A (i) Ajira ya watoto husababishwa na umaskini unaozikumba jamaa nyingi.
(ii) Ufahamu mdogo wa thamani ya elimu wa baadhi ya watu.
(iii) Watotokushurutikakujitafutiarizikiwenyewekwasababuyahaliduniyafamiliazao.
(iv) Wazazi kutelekeza majukumu yao yakimsingi ya kukimu jamaa yao.
(v) Kupukutika kwa viongozi wa jamaa kutokana na janga sugu la ukimwi.
(vi) Wazazi kutowaelekeza watoto wao kujua maadili mema.
B (i) Serikalikufanyajuhudikuhakikishakuwaumaskiniumepigwa vita.
(ii) Wananjamii wote wapewe nafasi sawa za kujikwamua kutoka lindi la umaskini.
(iii) Kupanua nafasi za elimu kukidhi idadi kubwa ya watoto.
(iv) Kuhakikisha kupitishwa kwa sheria zinazolinda motto dhidi ya ukatili
(v) Kusaidiavikundivinavyojitahidikuwasaidiawatoto.
(vi) Kuwahamasisha wanajamii kuhusu haki za watoto.
sharon kalunda answered the question on October 3, 2019 at 11:24
-
Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.
(Solved)
Tazamana na Mauti” (S.A. Mohammed)
Tamaa mbele mauti nyuma. Thibitisha ukweli ya methali hii ukirejelea hadithi ya Tazamana na mauti.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
(Solved)
Eleza namna mbinu ya Taharuki ilivyotumiwa na mwandishi wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,
(Solved)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Naingia ukumbini, nyote kuwakariria,
Ushairi niwapeni, hoja nitawaachia,
Mnipe masikioni, shike nachoelezea,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Naanza kwa uzalendo, nchi yetu tuipende,
Yadhihirishe matendo, nchi yetu tuilinde,
Wa kila mtu mwendo, usije kawa mpinde,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili
Wote tuwe na umoja, tuuache ukabila
Kabila lisiwe hoja, mwenza kumnyima hela,
Taifa letu ni moja, Mkenya ndilo kabila,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Linda demokrasia, uongozi tushiriki,
Haki kujielezea, wachotaka na hutaki.
Changu naweza tetea, demokrasia haki,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Tena adili usawa, mgao raslimali,
Bajeti inapogawa, isawazishe ratili.
Idara zilizoundwa, ‗faidi kila mahali,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Tuwe na uadilifu, twache tamaa ya hongo,
Tusiwe na udhaifu, wa kuwa watu waongo,
Tukomeshe uhalifu, kisha tuache maringo,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Ubinafsi si adili, ila ni kusaidia,
Ukiwa nayo mali, asiyenacho patia,
Kama mtu mswahili, ubinafsi achia,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
Na inavyoelezea, katiba ni kielezi,
Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi,
Kwa hayo nitamwachia. hiyo ya ziada kazi,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili
a) Eleza mambo yoyote manne ambayo mshairi anashauri taifa lifanye ili kuwa na aadili.
b) Taja tamathali yoyote moja inayojitokeza katika shairi hili.
c) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia kigezo kifuatacho :
Mpangilio wa vina
d) Bainisha nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili.
e) Eleza toni ya shairi hili
f) Eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa kishairi zilizotumiwa katika ubeti wa nne
g) Andika ubeti wa pili kw lugha nathari
h) Eleza maana ya neon lifuatalo kama ilivyotumiwa katika shairi:
i) hongo
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.
(Solved)
Vijana wana kumbwa na changamoto kadhaa katika jamii.Jadili baadhi ya changamoto hizi kwa kurejelea hadithi zozote tano kutoka diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.
(Solved)
"Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendowe"
Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi Mzizi na Matawi.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Wewe,Utazame mlolongo wa
(Solved)
SHAIRI A
Wewe,
Utazame mlolongo wa
Waja unaoshika njia likiwapo;
Unaofuata pembe za barabara zisokuwapo,
Kwenda kuisaka auni,
Kuitafuta kazi inayowachenga.
Itazame migongo ya wachapa kazi,
Watokwao na jasho kapakapana,
Wanaotafunwa uhai na jua liso huruma:
Wakiinua vyuma na magunia,
Wakiinua makontena,
Wakichubuka mashambani,
Wakiumia viwandani,
Wakiteseka makazini,
Halafu
Uangalie ule ujira wa kijungu meko,
Mshahara uso kifu haja,
Nguo zisizositiri miili dhaifu,
Kilio chao kisichokuwa na machozi,
Na
Ujiangalie
Mwili wako unaomereta ujana wa ufanisi,
Gari lako la kifahari lililozibwa vioo,
Jumba lako la kujishasha kama uwanja mdogo,
Malaki yapesa unayomiliki,
Ujiitapo mwajiri kwa raha, hunusi usaha wa hali yao?
SHAIRI B
Dunia kitendawili, hakuna ateguaye;
Dunia kama tapeli, hadaa nyingi ujuye;
Dunia mwenye akili, inampiku na yeye;
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.
Dunia na yake hali, hupumbaza hatimaye;
Dunia ina akili, binadamu sichezeye;
Dunia uwe na mali, huiwezi dhorubaye;
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu.
Dunia wenye muali, ambao waichezeye;
Dunia kipigo kali, huwakumba hatimaye;
Dunia wakaja kuli, ?menipata nini miye?
Dunia ina mizungu, tena yapika majungu
Maswali
(a) Je, mashairi haya mawili ni ya aina gani? Toa sababu.
(b) Taja dhamira kuu katika kila shairi.
(c) Kwa kutoa hoja zozote tatu linganua mashairi haya kiumbo.
(d) Taja na uelezee nafsi-pokezi katika mashairi haya mawili.
(e) Kwa kutolea mfano mmoja mmoja eleza matumizi ya mbinu hizi
(i) Kweli –kinzani
(ii) Mishata
(f) Tambua idhini ya kishairi iliyo tumika katika neno ?Waichezeye"
Na uelezee dhima yake katika utoshelezi wa kian ldhi.
(g) Dondoa mfano mmoja mmoja wa mbinu ya tashihisi kutoka kwenye Mashairi yote mawili.
(h) Andika ubeti wa tatu katika shairi la A kwa lugha nathari.
(i) Eleza maana ya msamiati huu kama ulivyotu? nika katika vifungu hivi.
(i) Inampiku.
(ii) Makontena.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.
(Solved)
Eleza namna mwandishi wa kidagaa Kimemwozea alivyofaulu kutumia fani ya barua kwa kutolea mifano mitano.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
(Solved)
Timothy Arege, Mstahiki Meya
"...Sote ni wafanyikazi wa baraza. Kile linachochuma Baraza tunagawana sote."
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Fafanua sifa tano za msemaji
(c) Tunagawana sote ni kinyume ejia hali halisi. Thibitisha.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
(Solved)
SIPENDI KUCHEKA
Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali,
Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
Sipendi unipe hidaya, sipendi kutenda hili
Sipendi mimi kucheka
Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi
Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi
Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika
Halafuye nikacheka!
Masikini akiteswa
Yatima akinyanyaswa
Mnyonge naye akinyonywa
Sipendi hata ikiwa
Unazo nguvu najuwa
Ni hili sitatekezwa
Mbona lakini nicheke, kwayo furaha?
Na wewe ukajiweke, uli na siha?
Na yatima ali pwek.e, wa anahaha?
Amenyimwa haki yake, hanayo raha!
Na moyo wangu ucheke, kwa ha ha, ha!
Kucheka kwa kucheka Mimi katu sitacheka.
MASWALI
a) Shairi hili ni la aina gani? Thibitisha.
b) Taj a sababu zinazomfanya mshairi asitake kucheka.
c) Chambua umbo la shairi hili kwa kuzingatia ubeti wa mwisho.
d) Tambua nafsineni na nafsinenewa katika shairi hili.
e) Tambua toni ya shairi hili.
f) Fafanua uhuru wa mshairi katika shairi hili.
g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi.
h) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi
i) Mawi
ii) Nyemi
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.
(Solved)
“Shaka ya Mambo” (Farouk Topan)
Eleza hali ya shaka ya mambo inavyojitokeza katika hadithi ya shaka ya mambo.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.
(Solved)
Mstahiki Meya
Eleza jinsi wanacheneo walivyotatua shida zinazowakumba.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
"Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
(Solved)
Mstahiki Meya
"Mtu huvuna alichopanda, ukipanda pojo huwezi kuvuna kunazi."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Anayeambiwa alisema nini baada ya kuambiwa haya?
c) Thibitisha kuwa wanacheneo walipanda pojo.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Taja aina nne za hadithi.
(Solved)
Taja aina nne za hadithi.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.
(Solved)
Kidagaa kimemwozea
Mtemi Nasaba Bora ni kielelezo cha viongozi wa kiafrika wanaondeleza uongozi mbaya. Jadili kauli hii.
Date posted:
October 3, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.
(Solved)
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika Diwani Damu Nyeusi, jadili namna ambavyo wahusika wa kike wamesawiriwa.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
(Solved)
Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
"Hizi kurani zako ndizo zifanyazo nisije huku …"
a) Eleza muktadha wa maneno haya.
b) Eleza umuhimu wa mrejelewa katika dondoo hili kwenye riwaya.
c) Eleza maisha ya msemaji yalivyokuwa kwa mujibu wa Riwaya ya Kidaa Kimemwozea.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
(Solved)
Damu nyeusi na hadithi zingine
"Leo ni siku, siku ya nyani kufa ambapo miti yote huteleza"
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili.
c) Huku ukitoa mifano, thibitisha maudhui sita ambayo yamejitokeza katika hadithi ya Damu Nyeusi na wanayoyaendeleza.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
(Solved)
Kidagaa kimemwozea
"Umenena ndipo ndugu yangu. Hiyo ndiyo tanzia ya Afrika huru."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Ni nini sifa za mvuto zinazowaleta pamoja mzungumzaji na mzungumziwa.
c) Tambua na ufafanue mbinu inayotumika katika dondoo.
d) Kwa mifano mwafaka fafanua tanzia hiyo inayorejelewa katika dondoo.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
(Solved)
Jadili mbinu zifuatazo kama zilivyotumika katika Mstahiki Meya.
(a) Jazanda
(b) Uzungumzi nafsia
(c) Majazi
(d) Methali
(e) Taharuki
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.
(Solved)
Eleza dhima ya lakabu kwa kurejelea hoja tano.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)