Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Weka shadda neno barabara kuonyesha maana ya shwari na baraste.

      

Weka shadda neno barabara kuonyesha maana ya shwari na baraste.

  

Answers


Kavungya
Shwari -Ba’rabara

Baraste -Bara’bara
Kavungya answered the question on November 21, 2022 at 13:21


Next: Choose the right word to from the options given to fill the blanks.i) We went home before it.............(begun/began) to rain.ii) Doctor Rank always...........(visit/visits) Torvald and...
Previous: Punctuate the following sentences correctly.i) I need a copy of memories we lost and other stories.ii) Why does he James like chicken?iii) Everyone knows hard...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Onyesha matamshi ya vokali ukitumia mchoro huu wa pembe tatu.(Solved)

    Onyesha matamshi ya vokali ukitumia mchoro huu wa pembe tatu.
    fig7.png

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • UFAHAMU Ajira ya watoto Kingi alizaliwa vuruni kijiji kilichosifika kwa ukarimu wa wanakijiji wake.Ingawa walikuwa karimu,Wavuruni wengi walikosa elimu.(Solved)

    UFAHAMU
    Ajira ya watoto
    Kingi alizaliwa vuruni kijiji kilichosifika kwa ukarimu wa wanakijiji wake.Ingawa walikuwa
    karimu,Wavuruni wengi walikosa elimu.Fauka ya hayo,walininginia katika umaskini
    uliokithiri.Hivyo,wengi waliselea katika kazi za kijungu jiko.Watot wa umri wa kwenda shule
    walikosa elimu na kuzurura mitaani.Udhaifu huu ulimpa faida Mwakisu,tajiri mmoja aliyemiliki
    shamba kubwa.Aliwaajiri watoto hao.
    Mwakisu alikuwa mkwasi alietononoka si haba.Kama ni senti ,alikuwa nazo.Kilichotia doa
    jina lake ni kiburi.Mbali na kiburi hicho,yeye hakujaliwa moyo wa huruma na utu.
    Hakubarikiwa kuwa mwema .Maadili hutuongoza kila mara kuwa ‘wema hauozi’.
    Kwa Mwakisu,wema ulioza na kuvunda .Utu uling’oka katika bawaba za moyo wake na
    ukawa msamiati aliouchukia.Aliwatumikisha watoto wa wenzake huku wake wakisoma shule.Tabia
    yake hiyo ndiyo iliyowafanya Wavuruni kumtoa katika orodhayao ya watu wema.
    Mwakisu alistaajabisha!Hakutaka kununua mashine zozote za kufanya kazi shambani ingawa
    alikuwa nao uwezo.Alistahabu kuajiri watoto wadogo na kuwadhulumu.Mkwasi huyu alifurahia
    kuona vitoto vikimenyana na kazi shambani kwake tangu mawio hadi machweo na hatimaye kuwapa
    ujira mdogo.
    Siku moja Kingi alimtaka radhi, “Bosi naomba uniongezee chochote ,kwani tuna shida
    nyumbani.” Mwasiku alimkodolea macho huku mdomo ukimcheza.Hapo alimchomolea mwajiriwa
    wake tusi kubwa kutoka kwenye hazina yake isiyopungua.Tusi ambalo lilimtaabisha Kingi
    kulisahau.Lilikaririwa akilini mwake kwa sonono.Tangu siku hiyo Kingi akaona kuwa kuajiriwa na
    Mwakisu ni kufadhiliwa u chini.
    Kiburi cha mwakisu kilidhihirika kila mara .Kila alipomwona motto akilia kwa uchovu au
    maumivu ,ungemsikia akimfokea ,”Chapa kazi!Unalilia nani hapa?Kama humudu kazi rudi kwa
    mamako ukanyonye.”
    Kazi nyingi zilikuwa ngumu na hazikuwastahili watoto wenye umri mdogo.Si kipupwe, si
    kaskazi,si vuli,si kiangazi ,si kusi:kazi ziliongezeka na kuwaumiza watoto.Kingi,kwa
    mfano,alitakikana akame ng’ombe kumi na abebe maziwa hadi kwenye tangi kubwa .Kisha
    angewakatia mg’ombe nyasi na kuwasafisha .Hatimaye angehitajika kuzoa samadi.
    Msimu wa kipupwe uliwadia.Baridi ikawatafuna watoto hao waliokosa mavazi bora.Kingin
    aliugua.Watoto wengi wakapatwa na maradhi.Wawili wakaaga dunia.Wazazi walipoona maisha ya
    watoto wao yamo hatarini,wakaandamana hadi kwa Mwakisu.tajiri huyo aliwajia kwa meno ya
    juu,’msiniitie kibuhuti.Mimi niliwaajiri watoto,sio watoto na wazazi wao”.Wazazi wakatanabahi
    kuwa , ‘Pa shoka hapaingii kisu’.Waliandamana hadi kwa chifu.Chifu alipoyaona yamempita
    kimo,akafululiza hadi kituo cha polisi.
    Mwakisu akakamatwa ,akashtakiwa na kuhukumiwa .Alipatikana na makosa ya kuwaajiri
    watoto wenye unri mdogo na kusababisha vifo vya wawili hao.
    Serikali ikatoa amri kwa wazazi kupeleka watoto wao shuleni.Ikatoa pia misaada ya
    kuendeleza elimu;elimu ya bure kwa shule za msingi.Kingi akasoma hadi kuhitimu chuo
    kikuu.Akawa daktari.
    Alfajiri moja mahabusu waliletwa hospitali kuu ya mkoa kwa matibabu.Kingi akampa huduma mzee
    aliyejawa mvi na kukoboka meno.Alipomtazama kwa makini akamkumbuka.
    Mwakisu akabahatisha,”sura yako….ni kama Kingi…”Kingi akamjibu,”Mimi ndiye
    Kingi.”Wakakondoleana macho, huku machozi yakimtiririka Mwakisu.

    Maswali
    1.Toa kichwa kingine kwa habari hii.
    2.Taja matatizo mawili yaliyowakabili wanakijiji cha Vuruni.
    3.Ni mambo gani yaliyowafanya wanakijiji kumtoa Mwasiku katika orodha yao?
    4.Taja kazi alizofanya Kingi.
    5. Mwasiku alishtakiwa kwa makosa gani?
    6.Eleza maana ya semi hizi.
    (a)Kazi ya kijungu jiko.
    (b)Tononoka si haba.
    (c)Kodolea macho.
    7.Toa maana ya methali hizi:
    (a)Wema hauozi.
    (b)Pa shoka hapaingii kisu.
    8.Toa maana ya msamiati huu kama ulivyoptumiwa katika makala:
    (a)Fauka ya
    (b)Alistahabu

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Taja mambo/dhana nne zinazozingatiwa katika matumizi ya lugha. (Solved)

    Taja mambo/dhana nne zinazozingatiwa katika matumizi ya lugha.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha silabi inayowekewa shadda kwenye maneno yafuatayo. Karatasi – Shairi – Barabara(njia kuu) Mto –(Solved)

    Onyesha silabi inayowekewa shadda kwenye maneno yafuatayo.
    Karatasi –
    Shairi –
    Barabara(njia kuu)
    Mto –

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Toa neno kwa kila moja ya sauti ambatano zifuatazo. Nyw – Nd – Ngw –(Solved)

    Toa neno kwa kila moja ya sauti ambatano zifuatazo.
    Nyw –
    Nd –
    Ngw –

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha Nomino (N), kitenzi , kielezi (E) Kiunganishi (U), na kivumishi (v) katika sentensi hizi. (i) Mtoto anacheza vizuri. (ii) Utacheza au utasoma? (iii) Wanafunzi wawili wanalala.(Solved)

    Onyesha Nomino (N), kitenzi , kielezi (E) Kiunganishi (U), na kivumishi (v) katika sentensi hizi.
    (i) Mtoto anacheza vizuri.
    (ii) Utacheza au utasoma?
    (iii) Wanafunzi wawili wanalala.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi zifuatazo. (i) Mkulima analima shamba. (ii) Mwanafunzi anasoma kitabu.(Solved)

    Kanusha sentensi zifuatazo.
    (i) Mkulima analima shamba.
    (ii) Mwanafunzi anasoma kitabu.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Andika vinyume vya sentensi zifuatazo:- (i) Mama anaanika nguo (ii) Baba anaenda sokoni. (Solved)

    Andika vinyume vya sentensi zifuatazo:-
    (i) Mama anaanika nguo
    (ii) Baba anaenda sokoni.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Bainisha maneno haya yanapatikana katika ngeli ipi? Ngoma – Ukuta – MachoUgonjwa – Mmea – Maiti –(Solved)

    Bainisha maneno haya yanapatikana katika ngeli ipi?
    Ngoma –
    Ukuta –
    MachoUgonjwa –
    Mmea –
    Maiti –

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Andika maneno yenya miundo ya silabi ifuatayo. KI (Konsonanti irabu) – KKI (Konsonanti, konsonanti, irabu) – II (irabu) –(Solved)

    Andika maneno yenya miundo ya silabi ifuatayo.
    KI (Konsonanti irabu) –
    KKI (Konsonanti, konsonanti, irabu) –
    II (irabu) –

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Andika majukumu tatu ya lugha.(Solved)

    Andika majukumu tatu ya lugha.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Taja vigezo vitatu vinavyotumika kuainisha konsonati.(Solved)

    Taja vigezo vitatu vinavyotumika kuainisha konsonati.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Jibu maswali yote kwenye nafasi zilizoachwa wazi. Mawasiliano ni neno ambalo asili yake ni wasili. Wasili lina maana ya kufika kwa mtu, kitu, au jambo fulani baada...(Solved)

    Jibu maswali yote kwenye nafasi zilizoachwa wazi.
    Mawasiliano ni neno ambalo asili yake ni wasili. Wasili lina maana ya kufika kwa mtu, kitu, au
    jambo fulani baada ya mwendo au safari. Kwa hivyo kuwasiliana kuna maana watu, kitu au
    mambo kufikiana kutoka mahali.
    Katika siku za jadi mawasiliano yalikuwepo lakini ya shida. Hata hivyo, watu waliwasiliana kwa
    kutumia moshi, ngomezi au kupiga mbiu. Mbinu hizi za jadi zilitumiwa baina ya vijiji ili
    kujulisha wanakijiji jambo la dharura au kuwajulisha jambo lingine lolote. Mbiu ilitumika kwa
    jambo la dharura. Njia za kusafirisha mizigo zilikuwa haba. Baadhi ya watu walitumia wanyama,
    kama fahali au farasi kukokotea mizigo yuao.
    Siku hizi mawasiliano yamepanuka sana. Mawasiliano ya kisasa yanahusisha simu, mtandao,
    televisheni na wavuti. Mawasiliano ya kisasa yamefanya ulimwengu wa kisasa kuwa kijiji kimoja
    kikubwa.
    Kwa kuzingatia maudhui haya, vyombo au njia kama redio, simu, waraka, ndege, meli, motokaa
    na wavuti vimepewa jina la vyombo vya mawasiliano. Hivyo basi yafaa tutathmini ni vipi
    vyombo au njia hizi hufanya kazi ya kuwasiliana na huwasilisha nini. Vyombo hivi vinaweza
    kuelezwa chini ya vichwa vitatu; usafiri, mazungumzo na picha. Vyombo mathalan baiskeli,
    ndege, meli na magari hufanya kazi ya kuwasafirisha watu kutoka janibu moja hadi nyingine.
    Watu wanaposafiri huwa wanasafirisha mali yao. Bidhaa kama kahawa, vyuma na mizigo
    mingine husafirishwa kwa meli, ndege na magari kupitia majini, hewani au barabarani.
    Bandari, viwanja vya ndege na barabara zimeimarishwa ili kukuza uchumi na kuleta maendeleo.
    Anayesafirisha bidhaa fulani na wakati huo anatakikana kukusanya nyingine, inamlazimisha
    asiambatane na bidhaa hizo lakini ahakikishe zimewasili alikozikusudia. Hivyo basi njia nyingine
    ya mawasiliano ilivumbuliwa.
    Njia hii ambayo ni mazungumzo hutumia vifaa kama barua, simu, barua pepe na kipepesi.
    Mtumiaji ataandika ujumbe na kuutuma kupitia shirika la posta au mashirika mengine ama
    mtandao. Yamkini ilihitajika kuweza kujibizana na kuulizana kati ya watu hao wawili ndipo simu
    ilipovumbuliwa na kumwezesha mtu kuzungumza na mwingine akiwa mbali sana. Watu
    huzungumza na kufahamiana. Ilipohitaji mtu kukiona kitu anachozungumzia ndipo ilibidi kuunda
    vifaa vya kuonyesha picha kama vile televisheni.
    Ilikuwa fahari kubwa sana kwa Wakenya kuwasiliana na nchi ya Ghana wakati wa michuano ya
    mpira ya kuwania kombe la taifa bingwa Afrika. Wakenya waliweza kuiona michezo hiyo moja
    kwa moja ingawa kijiografia Kenya na nchi hiyo zina majira tofauti.
    Mawasiliano tuliyotaja ni vyombo vya ufundi vilivyoundwa lakini kunayo maswasiliano ya ana
    kwa ana. Mwalimu na mwanafunzi darasani huwasiliana kutumia midomo, mikono, macho,
    kichwa na ishara nyinginezo. Wanapofanya hivyo huwa wanaelewana.
    Ndege kama kuku akihisi adui hufanya ishara au mlio fulani wa kutahadharisha viranga wakek
    katika michezo. Mwamuzi huwasiliana na wachezaji labda kwa kutumia firimbi au kipenga,
    kengelel au ishara za mkono. Kengele pia hutumiwa shuleni ili kuonyesha kukamilika kwa
    kipindi au kuhitajika mahali pengine.
    Kwa muhtasari, mawasiliano hutumia chochote ilimradi ujumbe utokao kwa mtu, kitu au mahali
    fulani ufike panapotarajiwa.

    MASWALI:
    (i) Taja anwani faafu ya kifungo hiki.

    (ii) Vyombo vya mawasiliano vimeleta manufaa gani katika maisha ya watu?

    (iii) Mawasiliano yameelezwa katika vipenge vitatu. Vitaje.

    (iv) Andika visawe vya:
    (a) Televisheni –
    (b) Waraka –

    (v) Nini maana ya:
    (a) Ana kwa Ana –
    (b) Ulimwengu umekuwa kijiji kimoja kikubwa –

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Taja majukumu matano ya fasihi simulizi.(Solved)

    Taja majukumu matano ya fasihi simulizi.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Fasihi simulizi ni nini?(Solved)

    Fasihi simulizi ni nini?

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi ifuatayo. Nyumba hiyo itafunguliwa.(Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo.
    Nyumba hiyo itafunguliwa.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Tambulisha maneno mbalimbali katika sentensi zifuatazo. i) Mwanafunzi mvumilivu alisoma vizuri. ii) Yule ameongea maneno mengi.(Solved)

    Tambulisha maneno mbalimbali katika sentensi zifuatazo.
    i) Mwanafunzi mvumilivu alisoma vizuri.

    ii) Yule ameongea maneno mengi.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Sentensi zifuatazo ziko katika nyakati / hali gani? a) Otieno hula samaki kila siku b) Yeye anaandika tu kitabu(Solved)

    Sentensi zifuatazo ziko katika nyakati / hali gani?
    a) Otieno hula samaki kila siku

    b) Yeye anaandika tu kitabu

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Andika sentensi zifuatazo kwa wingi. i) Ukuta ambao ulianguka ni huu. ii) Mwanagenzi yule amepita mtihani vizuri.(Solved)

    Andika sentensi zifuatazo kwa wingi.
    i) Ukuta ambao ulianguka ni huu.

    ii) Mwanagenzi yule amepita mtihani vizuri.

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)

  • Tenganisha neno lifuatalo katika viambiu vyake mbalimbali. Aliyempigia(Solved)

    Tenganisha neno lifuatalo katika viambiu vyake mbalimbali.
    Aliyempigia

    Date posted: November 21, 2022.  Answers (1)