Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Jadili dhana ya chozi katika chozi la heri

      

Jadili dhana ya chozi katika chozi la heri.

  

Answers


Raphael
Wahusika wengi katika riwaya hii wamepitia mikasa mingi mizito iliyowapelekea kuwa na huzuni na kutoa machozi
Kuna waliotao machozi ya huzunina wengine wakatoa machozi ya furaha wakati walipofikia hatima yajanga au majanga yaliyowakabili.
Vilio vya kite vilihanikiza wakati makundi mawili yalipopambana.Kundi liliomwuunga mkono Mwekevu na lililomwunga mkomo mpizani wake mwanaume.
Aghalabu machozi ya huzuni yamewabubujikia wahusika kama Ridhaa .Ridhaa alilia machozi wakati familia yake na juma lake la fahari lilipoteketezwa kwa moto.
Neema alilia kwa uchungu wakati alipokumbuka kisa cha Riziki Immaculata kitoto alichookota na akaoga kukichukua na kukitunza .
- Baadaye alidondokwa na machozi ya furaha wakati motto Mwaliko alipokubali kuwa motto wao wa kupanga.
- Umulkheri alilia mara nyingi alipowakumbuka ndugu zake wawii Dickson na Mwaliko.
- Aidha alihuzunika kwao nyumbani.
- Watoto wote watatu wa Lunga Kiriri Kangata walilia machozi ya furaha walipokutana katika hoteli ya Majaliwa.
- Mwangeka na Racheal Apondi walipofunga ndoa ,Ridhaa alilia machozi ya furaha.
- Mwangeka alilia machozi ya kujihurumia wakati baba yake Ridhaa alipomweleza kwa nini hakutaka kuzika mabaki ya familia yake. Yeye aliachilia machozi yamcharaze bila kujali miiko ya nyanyayake. Nyanya aliusia kwamba haipasi mwanamume kulia machozi.
- Mwageka na Annatila pamoja na watoto wengine walilia machozi wakati walipoigiza mbolezi ya mazishi ya mdogo wao Kim.
- Wenyeji walilia wakilizunguka kaburi ktika viviga vya motto wa Ridha,Kim ambaye alifariki akiwa na miaka sita.
- Kumbukumbu za Tila na Mukeli zilimfanya Mwangeka kutoa tone moja la chozi.
- Machozi ya uchungu yalmtirika Umu alipotoka katika kituo cha polisi kutoa taarifa kuwa ndugu zake walikuwa wametoroshwa na Sauna ili wakafanywe vitega uchumi
- Wakati Umu alipo alipokutana na Hazina alitokwa na machozi yenye mseto wa furaha na majonzi .Alifurahia kwa Hzina alijitoa kwenye maisha ya mtaani ya utegemezi na kupata kazi. Machozi ya uchungu yalitokana na fikira kwamba huenda ndugu zake wamo mitaani kama Hazina zamani
- Kairu ,mama yake na familia yake walilia machozi ya uchungu wakati mnuna wake mchanga alipofia mgongonimwa mama yake na wakamzika porini.
- Subira alikuwa na majonzi kutokana na chuki ya mama mkwe wake kwa vile hakuwa ametoka jamii moja na yeye.
- Mwanaheri alidondosha matone mazito ya machozi wakati akiwasimlia wenzake kifo cha mama yake.Aidha udhaifu alio nao Kaisari kutokana na unyama waliotendwa na pia kifo cha Subira.
- Mara nyingi Umu alipofikiria ndugu yake Dick machozi yalimtiririka mno;ingawa alikuwa na wazazi wa kupanga waliompenda mno.
- Wakati Umulhei na Dickson walikutana kisadfa katika uwanja wa ndege walitokwa na machozi ya furaha.
- Wakati Mwangeka na Mwangemi walipomtania babu Mwino Msubili walipopigwa na kulia kwa uchungu.
- Kaizari alitoa machozi ya huzuni wakati alipoona vijana wakipigwa risasi vifuani na askari baadae ya kusimama baabarani na kukataa kuondoka .Walisema “Hatungatuki”.
- Kuna kilio cha Ridhaa alipobaguliwa katika mchezo ‘kavuta” wakati walipohamia ‘msitu wa Heri’ .
- Kuna machozi ya mamba –yanayowatirirka viongozi wanafiki wakati wakigombea uongozi ;kujifanya kwamba wamewasikitikis wananchi wananchi zmbzo wamebanwa nz umasikini kupita kiasi.
-Wale waliochomewa ndani ya mgari na vijana walilia vilio vya uchungu.
- Ridhaa alilia machozi ya uchungu alipomwelezea Mwangeka mkasa wa kupoteza majumba yake.
- Aidha Ridhaa akiwa katika gofu la jumba lake alikumbuka kilio cha Mwangeka akiwa kitoto kichanga.
- Wakati Ridhaa alipokumbuka majadiliano yake na Terry macho yalifurika machozi akajijutia kuwa angelijua angemuuliza maswali yake yoke.
- Vitoo venye njaa katika kambi za wakimbizi walilia machozi ya uchungu kabla kuzimia kwa maumivu.
- Subira naye alikuwa akikilovya kifua chake kila siku kwa sababu a shutuma za mama mkwe, Alisikitika sana kumwacha mumewe na watoto.
- Selume alipolazimika kuacha nyumba yake na moto kwa sababu ya tofauti za kikabilaalilia
raphael answered the question on October 3, 2019 at 07:26


Next: Eleza dhamira ya mwandishi katika hadithi ya kidege
Previous: 'Wapi kile kidume chako kioga? Nasikia ni mmoja wa wale waliotuuza. (1) Weka dondoo hili katika muktadha wake. (2)Oonyesha sifa nne mhusika aliyerejelewa kama 'kidume kioga'

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions