Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.

      

“Shaka ya Mambo” (Farouk Topan)
Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.

  

Answers


sharon
(a) Esther ana shaka ya mambo iwapo atabadilishiwa zamu na Grace ili aingie asubuhi na kutoka saa nane aende chuoni kusomea usekretari.
(b) Esther ana shaka ya mambo kwa kuwa siku hiyo Kamata hakuja kumjulia hali kama ilivyo kawaida yake apatapo nafasi na isitoshe anapompigia simu haipokei.
(c) Esther ana shaka ya mambo iwapo kweli Kamata anamjali au anashughulika kutafuta pesa.
(d) Esther ana shaka ya mambo iwapo uhuru alioutafuta ataupata kwani hata mzee Mwinyi anamchunga kama alivyochungwa nyumbani kwao.
(e) Esther ana shaka ya mambo iwapo Kamata atamfikishia pesa yule mteja mzungu aliyezisahau mezani kwani hakumjua.
(f) Mzungu mteja ana shaka ya mambo iwapo atapata usafiri kuelekea Dubai kwa mkutano siku iliyofuata kwani ndege aliyostahili kusafiria imehairishwa mara mbili.
(g) Esther ana shaka ya mambo iwapo Grace na Kamata wana uhusiano wa kimapenzi kwani Grace alimwita kamata mpenzi na walitoka pamoja siku hiyo.
(h) Esther anaposimamiwa na mvulana kwenye matatu ana shaka ya mambo Kamata anaweza kusimama na kumwachia kiti.
(i) Abiria mmoja aliyetaka kuingia matatu ana magari ya matatu yanaruhusiwa kuingia uwanja wa ndege.
(j) Esther ana shaka ya mambo mle vilabuni anamopenda Kamata kumpeleka mna usalama.
(k) Esther ana shaka ya mambo iwapo Kamata bado anamjali hasa baada ya kukataa kwenda naye disko tena ikizingatiwa kwamba wavulana hukosa subira.
(l) Esther and shaka ya mambo kuhusu uhusiano wa Kamata kwa vile wanaishi mtaa mmoja, walisoma pamoja na huja kazini pamoja.

sharon kalunda answered the question on October 3, 2019 at 06:10


Next: Outline the specific skills involved in successful communication.
Previous: Study the ray diagram in figure below. The observer should be able to see the reflected image after the mirror M2. Show the position of...

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • "Nashangaa vile kwetu tunavyoabudu watu hao wasiotujali."(Solved)

    “Damu Nyeusi” (Ken Walibora)
    "Nashangaa vile kwetu tunavyoabudu watu hao wasiotujali."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Bainisha matumizi ya mbinu ya ishara kwa kurejelea hadithi ya gilasi ya mwisho makaburini.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Anayeambiwa alisema nini baada ya kuambiwa haya?
    c) Thibitisha kuwa wanacheneo walipanda pojo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Taja aina nne za hadithi.(Solved)

    Taja aina nne za hadithi.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Siwe ulosema jana, ya kuwa u mashuhuri? Ya kuwa wajuwa sana, aidha huna kiburi? Nchini wajulikana, mwanasiasa mahiri, Bungeni tukuajiri?(Solved)

    SIWE?

    1. Siwe ulosema jana, ya kuwa u mashuhuri?
    Ya kuwa wajuwa sana, aidha huna kiburi?
    Nchini wajulikana, mwanasiasa mahiri,
    Bungeni tukuajiri?

    2. Siwe ulotushawishi, kwa chumvi na kwa sukari,
    Na matamu matamshi, ukaziteka suduri,
    Ukanena penya moshi, moto ndiyo yakwe siri,
    Nawe ndiye hiyo nari?

    3. Siwe uloji‘ta moto, uwakao biribiri,
    Kamba ‗tatia fukuto, Litakalo leta kheri‘,
    Utatufunua mato, Maisha yawe mazuri,
    Tukupe kura waziri?

    4. Siwe ulosema hayo, na mengi ukabashiri,
    Ukamba wafata nyayo, nyayo ziso utiriri,
    Tusiwe na wayowayo, wa kufikirifikiri,
    Tukuachie ujari?

    5. Siwe tulokuinua, Mabegani kama mwari,
    Tungawa twalemelewa, waume tukajasiri,
    Kamba tukikuchaguwa, mema kwetu yatajiri,
    Tukakeyi kusubiri?

    6. Siwe ulotugeuka, kwamba leo u waziri,
    Wajiona melimuka, tena ukawa ayari,
    Walaghai ukicheka, ukuu umekughuri,
    Leo mekuwa hodari?

    7. Siwe ulojawa raha, za hino yetu sayari,
    Ukawa ja vile shaha, hatukupati shauri,
    kutuona ni karaha, wakatiwo twahasiri,
    Ushakiya msitari?

    8. Siwe uliyetughura, ukafunga na safari,
    Ukaelekea bara, Kwa wenzio matajiri,
    Ukatuacha majura, na tama kukithiri,
    Kanama Ushaghairi?

    9. Siwe uliyetuasi, ukenda pasi kwaheri,
    Mbona hutwambii nasi, tukajua yetu shari,
    Leo una masidisi, husemi na aso gari,
    Ndio mezidi jeuri?

    10. Siwe‘lotwaa mgwisho, ukawa wajifakhiri?
    Chenye mwanzo kina mwisho, hilo wajuwa dhahiri,
    Vyaja kutoka vitisho, kwani hayo sidahari,
    Mambo mengimdawari?

    11. Siwe utakayeiza, mwishowo ukidhihiri,
    Siku itayoteleza, kuja kwetu ansari,
    Kuja kutubembeleza, kwa nyunga nalo khamri,
    Tauya nazo nadhiri.

    MASWALI
    a) Mtunzi wa shairi hili ana dhamira gani?
    b) Taja na ueleze bahari tatu za shairi hili?
    c) Onyesha jinsi mtunzi alivyotumia idhini ya kishairi.
    d) Taja na ufafanue tamahali ya usemi iliyotawala katika shairi hili.
    e) Anayerejelewa alibailika vipi? Eleza.
    f) Andika ubeti wa tisa kwa lugha ya nathari.
    g) Mshairi ana maana gani kwa kusema:
    (i) Wakatiwo twahasiri.
    (ii) Ukaziteka suduri.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.(Solved)

    Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Nimemwita bwana huyu aje huku juu kusudi mumwone."(Solved)

    Damu nyeusi na hadithi zingine
    "Nimemwita bwana huyu aje huku juu kusudi mumwone."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa tatu za mzungumzaji.
    c) Jadili maudhui ya ubaguzi namna yanavyojitokeza katika hadithi husika

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"(Solved)

    Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
    "Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
    a) Eleza muktadha wa maneno haya.
    b) Eleza umuhimu wa mrejelewa katika dondoo hili kwenye riwaya.
    c) Eleza maisha ya msemaji yalivyokuwa kwa mujibu wa Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Kutowajibika kwa viongozi baada ya mkoloni kuondoka ni dhahiri." Jadili kauli hii kwa mujibu wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    "Kutowajibika kwa viongozi baada ya mkoloni kuondoka ni dhahiri." Jadili kauli hii kwa mujibu wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."(Solved)

    Mstahiki Meya.
    "Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa zozote nne za msemaji.
    c) Fafanua maudhui ya ufisadi kama yalivyoangaziwa na mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

    1) Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,
    Mpateni mweleweni, mchekeni, mlieni,
    Funzo lake mpateni, uamuzi mfanyeni,
    Kisa hiki asilani, sisahau maishani.

    2) Cha nne niliingiya, mtoto kafurahiya,
    Malkia ungedhaniya, duniani meingiya,
    Mapambo lijipambiya, kung‘ara kikang‘ariya,
    Kisa change chatokeya, mwanzowe nafunguliya.

    3) Darasani lizembea, bidii sikutilia,
    Starehe nakwambia, nilipenda najutia,
    Kimadaha litembea, tausi nilitulia,
    Kisa kilinigonjea, mtume! Ningalijua.

    4) Muhula kutamatika, dafu sikufua, kaka,
    Enda, Ewe, Embe, fika, alama duni, viraka,
    Nilipokea waraka, mzazi kahitajika,
    Kisa kijatambulika, nakuomba makinika.

    5) Muhula wa pili sasa, nikarudia makosa,
    Sikupigeni msasa, makali nikayakosa,
    Kisu sikunoa hasa, sikukata cha darasa,
    Kisa ndicho hicho sasa, ninakupa pasi pesa.

    6) Sasa muhula wa tatu, umetimia wanetu,
    Mtihani kama chatu, nimeuogopa, mtu,
    Sijausomea katu, ningalilindaje utu?
    Kisa mkasa wa chatu, kilinipata wa kwetu.

    7) Mbwa katu hafi maji, kiona ufuko, maji,
    Tajaribu sife maji, hata akiyanywa maji,
    Ilibidi twende jiji, kuwasaka wajuaji,
    Kisa change mfumbaji, sasa dawa lihitaji.

    8) Mpango ulitolewa, mchango ulipangiwa,
    Pesa tele litolewa, na simu kununuliwa,
    Mtandao liwekewa, ‗kunani‘ kupakuliwa,
    Kisa cha simu kujuwa, linifanya kupagawa.

    9) Tulikata dari ona, simu yetu kufichana,
    Usiku tulikutana, maswali kurushiana,
    Majibu tulipeana, "panga‘ kabadilishana,
    Kisa kinajulikana, vile nilivyokazana.

    10) Niliyangoja majibu, nikiwa na hamu, babu,
    Nilikimya kama bubu, nisije toa aibu,
    Nilivichoma vitabu, bila kuwa na sababu.
    Kisa kawa masaibu, kashindwa kuyaharibu.

    11) Kutangazwa matokeo, nakumbuka hadi leo,
    Lilishangaza toleo, sikuamini redio,
    Lipokea matokea, yalinitia kimbio,
    Kisa change mchocheo, haya yangu mapokeo.

    12) Nilifeli mtihani, sababu simu juweni,
    Najuta nisameheni, nijilaumu moyoni,
    Ningalijua mbeleni, ningalisoma jamani,
    Kisa nimemalizeli, wenzangu mzindukeni.

    13) Watahiniwa mlipo, msiwe mithili popo,
    Skuli kwenu kuwepo, nia mpate malipo,
    Bidii hapo mlipo, toa uzembe pasipo,
    Kisa change kingalipo, simu daima siwepo!

    MASWALI
    a) Taja anwani mwafaka ya shairi hili.
    b) Fafanua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi hili.
    c) Bainisha nafsi lengwa katika shairi hili.
    d) Changanua arudhi zilizotumiwa na mtunzi wa shairi hili.
    e) Andika ubeti wa kumi katika lugha nathari.
    f) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    g) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    (i) Sikukata cha darasa
    (ii) Yalinitia kimbio
    (iii) Kupagawa

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"(Solved)

    Damu nyeusi na hadithi zingine
    "Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili.
    c) Huku ukitoa mifano, thibitisha maudhui sita ambayo yamejitokeza katika hadithi ya Damu Nyeusi na wanayoyaendeleza.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kutoa mifano kumi,eleza vizingiti walivyokumbana navyo wanacheneo wakati wa kupigania mageuzi.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Kwa kutoa mifano kumi,eleza vizingiti walivyokumbana navyo wanacheneo wakati wa kupigania mageuzi.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Iwapo umefanya, yapo mengi ambayo hayakunyoka."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Iwapo umefanya, yapo mengi ambayo hayakunyoka."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Tambua mbinu moja iliyotumika katika muktadha wa dondoo.
    c) Fafanua kauli kwamba"yapo mengi ambayo hayakunyoka".
    d) Eleza jinsi baadhi ya wahusika walivyojaribu kuyanyoosha.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Ni nini sifa za mvuto zinazowaleta pamoja mzungumzaji na mzungumziwa.
    c) Tambua na ufafanue mbinu inayotumika katika dondoo.
    d) Kwa mifano mwafaka fafanua tanzia hiyo inayorejelewa katika dondoo.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".(Solved)

    DAMU NYEUSI
    "Ikamchagiza kama vile kiu ya mtu aliyekuwa akisafiri jangwani".
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili
    (b) Fafanua sifa zozote nne za mrejelewa
    (c) Eleza fani uliotumiwa na mwandishi katika dondoo hili
    (d) Kwa kurejea hadithi zozote tatu,eleza namna wahusika wowote watatu walivyoathiriwa na kiu.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?(Solved)

    Mstahiki Meya
    Nonsense! Hivi huyu ana nia gani?
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja na ueleze mbinu za lugha zinazojitokeza katika dondoo hili.
    (c) Jadili umuhimu wa msemaji katika tamthilia hii.
    (d) Jadili njia za kuondoa uozo katika jamii ukijikita katika tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.(Solved)

    Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
    (a) Jazanda
    (b) Uzungumzi nafsia
    (c) Majazi
    (d) Methali
    (e) Taharuki

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.(Solved)

    Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)