Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Kwa kutolea mifano tambua njia tofuati za kuunda maneno katika lugha ya kiswahili

Kwa kutolea mifano tambua njia tofuati za kuunda maneno katika lugha ya kiswahili

Answers


KELVIN
? Nomino kutokana na mzizi wa kitenzi
a) danganya-kudanganya, mdanganyifu,udanganyifu
b) soma-kusoma, masomo,msomi,usomaji
c) unda-kuunda, muundaji,uundaji,muundo
d) funika-kufunika, kifuniko, mfunikaji, ufunikaji
? Kitenzi kutokana na mzizi wa nomino
a) mlo-kula
b) mlevi-kulewa, kulevuka
c) mwimbaji-kuimba
d) fikra-kufikiri
e) malezi-kulea
f) fumbo-kufumba, kufumbua
? Nomino kutokana na mzizi wa nomino
a) mwimbaji-kuimba, wimbo, uimbaji, kiimbo
b) mchezo-kucheza, uchezaji, mchezaji
c) ulaghai-kulaghai, mlaghai
d) hesabu-kuhesabu,uhesabu
e) mdhalimu- kudhulumu, dhuluma, udhalimu
? Nomino kutokana na mzizi wa kivumishi
a) -refu-mrefu, urefu, urefushaji
b) -baya-mbaya, ubaya
c) -zuri-mzuri, uzuri
d) -kali-mkali, ukali
e) -eupe-mweupe,weupe
? Kivumishi kutokana na mzizi wa nomino
a) ujinga -jinga
b) werevu -erevu
c) mzuri -zuri
d) mpumbavu -pumbavu
e) mpyoro -pyoro
? Kitenzi kutokana na mzizi wa kivumishi
a) haramu-kuharamisha, kuharamika
b) halali-kuhalalisha, kuhalalika
c) -fupi-kufupisha, kufupika
d) bora-kuboresha, kuboreka
e) -refu-kurefusha, kurefuka
f) sahihi-kusahihisha, kusahihika
g) -sikivu-kusikia
h) -danganyifu-kudanganya
? Kivumishi kutokana na mzizi wa kitenzi
a) dunisha - duni
b) Haramisha - haramu
c) fupisha -fupi
d) sahilisha -sahili
e) tukuka -tukufu
f) fahamu -fahamivu
g) teua -teule
h) nyamaza -nyamavu
i) ongoka -ongofu
j) sahihisha -sahihi
k) danganya -danganyifu
? Kitenzi kutokana na kielezi
a) haraka-harakisha
b) zaidi-zidisha
c) bidii-bidiisha
d) hima-himiza

kalvinspartan answered the question on August 10, 2018 at 08:16

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions