Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Tia shadda ili kutoa maana mbili tofauti ya neno ‘katakata’.

      

Tia shadda ili kutoa maana mbili tofauti ya neno ‘katakata’.

  

Answers


Kavungya
Kata’kata -kuwa vipande vipande

‘katakata -kabisa kabisa (nahau)
Kavungya answered the question on November 22, 2022 at 09:08


Next: Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza maana ya aina zifuatazo za silabi: Silabi funge Silabi wazi Silabi mwambatano
Previous: Tambua aina za maneno katika sentensi zifuatazo: Msichana mrembo amechora haraka sana. Yeye ataenda sokoni.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza maana ya aina zifuatazo za silabi: Silabi funge Silabi wazi Silabi mwambatano(Solved)

    Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza maana ya aina zifuatazo za silabi:
    Silabi funge
    Silabi wazi
    Silabi mwambatano

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Eleza sifa za sauti zifuatazo: /e/ /p/(Solved)

    Eleza sifa za sauti zifuatazo:
    /e/
    /p/

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali FADHILA ZA PUNDA Rita na Evelyn walikuwa marafiki wa chanda na pete kwa muda mrefu.(Solved)

    Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali
    FADHILA ZA PUNDA
    Rita na Evelyn walikuwa marafiki wa chanda na pete kwa muda mrefu. Waliishi katika mtaa wa Kibokoni
    jijini Mombasa. Evelyn alikuwa mwanafunzi wa masomo ya uhazili katika chuo kimoja pale mjini. Naye
    Rita alifanya kazi ya ukarani papo hapo mjini. Waliishi kidugu katika chumba kimoja walichopanga pale
    mtaani. Ingawa marafiki hawa walishirikiana kwa kila njia katika shughuli za upishi, kupiga deki, kufagia,
    kufua na kazi nyinginezo za nyumbani, aliyekuwa akitoa msaada mkubwa zaidi alikuwa ni Rita. Rita
    alikuwa na mazoea ya kutunza pesa zake vyema. Aidha alijua maana ya haba na haba hujaza kibaba.
    Alijua kuwa Evelyn, kama mwanafunzi, hakuwa na uwezo wa kuyakidhi baadhi ya mahitaji yake.
    Alijitolea sabili hata kumnunulia Evelyn nguo, viatu na vim vingine alivyohitaji. Mara nyingine ilibidi Rita
    kulipa kodi ya nyumba peke yake kwa vile mwenzake hangeweza kupata pesa kwa wakati. Hakuwahi
    hata siku moja kumkera wala kumtesa Evelyn kwa jinsi yoyote ile. Fauka ya hayo, hakuwahi
    kumsemesha vibaya wala kuonyesha dharau kwake. Aliamini kama wanavyosema watu kuwa dunia
    rangi rangile, huenda siku moja atahitaji kusaidiwa yeye pia. Siku kama hiyo atamtegemea Evelyn,
    mwandani wake. Evelyn alipomaliza masomo yake alikuwa na bahati ya mtende. Alipata kazi nzuri mara
    moja katika kampuni moja ya maffita papo hapo jijini. Lakini muda si muda, mambo ya ajabu yalianza
    kutokea. Baada ya kupata kazi yenye kipato kizuri, kichwa cha Evelyn kilianza kufura mfano wa kaimati.
    Badala ya kunisaidia mwenzake katika kazi za pale nyumbani pamoja na gharama za maisha, alifhatilia
    raha za jijini kwa kuamini ule msemo wa ponda raha kufa kwaja. Rita alipomwuliza alimjibu kwa ukali,
    “Nikusaidie nini? Sasa si kama wakati nilipokuwa mwanafunzi. Kila mtu ana pesa zake.Ala!” Rita
    hakumwelewa tena Evelyn.Isistoshe, alianza kumwibia Rita vitu vyake wakati alipokuwa hayupo
    nyubani. Mara kwa mara Rita aligundua kuwa pesa alizokuwa ameficha sehemu Fulani nyumbani
    zimedokolewa. Alipomwuliza, Evelyn alikujajuu, “Unafikiri mimi sina pesa? Unadhani ni wewe tu
    uliyeajiriwa?” Rita alizidi kushangaa, Muda wote alioishi na kumfadhili rafiki yake aliamini kuwa atamlipa
    mema. “Kumbe fadhila za punda ni mateke?” Alijiuliza Rita. Baada ya muda, urafiki wao ulivunjika na
    Evelyn akahamia mtaa wa Furaha alikoendelea na maisha yake ya starehe na ureda. Hata hivyo mambo
    yalianza kumwendea mrama Evelyn. Wakubwa wake kazini hawakupendezwa najinsi alivyoendesha
    shughuli zake pale ofisini. Mara nyingi alifika kazini akiwa amechelewa na kila wakati alitoa vijisababu
    mbalimbali ambavyo havikumridhisha yeyote. Aidha, alipokuwa ofisini hakufanya mengi isipokuwa
    kutembea kutoka ofisi hii hadi nyingine akiwasumbua watu kazini mwao. Mara kwa mara alionekana
    akisinzia wakati wenzake walipokuwa wakichapa kazi. Lakini lililowakera zaidi wakuu wa kampuni hiyo
    ya mafuta ni jambo fulani lililoanza kutendeka pale. Vitu vya watu vilianza kupoteapotea.Mara
    mfanyikazi huyu anapoteza saa yake, mara mwingine anapoteza pesa, mara hiki mara kile. Wakuu
    walipoyatupa mawazo yao nyuma wakagundua kuwa mambo haya yalianza kutendeka mara tu
    alipowasili Evelyn. Wakaamua kumwekea mtego. Evelyn alioshikwa kimasomaso akidokoa mkoba wa
    msichana mwenzake. Mkoba huo ulikuwa umeaehwa juu ya dawati kimakusudi ili kumvuta Evelyn.
    Evelyn alifutwa kazi papo hapo. Fauka ya hayo, alitiwa mikononi na kukabidhiwa poisi waliomtupa
    korokoroni. Kesho yake Evelyn alifikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa la wizi. Alitozwa faini ya
    shilingi elfu tano au kifungo cha miezi sita. Hakuwa na pesa zozote za kulipia faini hii. Akawekwa
    rumande. Hata rafiki mmoja hakuwa naye wa kumuauni katika wakati huo wa majaribu. Kwa bahati, Rita
    alisikia kuhusu kadhia hiyo.Hakupoteza muda. Akashika njia moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
    Mpango ukafanywa na akamlipia. Evelyn ile faini. Evelyn alipoachiliwa hum akashangaa. “Yaani
    nimesamehewa ama nini?”Aliuliza.“La. Hujasamehewa.Faini uliyotozwa imelipwa na msichana yule.”
    Evelyn akageuka na kumwona Rita. Alimtazama kwa muda bila kujua la kusema. Mwishowe alimsogea
    kisha wakakaribiana polepole na kukumbatiana. Machozi yakaanza kumdondoka Evelyn, nde! Nde! Nde!
    Akalia kilio cha uchungu na soni. Akamwomba Rita msamaha, “Nisamehe, sikujua nililokuwa
    nikifanya.Nilidhani kuwa baada ya kupata kazi sitahitaji tena urafiki wako. Haya yaliyonipata
    yamenifunza,” alisema kwa masikitiko. “Evelyn, kijengacho mtu ni uth na tabia,” alisema Rita.“Ni kweli
    rafiki yangu” alitamka Evelyn, Sasa nimejitia kwenye shida.Hata kazi yangu nzuri nimeipoteza.Sina
    mahali pa kuishi. Itabidi nirudi kijijini kwa baba na mama. Kwaheri rafiki yangu naasante kwa yote
    uliyofanya.”“La! Hutaondoka”. Rita alimwambia lcwa dhati, “Tutakwenda nawe nyumbani mwangu
    tukaishi pamoja kama zamani. Nitayagharamia mahitaji yako yote hadi utakapopata kazi”. Basi Rita na
    Evelyn wakaungana tena na kuishi vizuri katika nyumba ile ile mtaani Kibokoni. Kweli akufaaye kwa dhiki
    ndiye rafiki.

    MASWALI:
    1. Maisha ya Evelyn na Rita yalikuwaje kabla ya Evelyn kupata kazi?
    2. Kutokana na jinsi Rita alivyomtunza Evelyn, unafikiri yeye alikuwa ni mtu wa ama gani?
    3. Eleza baadhi ya mambo ambayo Rita alimtendea mwenzake.
    4. Baada ya kupata kazi Evelyn alikuwa mtu mkarimu. Je, unakubali?Eleza ilivyokuwa.
    5. Evelyn alipokuwa mwanafunzi hakuwa na tabia ya udokozi. Unafikiri ni kwa nini alianza tabia
    hiyo baada ya kuajiriwa?
    6. ‘Asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu.’ Methali hii inahusianaje na Evelyn?
    7. ‘Akufaaye ukiwa dhiki ndiye rafiki.’ Methali hii inahusianaje na Rita?
    8. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu: (alama 3)
    (a) marafiki wa chanda na pete
    (b) enda mrama
    (c) jitolea sabili

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali. Hapo zamani za kale paliishi sungura na ndovu. Wanyama hawa waliishi baharini.(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
    Hapo zamani za kale paliishi sungura na ndovu. Wanyama hawa waliishi baharini.Maulana alikuwa
    amewatunukia mapenzi si haba.Makazi yao yalikuwa yamepambwa yakapambika. Walitegemea
    matunda mbalimbali yaliyokuwa baharini kama mapera, matomoko matikitimaji na kadhalika.
    Siku moja usiku wa manane, maji yakaanza kupwa. Ndovu aliathirika zaidi.Alijaribu kuinama majini
    lakini hakuweza.Alimwita sungura amsaidie lakini sungura alikuwa ametoweka.
    Ndovu aliamua kwenda kumtafuta sungura.Alimtafuta hadi msituni lakini hakumpata.Alihofia kurudi
    baharini na hadi wa leo yumo msituni.

    Maswali
    a. Tambua utanzu na kijipera chake.
    b. Taja fomyula zingine mbili za kutanguliza kifungu hiki.
    c. Eleza umuhimu wa kijipera hiki.
    d. Eleza sifa za kifungu hiki.
    e. Eleza umuhimu wa fomyula ya Kuhitimisha

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali. Kibiko: Hujambo dada Cheupe? Cheupe: (Akikohoa) Sijambo ndugu Kibiko.(Solved)

    Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali.
    Kibiko: Hujambo dada Cheupe?
    Cheupe: (Akikohoa) Sijambo ndugu Kibiko.
    Kibiko: Unaendelea namna gani?
    Cheupe: Niko poa isipokuwa maumivu kidogo ya chest.
    Kibiko: Usijali nitakupa pain relievers utakuwa sawa.
    Cheupe: Asante sana, nashukuru.
    Maswali
    a) Mazungumzo haya yanapatikana wapi?
    b) eleza sifa nne za lugha inayotumika katika mazungumzo haya

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Neno ‘chungu’ lina maana –enye kutokuwa na tamu. Eleza maana zake zingine mbili.(Solved)

    Neno ‘chungu’ lina maana –enye kutokuwa na tamu. Eleza maana zake zingine mbili.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tumia O’rejeshi badala ya amba- Wachezaji ambao hucheza kwa bidi ndio ambao hufaulu maishani.(Solved)

    Tumia O’rejeshi badala ya amba-
    Wachezaji ambao hucheza kwa bidi ndio ambao hufaulu maishani.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika upya sentensi ifuatayo kwa kufuata maagizo uliyopewa. Mbwa ambaye aliripotiwa kuwa ameibwa amepatikana katika bwawa la maji. (Solved)

    Andika upya sentensi ifuatayo kwa kufuata maagizo uliyopewa.
    Mbwa ambaye aliripotiwa kuwa ameibwa amepatikana katika bwawa la maji.
    (Anza: Katika bwawa............)

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja kudhihirisha maana ya vitate vifuatavyo: Kesi/gesi(Solved)

    Tunga sentensi moja kudhihirisha maana ya vitate vifuatavyo:
    Kesi/gesi

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika matumizi mawili ya mshazari.(Solved)

    Andika matumizi mawili ya mshazari.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika katika ukubwa. Mwanamwali huyu alijinunulia viatu vya ngozi.(Solved)

    Andika katika ukubwa.
    Mwanamwali huyu alijinunulia viatu vya ngozi.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Eleza maana mbili za sentensi ifuatayo: Mtoto anapendezwa na ziwa.(Solved)

    Eleza maana mbili za sentensi ifuatayo:
    Mtoto anapendezwa na ziwa.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Yakinisha katika wingi sentensi ifuatayo: Mtu asiyeugua anahitaji daktari.(Solved)

    Yakinisha katika wingi sentensi ifuatayo:
    Mtu asiyeugua anahitaji daktari.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika visawe vya maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi ifuatayo. Kulikuwa kioja kuona marafiki wakipigana.(Solved)

    Andika visawe vya maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi ifuatayo.
    Kulikuwa kioja kuona marafiki wakipigana.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Sahihisha sentensi hii. Mfua ulionyesha ulisababisha mafuriko. (Solved)

    Sahihisha sentensi hii.
    Mfua ulionyesha ulisababisha mafuriko.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika kinyume cha sentensi hii. Ubane mlango kidogo na umtwike mchukuzi mzigo huu.(Solved)

    Andika kinyume cha sentensi hii.
    Ubane mlango kidogo na umtwike mchukuzi mzigo huu.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo ili kuonyesha viambishi awali ,mzizi na viambishi tamati. Walioangaliana(Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo ili kuonyesha viambishi awali ,mzizi na viambishi tamati.
    Walioangaliana

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Weka Nomino hizi katika ngeli zake. Raha Kumbikumbi(Solved)

    Weka Nomino hizi katika ngeli zake.
    Raha
    Kumbikumbi

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Akifisha sentensi hii: alikufa siku ya jumapili tarehe 20 mwezi wa januari mwaka wa 2011.(Solved)

    Akifisha sentensi hii:
    alikufa siku ya jumapili tarehe 20 mwezi wa januari mwaka wa 2011.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Kwa kutoa mifano mwafaka, onyesha mianzo tofauti katika ngeli ya U-ZI.(Solved)

    Kwa kutoa mifano mwafaka, onyesha mianzo tofauti katika ngeli ya U-ZI.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)