Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

"Leo ndio mtanitambua. Mama gani anayemtazama mwana akigeuka afriti?"

      

Damu nyeusi na hadithi zingine
"Leo ndio mtanitambua. Mama gani anayemtazama mwana akigeuka afriti?"
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Tambua "mwana aliyegeuka afriti‘na ueleze hulka zake nne.
(c) Jadili maudhui yoyote matano yanayojitokeza katika hadithi husika.

  

Answers


sharon
(a) Mzungumzaji Mzee Butali
Mzungumziwa Sela na mamake
Mahali Nyumbani mwao
Walikuwa wamerudi nyumbani kutoka shuleni mwao ambapo walikuwa wamefulishwa hususu mimba ya Sela.
Kutokana na ghadhabu ya habari hii ndipo anayatamka maneno haya.
Hatimaye anaamua kuwafurusha Sela na mamake kutoka nyumbani licha ya tetesi kutoka kwa wana kijiji.
(b)
Sela: Huka zake ni;
- Mwepesi wa kushawishika - Anashawishiwa kwa wepesi na Chris na kushiriki ngono naye.
- Mwenye utu na huruma - Alimhurumia Chris alipokuwa mgonjwa.
- Mwenye upenod wa dhati - Alimpenda sana Chris na mwanawe Kadogo.
- Karimu - Alimpokea vizuri Chris shuleni mwao na kumsaidia kwenda zahanatini.
- Msaliti - Aliwasaliti wazazi wake kwa kushirikiana na Chris kumuiba Kadogo.
- Amewajibika - Anataka kumlea Kadogo. (al 6 x 1 = al 6)
(c)
- Usaliti - Sela aliwasaliti wazazi kwa kushirikiana na Chris kumuiba Kadogo.
- Ndoa ya mapema - Chris na Sela wanafanya mapenzi nje ya ndoa na kufunga ndoa wakiwa wangali wachanga.
- Nafasi ya mwanamke - Mwanmke amejitokeza kama chombo cha kutumiza ashiki ya mwanamme.
- Sela unashawishia kwa wepesi kushiriki mapenzi na Chris.
- Umaskini. - Kutokana na umaskini Chris anaamua kuhamia mjini kutafuta kibarua cha kuvuna mikonge ambacho mapato yake yalimwezesha tu kulipa kodi ya chumba kidogo na kununua chakula.
- Ulaghai / uongo. - Chris anamlaghai Sela kuwa ni mgonjwa huku nia yake ikiwa kuwa na uhusiano naye.
- Taasubi ya kiume - Mzee Butali anamlaumu mkewe kwa mienendo ya Sela.
sharon kalunda answered the question on October 4, 2019 at 08:43


Next: The table below shows the results of an experiment carried out to determine the rate of photosynthesis at different light intensities and varying Carbon (IV)...
Previous:  Chamkosi alipiga goti huku machozi yakimdondoka njia nne nne. Mbele yake, palikuwa na makaburi mawili. Waliokuwa wamelala mle hawakuwa na habari juu ya...

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Wanawake, wanaoishi katika maeneo ya mashambani katika nchi ambazo zinazoendelea ni baadhi ya watu waliotopea na kubobea katika uchochole mkubwa.(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo.
    Wanawake, wanaoishi katika maeneo ya mashambani katika nchi ambazo zinazoendelea ni baadhi ya watu waliotopea na kubobea katika uchochole mkubwa. Jumla ya idadi kubwa ya wanawake hawa wanaoishi chini ya kiwango cha chini, cha umaskini inakadiriwa kuwa zaidi ya milioni 600. Hii ni idadi kubwa hasa ikikumbukwa kuwa ni asilimia kubwa ya wanawake inayoishi kwa maeneo haya. Ulimwengu umeshuhudia ongezeko kubwa la idadi ya watu pamoja na kuwako kwa matatizo ya kiuchumi duniani.Kadhalika matatizo mengine ni mitarafuku na vita vya kikabila, majanga ya kiasili mathalani mafuriko , ukame na milipuko ya volkano. Usisahau kuwa pia kina uharibifu wa kimazingira, mabadiliko ya desturi na kusambaratika kwa familia na misingi yake. Tatizo lingine ni kuwa kuna kuongezeka kwa hali ya wanawake kuwa wazazi pekee na hivyo kuongeza familia zinazosimamiwa na wanawake ( ambao tumewataja kuwa wanakumbwa na umaskini mkubwa).Wanawake wanaoishi mashambani wanakumbwa na makubwa. Kwanza, kama maskini wanaishi katika mazingiramagumu. Vile vile kama wanawake wanakabiliana na mapendeleo ya kisera na kitamaduni yanayowadharau na kuwapuuza wanawake na mchango wao katika maendeleo. Tatu, kama viongozi wa familia hasa wanaolea na kutunza jamaa na mzazi mmoja, wanapambana na uogonzi wa familia pamoja na uzalishaji. Aghalabu hawapati usaidizi wowote katika majukumu kama haya bali wanalazimika kupambana nayo peke yao. Kutokana na hayo yote wanawake hawapati nafasi nzuri kushiriki katika maamuzi ya maswala yanayowahusu. Maswala mengi yanaamuliwa na wanaume pasipokuwahusisha wanawake. Licha ya dhiki yao kubwa, wanawake hawa wanachangia katika maendeleo ya jammi na kiuchumi kwa njia mbalimbali. Mchango huu unaonekana katika kiwango cha jamii,taifa na familia. Katika kiwango cha kijamii na kitaifa wanawake ndio chazo cha nguvukazi kwani ni wao na watoto wao wanatekeleza kazi nyingi hasa za nyumbani na mashambani. Mara nyingi huwa na uwezo bora wa kutunza chochote walichonacho kuliko wenzao wanaume.
    Kifamilia wanawake wa shambani wanashughulika mchana kutwa katika hali ngumu ya hewa aidha jua kali au mvua huku wameeleka wanao migongoni wakilima mashamba ili kupata chakula kwa familia zao. Jukumu la kuandaa chakula nyumbani bado linaachiwa wale wale wanawake wanaokizalisha mashambani.
    Jambo lisilopingika ni kwamba wanawake wanatekeleza majuku makubwa na muhimu katika kizazi cha binadamu na ndio hasa miimili ya jamii yoyote staarabu. Kwa hivyo, ni kinaya kitupu kudhalilisha wanawake. Mataifa mengi yaliyoendelea ni yale yaliyoondoa vikwazo vyote mbele ya wanawake na kuwaacha watekeleze wajibu wao. Kadhalika wanaume wa huko wanawaona wanawake kama wenzao katika kujenga jamii wala sio watumwa au watumishi wao wanaoumia na kutumikishwa kama vifaa na bidhaa. Inafaa jamii zinazodinisha wanawake zitambue kuwa ubaya wa tendo hili sio tu kudumaza maendeleo yake bali pia kutoa mfano mbaya kwa vijana ambao wataendeleza Ukandamizaji huu kwa vizazi vijavyo. Kwa hivyo, jamii inawajibika kutenda lililo sawa kwa kuwapa hadhi wanawake wote.

    Maswali
    a) Ipe taarifa hii anwani mwafaka
    b) Nakili maafa matatu ya kimaumbile yaliyotajwa katika kifungu hiki.
    c) Eleza sababu tatu zinazowazuia wanawake kushiriki katika maamuzi ya masuala yanayowahusu kulingana na makala haya.
    d) Wanawake hutekeleza majukumu gani katika jamii na taifa kutokana na makala haya?
    e) Kuna tofauti gani baina ya wanawake wa mataifa yaliyoendelea nay ale ambayo hayajastawi.
    f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa kwenye taarifa:
    i) uchochole
    ii) kudhalilisha
    iii) mitafuruku

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Jadili changamoto za elimu katika hadithi ya Kanda la Usufi.(Solved)

    Jadili changamoto za elimu katika hadithi ya Kanda la Usufi.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Sikufahamu ikiwa hisia zenyewe zilikuwa kwa sababu ya "furaha au huzuni." Potelea pote! Liwalo naliwe!! Nilisikia sauti Fulani ikinadi ndani katika nafsi yangu.(Solved)

    Damu Nyeusi na Hadithi nyingine
    Ndoa ya samani (Omar Babu)
    Sikufahamu ikiwa hisia zenyewe zilikuwa kwa sababu ya "furaha au huzuni." Potelea pote! Liwalo naliwe!! Nilisikia sauti Fulani ikinadi ndani katika nafsi yangu.
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Bainisha tamathali mbiliza usemi katika dondoo hili.
    c) Ni yapi yaliyodhihirisha 'furaha au huzuni' katika hisia za anayeelezwa?

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Uongozi mbaya una athari kadhaa. Thibitisha madai haya kwa kurejelea Tamthili ya Mstahiki Meya.(Solved)

    Uongozi mbaya una athari kadhaa. Thibitisha madai haya kwa kurejelea Tamthili ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Ndiyo yale ya "ngome in‘tuumiza naswi tu mumo ngomeni.‘(Solved)

    Mshtahiki Meya: T. Arege
    Ndiyo yale ya "ngome in‘tuumiza naswi tu mumo ngomeni.‘
    a) Weka dondoo hili katika muktadha wake.
    b) Tambua tamathali mbili za usemi zilizo tumika latika dondoo hili.
    c) Kwa kurejelea tamthilia onyesha jinsi ngome inavyowaumiza wanacheneo.
    d) Wanacheneo wanatumia mikakati gani kukabiliana na hali ya (c) hapo juu.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha jinsi mwandishi wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alivyoshughulikia Nafasi ya mwanamke.(Solved)

    Onyesha jinsi mwandishi wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alivyoshughulikia Nafasi ya mwanamke.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha jinsi mwandishi wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alivyoshughulikia Nafasi ya vijana.(Solved)

    Onyesha jinsi mwandishi wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alivyoshughulikia Nafasi ya vijana.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • Kuna mfanano mkubwa kati ya ulumbi na hotuba. Thibitisha.(Solved)

    Kuna mfanano mkubwa kati ya ulumbi na hotuba. Thibitisha.

    Date posted: October 4, 2019.  Answers (1)

  • "Wema wako umeniua kabisa………Nina jishtaki mwenyewe kila siku kwa miaka na miaka".(Solved)

    KIDAGAA KIMEMWOZEA: Ken Walibora.
    "Wema wako umeniua kabisa………Nina jishtaki mwenyewe kila siku kwa miaka na miaka".
    (a) Eleza muktadha wa maneno haya.
    (b) Onyesha kwa kutoa mifano kuwa anayeambiwa maneno haya alikuwa na wema.
    (c) Eleza umuhimu wa mhusika mashaka katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Dhiki mbalimbali zimekuwapo lakini heri nusu shari kuliko shari kamili".(Solved)

    Mstahiki Meya.
    "Dhiki mbalimbali zimekuwapo lakini heri nusu shari kuliko shari kamili".
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.
    (c) Eleza sifa zozote tatu za mzungumzaji.
    (d) Fafanua aina zozote nne za migogoro inayojitokeza katika tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Taja kitamkwa chenye sifa ifuatazo. Vokali ya nyuma, kati(Solved)

    Taja kitamkwa chenye sifa ifuatazo.
    Vokali ya nyuma, kati.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kuna sababu kadha za kuwako na kushamiri kwa ajira ya watoto.(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
    Kuna sababu kadha za kuwako na kushamiri kwa ajira ya watoto. Moja ya sababu hizo ni umaskini unaozikumba jamaa nyingi pamoja na welewa mdogo wa thamani ya elimu wa baadhi ya watu katika jamii. Wapo watoto ambao hushurutika kubeba jukumu la kujizumbulia riziki wenyewe kutokana na hali duni ya familia zao.
    Hali hii huweza kutokana na baadhi ya wazazi kutelekeza majukumu yao ya kimsingi ya kuikimu jamaa yao. Aidha kuna sehemu nyingine ambapo hali hii imetokana na janga sugu la ukimwi. Yapo maeneo ambako kuenea kwa ugonjwa huu kumewafanya viongozi wa jamaa kupukutika kama majani ya mti na kuwalazimisha watoto kuyakatiza masomo yao ili wawakidhie haja wadogo zao. Kuhusiana na kutelekeza majukumu, kuna wazazi ambao wanakosea kwa kutowaelekeza watoto wao kujua maadili mema ni yepi. Kwa njia hii watoto hao wanaishia kutumbukia kwenye matatizo makubwa.
    Baadhi ya ajira zina athari kubwa sana kwa watoto. Ukahaba, kwa mfano, ni mojawapo ya ajira ambazo watoto wa kike hulazimika kujiingiza. Hii ni ajira ambayo inaweza kuwatumbukiza watoto hao katika hatari kubwa kutokana na uwezekano mkubwa wa kuambukizwa maradhi ya ukimwi. Asillimia kubwa ya watoto wanaotumbukia katika ajira hii, inapatikana katika maeneo ya mijini na sehemu ambako utalii umeshamiri sana. Umaskini pamoja na dhiki za mijini huwalazimisha watoto hao wa kike kuishia kwenye biashara za aina hiyo. Wengine hufanyiwa hila na wafanyabiashara ambao wametovukwa na utu kutokana na tamaa yao kubwa ya kujitajirisha. Katika maeneo ambako utalii umeshamiri, ukahaba wa watoto unatokana na umaskini pamoja na kusambaa na kuenea kwa maadili ajinabi, ya ulimwengu usio wetu.
    Ikiwa umaskini ni chocheo kubwa la kuwapo kwa ajira ya watoto, basi inahalisi serikali zetu zifanye kila juhudi kuhakikisha kuwa umaskini umepigwa vita. Pana umuhimu wa kuhakikisha kuwa wanajamii wote wamepewa nafasi sawa za kujikwamua kutoka lindi la umaskini. Isitoshe, pana umuhimu wa juhudi nyingi kufanywa kuhakikisha kuwa nafasi za shule zimepanuliwa ili kuikidhi idadi kubwa ya watoto ambao wana kiu ya elimu. Serikali haina budi pia kuhakikisha kuwa zimepitishwa sheria zinazomlinda motto dhidi ya ukatili unaotokana na watu waliokosa hisia za utu na ubinadamu. Upo pia umuhimu wa kuvisaidia vikundi vinavyojitahidi kuwasaidia watoto ili kuzifanikisha juhudi zao kwa kuwa chanda kimoja hakivunji chawa kama tujuavyo.
    Hatua nyingine ambazo zinaweza kuchukuliwa ili kupunguza ajira ya watoto ni kuwahamasisha wanajamii kuhusu haki za mtoto. mtoto yeyote yule ana haki ya kupata elimu ya msingi. Mtoto pia ana haki ya kuishi na kupata mahitaji ya kimsingi na ya lazima kama chakula, malazi au makazi na matunzo ya kiafya. Aidha mtoto ana haki ya ukuaji, yaani kukua kikamilifu pasi na kizuizi na katika mazingira yasiyombana kwa njia yoyote ile. Isitoshe, mtoto ana haki ya kupata ulinzi dhidi ya unyanyaswaji au udhalilishwaji wa aina yoyote ile au hata maonevu kwenye misingi yoyote iwayo. Mtoto pia ana haki ya kuwa huru kushiriki katika jumuiya yake, kutoa maoni na kujieleza, kushirikiana na kujiunga na vikundi. Mwisho, na muhimu zaidi, mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya ajira au aina yoyote ya kazi ambayo inaihatarisha afya na siha yake au inamzuia asipate elimu.
    (a) Fupisha aya mbili za mwanzo bila kubadilisha maana. (maneno 60-70)
    (b) Eleza hoja muhimu zinazojitokeza katika aya mbili za mwisho. (Maneno 50-60)

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.(Solved)

    Tazamana na Mauti” (S.A. Mohammed)
    Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Uniulie nini na ndoa yetu na wewe inamhusu pia yeye?"(Solved)

    Mwana wa Darubini (K. Mwende Mbai)
    "Uniulie nini na ndoa yetu na wewe inamhusu pia yeye?"
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa zozote nne za msemewa.
    c) Jadili madhila yanayomkumba mwanamke katika hadithi hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Lazima kwanza mnihakikishie kuwa huyo sumu hapati hata fununu ya jambo hili."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Lazima kwanza mnihakikishie kuwa huyo sumu hapati hata fununu ya jambo hili."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Taja sifa zozote nne za msemaji.
    c) Andika umuhimu wa huyo sumu.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Tayari nimemkabidhi barua ya kujiuzulu ninapohusika."(Solved)

    Mstahiki Meya
    Tayari nimemkabidhi barua ya kujiuzulu ninapohusika."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Mbali na changamoto inayofanya msemaji kujiuzulu, jadili changamoto nyinginezo zinazowakumba wanacheneo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kufafanua hoja saba thibitisha kwamba kuna haja ya kuwa na Revolution.(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    Kwa kufafanua hoja saba thibitisha kwamba kuna haja ya kuwa na Revolution.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Lakini bila matumaini hatuwezi kwenda mbele na Revolution."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Lakini bila matumaini hatuwezi kwenda mbele na Revolution."
    i) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    ii) Bainisha tamathali moja ya usemi inayojitokeza katika dondoo hili.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
    Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,
    Ushairi niwapeni, hoja nitawaachia,
    Mnipe masikioni, shike nachoelezea,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Naanza kwa uzalendo, nchi yetu tuipende,
    Yadhihirishe matendo, nchi yetu tuilinde,
    Wa kila mtu mwendo, usije kawa mpinde,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili

    Wote tuwe na umoja, tuuache ukabila
    Kabila lisiwe hoja, mwenza kumnyima hela,
    Taifa letu ni moja, Mkenya ndilo kabila,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Linda demokrasia, uongozi tushiriki,
    Haki kujielezea, wachotaka na hutaki.
    Changu naweza tetea, demokrasia haki,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Tena adili usawa, mgao raslimali,
    Bajeti inapogawa, isawazishe ratili.
    Idara zilizoundwa, ‗faidi kila mahali,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Tuwe na uadilifu, twache tamaa ya hongo,
    Tusiwe na udhaifu, wa kuwa watu waongo,
    Tukomeshe uhalifu, kisha tuache maringo,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Ubinafsi si adili, ila ni kusaidia,
    Ukiwa nayo mali, asiyenacho patia,
    Kama mtu mswahili, ubinafsi achia,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Na inavyoelezea, katiba ni kielezi,
    Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi,
    Kwa hayo nitamwachia. hiyo ya ziada kazi,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili

    a) Eleza mambo yoyote manne ambayo mshairi anashauri taifa lifanye ili kuwa na aadili.
    b) Taja tamathali yoyote moja inayojitokeza katika shairi hili.
    c) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia kigezo kifuatacho :
    Mpangilio wa vina
    d) Bainisha nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili.
    e) Eleza toni ya shairi hili
    f) Eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa kishairi zilizotumiwa katika ubeti wa nne
    g) Andika ubeti wa pili kw lugha nathari
    h) Eleza maana ya neon lifuatalo kama ilivyotumiwa katika shairi:
    i) hongo

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)