Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Ni matatizo yapi yanayomkabili mkusanyaji wa Fasihi Simulizi

Ni matatizo yapi yanayomkabili mkusanyaji wa Fasihi Simulizi

Answers


KELVIN
a)Gharama ya utafiti kuwa kubwa kiasi cha mtafiti kutoimudu k.v. kusafiria, kununulia vifaa.
b)Kutojaziwa hojaji kutokana na mtazamo hasi wa jamii dhidi ya ujazaji wake.
c)Wanajamii kukataa kutoa habari wakishuku mtafiti anawapeleleza au kwa kuona haya.
d)Wanajamii wengine kudai walipwe kabla ya kutoa habari na hivyo kukwamiza utafiti.
e)Mbinu nyingine k.v. hojaji huhitaji watu wanaojua kusoma na kuandika na ikiwa mhojiwa hajui utafiti utakwamizwa.
f)Uchache wa wazee na wataalamu wa fasihi simulizi kusababisha kukosekana au kupatikana kwa data isiyo ya kutegemewa.
g)Utawala kukataa kutoa idhini ya kufanya utafiti.
h)Kukosa ufadhili na utafiti kutofanywa kwa kutomudu gharama.
i)Muda wa utafiti kutotosha na hivyo kutopata habari za kutosha kuhusiana na mada yake.

kalvinspartan answered the question on October 21, 2017 at 09:52

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions