Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza namna maudhui ya ndoa yalivyosawiriwa katika hadithi ya Masharti ya Kisasa.

      

Eleza namna maudhui ya ndoa yalivyosawiriwa katika hadithi ya Masharti ya Kisasa.

  

Answers


Francis
? Mwanaume humposa mwanamke. Dadi alienda nyumbani kwa Kidawa kumposa.
? Mwanamke ndiye huamua wakati wa kuolewa na nani wa kumwoa. Kidawa alimchagua Dadi baada ya muda mrefu.
? Ndoa huandamana na masharti. Dadi alipewa masharti na Kidawa ili akubali kuolewa naye.
? Wanandoa hufanya kazi pamoja ili kukidhi mahitaji ya nyumbani. Dadi anachuuza samaki na Kidawa ni metroni.
? Wanaume hawafurahi wake wao wanapotangamana na wanaume wengine. Kidawa anaposimama kuongea na wanaume, Dadi anaudhika sana.
? Wanandoa husaidiana kazi za nyumbani, Dadi anasaidia kidawa kazi za nyumbani kama vile kuosha vyombo na kufagia.
? Wanandoa wanapanga uzazi, Dadi na Kidawa wanapanga kuwa na mtoto mmoja pekee.
? Ndoa imekosa uaminifu. Dadi anashuku kuwa Kidawa ana mapenzi na mwalimu mkuu.
? Kiwango cha elimu si kikwazo katika ndoa. Kidawa anaolewa na Dadi licha ya kuwa ana kisomo cha juu kuliko Dadi.
? Mwanamke amekengeuka. Kidawa anapenda fasheni.
? Kuna makubaliano ya kufanya mambo kwa pamoja.
francis1897 answered the question on February 6, 2023 at 09:58


Next: “Ningeondoka ... mapema niende niibe au niue ili niwe mtu wa maana.” (Shibe Inatumaliza) (a) Eleza muktadha wa maneno haya. (b) Onyesha vile kinaya kinavyojitokeza katika dondoo. (c)...
Previous: Kwa kurejelea hadithi ya Shibe Inatumaliza, eleza namna maudhui ya ufisadi yanavyojitokeza.

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions