Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Tumia neno kitoto kama; i) kivumishi ii) kielezi

Tumia neno kitoto kama;
i) kivumishi
ii) kielezi

Answers


sharon
i) Ana tabia za kitoto.
ii) Anacheka kitoto.
sharon kalunda answered the question on October 4, 2019 at 13:19

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Taja na ueleze pingamizi zozote tano zinazokwamiza juhudi za kukuza Kiswahili (Solved)

    Taja na ueleze pingamizi zozote tano zinazokwamiza juhudi za kukuza Kiswahili

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi hii kwa kutumia kielelezo cha visanduku. Mzee aliyemdhulumu msichana yule ametiwa mbaroni tena. (Solved)

    Changanua sentensi hii kwa kutumia kielelezo cha visanduku.
    Mzee aliyemdhulumu msichana yule ametiwa mbaroni tena.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza juhudi zozote tano za serikali ya Kenya katika kukuza Kiswahili (Solved)

    Eleza juhudi zozote tano za serikali ya Kenya katika kukuza Kiswahili

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi sahihi ukitumia kitenzi — nywa katika kauli ya kutendesha (Solved)

    Tunga sentensi sahihi ukitumia kitenzi — nywa katika kauli ya kutendesha

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Yakinisha sentensi hii Mpishi asipokuwa mwangalifu chakula hakitaiva vizuri (Solved)

    Yakinisha sentensi hii
    Mpishi asipokuwa mwangalifu chakula hakitaiva vizuri

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Uchumi wa soko huria ni hali ya kiuchumi ambapo itokeapo amali, shughuli na harakati zote za kiuchumi ghairi ya zile... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

    Uchumi wa soko huria ni hali ya kiuchumi ambapo itokeapo amali, shughuli na harakati zote za kiuchumi ghairi ya zile ambazo ni za lazima kwa serikali au dola kama ulinzi, sheria na
    mpangilio wa jamii huwa huria kwa watu binafsi. Msingi wa soko huria, sifa kuu ya utandawazi, ni kuibua na kudumisha mazingira na hali zinazochochea na kumruhusu mtu yeyote kuongozwa na hawaa, au matamanio ya kibiashara anayoyaona sawa pasi na hofu ya kuingilia na udhibiti wa serikali.
    Mazingira hayo yanawapa watu satua ya kufanya maamuzi kuhusu hatima yao ya kiuchumi, uamuzi kuhusu suala la ajira yao, matumizi ya mtaji kipato na harija zake, na uwekezaji mzima. Suala mojawapo linaloibuka kuhusiana na mfano wa soko huria ni kuweka mipaka bainifu na wazi baina ya amali na shughuli zinazohusishwa na serikali na zile ambazo huachwa huria kwa watu. Kwa mfano, inaaminiwa kuwa haki ya kuishi na kulindwa dhidi ya shambulizi, liwe la kijambazi au la kigaidi, ni ya kimsingi ambayo haiwezi kuhusishwa na uwezo wa kiuchumi wa mtu binafsi. Aidha huduma za kimsingi za afya nazo zinaingia katika kumbo hili. Ikiwa huduma hizi zitaachwa huria pana uwezekano mkubwa kuwa zitaishia kuwa istihaki ya wenye mtaji na kipato cha juu tu.
    Licha ya kuwepo kwa sheria au kanuni huria kutoka nyanja maalum, hutokea hali ambapo adhibiti wa kiserikali ni lazima. Hii hutokea pale ambapo ipo haja ya kuyalinda mazingira hasa kutokana na uchafuzi wa viwanda au tasnia. Aidha udhibiti huo ni lazima pale ambapo haki za watu wengine zinahusika: yaani ikiwa uhuru wa hata mtu mmoja unaadhirika kutokana na sera hizo pana haja ya kuingilia ili kuisawazisha hali yenyewe.
    (a) Andika kwa muhtasari maana ya uchumi wa soko huria kulingana na taarifa hii.
    (maneno 25-30)
    (b) Eleza mawazo makuu yanayojitokeza katika aya ya pili na ya tatu.
    (maneno 70-75)

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Toa maana ya semi Shupaa mwili. (Solved)

    Toa maana ya semi Shupaa mwili.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Taja dhamira ya sentensi ifuatayo Kimbia mbio ulete sahani (Solved)

    Taja dhamira ya sentensi ifuatayo
    Kimbia mbio ulete sahani

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Akifisha sentensi ifuatayo iii ilete dhana tatu tofauti; Fatuma Khamisi mjukuu wa Rashid na Rehema wametoroka shule (Solved)

    Akifisha sentensi ifuatayo iii ilete dhana tatu tofauti;
    Fatuma Khamisi mjukuu wa Rashid na Rehema wametoroka shule

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi yenye muundo ufuatao KN(N+S)+KT(T+E+E) (Solved)

    Tunga sentensi yenye muundo ufuatao
    KN(N+S)+KT(T+E+E)

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Iandike sentensi ifuatayo upya katika hali yakinishi. Hapo napo sipo nitakapo. (Solved)

    Iandike sentensi ifuatayo upya katika hali yakinishi.
    Hapo napo sipo nitakapo.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Tumia maneno yafuatayo katika sentensi moja ili kubainisha tofauti zao kimaana; i) Chuuza ii) Chuza (Solved)

    Tumia maneno yafuatayo katika sentensi moja ili kubainisha tofauti zao kimaana;
    i) Chuuza
    ii) Chuza

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza tofauti kati ya ama za vielezi vifuatavyo; i) Vielezi vya namna mfanano na; Vielezi vya namna hali. ii) Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia vielezi vya hapo... (Solved)

    Eleza tofauti kati ya ama za vielezi vifuatavyo;
    i) Vielezi vya namna mfanano na;
    Vielezi vya namna hali.
    ii) Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia vielezi vya hapo juu.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Andika sentensi moja ukitumia kivumishi cha nomino. (Solved)

    Andika sentensi moja ukitumia kivumishi cha nomino.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Jadili sababu tano zinazofanya "sheng" isiwe lugha ya taifa. (Solved)

    Jadili sababu tano zinazofanya "sheng" isiwe lugha ya taifa.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya; i).Mkembe. ii).mkebe. (Solved)

    Eleza maana ya;
    i).Mkembe.
    ii).mkebe.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Uwezo wa kuyakumbuka mambo ni hazina kuu kutoka kwa mtu yeyote yule aliye hai. Uwezo huu wa kukumbuka ni mojawapo ya... (Solved)

    Soma taarifa kisha fupisha kwa mujibu wa maswali yafuatayo.

    Uwezo wa kuyakumbuka mambo ni hazina kuu kutoka kwa mtu yeyote yule aliye hai. Uwezo huu wa kukumbuka ni mojawapo ya shughuli changamano za ubongo. Ubongo wa mwanadamu hutekeleza shughuli hii kwa namna tatu. Kwanza ubongo hunasa jambo kisha
    huliihifadhi. Baadaye huanzisha mfumo wa kutoa kilicho hifadhiwa. Ubongo ukiathirika kwa
    namna yeyote katika moja wapo ya njia hizi, basi uwezo wa kuyakumbuka mambo huvurugika.
    Ingawa inaaminika kuwa uwezo wa kukumbuka hurithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine, wataalamu wa maswala ya kiakili wanabaini kuwa uwezo huu unaweza kuimarishwa.
    Uimarishaji huu huhitajika mikakati madhubuti.
    Njia mojawapo ya kustawisha uwezo wa kukumbuka ni kupitia kwa lishe. Vyakula vilivyosheheni vitamini B vyenye amino asidi husaidia kuimarisha uwezo wa kukumbuka. Vyakula kama hivi ni mboga, nyama (hasa maini), bidhaaa za soya, matunda, maziwa, ,bidhaa za ngano, samaki, pamoja na mayai. Vyakula vingine muhimu katika ustawishaji huu ni vile vyenye madini ya chuma. Madini haya huwezesha usambazaji wa hewa katika ubongo kwa wepesi. Vyakula ambavyo vina madina haya ni mboga za kijani, mawele, ndengu, soya, matunda kama maembe, ufuta (simsim) pamoja na nyama, hasa maini na mayai.
    Ubongo wa mwanadamu aliye hai hufanya kazi kila wakati awe macho au amelala. Utendaji kazi wake huendeshwa na glukosi mwilini. Kwa hivyo, vyakula vyenye sukari hii ni muhimu kuliwa. Hata hivyo, lazima mtu awe mwangalifu na kuhakikisha kuwa mwili una kiwango cha sukari kisicho hatarisha maisha. Haya yanawezekana kwa kula vyakula vyenye nyuzinyuzi kama vile mboga na matunda.
    Njia ya pili ni kupiga marufuku vileo kama pombe na nikotini. Vileo hivi huathiri utaratibu wa kunasa, kuhifadhi na kutoa yaliyo ubongoni.
    Iwapo mtu ana tatizo la kuyakumbuka majina ya watu, ni muhimu kufanya mazoezi ya
    kusikiliza kisha kurudia majina hayo wakati wa mazungumzo. Ni bora kulihusisha jina na sura
    ya mtu. Kwa njia hii ubongo utanasa jina na kile kinacholengwa.
    Woga na kuvurugika kiakili ni mambo mengine tunayopaswa kuepuka kila wakati. Ni kawaida mtu kupata woga wakati anapokabili jambo asilokuwa na uhakika na matokeo yake kama mtihani au mahojiano. Lakini anapaswa kuwa makini. Woga huo usikiuke mpaka na kumvuruga kiakili. Vurugu hizi huathiri kilichohifadhiwa ubongoni na pia namna ya kukitoa.
    Halikadhalika, mwili wenye siha nzuri huhakikisha kuwa ubongo ni timamu. Wataalamu wengi wa siha wanakubali kuwa na mazoezi ya kunyoosha viungo hustawisha ubongo na hivyo kuhakikisha kuweko kwa uwezo wa kukumbuka mambo. Ni muhimu kuwa na taratibu ya kunyoosha viungo kila wakati. Fauka ya hayo, mazoezi ya kiakili, kama vile kusoma makala yanayovutia, kujaza mraba na michezo mingine kama mafumbo, vitenzi ndimi ni muhimu katika kustawisha uwezo wa kukumbuka.
    Jamii ya watu wenye uwezo kuyakumbuka mambo ni ya jamii iliyopiga hatua kimaendeleo. Ni jukumu la kila mmoja wetu kuimarisha uwezo wa kukumbuka kila wakati.

    a) Kwa maneno 60 – 65 fupisha mchango wa chakula katika uimarishaji wa uwezo wa
    kukumbuka.
    b) Fupisha aya tatu za mwisho kwa maneno 80 – 90

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Toa maneno yenye maana sawa na haya. i. Izara ii. Anisi (Solved)

    Toa maneno yenye maana sawa na haya.
    i. Izara
    ii. Anisi

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi. Atanishughulikia vizuri. (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi.
    Atanishughulikia vizuri.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya nahau zifuatazo: i) Furaha ghaya ii) Maneo yalimkata maini. (Solved)

    Eleza maana ya nahau zifuatazo:
    i) Furaha ghaya
    ii) Maneo yalimkata maini.

    Date posted: October 4, 2019 .    Answers (1)