Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Tambua sauti yenye sifa zifuatazo. konsonanti, kipasuo, ghuna, sauti ya mdomo.

      

Tambua sauti yenye sifa zifuatazo.
konsonanti, kipasuo, ghuna, sauti ya mdomo.

  

Answers


Kavungya
/b/
Kavungya answered the question on November 25, 2022 at 07:18


Next: Taja ala sogezi mbili za kutamkia.
Previous: Tunga sentensi moja na uonyeshe nomino dhahania.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Taja ala sogezi mbili za kutamkia.(Solved)

    Taja ala sogezi mbili za kutamkia.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali FUNGUA SESAME Jina la Nimrod lilipotea mara tualipoanza kufanya kazi jijini Nairobi.(Solved)

    Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali
    FUNGUA SESAME
    Jina la Nimrod lilipotea mara tualipoanza kufanya kazi jijini Nairobi. Marafiki na jamaa zake
    waliamini kuwa alikuwa ameajiriwa huko mjini ingawa hakuna aliyeijua kazi yenyewe vizuri.
    Hata hivyo waliamini kuwa lazima alikuwa na kibonge cha kazi kwa sababu alivalia kinadhifu na
    kuishi maisha ya starehe. Tena yeye mwenyewe alikazania kusema kuwa amejiriwa kazi ya
    maana. Marafiki zake walimfahamu kama “Bwana Sesame”. Mtu wa kwanza aliyempa jina hilo
    alisema alipendezwa na ujuzi na maarifa yake. “huyu hakosi ufumbuzi wa tatizo lolote. Ni kama
    ule mlango wa kisa cha Ali Baba na Wezi arobaini. Ukisema ‘fungua Sesame’ unafungu katu,”
    alisema mtu huyo.
    Jamaa walioishi naye katika mtaa wa Urumo walishangazwa na utaratibu wake wa kazi. Mchana
    kutwa alishinda chumbani mwake. Mara nyingi utamkuta ametulia akitazama runinga yake
    ndogo. Wakati mwingine atakuwa akifanya kazi yake ndogo ndogo huku akipiga mluzi bubu,
    ambao haukusikika vizuri. Wakati mwingine atakuwa akiusikiliza muziki kwenye chombo chake
    cha muziki kilichotingisha jingo zima kutokana na sauti yake nene.
    Kwa kawaida alitoka chumbani jioni. Waliomjua walimchangamkia kutokana na
    uchangamfu wake. Alipenda sana mizaha. Waliopenda kupiga soga walivutiwa na maongezi
    yake hasa kuhusiana na magari. Aliyajua magari mengi. Mimi naweza kuijua aina ya gari kwa
    kuusikiliza mlio wake tu”, alisema kila wakati. “wacha kutuvungavunga Bwana wee,
    haiwezekani !” atasema mwingine. “nini? Unajua mimi ndiye Bwana Sesame mwenyewe!”
    atasema, halafu wote wataangua kicheko.
    Ilifika wakati kampuni kadha zilipoamua kuwapunguza wafanyakazi wake kutokana na hali
    mbaya ya kiuchumi. Lakini Bwana Sesame hakuwa mmoja wa hao. Hali yake ilibakia vile vile.
    Aliendelea kuvalia kinadhifu na kuishi maisha yake ya fawaishi. Wakati wenzake wanalalamikia
    hali ngumu ya maisha, Bwana Sesame hakuwa na lolote la kumsumbua. Aliendelea kukaa bila
    kazi wala bazi. Lakini watu walitambua kuwa alikua na mazoea yakutoka chumbani majira ya
    jioni. Hakuna aliyejua alirejea lini.
    Sikumoja Bwana Sesame alitoka jioni kama kawaida na kuelekea kwenye shughuli zake za
    kawaida. Siku hiyo jamaa mmoja wa mtaani alikumbana naye kwenye lango kuu. “Bwana
    Sesame,leo wapi yahe?alimwuliza. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, “natoka nje kidogo
    yahe. Jiji hili lataka ustaarabu,’ alijibu. Yule jamaa alimwangalia na kumwabia, “nina shida
    kidogo, sijui kama utanifaa mwenzangu. Wajua tena hali zenyewe siku hizi,” alisema. Nini
    tena?’ aliuliza Bwana Sesame.
    “Nina gari langu ambalo halina redio. Natafuta moja ya bei nafuu.... Kitu kama sony hivi,”
    alisema. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, “hiyo kazi nyepesi kwangu yahe, papai kwa
    kijiko!” alisema Bwana Sesame akicheka. Jamaa Yule alishukuru na wakaagana.
    Bwana Sesame alishika njia kuelekea sehemu zake za kawaida majira kama haya.Naye Yule
    jamaaa kapinda kama anaangalia mtaani, lakini baada ya muda akageuka na kuamua kumfuata
    Bwana Sesame.
    Bwana Sesame alishika tariki mpaka sehemu ya mazoea. Yule jamaa alimfuata kwambali na
    mwendo wa paka. Alimwona Bwana Sesame akiingia mahali palipokuwa na banda kuukuu.
    Muda si muda alitoka na jamaa wengine wakiwa wamevalia maguo ya ajabu. Yule jamaa
    aliwafuata hadi mahali palipokuwa na ujia mwembamba ulioachana na barabara kuu. Alijificha
    mahali, na kutokana nahali ya sehemu ile akawa haonekani.
    Muda si muda palitokeza gari dogolililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja. Bwana
    Sesame na wenzake walitokeza na kutupa gogo lililomzuia Yule mwanamke.
    Ghafla bin vuu walimvamia; wakaifungua milango ya gari mbio na kujivurumisha ndani. Gari
    lilitimuliwa kama risasi kuelekea upande wa pili. Wakati huo Yule jamaa ashaliangalia gari
    lenyewe na kuzihifadhi nambari zake. Alishika njia kurudi zake chumbani.
    Siku iliyofuata huyo jamaa hakuwa kazini. Alipokuwa akifungua kinywa alisikia sauti ya
    kugongwa kwa mlango. Aliinuka na kwenda kuufungua. Bwana Sesame aliingia ndani. “vipi
    yahe? Hujenda kazini leo? Au umelala sana Bwana?’ alisema Bwana Sesame kwa uchangamfu
    wake. Muda si muda alimwonyesha redio ya gari aliyokuwa nayo. “umeipata mara moja hii
    kumbe?’ aliuliza Yule jamaa. “si nilikwambia yahe! Mimi ndiyeBwana Sesame mwenyewe. Hii
    kwangu si kazi. Ninafahamiana na jamaa wengi wanaoifanya kazi hii,” alisema Bwana Sesame.
    “naona kweli. Ehh Bwana we! Ndipo waswahili wakasema,ukitaka kuvua vua na wavuvi!
    Alisema Yule jamaa. “ni kweli kabisa!’” alijibu Bwana Sesame huku akicheka kwa furaha.
    Yule jamaa alisimama kuelekea chumbani. Bwana Sesame alitulia akisubiri kupokea ujira
    wake. Muda mfupi ulipita, kasha mlango wa nyumba ukagongwa. “yahe Bwana, kunagogwa
    huku!” Bwana Sesame akasema. Yule jamaa alitoka chumbani na kuelekea mlangoni. Mlango
    ulipofunguliwa waliingia askari polisi wawili. Bwana Sesame hakuwa na upenyu wakutokea.
    Alitiwa mikononi.Hakujua kumbe Yule jamaa alikuwa kachero. Hapakuwa na ujanja tena. Siku
    hiyo pwagu alipata pwaguzi. Fungua Sesame haikufaa tena.

    Maswali
    1. Kwa nini Nimrod alibatizwa ‘Bwana Sesame’?
    2. Kwa nini watu walioishi mtaani Urumo walishangazwa na utaratibu wa kazi wa Bwana
    Sesame?
    3. Unafikiria ni kwanini Bwana Sesame alifahamu sana juu ya magari?
    4. Je, unafikiri yule jamaa aliagiza aletewe radio alikuwa na haja sana na kifaa hicho kama
    alivyosema?
    5. Bwana Sesame alikuwa kachero. Unakubali? Toa maelezo?
    6. Yule jamaa alipoingia chumbani na kumwancha Bwana Sesame sebuleni unafikiria
    alikwenda kufanya nini
    7. Je, hadithi hii ina mafunzo gani kwako?
    8. Eleza maana ya misemo ifuaayo kasha itumie katika sentensi
    a) Piga mluzi
    b) Piga soga
    c) Shika tariki

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Taja vipera vitano vya semi.(Solved)

    Taja vipera vitano vya semi.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma dondoo lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata. Mwatani: Rusha hiyo ball haraka tumechelewa five minutes. Twende daro. Omoshi: Harakisha mode anacome.(Solved)

    Soma dondoo lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata.
    Mwatani: Rusha hiyo ball haraka tumechelewa five minutes. Twende daro.
    Omoshi: Harakisha mode anacome.
    Bwana Kipiti: Nendeni darasani haraka! Kisha kiranja awape vitabu vyenu vya insha
    ili mwandike barua.
    Mwatani: Sawa mwalimu. Samahani kwa kuchelewa uwanjani.
    Omoshi: Je, tutaandika barua rasmi au barua ya kawaida?
    Bwana Kipiti: Mwandike barua rasmi. Je, mnakumbuka muundo wake?
    Omoshi na Mwatani: Ndio mwalimu. Ulitufundisha jana. Asante sana mwalimu.
    Bwana Kipiti: Kumbukeni idadi ya maneno. Idadi ya maneno ni muhimu katika uandishi
    wa insha.

    (i) Eleza sajili katika dondoo.
    (ii) Eleza sifa nane za sajili hii zinazopatikana katika dondoo.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Ainisha vielezi katika katika sentensi ifuatayo. Mwanafunzi mzuri ni yule afanyaye mazoezi vizuri kila siku shuleni.(Solved)

    Ainisha vielezi katika katika sentensi ifuatayo.
    Mwanafunzi mzuri ni yule afanyaye mazoezi vizuri kila siku shuleni.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tumia o-rejeshi kati katika sentensi ifuatayo. Kuta ambazo zilijengwa zimebomoka.(Solved)

    Tumia o-rejeshi kati katika sentensi ifuatayo.
    Kuta ambazo zilijengwa zimebomoka.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Kamilisha methali ifuatayo. Asiye na nadhari...(Solved)

    Kamilisha methali ifuatayo.
    Asiye na nadhari...

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika kwa wingi. Kuwepo kwa mshauri wake kulimfurahisha waziri.(Solved)

    Andika kwa wingi.
    Kuwepo kwa mshauri wake kulimfurahisha waziri.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Badilisha kitenzi kisaidizi kilicho kwenye sentensi ifuatayo kiwe kishirikishi. Mvule alikuwa akilala bwenini.(Solved)

    Badilisha kitenzi kisaidizi kilicho kwenye sentensi ifuatayo kiwe kishirikishi.
    Mvule alikuwa akilala bwenini.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo katika ukubwa. Uteo alionunuliwa umezeeka sana.(Solved)

    Andika sentensi ifuatayo katika ukubwa.
    Uteo alionunuliwa umezeeka sana.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Yakinisha: Usipolipa usiingie ndani.(Solved)

    Yakinisha:
    Usipolipa usiingie ndani.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja moja kudhihirisha matumizi ya i. Posa ii. Poza(Solved)

    Tunga sentensi moja moja kudhihirisha matumizi ya
    i. Posa
    ii. Poza

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi katika hali ya kuamrisha wingi. Kimbia haraka – Amka -(Solved)

    Kanusha sentensi katika hali ya kuamrisha wingi.
    Kimbia haraka –
    Amka -

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi yenye kivumishi cha jina.(Solved)

    Tunga sentensi yenye kivumishi cha jina.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tambulisha na ufafanue viambishi vilivyotumika katika Anamfundisha.(Solved)

    Tambulisha na ufafanue viambishi vilivyotumika katika Anamfundisha.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi ifuatayo kwa umoja. Nywele zenu hukatika mnapoachana.(Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo kwa umoja.
    Nywele zenu hukatika mnapoachana.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Huku ukitoa mifano taja miundo ya silabi.(Solved)

    Huku ukitoa mifano taja miundo ya silabi.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Sauti /p/ ni kipasuo, sauti hizi ni gani? i. / f / ii. / l /(Solved)

    Sauti /p/ ni kipasuo, sauti hizi ni gani?
    i. / f /
    ii. / l /

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma taarifa ifuatayo kasha ujibu maswali Ilikuwa Jumamosi. Nilifika nyumbani kwangu saa moja jioni. Tangu nistaafu miaka miwili awali sikupenda kuchelewa Taarifa ya Habari.(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kasha ujibu maswali
    Ilikuwa Jumamosi. Nilifika nyumbani kwangu saa moja jioni. Tangu nistaafu miaka miwili
    awali sikupenda kuchelewa Taarifa ya Habari.
    Mwezi mmoja ukawa umepita tangu nipewe pesa za kiinua mgongo. Mwezi mmoja mzima
    nilikuwa katika shughuli za kulipa deni hapa na kulipa karo huku. Kuwekeza kwenye mradi ule na
    kununua hili. Sasa shilingi laki mbili tu zilikuwa zimesalia katika benki.
    Watu wengi walinishawishi nijaribu kilimo cha mahindi. Bei ilikuwa imeanza kuimarika.
    Katika taarifa ya habari jioni hiyo, Waziri wa kilimo alitangazaa bei mpya , shilingi 1,500 kwa kila
    gunia. Nami nilikuwa naanza kuumakinikia mradi huu.
    Baada ya taarifa, nilioga nikala na nikaenda kulala. Kwa sababu ya uchovu, usingizi
    ulinichukuwa mara moja. Usingizini niliota. Katika ndoto niliutekeleza mradi wangu. Msimu huo wa
    kulima nilitenga hekari kumi za shamba langu. Wataalamu walinishauri kuwa wakati mzuri wa kulima
    ni wa kiangazi. Mwezi wa Januari ulipoanza tu nilitafuta trekta na kulima. Malipo yalikuwa shilingi
    1,200 kila ekari. Katikati ya mwezi wa Mechi, nilitafuta trekta la kutifua shamba tena kwa gharama ya
    shilingi 15,000 ekari zote kumi. Kufuatia ushauri wa manyakanga wa kilimo, nililipa shilingi elfu
    kumi na tatu kupiga shamba lote haro.
    Mwishoni mwa mwezi huo, nilienda mjini kutafuta pembejeo. Kwanza, nililipa shilingi 20,500
    kwa magunia 15 ya mbolea. Kisha nilinunua magunia manne ya mbegu ya mahindi yenye uzani wa
    kilo 25 kwa shilingi 3,300 kila gunia. Mwezi wa Aprili ulipotimia tu, niliamua kupanda ili nipate mazao
    bora, nilipanda kwa tandazi. Gharama ilikuwa shilingi 1,000 kila ekari. Mvua ilinyesha vizuri na baada
    ya siku saba, mahindi yalianza kuota. Ilifurahisha kuhesabu mistari ya kijani iliyonyooka. Hali hii
    iliwezekana tu baada ya kuajiri vijana wa kuwafukuza korongo na vidiri ili wasifukue mbegu
    mchangani.
    Baada ya mwezi mmoja, hatua ya kupalilia ilifika. Nilitafuta vibarua wa kupalilia. Malipo
    yalikuwa shilingi 700 kila ekari. Kumbe kupalilia kulichochea mtifuko wa mahindi. Punde yakawa
    yananifikia magotini. Hii ikawa ishara kuwa yanahitaji kumwagiwa mbolea ya kunawirisha iitwayo
    ‘amonia’. Gharama yake ikawa shilingi 1,300 kila gunia. Hivyo , nikalipa shilingi 19,500 kwa magunia
    kumi na matano.
    Mahindi yalibadilika kimiujiza. Ghafla tu yalirefuka na kunenepa mashina. Yalibadilika rangi
    yakapiga weusi. Shamba liligeuka likawa kama msitu wa rangi ya kijani iliyokolea. Wapita njia
    waliajabia mimea na juhudi zangu. Shamba langu sasa likawa kielelezo. Maafisa wa kilimo wakawa
    kila siku wanawaleta wakulima wengine kujifunza siri ya ufanisi wangu. Hapo nikaanza kuhesabu
    mavuno nitakayopata na kukadiri faida. Nilipuuza kabisa ushauri wa wahenga kuwa ‘Usikate majani,
    mnyama hajauawa.’
    Bila taarifa wala tahadhari mvua ilitoweka. Hayakupita majuma mawili mahindi yakaanza
    kubadilika. Juma moja baadaye mahindi yalinyauka. Badala ya mahindi, shamba likageuka la vitunguu
    vilivyochomwa na jua. Makisio yangu ya faida yaliyeyuka jinsi ufanyavyo moshi.
    Lakini ‘Muumba ndiye Muumbua.’Siku moja mawingu yalitanda na mvua ikanyesha , muda si
    muda mahindi yalianza kunawiri. Kumbe tukio lililowavunja moyo lilikuwa laja. Siku moja mvua
    kubwa ilinyesha. Asubuhi nilipotoka nje nilipigwa na butwa. Barafu ilitapakaa pote. Shamba lilikuwa
    limetapakaa barafu nafuu. Nilipotazama upande wa shamba niliona dalili za majani mapya ya mahindi
    yakianza kuchomoza. Maumbile ni kitu cha ajabu kweli.
    Muda si mrefu mahindi yalirudia hali yake tena, kasha yakakomaa. Harakati za kutafuta watu
    wa kuyakata na kuyakusanya zilianza. Gharama ya shughuli hii ikawa shilingi 5,000 kuvuna kusafirisha
    kutoka shamba na kukoboa kwa mashine magunia 200 yakachukua shilingi 20,500. Kufikia hapo
    nilikuwa nimetumia takribani shilingi 192,700. Gharama nyingine zilikuwa za usafiri, gharama ya
    dharura na usimamizi, usumbufu wangu binafsi, gharama ya magunia na kadhalika. Mahindi
    yalipokuwa tayari kwenye magunia nilifunga safari kwenda mjini kutafuta soko. Niliposhuka tu niliona
    gazeti. Habari motomoto siku hiyo ilikuwa ‘MAHINDI GUNIA 900/=’ Niligutuka usingizini.

    MASWALI
    a) Ni changamoto zipi zinazokumba kilimo.
    b) Msimulizi alikuwa na kiasi gani cha pesa katika benki baada ya mradi kukamilika?
    c) Eleza maana ya methali zifuatazo kwa mujibu wa makala.
    i. Usikate majani, mnyama hajauawa.
    ii. Muumba ndiye Muumba.
    d) Eleza mambo mawili yaliyosababisha msimulizi asipate faida alivyotarajia.
    e) Kwa nini msimulizi alisema maumbile ni kitu cha ajabu?
    f) Eleza maana ya:
    i. Kiinua mgongo
    ii. Manyakanga wa kilimo.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Bainisha nomino katika utungo huu. Watoto wameenda kucheza.(Solved)

    Bainisha nomino katika utungo huu.
    Watoto wameenda kucheza.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)