Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Eleza maana tatu za neno chungu kama lilivyotumika katika shairi

1.Kijana tuza makini, nikwambie usikile
Chakula mahotelini, si kizuri usikile
Ufikapo mlangoni, kizingiti usikile

2. Nenda kaseme nyumbani, kesho asubuhi siji
Nitakwenda makondeni, kawashunge shunge siji
Na hata hapo jioni, kama nitakuja siji

3. Na kama wenda mjini, upatapo nyumba panga
Upahame mizimuni, palozingirwa na panga
Hapana tena amani, kutwa mwapigana panga

4. Na kesho kija shambani, uonapo mti panda
Kwea hadi kileleni, ujifiche kwenye panda
Kaziyo ulinde chini, mimea tuliyopanda

5. Kishuka ola shinani, njugu merundika chungu
Njugu peleka nyumbani, zisije zikawa chungu
Kaanga sufuriani, au pia kwenye chungu

6. Kileta maji jioni, ndoo jitwike na kata
Kata njema ya majani, laini wezayo kata
Kumbuka ya kisimani, huteki ela kwa kata

7. Ninawahi kibandani, nikaliezeke paa
Nipate lindia nyuni, na wanyama kama paa
Kwani kiola angani, naona jua lapaa

8.Kisha takwea mtini, nimeona bivu tunda
Sina usono moyoni, ela tunda kisha tunda
Nimpe wangu mwendeni, jioni nishike tunda

9.Meanza wao uneni, hapo nami ndipo kamba
Leo wenda hawaoni, kama wa bahari kamba
Wajijaza kimiani, wakijitatia kamba

10. Mtoto wachoma yakini, japo liwe moja kaa
Ukikupata takoni, ni shida huwezi kaa
Ela hufaa mekoni, kutoka nswi na kaa


Eleza maana tatu za neno chungu kama lilivyotumika katika shairi

Answers


Maurice
Maana za neno ‘chungu’

(i) Tele/ ingi

(ii) Chachu

(iii) Kifaa cha kupikia
maurice.mutuku answered the question on August 6, 2019 at 06:00

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions