Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Taja sauti mbili ambazo ni vikwamizo na hutamkiwa kwenye ufizi.

      

Taja sauti mbili ambazo ni vikwamizo na hutamkiwa kwenye ufizi.

  

Answers


Kavungya
/s/ na /z/
Kavungya answered the question on November 25, 2022 at 11:33


Next: Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata Wakaazi wengi wa maeneo ya kitajiri miji yetu hawajui wapo chini ya utawala wa machifu.
Previous: Taja sifa mbili bainifu za vokali 'U'

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata Wakaazi wengi wa maeneo ya kitajiri miji yetu hawajui wapo chini ya utawala wa machifu.(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
    Wakaazi wengi wa maeneo ya kitajiri miji yetu hawajui wapo chini ya utawala wa
    machifu.Huenda wakasalia katika hali hii ya kutojua hadi wanapokosa kulipa ujira wa watumishi wao wa
    nyumbani halafu maskini mwajiriwa huyu anaripoti kwa chifu, kwa kuwa ni hali yake.
    Chifu ni uzi muhimu katika vazi Ia kijamii. Bila hawa maafisa, jamii kama tunavyoijua ingeporomoka.
    Wakati mwingine hawaungwi mkono. Mfano mzuri ni kukataliwa kwa katiba kielelezo cha Wako,
    Novembe 2005, wakati wa kura ya maoni. Kwa sababu jukumu la chifu au kibadala chake
    halikudhihirishwa wazi wazi katika kielelezo, wengi walikataa stakabadhi hiyo, wakihofia sasa
    hawataweza kufikia mtawala wao kushughulikia malalamishi yao.
    Nimeishi mtaa wa Nairobi West miaka mingi na kuhudhuria kamati nyingi za lokesheni, chini ya
    uwenye kiti wa chifu akisaidiwa na naibu na wazee. Mikutano, pia inahudhuriwa na madiwani, inspekta
    wa askari tawala na wawakilishi wengi na washia dau katika lokesheni. Takribani kila swali linalogusia
    maslahi ya jamii linajadiliwa na kuchunguzwa na maazimio kupitishwa. Mada muhimu wakati wa
    mikutano hii ni usalama, taa za barabarani, ulanguzi wa mihadarati hasa karibu na taasisi za elimu,
    kudumisha usafi wa vyoo vya umma, kudumisha usalama kupitia kwa raia na swala nyeti la vioski.
    Kazi ngumu ya chifu ni kuwazia kila kju. Kwa mfano, mwenye kioski ni sharti apate mkate wa
    kila siku na sehemu ya biashara yake iliyoko ni muhimu. Ikiwa kioski kitajengwa na kukiuka sheria za
    baraza la jiji au ikiwa wizi usiofahamika na utumizi wa dawa za kulevya unatokea kufuatia kukua kwa
    idadi ya vioski katika eneo, shinikizo zinaelekezwa kukuwa kwa wenye vioski. Chifu lazima azingatie
    shinikizo za umma hatari za kiusalama na hofu za wenye vioski kabla ya kufanya uamuzi ikiwa mijengo
    hiyo ibomolewe.
    Tatizo jingine ni watoto wa barabarani. Makao ya kuwakimu ni machache kama walivyo
    wahudumu wa kijamii, suluhu ni nini? Tuwatupe katika ukumbi wa kijamii, ambao watahepa pindi tu,
    wapatapo fürsa ndogo au wapelekwe huduma kwa vijana wa Taifa, ambapo wachache wanaweza
    kutunzwa kwa wakati mmoja. Ili kufaulu kwa wengine, sharti wawe katika vituo vya urekebishaji tabia
    za matumizi ya dawa za kulevya. Tuwakabidhi polisi kwa sababu wanaranda au tujaribu kuungana na
    vituo vya urekebishaji tabia kuhakikisha hawatarudi barabarani.
    Mazingira ya lokesheni pia huibuka katika ajenda. Hali ya barabara, juhudi za kusafisha
    mazingira, wizi wa maji na umeme, usafiri wa umma, uchafuzi wa mazingira, hewa na kelele, hii
    inatokea kupitia malalamishi ya watu wanaoishi karibu na mabaa na uzingativu wa saa ya biashara
    hujadiliwa kila mara. Chifu ni sharti afahamu sheria na kanuni zinazotawala hali hizo, halafu ajadili na
    wahusika kabla ya kutoa mwelekeo. Usawa na uwazi katika kugawa fedha za Hazina ya maendeleo ya
    maeneo Bunge, pia hujadiliwa.
    Katika maswala haya mengine, chifu ndiye aliye nyanjani. Anawajibikia jamii na wakubwa
    wake na hatarajii shukrani au kutambuliwa kwa kazi njema aliyofanya. Isipokuwa hukashifiwa anapofeli.
    Watu wengine wana taswira ya Chifu kama mtu kwenye jukwa, kofia yake. na kifimbo kinachompa
    mamlaka ya kuhutubia baraza, Kajubu tyji zaidi ya hivyo. Kwa mujibu wa kitabu cha
    mafunzo ya machifu na Naibu wao (Januari 2004), wajibu wa chifu ni kuwakilisha sera na mipango ya
    serikali kwa wananchi. Chifu ni ajenti wa “mabadiliko” mwenye wajibu Wa kuhamasisha watu katika
    maendeleo. Anajishughulisha na kujua ni nani maskini katika lokesheni, mkoa, mgonjwa asiyeweza
    kupata tiba na kupanga jinsi mhasiriwa atakavyopelekwa hospitali kama anavyoweza. Ni sharti
    ashughulikie ugomvi wa kinyumbani, uhalifu wa watoto, dhuluma za watoto, agawe chakula na mavazi
    kwa wahitaji na kuhukumu kesi ndogo za wizi na uharibifu. Chifu hutatua kesi za kisheria kwa
    wasioweza kumudu wakili. Wakati wananchi wanapohisi mbunge wao hafikiliki na hawana imani na
    polisi, chifu ndiye suluhisho.
    Lakini kuna machifu wachache ambao hawafanyi kazi yao vyema. Kwa ufupi, chifu ni
    mkusanyiko wa kushngaza; mfalme katika himaya yake, pasta, baba msikivu, wanasaikolojia, mtunga
    sheria na mdumisha sheria, balozi mchaguzi, mama, mlumbi na askari asiyechelewa. Ingawa halipwi
    vyema, anafanya kazi bila tarakilishi, na aghalabu hujilipia gharama ya kodi ya afisi yake kutoka mfuko
    wake. Kwa sababu ni mtumishi wa umma, tunataraji afanye kazi mufti. Hiyo haimaanishi tusishukuru
    kwa kazi njema aliyofanya. Serikali inaweza kufanya hivi kwa kuimarisha hali yake ya kazi, mazingira
    yake ya kikazi, na kuhakikisha yana tarakilishi, anapata mafunzo ya uongozi na usimamizi. Wananchi
    sharti washukuru watu hawa kwa kujitolea sabili.

    Maswali
    a) Fupisha aya nne za kwanza (Maneno 60)
    Matayarisho
    Jibu
    b) Kwa maneno kati ya 80-90 fupisha aya ya tano hadi mwisho.
    Matayarisho
    Jibu

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma taarifa ifuatayo halafu ujibu maswali Kama kuna jambo ambalo limeiparaganya akili yamahuluki ni kuielewa dhana ya demokrasia. Kiumbe huyu heshi kuuliza mkururo wa maswali. Demokrasia ni...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo halafu ujibu maswali
    Kama kuna jambo ambalo limeiparaganya akili yamahuluki ni kuielewa dhana ya demokrasia.
    Kiumbe huyu heshi kuuliza mkururo wa maswali. Demokrasia ni nini hasa? Tunaweza kula demokrasia?
    Ni dude gani hili lina kichwa au mkia pekee yake? Je demokrasia inazuia njaa? Demokrasia ni himaya ya
    wasomi tu au vilevile ni haki ya mafalahi? Kwa muda mrefu kumekuwa na kinyang‟anyiro kikubwa
    katika jamii ambacho azma na. matokeo yake yamekuwa ya kutatanisha. Baadhi ya watu wamejitokeza
    kama mchuzi wa ugali na kuzusha zahama ambazo si za kuyumkinika. Vichwa vya adinasi vikafyekwa
    kwa miundo na maparange na matumbo yakapasuliwa na kuapakaza utumbo na vijusi kila mahali. Shingo
    zikapigiwa vigingi na kukomewa ardhini. Demokrasia si mchezo wa lelemama. Ni sharti tujifunge
    vibwebwe tumwage damu na tufe ili tupate demokrasia ya kweli!” Mmoja wa mibabe wa demokrasia
    alinguruma kadamnasi ya umati huku ngoma za vita zikirindima.” Hata Marekani na ulaya walimwaga
    damu. Mamilioni ya watu walipukutishwa na kimbunga cha demokrasia. Chini walilaliana kama Vimatu
    na tunutu. Hawa manafiki wanafikiri hatuwajui. Katu hatutakubali porojo zao. Wanatupikia majungu
    kisha wakatoweka. Kuna demokrasia ya Afrika na ile ya Ulaya „ mkereketwa wa Uafrika akachanganua.
    Demokrasia ya Afrika basi imefuata mkondo huu wa umwagikaji damu. Kila kukijiri uchaguzi
    zahama hutawala. Walio madarakani hawataki kubanduka. Hutaruta visababu vya kukwepa wimbi la
    ushinde. Demokrasia ni mchezo wa mizengwe tu ati. Hali hil imesababisha maafa makubwa, uharibifu
    mkubwa wa mali, majeraha, ukimbizi wa raia ndani na nje ya mataifa husika, dhuluma za kimapenzi
    dhidi ya wanawake, kuzagaa kwa magonjwa ainati, uhasama wa kikabila. Jambo la kusikitisha ni
    kwamba raia na viongozi hawaelekei kujifundisha chochote kutokana na hali. Huku mataifa mengi
    Ulayani na Asia yakikwea daraja moja baada ya nyingine kimaendeleo, Afrika imedumaa tu. Imesalia
    kuimba ule wimbo wake wa kutokea azali„ Tutaendelea vipi na tunadhulimiwa na kaka wakubwa”. Siasa
    ya demokrasia katika bara la Afrika ina tija kubwa hususan kwa wale wachache wanaofanikiwa kudhibiti
    nyenzo za kutia tonge kinywani. Ulitima wa umma husalia miradi hewa ya tabaka la viongozi ambayo
    hutumiwa kujinadi zamu nyingine ifikapo tena. Demokrasia ya kweli imo mikononi mwa umma pale
    utakapojikomboa kimawazo na kwa ujasiri kudai huduma bora, uajibikaji na kuheshimiwa kwa mkataba
    wa kijamii uliosisiwa na Jean Jacques Rousseau.

    Maswali
    a) Binadamu amechanganyika kwa njia ipi?
    b) Ni vipi Demokrasia ya kweli inaweza kufikiwa
    c) Kwa nini inasemekana kuwa „Demokrasia ni mchezo wa mizengwe?
    d) Ni athari gani hutokana na kinyang‟anyiro cha Demokrasia?
    e) “Dhiki za raia zimesalia kuwa mradi-hewa wa wanasiasa” Eleza.
    f) Fafanua maana ya maneno na mafungu yafuatayo jinsi yalivyotumika katika taarifa.
    i) Mafahali
    ii) Wanatupikia majungu
    iii) Ukarabati

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Toa maana mbili ya sentensi ifuatayo: Laleni!(Solved)

    Toa maana mbili ya sentensi ifuatayo:
    Laleni!

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Nomino zifuatazo ziko katika ngeli gani? i. Nyasi ii. Furaha(Solved)

    Nomino zifuatazo ziko katika ngeli gani?
    i. Nyasi
    ii. Furaha

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi mbili ukitumia mzizi uliopewa ili kuonyesha mwingiliano wa maneno katika mabano. -baya (kivumishi kuwa kiwakilishi)(Solved)

    Tunga sentensi mbili ukitumia mzizi uliopewa ili kuonyesha mwingiliano wa maneno katika mabano.
    -baya (kivumishi kuwa kiwakilishi)

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tofautisha maana ya sentensi zifuatazo. i. Ningeenda leo ningefika mapema. ii. Ningalienda ningalifika mapema.(Solved)

    Tofautisha maana ya sentensi zifuatazo.
    i. Ningeenda leo ningefika mapema.
    ii. Ningalienda ningalifika mapema.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika maana mbili za sentensi ifuatayo. Wanafunzi walipigia wazazi wao simu.(Solved)

    Andika maana mbili za sentensi ifuatayo.
    Wanafunzi walipigia wazazi wao simu.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi uliyopewa upya bila matumizi ya ‘amba’ Ndoo ambayo ilinunuliwa ilivunjwa jana.(Solved)

    Tunga sentensi uliyopewa upya bila matumizi ya ‘amba’
    Ndoo ambayo ilinunuliwa ilivunjwa jana.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha Nomino na ueleze aina katika sentensi ifuatayo: Warembo walijifukiza manukato na kuvalia mavazi ya kupendeza.(Solved)

    Onyesha Nomino na ueleze aina katika sentensi ifuatayo:
    Warembo walijifukiza manukato na kuvalia mavazi ya kupendeza.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Sahihisha sentensi zifuatazo. i. Hao mandugu wamekosana juu ya pesa. ii. Mtu mwenye anakula mkate ametumana aletewe chai.(Solved)

    Sahihisha sentensi zifuatazo.
    i. Hao mandugu wamekosana juu ya pesa.
    ii. Mtu mwenye anakula mkate ametumana aletewe chai.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Geuza kwa wingi. i. Njia hii huenda Kisumu ii. Wembe huu utafaa.(Solved)

    Geuza kwa wingi.
    i. Njia hii huenda Kisumu
    ii. Wembe huu utafaa.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi ifuatayo: Ningalifuzu katika mtihani wangu ningalituzwa.(Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo:
    Ningalifuzu katika mtihani wangu ningalituzwa.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Sahihisha sentensi ifutayo. Sukari zilizowekwa mfukoni zimenyeshewa.(Solved)

    Sahihisha sentensi ifutayo.
    Sukari zilizowekwa mfukoni zimenyeshewa.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha vitenzi kisha uvieleze ni vya aina gani. i. Kakangu amewahi kutembelea makavazi ya kitaifa. ii. Hamisi ni daktari wa meno.(Solved)

    Onyesha vitenzi kisha uvieleze ni vya aina gani.
    i. Kakangu amewahi kutembelea makavazi ya kitaifa.
    ii. Hamisi ni daktari wa meno.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Ainisha sentensi hii: Kilichopikwa(Solved)

    Ainisha sentensi hii:
    Kilichopikwa

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Andika maneno yaliyo na aina za silabi zifuatazo: i. Silabi za irabu pekee ii. Silabi za konsonanti, nusu irabu na irabu iii. Silabi za konsonanti pekee(Solved)

    Andika maneno yaliyo na aina za silabi zifuatazo:
    i. Silabi za irabu pekee
    ii. Silabi za konsonanti, nusu irabu na irabu
    iii. Silabi za konsonanti pekee

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • SOMA SHAIRI LIFUATALO KISHA UJIBU MASWALI. Malezi mema Malezi bora si yale, mtoto kumdekeza Atafikia kilele, mzazi atampuza(Solved)

    SOMA SHAIRI LIFUATALO KISHA UJIBU MASWALI.
    Malezi mema
    Malezi bora si yale, mtoto kumdekeza
    Atafikia kilele, mzazi atampuza
    Utapiga makelele, wala hatasikiza.
    Daima usikubali, kuridhi kumpendeza
    Lazima uwe mkali, mengine kumkataza
    Na wala usikubali, maneno kuyaigiza.
    Mtoto ukimuita, hana budi kuginiza
    Sio mdomo kufyata, mamboye kuendeleza
    Ama dakika zapita,aje ikimpendeza.
    Mzazi usithubutu,mwanao kumteteza
    Uambiwapo na watu, mwanao alifanyiza
    Kuwa na hali ya utu, Kadhia kuchunguza.
    Iwapo amekusudi, makossa kuyatimiza
    Kumrudi huna budi,jukumu kutekekeza
    Lau usipomrudi, kosa taliendeleza.

    Maswali
    a) Eleza malezi mema jinsi yanavyosimuliwa na mshairi.
    b) Taja mambo matano wanayoshauriwa wazazi kutoyatenda
    c) Je, mzazi asipochukua jukumu lake, kuna athari gani kwa mtoto
    d) Toa methali moja inayoambatana na ujumbe wa Shairi hili
    e) Shairi hili lina mishororo ngapi
    f) eleza vina,vipande na mizani vya Shairi hili
    g) eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika Shairi.
    i. kumdekeza
    ii. kuginiza
    iii. mdomo kufyata
    iv. alofanyiza
    v. lau usipomrudi

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • “nikitembea yuko, nikikimbia yuko, nikiingia ndani hayuko" i. tambua kipera hiki ii. taja dhima moja ya kipera hiki kijumla(Solved)

    “nikitembea yuko, nikikimbia yuko, nikiingia ndani hayuko"
    i. tambua kipera hiki
    ii. taja dhima moja ya kipera hiki kijumla

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuatia Malenga mlotukuka, kwa tungo zenu teule Tungo zenye kusifika, zenye nasaha tele(Solved)

    Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuatia
    Malenga mlotukuka, kwa tungo zenu teule
    Tungo zenye kusifika, zenye nasaha tele
    Naomba la uhakika, jawabu enyi wavyele
    Wa kuume tangu lini, kuukata wakushoto!
    Tangu dahari miaka, mikono ina upole
    Meungana pasi shaka, ni miwili vile vile
    Mmoja ukisumbuka, mwingine hujaa ndwele
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto!

    MASWALI
    a. Shairi hili ni la arudhi. Dhibitisha kwa kutoa sababu tatu
    b. Nakili kibwagizo cha shairi hili
    c. Eleza ujumbe mmoja unaojitokeza kwenye shairi

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)

  • Matumizi ya lugha hutegemea mambo kadhaa. Yaeleze yoyote manne.(Solved)

    Matumizi ya lugha hutegemea mambo kadhaa. Yaeleze yoyote manne.

    Date posted: November 25, 2022.  Answers (1)