Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Tumia neno kitoto kama; i) kivumishi ii) kielezi

Tumia neno kitoto kama;
i) kivumishi
ii) kielezi

Answers


sharon
i) Ana tabia za kitoto.
ii) Anacheka kitoto.
sharon kalunda answered the question on October 4, 2019 at 13:19

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Taja na ueleze pingamizi zozote tano zinazokwamiza juhudi za kukuza Kiswahili (Solved)

    Taja na ueleze pingamizi zozote tano zinazokwamiza juhudi za kukuza Kiswahili

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi hii kwa kutumia kielelezo cha visanduku. Mzee aliyemdhulumu msichana yule ametiwa mbaroni tena. (Solved)

    Changanua sentensi hii kwa kutumia kielelezo cha visanduku.
    Mzee aliyemdhulumu msichana yule ametiwa mbaroni tena.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza juhudi zozote tano za serikali ya Kenya katika kukuza Kiswahili (Solved)

    Eleza juhudi zozote tano za serikali ya Kenya katika kukuza Kiswahili

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza matumizi ya "ku" katika sentensi hii. Kucheza kwake kulifurahisha wengi (Solved)

    Eleza matumizi ya "ku" katika sentensi hii.
    Kucheza kwake kulifurahisha wengi

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi sahihi ukitumia kitenzi — nywa katika kauli ya kutendesha (Solved)

    Tunga sentensi sahihi ukitumia kitenzi — nywa katika kauli ya kutendesha

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Yakinisha sentensi hii Mpishi asipokuwa mwangalifu chakula hakitaiva vizuri (Solved)

    Yakinisha sentensi hii
    Mpishi asipokuwa mwangalifu chakula hakitaiva vizuri

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Ainisha viwakilishi katika sentensi hii Usibanduke papa hapa (Solved)

    Ainisha viwakilishi katika sentensi hii
    Usibanduke papa hapa

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Uchumi wa soko huria ni hali ya kiuchumi ambapo itokeapo amali, shughuli na harakati zote za kiuchumi ghairi ya zile... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

    Uchumi wa soko huria ni hali ya kiuchumi ambapo itokeapo amali, shughuli na harakati zote za kiuchumi ghairi ya zile ambazo ni za lazima kwa serikali au dola kama ulinzi, sheria na
    mpangilio wa jamii huwa huria kwa watu binafsi. Msingi wa soko huria, sifa kuu ya utandawazi, ni kuibua na kudumisha mazingira na hali zinazochochea na kumruhusu mtu yeyote kuongozwa na hawaa, au matamanio ya kibiashara anayoyaona sawa pasi na hofu ya kuingilia na udhibiti wa serikali.
    Mazingira hayo yanawapa watu satua ya kufanya maamuzi kuhusu hatima yao ya kiuchumi, uamuzi kuhusu suala la ajira yao, matumizi ya mtaji kipato na harija zake, na uwekezaji mzima. Suala mojawapo linaloibuka kuhusiana na mfano wa soko huria ni kuweka mipaka bainifu na wazi baina ya amali na shughuli zinazohusishwa na serikali na zile ambazo huachwa huria kwa watu. Kwa mfano, inaaminiwa kuwa haki ya kuishi na kulindwa dhidi ya shambulizi, liwe la kijambazi au la kigaidi, ni ya kimsingi ambayo haiwezi kuhusishwa na uwezo wa kiuchumi wa mtu binafsi. Aidha huduma za kimsingi za afya nazo zinaingia katika kumbo hili. Ikiwa huduma hizi zitaachwa huria pana uwezekano mkubwa kuwa zitaishia kuwa istihaki ya wenye mtaji na kipato cha juu tu.
    Licha ya kuwepo kwa sheria au kanuni huria kutoka nyanja maalum, hutokea hali ambapo adhibiti wa kiserikali ni lazima. Hii hutokea pale ambapo ipo haja ya kuyalinda mazingira hasa kutokana na uchafuzi wa viwanda au tasnia. Aidha udhibiti huo ni lazima pale ambapo haki za watu wengine zinahusika: yaani ikiwa uhuru wa hata mtu mmoja unaadhirika kutokana na sera hizo pana haja ya kuingilia ili kuisawazisha hali yenyewe.
    (a) Andika kwa muhtasari maana ya uchumi wa soko huria kulingana na taarifa hii.
    (maneno 25-30)
    (b) Eleza mawazo makuu yanayojitokeza katika aya ya pili na ya tatu.
    (maneno 70-75)

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Toa maana ya semi Shupaa mwili. (Solved)

    Toa maana ya semi Shupaa mwili.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Taja dhamira ya sentensi ifuatayo Kimbia mbio ulete sahani (Solved)

    Taja dhamira ya sentensi ifuatayo
    Kimbia mbio ulete sahani

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Vijana wa siku hizi hujifikiria kuwa wao ni bora kuliko wazee wao. Wao hujifikiria kuwa wameelimika zaidi, wana busara... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

    Vijana wa siku hizi hujifikiria kuwa wao ni bora kuliko wazee wao. Wao hujifikiria kuwa wameelimika zaidi, wana busara zaidi, wanauelewa ulimwengu vizuri zaidi na wanaweza kujiamulia hatima yao bila uongozi wa wazazi wao. Wazee kwa upande wao, hawakubali kabisa madai ya aina hiyo. Kwao ni maasi tu. Wanachojua wazee kwa hakika ni kuwa vijana wa siku hizi hawaajibiki kwa lolote, wamedekezwa mno na wanapenda sana nafsi zao. Kwa sababu hiyo, vijana wanahitaji uongozi na ushauri wa wazeee.
    Je, kuishi kwingi ni kuona mengi? Ingawa wazee wanafikiria wanajua mengi kwa sababu ya umri wao, vijana hupenda sana kukosoa fikira za wazee wao. Hawakubali imani na itikadi za wazee wao. Kwa mfano; vijana hupendelea mitindo ya mywele ambayo wazee wao hufikiria kuwa kichaa tu.
    Wazee husifiwa sana enzi zao. Husifia jinsi walivyolelewa kwa kuchapwa na kufanyishwa kazi zinazohitaji uvumilivu mkubwa kama vile kuchanja kuni, kufyeka misitu, kutayarisha mashamba, kuwinda na kadhalika. Kwa sababu ya malezi hayo, wazee husema wao walirithi nidhamu nzuri na ushujaa. Vijabna kwa upande wao hawaoni chochote cha kujivunia katika zama za wazee wao; wao hufikiria kuwa wazee wao walilelewa kwa ukatili kwa sababu zama zao zilikuwa enzi za giza, kabla ya majilio ya uungwana na ustaarabu wa kisasa.
    Wazee husifia kuwakumbusha vijana ule msemo mashuhuri wa wahenga usemao kuwa ‘mwacha mila ni mtumwa.’ Kwa maoni ya wazee, vijana wengi wamekuwa watumwa kwa sababu wao huonyesha kwa vitendo kuwa hawadhamini desturi za wazee wao. Ka mfano; vijana hawafuati miiko ya jadi, hawapendi kuhudhuria sherehe za kienyeji, kwa mfano sherehe za kutoa makafara. Vijana pia hawapendi ngoma za kitamaduni, na isitoshe vijana hawazionei fahari koo zao. Vijana hawakubali kuwa wao ni watumwa wa mtu yeyote. Mila wanazosifia wazeee wao si vitu vyenye umuhimu wowote kwa vijana. Kwa mfano; baadhi ya miiko ni kisayansi. Kuhusu ukoo, si vijana wengi wanaona umuhimu wake. Ukoo na kabila zilikuwa muhimu zamani wakati ambapo kulikuwa hakuna serikali, bima na hata kazi ya mtu binafsi. Mambo haya sasa ni kama masalia ya zamani ambayo yamepitwa na wakati.
    Je, vijana hupenda sana burudani na anasa tu kama wanavyodai wazee! Wazee wengi hufikiria kuwa vijana hupoteza muda wao mwingi kujitafutia anasa na burudani kwa mfano vijana wengi hurandaranda barabarani au mitaani wakisingizia kupunga hewa. Wengine huenda sinema na kuhudhuria dansi na karamu zisizo na manufaa. Vijana kwa upande wao hawaoni kinachowawasha wazee wao; pilipili wasioila yawashia nini?
    (i) Katika makala haya wazee wana malalamiko yapi kuhusu vijana? (maneno 50-60)
    (ii) Msemo unaosema “Mwacha mila ni mtumwa” unathibitishwa vipi katika maoni ya wazee
    katika makala haya? (maneno 15- 25)

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Akifisha sentensi ifuatayo iii ilete dhana tatu tofauti; Fatuma Khamisi mjukuu wa Rashid na Rehema wametoroka shule (Solved)

    Akifisha sentensi ifuatayo iii ilete dhana tatu tofauti;
    Fatuma Khamisi mjukuu wa Rashid na Rehema wametoroka shule

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Andika sentensi hii katika hali ya umoja. Vilifi vivi hivi ndivyo vimekuwa vikitumiwa na meli zizi hizi kutia nanga bandarini. (Solved)

    Andika sentensi hii katika hali ya umoja.
    Vilifi vivi hivi ndivyo vimekuwa vikitumiwa na meli zizi hizi kutia nanga bandarini.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa. “Michezo yetu ya mpira itang’oa nanga kesho,” mwalimu alimwambia mwanafunzi yule. (Solved)

    Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa.
    “Michezo yetu ya mpira itang’oa nanga kesho,” mwalimu alimwambia mwanafunzi yule.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana mbili zinazopatikana katika sentensi ifuatayo; Tafadhali niletee pia nichezee. (Solved)

    Eleza maana mbili zinazopatikana katika sentensi ifuatayo;
    Tafadhali niletee pia nichezee.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Kwa hali nyingine , tunaweza kusema kuwa uchafuzi wa mazingira ni uharibifu wa vile vitu vinavyowazunguka binadamu na wanyama maishani mwao.... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

    Kwa hali nyingine , tunaweza kusema kuwa uchafuzi wa mazingira ni uharibifu wa vile
    vitu vinavyowazunguka binadamu na wanyama maishani mwao. Kuna uchafuzi wa aina mbalimbali na kila uchafuzi humhusu binadamu kwa njia fulani.
    Maendeleo ya viwanda duniani ni sababu mojawapo ya uchafuzi wa hewa. Mitambo katika karakana huwa inatoa moshi mwingi wakati bidhaa zinapotengenezwa. Moshi husambaa eneo kubwa na kuchanganyika na hewa inayovutwa na binadamu. Uchafu hutupwa ovyo ovyo na kuwa hatari kwa afya ya binadamu. Maji machafu huweza kutiririkia mtoni, maziwani na hata baharini. Yale yanayotiririka mitoni na maziwani huchafua maji ambayo hutumiwa na watu wa eneo hilo kwa kunywa, kupika na kunywesha mifugo wao. Yale yanayotiririka baharini huwa ni hatari kwa samaki wanaotegemewa na binadamu kuwa kitoweo muruwa.
    Ongezeko la watu pia ni hali nyingine ya uchafuzi wa mazingira. Halaiki ya watu hufanya
    uharibifu wa misitu ya asili. Hii ni kwa sababu ya kutaka kuongeza ekari za mashamba. Hili husababisha mmomonyoko wa udongo ; hivyo basi kuiacha ardhi bila rutuba yoyote. Katika hali hii, kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa nchi nyingi duniani huzoroteshwa. ‘‘Maisha ya binadamu hutegemea kilimo kwa kila hali kwa hivyo kilimo kinapozoroteka hata uchumi nao huathirika. Kila uchao tunasikia kwamba nchi fulani imekabiliwa na njaa.
    Ufugaji wa wanyama wengi bila mpango maalum pia huharibu mazingira ya asili kama nyasi na vichaka. Watu wengi hufuga ng’ombe, mbuzi na kondoo. Kwa kuwa hawana mahali maalum pa kuwalisha, huzunguka nao huku na huko kutafuta nyasi na majani ya kuwalisha. Wanyama wanaotangishwatangishwa namna hiyo humaliza majani na nyasi zote na kuacha ardhi tupu ambayo hatimaye huyabisika kwa jua. Ardhi ya namna hii haishiki maji mvua inyeshapo. Nchi iliyoneemeka huweza kuwa jangwa lililo na chungu ya mchanga.
    Watu wanapoongezeka huko mashambani huwabidi wakate misitu ili waanzishe maskani mapyapamoja na mashamba yao. Miti hukatwa bila hadhari na mabiwi ya matawi pamoja na majani huchomwa moto. Jambo la kusikitisha ni kwamba miti hiyo inapokatwa hakuna mingine inayopandwa kuchukua mahali pake.
    Mahitaji ya binadamu ya kuendeleza njia za mawasiliano pia huzusha balaa nyingine. Barabara zinazidi kuongezeka na pia watu wanaozidi kuongezeka pamoja na mazao yao. Kwanza, barabara zinapotengenezwa misitu hukatwa mahali zinapopitia. Pili, wingi wa magari huzidi na baadhi ya hayo hutoa moshi unaoharibu hewa.
    Njia kadha wa kadha za kuzuia uharibifu wa mazingira zimependekezwa. Ingawa suluhisho timamuhalijafikiwa, Serikali nyingi duniani zimo katika harakati za kutafuta suluhisho la uchafuzi huo.
    Njia mojawapo ni kukomesha ujenzi wa viwanda katika miji mikuu na mahali palipo na watu wengi.Wenye viwanda pia wanahimizwa kufikiria jinsi ya kutupa takataka na maji machafu bila kudhuru afya ya binadamu.
    Watu wakizingatia suala la upangaji wa uzazi na kuwa na familia ndogo ndogo, idadi ya watu haitaongezeka kwa kasi kwa hivyo itakuwa hakuna haja ya kuanzisha makao mapya mara kwa mara.
    Serikali nyingi zimechukua jukumu la kuwaelimisha raia juu ya madhara yanayotokana na uharibifuwa mazingira. Raia wanahimizwa kupanda miti kwa wingi.
    Jitihada zinazofanywa kuzuia uchafuzi wa mazingira hukumbana na matatizo. Tatizo kubwa ni fedha za kuendeleza miradi inayopendekezwa. Shida nyingine ni kwamba juhudi zingine huwa zinamwingilia binadamu na mali yake.
    Maswali.
    (a) Fupisha aya za kwanza sita za taarifa uliyosoma (maneno 50-60)
    (b) Fupisha aya za mwisho tano kwa maneno 40-45

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Kanusha sentensi ifuatayo; Angalimpata babu yangu angalimpeleka hospitalini. (Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo;
    Angalimpata babu yangu angalimpeleka hospitalini.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Bainisha aina za virai vilivyopigiwa mistari. Uchochole wa kijinsia umepigwa marufuku na kiongozi mwenye msimamo dhabiti mno. (Solved)

    Bainisha aina za virai vilivyopigiwa mistari.
    Uchochole wa kijinsia umepigwa marufuku na kiongozi mwenye msimamo dhabiti mno.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi yenye muundo ufuatao KN(N+S)+KT(T+E+E) (Solved)

    Tunga sentensi yenye muundo ufuatao
    KN(N+S)+KT(T+E+E)

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Iandike sentensi ifuatayo upya katika hali yakinishi. Hapo napo sipo nitakapo. (Solved)

    Iandike sentensi ifuatayo upya katika hali yakinishi.
    Hapo napo sipo nitakapo.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)