Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Kanusha: Asha aliwapelekea wageni chakula na akawanavya mikono.

      

Kanusha:
Asha aliwapelekea wageni chakula na akawanavya mikono.

  

Answers


Kavungya
Asha hakuwapelekea wageni chakula wala hakuwanavya mikono.
Kavungya answered the question on November 26, 2022 at 08:04


Next: Tumia neno ‘kuwa’ kama kitenzi kishirikishi kikamilifu katika sentensi.
Previous: Soma makala haya kisha ujibu maswali. Kwani mnauza salamu? Sina time ya kuwaste hapa. Am a busy person leta order yako haraka... Nimesema samaki wa kupaka. Mimi...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Tumia neno ‘kuwa’ kama kitenzi kishirikishi kikamilifu katika sentensi.(Solved)

    Tumia neno ‘kuwa’ kama kitenzi kishirikishi kikamilifu katika sentensi.

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Eleza matumizi ya neno ‘mzee’ katika sentensi zifuatazo: Baba mzee amelewa Mzee amelewa(Solved)

    Eleza matumizi ya neno ‘mzee’ katika sentensi zifuatazo:
    -Baba mzee amelewa

    -Mzee amelewa

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Andika katika usemi wa taarifa. “Tafadhali nifungulie mlango sasa. Nitanyeshewa.” Mtoto akamwambia(Solved)

    Andika katika usemi wa taarifa.
    “Tafadhali nifungulie mlango sasa. Nitanyeshewa.” Mtoto akamwambia

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Eleza matumizi matatu ya viambishi awali.(Solved)

    Eleza matumizi matatu ya viambishi awali.

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Andika sifa za sauti zifuatazo: /m/ /gh/(Solved)

    Andika sifa za sauti zifuatazo:
    /m/
    /gh/

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali. Dawa za kulevya ni donda ndugu katika taifa letu. Ni zimwi linalotesa na kufisha wazee kwa vijana.(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
    Dawa za kulevya ni donda ndugu katika taifa letu. Ni zimwi linalotesa na kufisha wazee kwa vijana.
    Halichagui jinsia, tabaka, rangi wala umri. Uraibu wa dawa hizi hauna faida yoyote. Wanaotumia dawa
    za kulevya huzitia mwili kwa kunusa, kuvuta, kumeza na kujidunga sindano. Zinapoingia katika miili ya
    watu madhara huwa mengi.
    Kuna wale wanaokosa hamu ya kula, wengine huambukizwa maradhi kama vile ukimwi
    wanapotumia sindano zilizotumiwa na watu wenye virusi vya maradhi hayo kujidunga sindano na kutia
    dawa mwilini.
    Mihadarati pia inaweza kufanya mtu awe mwendawazimu. Vifo pia hutokea ikiwa uraibu utazidi
    na mtu akose kupata matibabu. Mtu anayetumia dawa za kulevya huathirika akili. Yeye huwa hana
    uamuzi wenye hekima katika maisha yake .wengi wao hushiriki katika vitendo vya uhayawani. Wao
    hukosa fikra za utu. Baadhi yao wamebaka kina mama na watoto wadogo na wengine wamezua vita
    katika familia na kusababisha madhara makubwa katika jamii zao kwa sababu ya ulevi.
    Familia za wanaotumia mihadarati hazina amani. Jamaa zao hutumia hala nyingi kuwalipia ada
    ya hospitali ili wapate matibabu baada ya kuzidiwa na uraibu. Mali hufujwa na watu wenye uraibu wa
    dawa hizo pale wanapohakikisha hawazikosi kila siku. Mzazi kwa mfano anaweza kutumia hela kununua
    dawa za kulevya badala ya kumlipia mwanawe karo. Kuna wale wanaowaibia majirani na marafiki ili
    wakidhi mahitaji yao.
    Ajali barabarani pia husababishwa na malevi. Dereva yeyote awe wa matatu au gari la kibinafsi
    anapoedesha gari akiwa mlevi huwa anahatarisha maisha yake mwenyewe, abiria na wananchi
    wanaopiga miguu barabarani .Uchumi wa taifa huzorota baada ya wananchi kutumia mihadarati. Watu
    wenye uraibu hukaa mbumbumbu bila kufanya lolote hasa kutokana na kudhoofika kwa afya yao au
    ulegevu unaosababishwa na ulevi. Watu wa aina hiyo huwa wanamchango haba katika ukuzi wa
    uchumi wa taifa.
    Dawa hizi zimesambaa kila mahali utapata zinauzwa masokoni, shuleni, njiani na hata pahali
    popote pale penye watu. Dawa za kulevya haziuzwi hadharani nchini Kenya kwa sababu serikali imepiga
    marufuku uuzaji wa bidhaa hiyo. Waja wanaoziuza hufanya hivyo kisiri. Walanguzi wa mihadarati
    aghalabu hutumia watu wengine kuuza kwa niaba yao. Kuna wale wanaotumia watoto ,
    wanaorandaranda almaarufu chokoraa na wengine hutumia vijana katika shule za misingi, upili na vyuo
    vikuu kama mawakala.
    Vijana hasa wamejipata katika mtego huu kwa kuwafanyia walanguzi biashara hii haramu hili
    waweze kupata hela za kukidhi matakwa yao ukweli ni kuwa pesa wanazo patiwa na waajiri wao ni
    chache mno na hatimaye wao hutumia daw zile na kuishia kuwa na uraibu unaosababisha wao wenyewe
    kuwa wateja wa mabwenyenye hao wasio na utu.
    Watu maarufu kama vile wafanyabiashara, wanamuziki na wanasiasa wametuhumiwa kushiriki
    katika biashara hii . washukiwa hawa mara nyingi hukosa kufikishwa mahakamani kwa sababu jamii
    hukosa ushahidi wa kutosha dhidi ya tabia hiyo. Ni nani hasa muhusika katika kuingiza sumu hii katika
    nchi yetu ? hakuna mtu anayeweza kusimama kadamnasi na kusema hiyo ndiyo kazi yake. Mbona
    tushiriki katika biashara tusiyoweza kujivunia?
    Ni mwito wangu kwa kila mwananchi mzalendo kuungana na wenzake ili kupinga biashara hii haramu.
    Tuhubiri makanisani, shuleni misikitini, hekaluni na mahali popote pale. Tukemee adui huyu, wa afya na
    mali. Washauri nasaha washike usukani wawashauri wazee kwa vijana, wakubwa kwa wadogo, weusi
    kwa weupe tuizike mihadarati katika kaburi la sahau.

    Maswali
    1. Yape makala haya anwani mwafaka.
    2. Mwandishi anamaanisha nini anaposema kuwa dawa za kulevya ni donda ndugu katika taifa
    letu.
    3. Taja namna ambavyo dawa za kulevya zinavyotumiwa.
    4. Eleza athari ya dawa za kulevya kwa familia za wanaotumia .
    5. Kuna changamoto gani katika kupiga vita matumizi ya mihadararati.
    6. Eleza sera ya serikali kuhusu dawa za kulevya.
    7. Msamiati ufuatao umetumika kumaanisha nini kwa mjibu wa taarifa.
    i. mawakala
    ii. kadamnasi
    iii. washauri nasaha

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Eleza sifa za sajili ya maabadani.(Solved)

    Eleza sifa za sajili ya maabadani.

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Unda nomino mbilimbili kutokana na mizizi ifuatayo. i) -f- ii) -l-(Solved)

    Unda nomino mbilimbili kutokana na mizizi ifuatayo.
    i) -f-
    ii) -l-

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Bainisha kirai nomino na kirai kivumishi katika sentensi hizi. i) Nguo aliyonunua mzazi ni mpya. ii) Kondoo mwenye manyoya mengi hupendeza.(Solved)

    Bainisha kirai nomino na kirai kivumishi katika sentensi hizi.
    i) Nguo aliyonunua mzazi ni mpya.
    ii) Kondoo mwenye manyoya mengi hupendeza.

    Date posted: November 26, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ya neno moja yenye visehemu vifuatavyo vya sarufi. i) Kiambishi kiwakilishi cha kiima ii) Kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopo iii) Kiambishi kiwakilishi cha kitendewa/mtendewa iv) Shina la...(Solved)

    Tunga sentensi ya neno moja yenye visehemu vifuatavyo vya sarufi.
    i) Kiambishi kiwakilishi cha kiima
    ii) Kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopo
    iii) Kiambishi kiwakilishi cha kitendewa/mtendewa
    iv) Shina la kitenzi
    v) Kiambishi cha kauli ya kutendesha
    vi) Kiishio

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tumia neno dhahiri katika setensi kulingana na maagizo Kama: i) Kiambishi ii) Kivumishi(Solved)

    Tumia neno dhahiri katika setensi kulingana na maagizo
    Kama:
    i) Kiambishi
    ii) Kivumishi

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Bainisha yambwa tendwa na yambwa tendewa katika sentensi hii. Mbunge wa Mtondo Kaskazini atawajengea wanakijiji josho kisha aghurie mjini.(Solved)

    Bainisha yambwa tendwa na yambwa tendewa katika sentensi hii.
    Mbunge wa Mtondo Kaskazini atawajengea wanakijiji josho kisha aghurie mjini.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia nomino zifuatazo pamoja na kivumishi __ingine i) dau ii) urembo(Solved)

    Tunga sentensi ukitumia nomino zifuatazo pamoja na kivumishi __ingine
    i) dau
    ii) urembo

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika katika usemi taarifa. “Tutawatembelea wazazi wetu leo jioni” Leo alimwambia Asha.(Solved)

    Andika katika usemi taarifa.
    “Tutawatembelea wazazi wetu leo jioni” Leo alimwambia Asha.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika katika ukubwa wingi. Kitoto kijeuri kikiletwa kitarejeshwa kwao.(Solved)

    Andika katika ukubwa wingi.
    Kitoto kijeuri kikiletwa kitarejeshwa kwao.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia mbinu ya matawi. Mwanafunzi stadi amenunua kitabu kizuri.(Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia mbinu ya matawi.
    Mwanafunzi stadi amenunua kitabu kizuri.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Yakinisha sentensi hii. Simba asiponguruma wanyama wote hawababaiki.(Solved)

    Yakinisha sentensi hii.
    Simba asiponguruma wanyama wote hawababaiki.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Taja sifa mbili bainifu za vokali 'U'(Solved)

    Taja sifa mbili bainifu za vokali 'U'

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Taja sauti mbili ambazo ni vikwamizo na hutamkiwa kwenye ufizi.(Solved)

    Taja sauti mbili ambazo ni vikwamizo na hutamkiwa kwenye ufizi.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata Wakaazi wengi wa maeneo ya kitajiri miji yetu hawajui wapo chini ya utawala wa machifu.(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
    Wakaazi wengi wa maeneo ya kitajiri miji yetu hawajui wapo chini ya utawala wa
    machifu.Huenda wakasalia katika hali hii ya kutojua hadi wanapokosa kulipa ujira wa watumishi wao wa
    nyumbani halafu maskini mwajiriwa huyu anaripoti kwa chifu, kwa kuwa ni hali yake.
    Chifu ni uzi muhimu katika vazi Ia kijamii. Bila hawa maafisa, jamii kama tunavyoijua ingeporomoka.
    Wakati mwingine hawaungwi mkono. Mfano mzuri ni kukataliwa kwa katiba kielelezo cha Wako,
    Novembe 2005, wakati wa kura ya maoni. Kwa sababu jukumu la chifu au kibadala chake
    halikudhihirishwa wazi wazi katika kielelezo, wengi walikataa stakabadhi hiyo, wakihofia sasa
    hawataweza kufikia mtawala wao kushughulikia malalamishi yao.
    Nimeishi mtaa wa Nairobi West miaka mingi na kuhudhuria kamati nyingi za lokesheni, chini ya
    uwenye kiti wa chifu akisaidiwa na naibu na wazee. Mikutano, pia inahudhuriwa na madiwani, inspekta
    wa askari tawala na wawakilishi wengi na washia dau katika lokesheni. Takribani kila swali linalogusia
    maslahi ya jamii linajadiliwa na kuchunguzwa na maazimio kupitishwa. Mada muhimu wakati wa
    mikutano hii ni usalama, taa za barabarani, ulanguzi wa mihadarati hasa karibu na taasisi za elimu,
    kudumisha usafi wa vyoo vya umma, kudumisha usalama kupitia kwa raia na swala nyeti la vioski.
    Kazi ngumu ya chifu ni kuwazia kila kju. Kwa mfano, mwenye kioski ni sharti apate mkate wa
    kila siku na sehemu ya biashara yake iliyoko ni muhimu. Ikiwa kioski kitajengwa na kukiuka sheria za
    baraza la jiji au ikiwa wizi usiofahamika na utumizi wa dawa za kulevya unatokea kufuatia kukua kwa
    idadi ya vioski katika eneo, shinikizo zinaelekezwa kukuwa kwa wenye vioski. Chifu lazima azingatie
    shinikizo za umma hatari za kiusalama na hofu za wenye vioski kabla ya kufanya uamuzi ikiwa mijengo
    hiyo ibomolewe.
    Tatizo jingine ni watoto wa barabarani. Makao ya kuwakimu ni machache kama walivyo
    wahudumu wa kijamii, suluhu ni nini? Tuwatupe katika ukumbi wa kijamii, ambao watahepa pindi tu,
    wapatapo fürsa ndogo au wapelekwe huduma kwa vijana wa Taifa, ambapo wachache wanaweza
    kutunzwa kwa wakati mmoja. Ili kufaulu kwa wengine, sharti wawe katika vituo vya urekebishaji tabia
    za matumizi ya dawa za kulevya. Tuwakabidhi polisi kwa sababu wanaranda au tujaribu kuungana na
    vituo vya urekebishaji tabia kuhakikisha hawatarudi barabarani.
    Mazingira ya lokesheni pia huibuka katika ajenda. Hali ya barabara, juhudi za kusafisha
    mazingira, wizi wa maji na umeme, usafiri wa umma, uchafuzi wa mazingira, hewa na kelele, hii
    inatokea kupitia malalamishi ya watu wanaoishi karibu na mabaa na uzingativu wa saa ya biashara
    hujadiliwa kila mara. Chifu ni sharti afahamu sheria na kanuni zinazotawala hali hizo, halafu ajadili na
    wahusika kabla ya kutoa mwelekeo. Usawa na uwazi katika kugawa fedha za Hazina ya maendeleo ya
    maeneo Bunge, pia hujadiliwa.
    Katika maswala haya mengine, chifu ndiye aliye nyanjani. Anawajibikia jamii na wakubwa
    wake na hatarajii shukrani au kutambuliwa kwa kazi njema aliyofanya. Isipokuwa hukashifiwa anapofeli.
    Watu wengine wana taswira ya Chifu kama mtu kwenye jukwa, kofia yake. na kifimbo kinachompa
    mamlaka ya kuhutubia baraza, Kajubu tyji zaidi ya hivyo. Kwa mujibu wa kitabu cha
    mafunzo ya machifu na Naibu wao (Januari 2004), wajibu wa chifu ni kuwakilisha sera na mipango ya
    serikali kwa wananchi. Chifu ni ajenti wa “mabadiliko” mwenye wajibu Wa kuhamasisha watu katika
    maendeleo. Anajishughulisha na kujua ni nani maskini katika lokesheni, mkoa, mgonjwa asiyeweza
    kupata tiba na kupanga jinsi mhasiriwa atakavyopelekwa hospitali kama anavyoweza. Ni sharti
    ashughulikie ugomvi wa kinyumbani, uhalifu wa watoto, dhuluma za watoto, agawe chakula na mavazi
    kwa wahitaji na kuhukumu kesi ndogo za wizi na uharibifu. Chifu hutatua kesi za kisheria kwa
    wasioweza kumudu wakili. Wakati wananchi wanapohisi mbunge wao hafikiliki na hawana imani na
    polisi, chifu ndiye suluhisho.
    Lakini kuna machifu wachache ambao hawafanyi kazi yao vyema. Kwa ufupi, chifu ni
    mkusanyiko wa kushngaza; mfalme katika himaya yake, pasta, baba msikivu, wanasaikolojia, mtunga
    sheria na mdumisha sheria, balozi mchaguzi, mama, mlumbi na askari asiyechelewa. Ingawa halipwi
    vyema, anafanya kazi bila tarakilishi, na aghalabu hujilipia gharama ya kodi ya afisi yake kutoka mfuko
    wake. Kwa sababu ni mtumishi wa umma, tunataraji afanye kazi mufti. Hiyo haimaanishi tusishukuru
    kwa kazi njema aliyofanya. Serikali inaweza kufanya hivi kwa kuimarisha hali yake ya kazi, mazingira
    yake ya kikazi, na kuhakikisha yana tarakilishi, anapata mafunzo ya uongozi na usimamizi. Wananchi
    sharti washukuru watu hawa kwa kujitolea sabili.

    Maswali
    a) Fupisha aya nne za kwanza (Maneno 60)
    Matayarisho
    Jibu
    b) Kwa maneno kati ya 80-90 fupisha aya ya tano hadi mwisho.
    Matayarisho
    Jibu

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)