
a)
- kuwa wazalendo / kuipenda nchi yako.
- kuwa na umoja / kuacha ukabila.
- kuiinda demokrasia
- kuwa na mgao sawa wa raslimali
- kuacha tamaa
- kukomesha uhalifu
- kuacha maringo
- kuacha ubinafsi / kusaidiana.
- kutii katiba za kwanza
b)
- Msemo - Nipe masikioni - Nipe sikio.
- Jazanda / isliari - kawa mpinde.
- Takriri - taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
- Tashbihi - kama mtu mswahiii.
- Utohozi - Demokrasia, bajeti ya kwanza
c) Ukaraguni - Vina vya kati na vya niwisho vinabadilikabadilika kutoka ubeti hadi mwigine.
d) Mwananchi / raia / mzalendo / mkereketwa
e) Himiza / nasihi / shawishi.
F) I) Kubananga / kufmyanga / kuboronga sarufi - Uongozi tushiriki - tushiriki uongozi, changu naweza tetea - naweza tetea
changu. Umuhimu - Kuleta urari wa vina
ii) Utohozi - Demokrasia
Umuhimu - Kuleta urari wa mizani - Kulipa upekee
iii) Inkisari - Pasi - pasipo
Wachotaka - Wachotaka.
Umuhimu - Kuleta urari wa mizani za kwanza
aina –
umuhimu-
g) Naanza kwa kueleza uzalendo kwamba tuipende nchi vetu / matendo yetu yaonyeshe kuwa tunailitida nchi yetu / tabia ya kila mtu ionveshe rnsimamo / nchi haikamiliki bila kuwa na mtendo mema.
h) hongo - rushwa /' mlunguva / chai / kadhongo.
sharon kalunda answered the question on October 3, 2019 at 09:55
-
Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.
(Solved)
Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.
(Solved)
"Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Wewe,Utazame mlolongo wa
(Solved)
SHAIRI A
Wewe,
Utazame mlolongo wa
Waja unaoshika njia likiwapo;
Unaofuata pembe za barabara zisokuwapo,
Kwenda kuisaka auni,
Kuitafuta kazi inayowachenga.
Itazame migongo ya wachapa kazi,
Watokwao na jasho kapakapana,
Wanaotafunwa uhai na jua liso huruma:
Wakiinua vyuma na magunia,
Wakiinua makontena,
Wakichubuka mashambani,
Wakiumia viwandani,
Wakiteseka makazini,
Halafu
Uangalie ule ujira wa kijungu meko,
Mshahara uso kifu haja,
Nguo zisizositiri miili dhaifu,
Kilio chao kisichokuwa na machozi,
Na
Ujiangalie
Mwili wako unaomereta ujana wa ufanisi,
Gari lako la kifahari lililozibwa vioo,
Jumba lako la kujishasha kama uwanja mdogo,
Malaki yapesa unayomiliki,
Ujiitapo mwajiri kwa raha, hunusi usaha wa hali yao?
SHAIRI B
Dunia kitendawili, hakuna ateguaye;
Dunia kama tapeli, hadaa nyingi ujuye;
Dunia mwenye akili, inampiku na yeye;
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.
Dunia na yake hali, hupumbaza hatimaye;
Dunia ina akili, binadamu sichezeye;
Dunia uwe na mali, huiwezi dhorubaye;
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.
Dunia wenye muali, ambao waichezeye;
Dunia kipigo kali, huwakumba hatimaye;
Dunia wakaja kuli, ?menipata nini miye?
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu
Maswali
(a) Je, mashairi haya mawili ni ya aina gani? Toa sababu.
(b) Taja dhamira kuu katika kila shairi.
(c) Kwa kutoa hoja zozote tatu linganua mashairi haya kiumbo.
(d) Taja na uelezee nafsi-pokezi katika mashairi haya mawili.
(e) Kwa kutolea mfano mmoja mmoja eleza matumizi ya mbinu hizi
(i) Kweli –kinzani
(ii) Mishata
(f) Tambua idhini ya kishairi iliyo tumika katika neno ?Waichezeye"
Na uelezee dhima yake katika utoshelezi wa kian ldhi.
(g) Dondoa mfano mmoja mmoja wa mbinu ya tashihisi kutoka kwenye Mashairi yote mawili.
(h) Andika ubeti wa tatu katika shairi la A kwa lugha nathari.
(i) Eleza maana ya msamiati huu kama ulivyotu? nika katika vifungu hivi.
(i) Inampiku.
(ii) Makontena.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.
(Solved)
Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
(Solved)
Timothy Arege, Mstahiki Meya
"...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Fafanua sifa tano za msemaji
(c) Tunagawana sote ni kinyume ejia hali halisi. Thibitisha.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
(Solved)
SIPENDI KUCHEKA
Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
Sipendi unipe hidaya, sipendi kutenda hili
Sipendi mimi kucheka
Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi
Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi
Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika
Halafuye nikacheka!
Masikini akiteswa
Yatima akinyanyaswa
Mnyonge naye akinyonywa
Sipendi hata ikiwa
Unazo nguvu najuwa
Ni hili sitatekezwa
Mbona lakini nicheke, kwayo furaha?
Na wewe ukajiweke, uli na siha?
Na yatima ali pwek.e, wa anahaha?
Amenyimwa haki yake, hanayo raha!
Na moyo wangu ucheke, kwa ha ha, ha!
Kucheka kwa kucheka Mimi katu sitacheka.
MASWALI
a) Shairi hili ni la aina gani? Thibitisha.
b) Taj a sababu zinazomfanya mshairi asitake kucheka.
c) Chambua umbo la shairi hili kwa kuzingatia ubeti wa mwisho.
d) Tambua nafsineni na nafsinenewa katika shairi hili.
e) Tambua toni ya shairi hili.
f) Fafanua uhuru wa mshairi katika shairi hili.
g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi.
h) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi
i) Mawi
ii) Nyemi
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.
(Solved)
“Shaka ya Mambo” (Farouk Topan)
Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.
(Solved)
Mstahiki Meya
Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
(Solved)
Mstahiki Meya
"Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Anayeambiwa alisema nini baada ya kuambiwa haya?
c) Thibitisha kuwa wanacheneo walipanda pojo.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Taja aina nne za hadithi.
(Solved)
Taja aina nne za hadithi.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.
(Solved)
Kidagaa kimemwozea
Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.
(Solved)
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
(Solved)
Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
"Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
a) Eleza muktadha wa maneno haya.
b) Eleza umuhimu wa mrejelewa katika dondoo hili kwenye riwaya.
c) Eleza maisha ya msemaji yalivyokuwa kwa mujibu wa Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
(Solved)
Damu nyeusi na hadithi zingine
"Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili.
c) Huku ukitoa mifano, thibitisha maudhui sita ambayo yamejitokeza katika hadithi ya Damu Nyeusi na wanayoyaendeleza.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
(Solved)
Kidagaa kimemwozea
"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Ni nini sifa za mvuto zinazowaleta pamoja mzungumzaji na mzungumziwa.
c) Tambua na ufafanue mbinu inayotumika katika dondoo.
d) Kwa mifano mwafaka fafanua tanzia hiyo inayorejelewa katika dondoo.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
(Solved)
Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
(a) Jazanda
(b) Uzungumzi nafsia
(c) Majazi
(d) Methali
(e) Taharuki
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.
(Solved)
Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine
(Solved)
Eleza maudhui ya ukengeushi ukirejea hadithi zifuatazo katika diwani ya Damu nyeusi na hadithi nyingine
(i) Mke wangu
(ii) Damu Nyeusi
(iii) Tazamana na Mauti
(iv) Mizizi na matawi
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
(Solved)
"Wanyonge ndio wanyongwao" ni kauli inayodhihirika vyema kupitia wahusika tofauti katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
Jadili.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,
(Solved)
Soma mashairi yafuatayo kisha ujibu maswali.
SIKUJUA!
1. Kama ningefuga ng‘ombe, mafahali na vindama,
Zisingenidhuru pembe, ngeu kuniandama,
Samli ni lembelembe, na minofu ya minyama.
2. Kama ningefuga mbuzi, na kondoo kundi zima,
Ningewajengea zizi, na maziwa nikakama,
Ningewachuna na ngozi, kutengenezea ngoma.
3. Kama ningefuga bata, nao kuku kwa ujima,
Chakula siyo matata, ni machicha na mtama,
Mayai ningeyapata, na kitoweo kizima.
4. Kumbe nimefuga punda, mashuzi ndio heshima,
Ni ukaidi na inda, mateke kurusha nyuma,
Nyama limekuwa nunda, mfugaji humuuma.
Kiitikio
Sikujua wa kufuga, mnyama mwenye faida
SHAIRI B
Afrika na Watu Wake
Mimi ninaona mgonjwa
Bado amelala kitandani.
Kama hatutamtoa miiba iliyobaki
Mgonjwa hataweka miguu yake chini
Ili kutembea bila ya kujiegemeza.
Miiba iliyomo ndani mwetu lazima
Pia iondolewe upesi kabla haijaingia
Kati ya mfupa na kufa pamoja nasi.
Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma
Halafu tucheze nao mchezo wa siasa na uchumi.
Lakini kuitoa miiba hii
Tunahitaji macho makali
Mikono isiyotetemeka
Moyo usio na huruma
Na kuona miiba ilipoingilia.
MASWALI
(a) Onyesha jinsi ujumbe unaopatikana katika ubeti wa nne wa Shairi A na Shairi la B unavyokatisha tamaa.
(b) Eleza maana ya mshororo huu kama unavyojitokeza kwenye ubeti wa pili wa shairi B.
Baada ya kuitoa tuvae viatu vya chuma.
(c) Linganua sifa za kimuundo ukizingatia ubeti wa pili wa Shairi A na Shairi B.
(d) Ukizingatia Mshororo wa kwanza kwenye ubeti wa pili wa Shairi A, onyesha jinsi Mshairi alivyotumia kibali chake.
(e) Onyesha sifa moja ambayo inadhihirika kwenye shairi la B na ambayo hutawala tungo za aina hii.
(f) Nafsi neni amedhihirisha toni gani kwenye shairi A?
(g) Taja nafsi mbili nenwa kwenye shairi la B.
(h) Andika ubeti wa mwisho wa shairi B kwa lugha ya nadhari.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)