchi za Skandinevia zimetia fora, pamoja na kufunza lugha hii, vyuo vinafadhili utafiti na uchapishaji wa mambo kuhusu Kiswahili. aidha nchi hizo huwadhamini wengi kusomea huko. Muhimu zaidi ni kuwa vyuo vikuu katika nchi hizo zimehifadh maandishi mengi ya Kiswahili. Hivi sasa masomo mengi wanayatumia kufanya utafiti hasa hukusu ushairi. Moja ya asasi hizi ni School of Oriental and African studies. Jijini London. Wataalamu waliosomea vyuo hivi wamerudi nyumbani na sasa wanajihusisha na uchapishaji wa vitabu vya nadharia, isimu, surufi, fasihi andishi na fasihi simulizi.
    Hata hivyo, ni Marekani ambapo matumizi na mafunzo ya Kiswahili katika vyuo vikuu yamepanuka sana. Lugha hii inafunzwa katika majimbo kama Washington, New York, Chicago, Texas, California, New Jersey n.k. vyuo maarufu sana vile Cornel, Yale na Havard vinafunza Kiswahili. Hali hii imesaidia kuingizwa kwa lugha hii katika mtandao.Lugha hii inafunzwa kama ishara ya hisia za Uafrika. Wamerekani weusi wanaona fahari kuzungumza Kiswahili. Hii huwakumbusha kuwa wao wana asili ya barani Afrika. Kupitia mafunzo haya, Wamerekani wengi wanaiga utamaduni wa Kiafrika. Wengi wao wamejipa majina ya Kiswahili kama vile Baruti Katembo Maulana, Simba n.k. kwa hakika Kiswahili kinapata hadhi.

    Maswali.
    (a) Bila kupoteza maana illiyokusudiwa na mwandishi, fupisha aya ya kwanza na ya pili.
    (maneno 50 - 60)
    (b) Kwa kuzingatia aya zilizobaki, eleza mambo muhimu anayoeleza mwandishi kuhusu ufundishaji
    wa Kiswahili katika vyuo vikuu. (maneno 60 - 70)

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Kitabu kinaeleza Mungu kamuumba mwanamke kutokana na ubavu tu wa mwanamume. Na hapa bila shaka ndipo linapojisalimishia shina lisilokuwa na mzizi thabiti...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali:-

    Kitabu kinaeleza Mungu kamuumba mwanamke kutokana na ubavu tu wa mwanamume. Na hapa bila shaka ndipo linapojisalimishia shina lisilokuwa na mzizi thabiti la ubinafsi wa kiume – mwanamume akijijadilia kimoyomoyo. Ikiwa huyu mwanamke alitokana na ubavu wangu, yeye awe nani kwangu? Hakuna shaka ni wangu, mali yangu. Kwa sababu hii, miaka nenda miaka rudi mwanamke amekuwa akiugua na kuguna chini ya uonevu wa mwanamume.
    Swala la kitabu kumleta duniani mwanamke kupitia ubavu wa mwanamume laweza kueleweka katika muktadha wa kile ambacho kimekuja kujulikana kama taasubi ya kiume. Na ili tuelewane barabara kuhusu maoni haya, tujisitishe kidogo katika kunusa tumbako huku tukijiuliza: ni nani au ni kina nani walihusika katika kubuni au kuandika hadithi ya asili ya mwanamke kitabuni? Ni kawaida ya binadamu kutazama na kueleza jambo kibinafsi. Asili ya mwanamke ilivyoelezwa kitabuni katika mkururo wa fikra hii yaweza kutambulikana kama uzushi tu.
    Kiutamaduni, hasa wa Kiafrika, huku akiwa yuakua, mtoto wa kike husombezewa kasumba ya mawazo akilini, na kwa bahati mbaya sana, aghalabu na mamake au nyanyake, kuhusu namna anavyotarajiwa kutabasamu, kujinyenyekeza, na jumla kujidunisha mbele ya mvulana. Ni mwiko kwake kudhihirisha tabia za kimabavu, sitaji kujitetea, ili asije akatiwa mdomoni mitaani! Msichana atacharazwa na wazazi wake kwa ujasiri licha ya kuthubutu kupigana na mvulana. Na hapo ndipo ilipojificha siri ya kuwa anapoolewa na akosane na mumewe, daima yeye hutolewa makosa na kupatikana na hatia mbele ya wazee.
    Wavulana kwa upande wao ni wanaume na lazima afanye mambo kiume. Si ajabu kuwa kinyume cha yale yanayowafika wasichana, wavulana wengi huonyeshwa mbovu na baba zao kwa sababu wamepigwa na wenzao. Ni vibaya baba kusikia mtoto (mvulana) wake amepigwa.
    Nyumbani msichana hutarajiwa kujilindia heshima kimwili hasa kwa kuhifadhi ubikira mpaka aolewe. Anapotembea na wanaume huitwa Malaya. Ni ajabu kuwa hakuna bikira wala Malaya mwanaume. Mvulana ambaye hajajuana kimwili na mwanamke kabla ya ndoa huchukuliwa kuwa zuzu; ilhali anayetembea ovyo na wanawake ndiye dume.
    Fauka ya hayo, inasikitisha kabisa kuwa mwanamke hana mahali pa kutua kikamilifu duniani. Kabla hajaolewa nyumbani, huchukuliwa kuwa mpita njia tu. Na anapoolewa ni poa kaolewa. Isitoshe mwanamke huolewa, haoi wala yeye na mume hawaoani. Mwanamke mahali pake ni jikoni pia anaonekana tu; ni hatia kwake kujaribu kusikika.
    Mkutano kuhusu mwongo wa wanawake uliofanyika miaka miwili iliyopita jijini Nairobi ilinuiwa kupalilia vizuri mwamko juu ya ukweli kuwa binadamu ni binadamu na hakuna haja ya wao kubaguana. Tofauti za kimaumbile haziwezi kuwa hoja. Tusiupigie makelele ubaguzi wa rangi huko Afrika kusini ilhali kwetu tuna ubaguzi wa kimaumbile. Tusipozingatia ushauri huu daima tutakuwa kwenye kile kinaya cha kuchekwa katika muktadha wa methali kuwa nyani haoni ngokoye.
    Ni kweli kosa lilifanyika tangu awali ambapo kufumba na kufumbua, mwanamke akapigwa jeki na kuachwa akilewalewa katika hali ambayo hangeweza kujitetea hivyo basi akachukuliwa kuwa kiumbe duni. Lakini haidhuru, yaliyopita si ndwele, tugange yajayo. Kinachohitajika ni wanawake kuwa na nia na msimamo imara. Ni lazima wajifunge kibwebwe na kujitoa mhanga na kupambana dhidi ya taasubi ya kiume.


    (a) Andika kichwa kinachofaa kutokana na taarifa uliyoisoma
    (b) Taasubi ya kiume ilianzaje?
    (c) Katika utamaduni wa mwafrika ni kasumba gani anayosombezewa mtoto wa kike anapokua?
    (d) “Wavulana walidekezwa na utamaduni”. Eleza
    (e) Taja kwa ufupi mambo muhimu yaliyoshughulikiwa katika mkutano wa mwongo wa wanawake mjini Nairobi
    (f) Eleza maana ya semi zifuatazo kama zilivyotumiwa katika taarifa uliyosoma:-
    (i) Nyani haoni ngokoye .
    (ii) Akatiwa midomoni
    (iii) Huonyeshwa mbovu
    (iv) Wajifunge kibwebwe
    (v) Yaliyopita si ndwele ganga yajayo

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Uundaji wa istilahi – hasa za lugha ya Kiswahili ni shughuli nyeti na nzito hivi kwamba, haipaswi kupapiwa na mtu yeyote. Hii...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali:-

    Uundaji wa istilahi – hasa za lugha ya Kiswahili ni shughuli nyeti na nzito hivi
    kwamba, haipaswi kupapiwa na mtu yeyote. Hii ni shughuli inayohitaji umakinifu zaidi kwa wanaoshiriki katika mchakato wa uundaji istilahi za kutufaa katika mawasiliano na kukuza Kiswahili kwa jumla. Ufanisi wa watu binafsi, vyombo vya habari kama vile Shirika la Habari la Kenya (KBC), Taifa Leo na mashirika mengineyo katika ukuzaji wa lugha hutegemea mno sera na utayarishaji wa serikali katika kugharamia shughuli hii. Aidha, shughuli za kukuza lugha hukwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha pamoja na sera maalum ya serikali kuhusu lugha.
    Hata hivyo, katika kuyakwepa matatizo haya, pamekuwepo na hatua za kimataifa za kujaribu kusawazisha shughuli ya uundaji wa maneno. Hatua hii ilichochea kubuniwa kwa shirikisho la kimataifa la vyama vya usanifishaji istilahi mnamo 1936. Lengo la kitengo hiki lilikuwa ni kufafanua msingi madhubuti ya uundaji wa istilahi duniani. Kwa hakika, shirikisho hilo limesaidia mno katika kuweka misingi ya shughuli za ukuzaji wa istilahi. Misingi hiyo ni ya jumla na haihusu taaluma yoyote mahususi. Katika makala hii, tunapiga darubini baadhi ya misingi hiyo pamoja na mapendekezo yake.
    Mosi, uundaji istilahi unafaa uanzie kwenye dhana na wala sio neno. Hii ina maana kwamba, kwanza pawepo na dhana au hali ambayo inahitaji itafutiwe neno au istilahi ya kuielezea. Inasikitisha sana kwamba pana wataalamu ambao wanaukaidi au kuukiuka msingi huu. Wanataaluma hawa hufanya mambo kinyume kwa kujibunia maneno yao na kuyahifadhi kwenye mikoba yao – halafu wakasubiri dhana izuke ndiposa waipachike istilahi yao. Pili, dhana zinabuniwa au kutolea istilahi au maneo ni muhimu zielezwe kwa ukamilifu na uwazi. Istilahi zinazoundwa zinafaa ziwe fupi iwezekanavyo na ziwe na uwezo wa kuelezea dhana kwa njia inayoeleweka bila utata. Tatu, maneno yanayoundwa sharti yawe na uhusiano wa aina fulani na dhana zinazowakilishwa na maneno hayo.
    Uhusiano huo unaweza kuwa ama ni wa kimaumbile au wa kiutendaji. kwa mfano, Mzee Sheikh Nanhany wa Mombasa alipobuni istilahi ‘uka’ kwa maana ya ‘ray’. Neno hili latokana na kupambauka au (kupambazuka kwa lafudhi ya kiamu. Neno ‘image’ ni jazanda kwa Kiswahili. ‘Mirage’ kwa Kiswahili ni ‘mangati’ (kutoka kwa mang’aanti) – yaani kung’aa kwa nchi. Mtaalamu mwingine aliyewazia uendajikazi wa kifaa na kubuni istilahi inayokubalika mpaka sasa ni Prof. Rocha Chimerah ambaye alibuni istilahi ‘tarakilishi’. Pengine Prof. Chimerah alifikiria kazi ni kifaa husika na kuunda neno la Kiswahili linaloakisi kazi hiyo. Tunajua kwamba kompyuta hufanya kazi inayohusu tarakimu kwa haraka kama umeme. Labda Chimerah ameegemea sifa hii kuibuka na istilahi hii.
    Maneno mengine ambayo yamebuniwa kufuatana na msingi huu ni ya Mzee Nabhany-mathalan ‘barua pepe’ (e-mail), na wavuti (website). Tukiegemea maumbile, neno ‘kifaru’ lina maana ya vita ilihali tuna zana ya vita iliyopewa jina hilo kwa sababu ya labda kuwa na maumbile sawa na kifarumnyama. Nne, istilahi zinaweza kukopwa kutoka lugha nyingine. Yamkini hakuna lugha hata moja ulimwenguni-zikiwemo lugha duniani kama vile kiingereza zinazoweza kujitosheleza. Takriban asilimia 80 ya maneno katika kiingereza ni ya kukopwa. Kwa hivyo, lugha ya Kiswahili inapokopa, hali hiyo haipaswi kuchukuliwa kuwa ni lugha dhaifu.
    Hata hivyo, istilahi zinazokopwa zi-nafaa zichukuliwe zilivyo katika umbo lao asili. Umbo hili linaweza kufanyiwa marekebisho machache tu, kulingana na sarufi na matumizi ya lugha kopaji. Mifano ya istilahi kama hizi ni ‘televisheni’ (television), kopmpyuta (computer), kioski (kutokana na jina ‘kiosk’ la Kijerumani) na redio (radio), Tano, pale istilahi haiwezi kukopwa, lugha husika ijaribu kubuni msamiati ufaao, kufanya hivyo ni kuhakikisha kwamba, lugha inastawi. Lakini tahadhari inapaswa kuchukuliwa hivi kwamba, Kiswahili kisikope maneno kiasi cha kupoteza upekee wake. Mwisho, uundaji wa istilahi uzingatie mofolojia ya kawaida ya lugha. Istilahi zinazoundwa kwa kuzingatia mofolojia huwa rahisi kuiua maneno yenye uhusiano wa istilahi asili kwa njia ya mnyambuliko.



    (i) Taja mambo ambayo huchangia ukuaji na ufanisi wa jumla wa lugha ya Kiswahili
    (ii) “Lugha ya Kiswahili ni dhaifu na isiyotosheleza” Je, mwandishi wa makala haya
    ana msimamo upi kuhusu kauli hii?
    (iii) Tahadhari zipi zinazofaa kuchukuliwa kabla ya kukopa istilahi kutoka lugha zingine?
    (iv) Yape makala haya anwani mwafaka
    (v) Eleza maana ya maneno yafuatayo:
    (a) Dhana-
    (b) Takribani –
    (c) Istilahi – .
    (d) Mofolojia –...

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Kuna fikra inayotawala siku hizi kuwa jela si mahali pa adhabu bali matibabu.(Solved)

    Kuna fikra inayotawala siku hizi kuwa jela si mahali pa adhabu bali matibabu. Yaani lengo la kumfunga mhalifu si kumuadhibu bali kumtibu kwa njia ya kurekebisha tabia ili aweze kuchangia katika maendeleo ya jamii yake anapoachiliwa.Wataalamu wa masuala ya urekebishaji tabia wanasema kuwa mhalifu akiadhibiwa sana na kufanyishwa kazi ngumu anapokuwa kifungoni, huisha kuwa sugu zaidi kuliko alipofungwa. Kwa hivyo, wataalamu wanasisitiza umuhimu wa kutilia mkazo lengo la kumtia mtu jela kuwa ni kumjenga kitabia. Mijizi, minyang‘anyi na wauaji wanapotoka gerezani kama hawakubadilishwa hurejelea tabia zao za kuhatarisha zaidi maisha ya watu wengi.Ajabu na kinaya ni kwamba baadhi ya wahalifu nchini na kwingineko wametokea kupata faida kuu kutokana na vifungo vyao. Kuna wagungwa ambao wamewahi kuandika hadithi za kusisimua kuhusu maisha yao na kutokea kuwa mabilionea.Magazeti na vyombo vya habari pia huvutiwa na habari kuhusu maisha yao. Mara kwa mara, magazeti hujaa habari kuhusu mambo kama haya. Pia kuna sinema nyingi ambazo zimetungwa kufuata maisha ya wahalifu Fulani.Watetezi wa haki za kibinadamu wanadai kuwa yale wafungwa walikuwa wakitendewa, nab ado wanatendewa katika nchi nyingine ni kinyume nah akin za kimsingi za binadamu. Hali hii imepelekea magereza mengi kukarabatiwa ili kuweza kukidhi mahitaji ya "uibinadamu."
    Nchini kenya, wafungwa sasa wameanza kushughulikiwa kwa kila hali. Sikwambii wanapata chakula kizuri chenye viini lishe bora, malazi bora, maji safi na mazingira nadhifu kwa jumla. Kumeanzishwa pia mpango wa elimu ambao ni maalum kwa wafungwa magerezani. Sasa wafungwa wanapata elimu na kuhudhuria madarasa na hata kuufanya mtihani wa kitaifa.Vile vile magereza nchini wameanzisha pia mpango wa kuwa na mashindano ya kila aina, ya kati ya magereza mbalimbali.Kuna mashindano ya michezo mathalan kandanda, voliboli, na michezo mingine na juu ya yote majuzi magereza yalianzisha mashindano ya urembo baina ya wafungwa wa kike.
    Kilele cha kuboresha kwa hali ya magereza nchini Kenya ni kuanzishwa kwa huduma za kuwastarehesha wafungwa hao. Sasa wafungwa wa humu nchini wanaweza kusoma magazeti na hata kutazama runinga ili kupata habari kuhusu
    yanayotendeka nchini wanapoendelea kutumikia vifungo vyao.
    Hata ingawa serikali imeanzisha mipango hii ya kuboresha hali katika magereza ya kenya, kuna matatizo mbalimbali ambayo yanaendelea kukumba taasisi hii. Kwanza, ni msongamano wa wafungwa uliopo. Magereza mengi yana wafungwa maradufu ikilinganishwa na idadi yanayofaa kuwa nayo. Hali hii imepelekea kuzuka kwa magonjwa na madhara mengine.
    Hii imewafanya watetezi wa haki za kibinadamu kuitaka serikali ianzishe mpango wa kutoa vifungo vya nje kwa wahalifu wenye makosa madogo madogo kuondoka msongamano huo.

    Maswali
    a) Eleza ujumbe muhimu unaojitokeza katika aya nne za kwanza. (maneno 50-60)
    b) Eleza mabadiliko ambayo yamefanywa katika idara ya magereza nchini Kenya

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Nchini Kenya, pamoja na kuwa mwanamke amepewa hadhi kubwa ikilinganishwa na hapo awali, kumetokea visa vingi vya unyanyasajiwa wanawake. Visa hivi haviwakati...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali

    Nchini Kenya, pamoja na kuwa mwanamke amepewa hadhi kubwa ikilinganishwa na hapo awali, kumetokea visa vingi vya unyanyasajiwa wanawake. Visa hivi haviwakati wengi maini, bali ni vyombo vya kuwazindua viongozi kuona kwamba hali haijafika kiwango cha kuridhisha. Visa vya ubakaji wa watoto wa kike na wazee, na wakati mwingine baba zao, vimetokea katika miaka ya hivi karibuni. Isitoshe, akina mama wengi wamekuwa wahasiriwa wa mivua ya makonde kutoka kwa waume zao, hata kwa makosa madogo madogo. Hivi majuzi mmoja wa wanawake hawa, ambao maisha kwao ni shairi tu, alichomwa vibaya na mumewe, kisa na maanaamejitia kujua kuwa kuna siku ya wapenzi, yaani Valentine day. Mwanamke huyu, baada ya kutoa mashambani kuja kujumuika na mumewe kusherehekea siku ya wapenzi, alipata sherehe za kuchoma moto huku mumewe akilalamika kuingiliwa uhuruwake. Mama huyu bado anauguza majeraha ya mwili na moyo!
    Mwanamke aliyesoma na kupewa fursa ya kufanya kazi na ajira ofisini naye amekabiliwa na changamoto nyingi. Huyu lazima atekeleze majukumu yake kama mama, mke na mfayikazi. Wengi wa wanawake wanaofanya kazi mjini hulalamika wanafanya kazi maradufu ya wanaume. Mwanamke kama huyu, kama alivyolalamika mmoja wao ambaye ni afisa wa utawala wa mikoa, huanza siku yake alfajiri na mapema kuitayarishia familia staftahi, kisha kuelekea ofisisni ambapo anakabiliwa na migogoro mingi ya kusuluhisha. Arejeapo nyumbani jioni, hali huwa hiyo hiyo, kutayarisha chajio, kushughulikia kazi za shule za watoto na kuichangamsha familia. Maisha yake huwa hivyo, siku nenda siku rudi. Utashangaa mja huyu atayabeba mangapi?
    Hali huwa mbaya zaidi kwa wanawake ambao wameingia siasa. Hawa mikasa yao haihesabiki. Mara watupiwe mabezo ya kila aina na wanasiasa wenzao, mara washutumiwe na kutiwa midomoni na wanajamii kwa kuonekana wakichapa kazi na kuwa na uhusiano wa karibu na wazalendo wenzao wa kiume. Maisha yake hupigwa darubini hata nyakati ambazo hayahitaji kuangazwa.
    Mwanamke amekuwa kinyago cha kufanyiwa mzaha. Juzi karibu mbingu zianguke alipojitokeza mwana vitimbi mmoja aliyejitia kufanyia utani yasiyohitaji. Alimwasiri mwanamke kama aliyechangia kukosewa heshima kwake kwa kule kutamani kufanywa hivyo. Ingawa wanawake walimshinikiza mhusika huyu kuomba msamaha, upayukaji wake haupaswi kuchukuliwa kama mzaha. Ni ishara ya hisia ya ndani za watu wengi kuhusu mwanamke; kwamba ingawa wakenya wamejitahidi kupigania haki za wanawake; baadhi yetu bado wana zile fikira za kijadi kuhusu wanawake.
    Uchumi wa nchi kamwe hauwezi kuendelea bila kumhusisha kila mtu. Nchini humu, baada ya kutambua haya, mwanamke amepewa nyadhifa mbalimbali katika serikali. Ingawa kuna baadhi ya wanawake waliohusika na kashfa mbalimbali za kifisadi, Kuna wale ambao wametumia nyadhifa zao kuhifadhi nchi. Mmoja wa wanawake amejaribu kwa jino na ukucha kuyalinda mazingira dhidi ya mapapa. Nani asiyekumbuka matusi na mabezo aliyopata mwanamke huyu anayejitoa mhanga kuikinga sehemu Fulani ya burudani dhidi ya kunyakuliwa na wanaostahili? Hakuyajutia yaliyompata. Aliowatisha walijaribu kummeza mzimamzima lakini mwishowe walisalimu amri na kuliacha eneo hilo. Hiki kilikuwa kitendo cha ujasiri na uzalendo mkubwa. Matunda yake yamewafaidi wengi, vijana kwa wazee. Kila mwisho wa wiki huwaona watu wakimiminika kwenye eneo hili kujipumbaza. Hii si fahari kwake tu, bali kwa nchi kwa jumla. Wale waliompinga na kumwita punguani wakati huo wamebaki kuinamisha nyuso tu; bila shaka wamefunzwa mengi.
    Wanawake sasa wana haki ya kumiliki mali mathalani shamba. Kutokana na hili tumeshuhudia ongezeko kubwa la uzalishaji wa chakula mashambani na kwa hivyo kupunguza njaa na umaskini.
    Biashara ndogondogo zinazoendelezwa sokoni na mitaani, kwa kiasi kikubwa, huhusisha wanawake. Biashara hizi huchangia pakubwa katika kuimarisha uchumi wa nchi kwani hutoa ajira ya kibinafsi kwa maelfu ya watu. Ushuru na leseni zinazokatiwa biashara hizi huongezea serikali pato la ndani.
    Mgala muuwe na haki umpe. Ni ukweli kwamba tumekuwa na visa vya hapa na pale vya ukiukaji wa haki za wanawake. Hata hivyo, ni dhahiri kwamba nchi hii imejitahidi mno kuendelea kumkwamua mwanamke kwayo. Hata mashirika ambayo hapo awali hayakupenda kuwaajiri wanawake, sasa yanawapa nafasi sawa na wanaume. Vyuo vikuu vya kibinafsi vimeanzishwa kuwasajili wanawake. Jijini humu, mna chuo kikuu cha sayansi cha wanawake. Aidha kumeanzishwa kituo (shule) cha kuwasajili wasichana kutoka familia maskini kujiunga na kidato cha kwanza. Wasichana hawa watapata wadhamini kutoka mashrika na watu mbalimbali ili kujiendeleza kimasomo.
    Kumheshimu mwanamke ni miongoni mwa haki za kibinadamu ambazo shart zitekelezwe. Hata hivyo, wanawake wakumbuke kwamba hata wanapopuliza siwa kuhusu pupewa haki, lazima wao pia wawajibike. Wao ndio walimu wa kwanza wa wanao; ikiwa basi wataonekana kwenye vyombo vya habari wakining’inia juu ya magari ya wachunga magereza kwa kuzitafutia pesa za mayatima maumizi bora, watakuwa wanapotosha watoto wao. Wawe watu wa vitendo zaidi ya upayukaji.


    a) Kwa mujibu wa taarifa, ni mambo yapi yanayoonyesha ukiukaji wa haki za wanawake
    b) Fafanua jinsi mwanamke aliyesoma huteseka maradufu zaidi ya mwanamme
    c) Ni faida gani ambazo zimepatikana kutokana na wanawake kupigania haki zao?
    d) Hatimaye wanawake wanahimizwa kufanya nini?
    e) Eleza maana ya msamiati ufuatao jinsi ulivyotumiwa katika nakala
    Kinyago…
    Mabezo
    f) Andika mfano wa mbalagha na uhuishi uliotumiwa katika makala haya
    i) Mbalagha
    ii) Uhuishi

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Ufisadi ni uhalifu unaohusu kuzitumia njia za ulaghai kujipatia pesa, mali au vitu hasa vya umma. Nchini Kenya ufisadi hujitokeza...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali.

    Ufisadi ni uhalifu unaohusu kuzitumia njia za ulaghai kujipatia pesa, mali au vitu hasa vya umma.
    Nchini Kenya ufisadi hujitokeza kwa njia mbalimbali na kila mojawapo ina athari zake. Kwa mfano kuna maafisa wa serikali wajipatiao pesa kwa kuuza stakabadhi za serikali kama vile pasi, vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya kumiliki mashamba, vitambulisho n.k. kwa raia, kuna hatari kubwa kwa sababu watu wasio raia wa Kenya wameweza kusajiliwa kama wakenya na kuendeleza uhalifu kama ugaidi, wizi na ulanguzi wa dawa za kulevya.
    Wengine hujipatia vibali vya kufanya kazi na kuajiriwa kazi ambazo zingefanywa na wakenya. Hii imechangia ongezeko la uhaba wa kazi nchini.
    Watumizi wengine wa umma huuza mali ya serikali kama vile magari nyumba na ardhi na kufutika pesa za mauzo mifukoni mwao. Wengine wao hujinyakulia na kufanya vitu hivyo kuwa mali yao. Ufisadi wa aina hii umegharibu serikali kiasi kikubwa cha fedha. Serikali imelazimika kununulia maafisa wake magari baada ya muda mfupi, kulipia wafanyi kazi wake kodi za nyumba na kukosa viwanja vya upanuzi na ujenzi wa shule hospitali, vituo vya polisi na taasisi zingine maalumu.
    Baadhi ya wataalamu kama madaktari huiba dawa kutoka hospitali za umma kupeleka vituo vyao vyaafya. Pia hutumia wakati wao mwingi katika kazi zao za kibinafsi na kuwaacha wagonjwa katika hospitali za umaa wakihangaika. Sio madaktari tu, kuna masoroveya, whandisi, mawakili, walimu na mahesibu ambao hukwepa majukumu yao serikalini na kufanya kazi za kibinafsi.. Wengine wasio wataalam huendesha biashara za aina tofauti, na huku wanaendelea kupokea mishahara.
    Wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo na shule bora za umma na hawakuhitimu wakati mwinginehulazimika kusalimu amri na kutoa hongo hili wapate nafasi za kusoma. Kiasi cha pesa kinachohitajika huwa kikubwa hivi kwamba ni wachache humudu hizo rushwa. Wale wasiojimudu kifedha hubaki wakilia ngoa. Kuna wazazi ambao hutumia vyeo vyao na ‘undugu’ kupata nafasi zilizotajwa, jambo ambalo huwanyima wanafunzi werevu kutoka jamii maskini nafasi ya kupata elimu. Matokeo huwa ni kuelimisha watu wasiostahili na ambao mwishowe hawaziwezi kazi wanazosomea wakihitimu na kuanza hudumia jamii.
    Ufisadi umekita mizizi na kushamiri katika sekta za umma za kibinafsi kwa upande wa kuajiri wafanyikazi. Ni vigumu kupata kazi ikiwa hujui mtu mkubwa katika shirika linalohusika au uzunguke mbuyu. Matokeo ni kuajiri wafanyikazi wasiohitimu na wasiohitimu na wasiowajibika kazini.
    Vyeo na madaraka katika baadhi ya mashirika hutolewa kwa njia ya mapendeleo na ufisadi. Kwa hivyo, wafanyikazi wenye biddi hufa moyo kwa sababu hawasaidiwi ipasavyo. Badala yake wale wasioleta bidii hupandishwa vyeo na kuwaacha palepale.

    Hata hivyo, mbio za sakafuni huishaia ukingoni. Serikali imetangaza vita dhidi ya ufisadi. Tayari tume kadhaa zimeteuliwa kuchunguza visa vya ufisadi uliotekelezwa hapo mbeleni. Mojawapo ya tume hizo ni Tume ya Kuchunguzavisa vya ufisadi uliotekelezwa hapo mbeleni. Mojawapo ya tume hizo ni Tume ya kuchunguza Kashfa ya “Goldenberg” ambapo pesa za umma (mabilioni ya shilingi) ziliporwa na mashirika na watu binafsi kwa njia siziso halali. Watakaopatikana na hatia ya kushiriki ufisadi huo watahitajika kurudisha pesa hizo.
    Serikali pia imeunda kamati ya kupikea malalamiko kutoka kwa wananchi waliohasiriwa na mawakili walaghai ambao hupokea ridhaa kwa niaba ya wateja wao na kukosa wakalipa, au wakilipwa kuwatetea mahakamani wanakwepa jukumu hilo ilhali wamekwishalipwa. Ni matumaini yetu kuwa ulaghai huu utaangamizwa kabisa kwani hakuna refu lisilokuwa na ncha.


    1. Eleza aina nne za ufisadi zilizotajwa katika kifungu ulichosoma
    2. Kulingana na kifungu ulichosoma, ufisadi umeathiri nchi yetu kwa njia gani?
    3. Serikali inafanya jitihada gani ili kukomesha ufisadi?
    4. Kwa maoni yako, unafikiri ufisadi husababishwa na nini?
    5. Toa msamiati mwingine wenye maana sawa na rushwa
    6. Eleza mana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa kifunguni;
    (a) Majukumu
    (b) Kashfa
    (c) Shamiri
    (d) wakilia ngoa
    (e) Waliohasiriwa
    (f) Kita mizizi

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)