Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Huku ukitoa mifano mwafaka ,eleza miundo tano ya methali.

      

Huku ukitoa mifano mwafaka ,eleza miundo tano ya methali.

  

Answers


Maurice
(i) Sitiari-ahadi ni deni.

(ii) Tashbihi-usilolijua ni kama usiku wa giza

(iii) Tashhisi-paka akiondoka panya hutawala.

(iv) Takriri- chovya chovya humaliza buyu la asali.

(v) Swali balagha- mla ni mla leo mla jana kalani?

(vi) Taswira-mpanda farasi wawili hupasuka msamba.

(vii) Chuku- mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.

(viii) Tanakali za sauti- chururu si ndondondo!

(ix) Kinaya- kwenye miti hakuna wajenzi.

(x) Kejeli-ucha mungu si kilemba cheupe

(xi) Jazanda-kupanda mchongoma kushuka ndio kazi.

(xii) Kweli kinzani-wagombanao ndio wapatanao.

(xiii) Taashira- kuku mgeni hakosi Kamba mguuni.
maurice.mutuku answered the question on August 3, 2019 at 09:01


Next: Define Service
Previous: Eleza tofauti nne kati ya methali na vitendawili.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions