Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

"Wema wako umeniua kabisa………Nina jishtaki mwenyewe kila siku kwa miaka na miaka".

      

KIDAGAA KIMEMWOZEA: Ken Walibora.
"Wema wako umeniua kabisa………Nina jishtaki mwenyewe kila siku kwa miaka na miaka".
(a) Eleza muktadha wa maneno haya.
(b) Onyesha kwa kutoa mifano kuwa anayeambiwa maneno haya alikuwa na wema.
(c) Eleza umuhimu wa mhusika mashaka katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

  

Answers


sharon
a) Ni maneno ya mtemi Nasaba bora.
Kwa Amani
Walikuwa nyumbani kwa mtemi baada ya Amani kumkabili na kushurutisha amweleze ukweli kuhusu kuuliwa kwa babake na pia jinsi amuye Yusufu alivyoishia kufungwa jela.
b) Alimwokoa mtemi Nasabora kutoka kwa Oscar kambora.
Alikilea kitoto uhuru
Alifanya kazi ya uchungaji vizuri
Alimsaidia Bi, zuhura wakati Mashaka alikuwa mgonjwa.
Aligawa shamba lake alipolipata
Alimuokoa amu yake Yusufu.
c) Kielelezo cha mapenzi yasiyokomaa kwa vijana katika jamii.
Ametumiwa kuonyesha uozo wa jamii anapowachekelea vilema.
Ametumiwa kuonyesha udanganyifu na uvivu wa mwalimu majisifu.
Anaonyesha maudhui ya elimu na vile yalivyokatizwa na uhusiano wake wa kimapenzi akiwa shuleni.
sharon kalunda answered the question on October 3, 2019 at 13:22


Next: Kamilisha jedwali
Previous: Zingatia picha ifuatayo kisha ujibu maswali.

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • "Dhiki mbalimbali zimekuwapo lakini heri nusu shari kuliko shari kamili".(Solved)

    Mstahiki Meya.
    "Dhiki mbalimbali zimekuwapo lakini heri nusu shari kuliko shari kamili".
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Taja tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.
    (c) Eleza sifa zozote tatu za mzungumzaji.
    (d) Fafanua aina zozote nne za migogoro inayojitokeza katika tamthilia ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Taja kitamkwa chenye sifa ifuatazo. Vokali ya nyuma, kati(Solved)

    Taja kitamkwa chenye sifa ifuatazo.
    Vokali ya nyuma, kati.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kuna sababu kadha za kuwako na kushamiri kwa ajira ya watoto.(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
    Kuna sababu kadha za kuwako na kushamiri kwa ajira ya watoto. Moja ya sababu hizo ni umaskini unaozikumba jamaa nyingi pamoja na welewa mdogo wa thamani ya elimu wa baadhi ya watu katika jamii. Wapo watoto ambao hushurutika kubeba jukumu la kujizumbulia riziki wenyewe kutokana na hali duni ya familia zao.
    Hali hii huweza kutokana na baadhi ya wazazi kutelekeza majukumu yao ya kimsingi ya kuikimu jamaa yao. Aidha kuna sehemu nyingine ambapo hali hii imetokana na janga sugu la ukimwi. Yapo maeneo ambako kuenea kwa ugonjwa huu kumewafanya viongozi wa jamaa kupukutika kama majani ya mti na kuwalazimisha watoto kuyakatiza masomo yao ili wawakidhie haja wadogo zao. Kuhusiana na kutelekeza majukumu, kuna wazazi ambao wanakosea kwa kutowaelekeza watoto wao kujua maadili mema ni yepi. Kwa njia hii watoto hao wanaishia kutumbukia kwenye matatizo makubwa.
    Baadhi ya ajira zina athari kubwa sana kwa watoto. Ukahaba, kwa mfano, ni mojawapo ya ajira ambazo watoto wa kike hulazimika kujiingiza. Hii ni ajira ambayo inaweza kuwatumbukiza watoto hao katika hatari kubwa kutokana na uwezekano mkubwa wa kuambukizwa maradhi ya ukimwi. Asillimia kubwa ya watoto wanaotumbukia katika ajira hii, inapatikana katika maeneo ya mijini na sehemu ambako utalii umeshamiri sana. Umaskini pamoja na dhiki za mijini huwalazimisha watoto hao wa kike kuishia kwenye biashara za aina hiyo. Wengine hufanyiwa hila na wafanyabiashara ambao wametovukwa na utu kutokana na tamaa yao kubwa ya kujitajirisha. Katika maeneo ambako utalii umeshamiri, ukahaba wa watoto unatokana na umaskini pamoja na kusambaa na kuenea kwa maadili ajinabi, ya ulimwengu usio wetu.
    Ikiwa umaskini ni chocheo kubwa la kuwapo kwa ajira ya watoto, basi inahalisi serikali zetu zifanye kila juhudi kuhakikisha kuwa umaskini umepigwa vita. Pana umuhimu wa kuhakikisha kuwa wanajamii wote wamepewa nafasi sawa za kujikwamua kutoka lindi la umaskini. Isitoshe, pana umuhimu wa juhudi nyingi kufanywa kuhakikisha kuwa nafasi za shule zimepanuliwa ili kuikidhi idadi kubwa ya watoto ambao wana kiu ya elimu. Serikali haina budi pia kuhakikisha kuwa zimepitishwa sheria zinazomlinda motto dhidi ya ukatili unaotokana na watu waliokosa hisia za utu na ubinadamu. Upo pia umuhimu wa kuvisaidia vikundi vinavyojitahidi kuwasaidia watoto ili kuzifanikisha juhudi zao kwa kuwa chanda kimoja hakivunji chawa kama tujuavyo.
    Hatua nyingine ambazo zinaweza kuchukuliwa ili kupunguza ajira ya watoto ni kuwahamasisha wanajamii kuhusu haki za mtoto. mtoto yeyote yule ana haki ya kupata elimu ya msingi. Mtoto pia ana haki ya kuishi na kupata mahitaji ya kimsingi na ya lazima kama chakula, malazi au makazi na matunzo ya kiafya. Aidha mtoto ana haki ya ukuaji, yaani kukua kikamilifu pasi na kizuizi na katika mazingira yasiyombana kwa njia yoyote ile. Isitoshe, mtoto ana haki ya kupata ulinzi dhidi ya unyanyaswaji au udhalilishwaji wa aina yoyote ile au hata maonevu kwenye misingi yoyote iwayo. Mtoto pia ana haki ya kuwa huru kushiriki katika jumuiya yake, kutoa maoni na kujieleza, kushirikiana na kujiunga na vikundi. Mwisho, na muhimu zaidi, mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya ajira au aina yoyote ya kazi ambayo inaihatarisha afya na siha yake au inamzuia asipate elimu.
    (a) Fupisha aya mbili za mwanzo bila kubadilisha maana. (maneno 60-70)
    (b) Eleza hoja muhimu zinazojitokeza katika aya mbili za mwisho. (Maneno 50-60)

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.(Solved)

    Tazamana na Mauti” (S.A. Mohammed)
    Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Uniulie nini na ndoa yetu na wewe inamhusu pia yeye?"(Solved)

    Mwana wa Darubini (K. Mwende Mbai)
    "Uniulie nini na ndoa yetu na wewe inamhusu pia yeye?"
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Eleza sifa zozote nne za msemewa.
    c) Jadili madhila yanayomkumba mwanamke katika hadithi hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Lazima kwanza mnihakikishie kuwa huyo sumu hapati hata fununu ya jambo hili."(Solved)

    Mstahiki Meya
    "Lazima kwanza mnihakikishie kuwa huyo sumu hapati hata fununu ya jambo hili."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Taja sifa zozote nne za msemaji.
    c) Andika umuhimu wa huyo sumu.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Tayari nimemkabidhi barua ya kujiuzulu ninapohusika."(Solved)

    Mstahiki Meya
    Tayari nimemkabidhi barua ya kujiuzulu ninapohusika."
    a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    b) Mbali na changamoto inayofanya msemaji kujiuzulu, jadili changamoto nyinginezo zinazowakumba wanacheneo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.(Solved)

    Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kufafanua hoja saba thibitisha kwamba kuna haja ya kuwa na Revolution.(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    Kwa kufafanua hoja saba thibitisha kwamba kuna haja ya kuwa na Revolution.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Lakini bila matumaini hatuwezi kwenda mbele na Revolution."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Lakini bila matumaini hatuwezi kwenda mbele na Revolution."
    i) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    ii) Bainisha tamathali moja ya usemi inayojitokeza katika dondoo hili.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
    Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,
    Ushairi niwapeni, hoja nitawaachia,
    Mnipe masikioni, shike nachoelezea,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Naanza kwa uzalendo, nchi yetu tuipende,
    Yadhihirishe matendo, nchi yetu tuilinde,
    Wa kila mtu mwendo, usije kawa mpinde,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili

    Wote tuwe na umoja, tuuache ukabila
    Kabila lisiwe hoja, mwenza kumnyima hela,
    Taifa letu ni moja, Mkenya ndilo kabila,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Linda demokrasia, uongozi tushiriki,
    Haki kujielezea, wachotaka na hutaki.
    Changu naweza tetea, demokrasia haki,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Tena adili usawa, mgao raslimali,
    Bajeti inapogawa, isawazishe ratili.
    Idara zilizoundwa, ‗faidi kila mahali,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Tuwe na uadilifu, twache tamaa ya hongo,
    Tusiwe na udhaifu, wa kuwa watu waongo,
    Tukomeshe uhalifu, kisha tuache maringo,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Ubinafsi si adili, ila ni kusaidia,
    Ukiwa nayo mali, asiyenacho patia,
    Kama mtu mswahili, ubinafsi achia,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.

    Na inavyoelezea, katiba ni kielezi,
    Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi,
    Kwa hayo nitamwachia. hiyo ya ziada kazi,
    Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili

    a) Eleza mambo yoyote manne ambayo mshairi anashauri taifa lifanye ili kuwa na aadili.
    b) Taja tamathali yoyote moja inayojitokeza katika shairi hili.
    c) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia kigezo kifuatacho :
    Mpangilio wa vina
    d) Bainisha nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili.
    e) Eleza toni ya shairi hili
    f) Eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa kishairi zilizotumiwa katika ubeti wa nne
    g) Andika ubeti wa pili kw lugha nathari
    h) Eleza maana ya neon lifuatalo kama ilivyotumiwa katika shairi:
    i) hongo

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.(Solved)

    Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe" Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.(Solved)

    "Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
    Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Hivi vitu lazima viwepo,au kama havipo ni lazima viwe ni vipengee mahususi vya uhalisia wamaisha yetu:(Solved)

    Damu Nyeusi Na Hadithi Nyingine-Ken Wal'ibora Na S.Ahmed
    "Hivi vitu lazima viwepo,au kama havipo ni lazima viwe ni vipengee mahususi vya uhalisia wa maisha yetu:
    (a) Liweke dondoo katika muktadha wake faafu.
    (b) Fafanua sifa zozote nne za msemaji wa maneno haya.
    (c) Eleza kwa tafsili matatizo yoyote mawili yanayoikumba jamii ya hadithi mlimotolewa nukuu hii.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Wewe,Utazame mlolongo wa(Solved)

    SHAIRI A
    Wewe,
    Utazame mlolongo wa
    Waja unaoshika njia likiwapo;
    Unaofuata pembe za barabara zisokuwapo,
    Kwenda kuisaka auni,
    Kuitafuta kazi inayowachenga.

    Itazame migongo ya wachapa kazi,
    Watokwao na jasho kapakapana,
    Wanaotafunwa uhai na jua liso huruma:
    Wakiinua vyuma na magunia,
    Wakiinua makontena,
    Wakichubuka mashambani,
    Wakiumia viwandani,
    Wakiteseka makazini,
    Halafu
    Uangalie ule ujira wa kijungu meko,
    Mshahara uso kifu haja,
    Nguo zisizositiri miili dhaifu,
    Kilio chao kisichokuwa na machozi,
    Na
    Ujiangalie
    Mwili wako unaomereta ujana wa ufanisi,
    Gari lako la kifahari lililozibwa vioo,
    Jumba lako la kujishasha kama uwanja mdogo,
    Malaki yapesa unayomiliki,
    Ujiitapo mwajiri kwa raha, hunusi usaha wa hali yao?

    SHAIRI B
    Dunia kitendawili, hakuna ateguaye;
    Dunia kama tapeli, hadaa nyingi ujuye;
    Dunia mwenye akili, inampiku na yeye;
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.

    Dunia na yake hali, hupumbaza hatimaye;
    Dunia ina akili, binadamu sichezeye;
    Dunia uwe na mali, huiwezi dhorubaye;
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.

    Dunia wenye muali, ambao waichezeye;
    Dunia kipigo kali, huwakumba hatimaye;
    Dunia wakaja kuli, ?menipata nini miye?
    Dunia ina mizungu, tena yapika majungu


    Maswali
    (a) Je, mashairi haya mawili ni ya aina gani? Toa sababu.
    (b) Taja dhamira kuu katika kila shairi.
    (c) Kwa kutoa hoja zozote tatu linganua mashairi haya kiumbo.
    (d) Taja na uelezee nafsi-pokezi katika mashairi haya mawili.
    (e) Kwa kutolea mfano mmoja mmoja eleza matumizi ya mbinu hizi
    (i) Kweli –kinzani
    (ii) Mishata
    (f) Tambua idhini ya kishairi iliyo tumika katika neno ?Waichezeye"
    Na uelezee dhima yake katika utoshelezi wa kian ldhi.
    (g) Dondoa mfano mmoja mmoja wa mbinu ya tashihisi kutoka kwenye Mashairi yote mawili.
    (h) Andika ubeti wa tatu katika shairi la A kwa lugha nathari.
    (i) Eleza maana ya msamiati huu kama ulivyotu? nika katika vifungu hivi.
    (i) Inampiku.
    (ii) Makontena.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.(Solved)

    Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "Tembo itakuua ndugu yangu. Punguza ulevi bwana.Siku hizi naona aibu kukuita ndugu yangu."(Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Tembo itakuua ndugu yangu. Punguza ulevi bwana.Siku hizi naona aibu kukuita ndugu yangu."
    (a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
    (b) Wahusika hawa wawili ni kama shilingi kwa ya pili.Thibitisha.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • "...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."(Solved)

    Timothy Arege, Mstahiki Meya
    "...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
    (a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
    (b) Fafanua sifa tano za msemaji
    (c) Tunagawana sote ni kinyume ejia hali halisi. Thibitisha.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali, (Solved)

    SIPENDI KUCHEKA

    Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
    Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
    Sipendi unipe hidaya, sipendi kutenda hili
    Sipendi mimi kucheka

    Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi
    Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi
    Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika
    Halafuye nikacheka!
    Masikini akiteswa
    Yatima akinyanyaswa
    Mnyonge naye akinyonywa
    Sipendi hata ikiwa

    Unazo nguvu najuwa
    Ni hili sitatekezwa
    Mbona lakini nicheke, kwayo furaha?
    Na wewe ukajiweke, uli na siha?
    Na yatima ali pwek.e, wa anahaha?
    Amenyimwa haki yake, hanayo raha!
    Na moyo wangu ucheke, kwa ha ha, ha!
    Kucheka kwa kucheka Mimi katu sitacheka.

    MASWALI
    a) Shairi hili ni la aina gani? Thibitisha.
    b) Taj a sababu zinazomfanya mshairi asitake kucheka.
    c) Chambua umbo la shairi hili kwa kuzingatia ubeti wa mwisho.
    d) Tambua nafsineni na nafsinenewa katika shairi hili.
    e) Tambua toni ya shairi hili.
    f) Fafanua uhuru wa mshairi katika shairi hili.
    g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi.
    h) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi
    i) Mawi
    ii) Nyemi

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)

  • Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.(Solved)

    “Shaka ya Mambo” (Farouk Topan)
    Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.

    Date posted: October 3, 2019.  Answers (1)