Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Katika Jimbo La Sagamoyo uhuru ni ndoto ambayo haijatimia dhihirisha ukweli wa Kauli hii kwa kutumia tamthilia ya kidogo by Pauline Kea

Katika Jimbo La Sagamoyo uhuru ni ndoto ambayo haijatimia dhihirisha ukweli wa Kauli hii kwa kutumia tamthilia ya kidogo by Pauline Kea

Answers


Caroline
1. wanasagamoyo walipata Uhuru takriban miaka 60 iliyopita lakini hakuna mabadiliko kwa sababu kuna ukoloni mambo Leo unaendelezwa na viongozi kama kenga na Majoka.
2. wanasagamoyo hawana Uhuru wa kujieleza Tunu anajaribu kuleta wananchi pamoja waeleze matakwa yao wanaangaishwa na polisi wa Majoka.
3. wanasagamoyo hawana Uhuru wa maandamano. wakijaribu kuandamana kwa shida zinazawakumba wanapigwa risasi na kutawanyishwa na polisi.
4. wanasagamoyo hawana Uhuru wa vyombo vya habari kwani vinadhibitiwa na serikali ya Majoka.
5. wengine wanafungwa hata bila hatia kama vile Ashua anasingiziwa na kutiwa jela bila kufanya makosa yoyote.
6.wanasagamoyo hawana Uhuru wa kujiunga na vyama vya kisiasa , Majoka anahakikisha ameangamiza chama cha upinzani kabisa kwa kuua Jabali na wafuasi wake ili kila mtu amuunge mkono.
7. wanasagamoyo hawana Uhuru wa kufanya biashara kwa soko ya chapakazi wanafungiwa na Majoka ili anyakue shamba hilo ajenge hoteli ya kifahari.

mwalimu caroline answered the question on March 19, 2019 at 05:52

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions