Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.

      

Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.

  

Answers


sharon
Dawa za kulevya/pombe-glasi ya mwisho makaburini
-Anasa na starehe -Glasi ya mwisho makaburini
-Mke wangu -Samaki wa nchi za joto
-Mzizi na matawi
-Kanda la usufi
-Umaskini -Mke wangu
-Mwana wa darubini
-Mzizi na matawi
-Mwana wa darubini
-Mapenzi yasiyo ya dhati/dhuluma za kimapenzi
-Maeko
-Mke wangu
-Mzizi na matawi
-Kanda la usufu -Shaka ya mambo
Ndoa ya sanani
-Samaki wa nch za joto
-Mwana wa darubini
-Ubaguzi
-Damu Nyeusi
-Ndoa ya zamani
-Samaki wa nch za joto
-Ukosefu wa ajira/kazi/kazi za kijungujiko
-Mke wangu -Samaki wan chi za joto
-Mwana wa darubini
-Kanda la usufu
sharon kalunda answered the question on October 3, 2019 at 07:48


Next: The equation below represents a process that takes place in plants. (i) Name the process. (ii) State two factors not shown in the equation that are necessary...
Previous: List the positive verbal reinforcements.

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • "Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe" Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.(Solved)

    "Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
    Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Hivi vitu lazima viwepo,au kama havipo ni lazima viwe ni vipengee mahususi vya uhalisia wamaisha yetu:(Solved)

    Damu Nyeusi Na Hadithi Nyingine-Ken Wal'ibora Na S.Ahmed
    "Hivi vitu lazima viwepo,au kama havipo ni lazima viwe ni vipengee mahususi vya uhalisia wa maisha yetu:
    (a) Liweke dondoo katika muktadha wake faafu.
    (b) Fafanua sifa zozote nne za msemaji wa maneno haya.
    (c) Eleza kwa tafsili matatizo yoyote mawili yanayoikumba jamii ya hadithi mlimotolewa nukuu hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Wewe,Utazame mlolongo wa(Solved)

    SHAIRI A
    Wewe,
    Utazame mlolongo wa
    Waja unaoshika njia likiwapo;
    Unaofuata pembe za barabara zisokuwapo,
    Kwenda kuisaka auni,
    Kuitafuta kazi inayowachenga.

    Itazame migongo ya wachapa kazi,
    Watokwao na jasho kapakapana,
    Wanaotafunwa uhai na jua liso huruma:
    Wakiinua vyuma na magunia,
    Wakiinua makontena,
    Wakichubuka mashambani,
    Wakiumia viwandani,
    Wakiteseka makazini,
    Halafu
    Uangalie ule ujira wa kijungu meko,
    Mshahara uso kifu haja,
    Nguo zisizositiri miili dhaifu,
    Kilio chao kisichokuwa na machozi,
    Na
    Ujiangalie
    Mwili wako unaomereta ujana wa ufanisi,
    Gari lako la kifahari lililozibwa vioo,
    Jumba lako la kujishasha kama uwanja mdogo,
    Malaki yapesa unayomiliki,
    Ujiitapo mwajiri kwa raha, hunusi usaha wa hali yao?

    SHAIRI B
    Dunia kitendawili, hakuna ateguaye;
    Dunia kama tapeli, hadaa nyingi ujuye;
    Dunia mwenye akili, inampiku na yeye;
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.

    Dunia na yake hali, hupumbaza hatimaye;
    Dunia ina akili, binadamu sichezeye;
    Dunia uwe na mali, huiwezi dhorubaye;
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.

    Dunia wenye muali, ambao waichezeye;
    Dunia kipigo kali, huwakumba hatimaye;
    Dunia wakaja kuli, ?menipata nini miye?
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu


    Maswali
    (a) Je, mashairi haya mawili ni ya aina gani? Toa sababu.
    (b) Taja dhamira kuu katika kila shairi.
    (c) Kwa kutoa hoja zozote tatu linganua mashairi haya kiumbo.
    (d) Taja na uelezee nafsi-pokezi katika mashairi haya mawili.
    (e) Kwa kutolea mfano mmoja mmoja eleza matumizi ya mbinu hizi
    (i) Kweli –kinzani
    (ii) Mishata
    (f) Tambua idhini ya kishairi iliyo tumika katika neno ?Waichezeye"
    Na uelezee dhima yake katika utoshelezi wa kian ldhi.
    (g) Dondoa mfano mmoja mmoja wa mbinu ya tashihisi kutoka kwenye Mashairi yote mawili.
    (h) Andika ubeti wa tatu katika shairi la A kwa lugha nathari.
    (i) Eleza maana ya msamiati huu kama ulivyotu? nika katika vifungu hivi.
    (i) Inampiku.
    (ii) Makontena.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.(Solved)

    Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Tembo itakuua ndugu yangu. Punguza ulevi bwana.Siku hizi naona aibu kukuita ndugu yangu."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Tembo itakuua ndugu yangu. Punguza ulevi bwana.Siku hizi naona aibu kukuita ndugu yangu."
    (a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
    (b) Wahusika hawa wawili ni kama shilingi kwa ya pili.Thibitisha.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."(Solved)

    Timothy Arege, Mstahiki Meya
    "...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Fafanua sifa tano za msemaji
    (c) Tunagawana sote ni kinyume ejia hali halisi. Thibitisha.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali, (Solved)

    SIPENDI KUCHEKA

    Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
    Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
    Sipendi unipe hidaya, sipendi kutenda hili
    Sipendi mimi kucheka

    Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi
    Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi
    Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika
    Halafuye nikacheka!
    Masikini akiteswa
    Yatima akinyanyaswa
    Mnyonge naye akinyonywa
    Sipendi hata ikiwa

    Unazo nguvu najuwa
    Ni hili sitatekezwa
    Mbona lakini nicheke, kwayo furaha?
    Na wewe ukajiweke, uli na siha?
    Na yatima ali pwek.e, wa anahaha?
    Amenyimwa haki yake, hanayo raha!
    Na moyo wangu ucheke, kwa ha ha, ha!
    Kucheka kwa kucheka Mimi katu sitacheka.

    MASWALI
    a) Shairi hili ni la aina gani? Thibitisha.
    b) Taj a sababu zinazomfanya mshairi asitake kucheka.
    c) Chambua umbo la shairi hili kwa kuzingatia ubeti wa mwisho.
    d) Tambua nafsineni na nafsinenewa katika shairi hili.
    e) Tambua toni ya shairi hili.
    f) Fafanua uhuru wa mshairi katika shairi hili.
    g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi.
    h) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi
    i) Mawi
    ii) Nyemi

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.(Solved)

    “Shaka ya Mambo” (Farouk Topan)
    Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Nashangaa vile kwetu tunavyoabudu watu hao wasiotujali."(Solved)

    “Damu Nyeusi” (Ken Walibora)
    "Nashangaa vile kwetu tunavyoabudu watu hao wasiotujali."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Bainisha matumizi ya mbinu ya ishara kwa kurejelea hadithi ya gilasi ya mwisho makaburini.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.(Solved)

    Mstahiki Meya
    Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Anayeambiwa alisema nini baada ya kuambiwa haya?
    c) Thibitisha kuwa wanacheneo walipanda pojo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Taja aina nne za hadithi.(Solved)

    Taja aina nne za hadithi.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Siwe ulosema jana, ya kuwa u mashuhuri? Ya kuwa wajuwa sana, aidha huna kiburi? Nchini wajulikana, mwanasiasa mahiri, Bungeni tukuajiri?(Solved)

    SIWE?

    1. Siwe ulosema jana, ya kuwa u mashuhuri?
    Ya kuwa wajuwa sana, aidha huna kiburi?
    Nchini wajulikana, mwanasiasa mahiri,
    Bungeni tukuajiri?

    2. Siwe ulotushawishi, kwa chumvi na kwa sukari,
    Na matamu matamshi, ukaziteka suduri,
    Ukanena penya moshi, moto ndiyo yakwe siri,
    Nawe ndiye hiyo nari?

    3. Siwe uloji‘ta moto, uwakao biribiri,
    Kamba ‗tatia fukuto, Litakalo leta kheri‘,
    Utatufunua mato, Maisha yawe mazuri,
    Tukupe kura waziri?

    4. Siwe ulosema hayo, na mengi ukabashiri,
    Ukamba wafata nyayo, nyayo ziso utiriri,
    Tusiwe na wayowayo, wa kufikirifikiri,
    Tukuachie ujari?

    5. Siwe tulokuinua, Mabegani kama mwari,
    Tungawa twalemelewa, waume tukajasiri,
    Kamba tukikuchaguwa, mema kwetu yatajiri,
    Tukakeyi kusubiri?

    6. Siwe ulotugeuka, kwamba leo u waziri,
    Wajiona melimuka, tena ukawa ayari,
    Walaghai ukicheka, ukuu umekughuri,
    Leo mekuwa hodari?

    7. Siwe ulojawa raha, za hino yetu sayari,
    Ukawa ja vile shaha, hatukupati shauri,
    kutuona ni karaha, wakatiwo twahasiri,
    Ushakiya msitari?

    8. Siwe uliyetughura, ukafunga na safari,
    Ukaelekea bara, Kwa wenzio matajiri,
    Ukatuacha majura, na tama kukithiri,
    Kanama Ushaghairi?

    9. Siwe uliyetuasi, ukenda pasi kwaheri,
    Mbona hutwambii nasi, tukajua yetu shari,
    Leo una masidisi, husemi na aso gari,
    Ndio mezidi jeuri?

    10. Siwe‘lotwaa mgwisho, ukawa wajifakhiri?
    Chenye mwanzo kina mwisho, hilo wajuwa dhahiri,
    Vyaja kutoka vitisho, kwani hayo sidahari,
    Mambo mengimdawari?

    11. Siwe utakayeiza, mwishowo ukidhihiri,
    Siku itayoteleza, kuja kwetu ansari,
    Kuja kutubembeleza, kwa nyunga nalo khamri,
    Tauya nazo nadhiri.

    MASWALI
    a) Mtunzi wa shairi hili ana dhamira gani?
    b) Taja na ueleze bahari tatu za shairi hili?
    c) Onyesha jinsi mtunzi alivyotumia idhini ya kishairi.
    d) Taja na ufafanue tamahali ya usemi iliyotawala katika shairi hili.
    e) Anayerejelewa alibailika vipi? Eleza.
    f) Andika ubeti wa tisa kwa lugha ya nathari.
    g) Mshairi ana maana gani kwa kusema:
    (i) Wakatiwo twahasiri.
    (ii) Ukaziteka suduri.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.(Solved)

    Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Nimemwita bwana huyu aje huku juu kusudi mumwone."(Solved)

    Damu nyeusi na hadithi zingine
    "Nimemwita bwana huyu aje huku juu kusudi mumwone."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa tatu za mzungumzaji.
    c) Jadili maudhui ya ubaguzi namna yanavyojitokeza katika hadithi husika

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"(Solved)

    Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
    "Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
    a) Eleza muktadha wa maneno haya.
    b) Eleza umuhimu wa mrejelewa katika dondoo hili kwenye riwaya.
    c) Eleza maisha ya msemaji yalivyokuwa kwa mujibu wa Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Kutowajibika kwa viongozi baada ya mkoloni kuondoka ni dhahiri." Jadili kauli hii kwa mujibu wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    "Kutowajibika kwa viongozi baada ya mkoloni kuondoka ni dhahiri." Jadili kauli hii kwa mujibu wa Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • "Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."(Solved)

    Mstahiki Meya.
    "Nashukuru sasa umeanza kuona mambo yanavyostahili kwenda."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa zozote nne za msemaji.
    c) Fafanua maudhui ya ufisadi kama yalivyoangaziwa na mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)

  • Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

    1) Hadhira e pulikeni, kisa changu mpaeni,
    Mpateni mweleweni, mchekeni, mlieni,
    Funzo lake mpateni, uamuzi mfanyeni,
    Kisa hiki asilani, sisahau maishani.

    2) Cha nne niliingiya, mtoto kafurahiya,
    Malkia ungedhaniya, duniani meingiya,
    Mapambo lijipambiya, kung‘ara kikang‘ariya,
    Kisa change chatokeya, mwanzowe nafunguliya.

    3) Darasani lizembea, bidii sikutilia,
    Starehe nakwambia, nilipenda najutia,
    Kimadaha litembea, tausi nilitulia,
    Kisa kilinigonjea, mtume! Ningalijua.

    4) Muhula kutamatika, dafu sikufua, kaka,
    Enda, Ewe, Embe, fika, alama duni, viraka,
    Nilipokea waraka, mzazi kahitajika,
    Kisa kijatambulika, nakuomba makinika.

    5) Muhula wa pili sasa, nikarudia makosa,
    Sikupigeni msasa, makali nikayakosa,
    Kisu sikunoa hasa, sikukata cha darasa,
    Kisa ndicho hicho sasa, ninakupa pasi pesa.

    6) Sasa muhula wa tatu, umetimia wanetu,
    Mtihani kama chatu, nimeuogopa, mtu,
    Sijausomea katu, ningalilindaje utu?
    Kisa mkasa wa chatu, kilinipata wa kwetu.

    7) Mbwa katu hafi maji, kiona ufuko, maji,
    Tajaribu sife maji, hata akiyanywa maji,
    Ilibidi twende jiji, kuwasaka wajuaji,
    Kisa change mfumbaji, sasa dawa lihitaji.

    8) Mpango ulitolewa, mchango ulipangiwa,
    Pesa tele litolewa, na simu kununuliwa,
    Mtandao liwekewa, ‗kunani‘ kupakuliwa,
    Kisa cha simu kujuwa, linifanya kupagawa.

    9) Tulikata dari ona, simu yetu kufichana,
    Usiku tulikutana, maswali kurushiana,
    Majibu tulipeana, "panga‘ kabadilishana,
    Kisa kinajulikana, vile nilivyokazana.

    10) Niliyangoja majibu, nikiwa na hamu, babu,
    Nilikimya kama bubu, nisije toa aibu,
    Nilivichoma vitabu, bila kuwa na sababu.
    Kisa kawa masaibu, kashindwa kuyaharibu.

    11) Kutangazwa matokeo, nakumbuka hadi leo,
    Lilishangaza toleo, sikuamini redio,
    Lipokea matokea, yalinitia kimbio,
    Kisa change mchocheo, haya yangu mapokeo.

    12) Nilifeli mtihani, sababu simu juweni,
    Najuta nisameheni, nijilaumu moyoni,
    Ningalijua mbeleni, ningalisoma jamani,
    Kisa nimemalizeli, wenzangu mzindukeni.

    13) Watahiniwa mlipo, msiwe mithili popo,
    Skuli kwenu kuwepo, nia mpate malipo,
    Bidii hapo mlipo, toa uzembe pasipo,
    Kisa change kingalipo, simu daima siwepo!

    MASWALI
    a) Taja anwani mwafaka ya shairi hili.
    b) Fafanua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi hili.
    c) Bainisha nafsi lengwa katika shairi hili.
    d) Changanua arudhi zilizotumiwa na mtunzi wa shairi hili.
    e) Andika ubeti wa kumi katika lugha nathari.
    f) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    g) Eleza maana ya maneno na vifungu vifuatavyo kwa mujibu wa shairi.
    (i) Sikukata cha darasa
    (ii) Yalinitia kimbio
    (iii) Kupagawa

    Date posted: October 2, 2019.  Answers (1)