-
Eleza matumizi mawili ya kiambishi ‘ku’
Date posted:
October 5, 2019
-
Unda kitenzi kimoja kutokana na nomino ‘Mtubia”
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja moja kudhihirisha ngeli zifuatazo:-
(i) U-U
(ii) Pokomo /Pa-ku-mu
Date posted:
October 5, 2019
-
Andika sifa bainifu za sauti
(i) e:-
(ii) n:-
Date posted:
October 5, 2019
-
Andika kwa udogo:-
Gari la Mzee Maritu limegonga ng’ombe wa jirani wake
Date posted:
October 5, 2019
-
Kwa kurejelea hadithi ya Mke Wangu eleza mambo yanayochangia kuimarika kwa ndoa
Date posted:
October 5, 2019
-
Ken Walibora na Said A. Mohamed: Damu Nyeusi
“Hapa huingii bila kuninyoshea mkono…”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Eleza sifa nne za mzungumziwa.
c) Kwa kurejelea muktadha wa hadithi nzima. Thibisha ukweli wa kauli kuwa mkono mtupu haulambwi
Date posted:
October 5, 2019
-
Geuza zentensi zifuatazo katika kauli kwenye mabano:-
(i) Fundi ameharibu saa (kutendea)
(ii) Umemwona mgeni? (kutendewa)
Date posted:
October 5, 2019
-
Tamthilia ya Mstahiki Meya ni taswira kamili ya mataifa mengi barani Afrika. Thibitisha kauli hii
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza jinsi mbinu ya tabaini inavyojitokeza katika riwaya ya kidagaa kimemwozea
Date posted:
October 5, 2019
-
“Hawa ndio watu muhimu katika ulimwengu wa sasa”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Fafanua mchango wa mrejelewa katika kusambaratisha baraza la Cheneo.
c) Cheneo imekandamizwa kutokana na wakazi wake kutotumia akili. Fafanua kauli hii kwa kurejelea tamthilia nzima.
Date posted:
October 5, 2019
-
…unaa…seema mimiiii sipakui?...wataka mimi nipike? Ehee? Ati mimi nalaza damu? Wewe unaiamsha damu?
a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
b) Eleza mbinu zozote tatu za lugha zilizotumika katika dondoo hili.
c) Jadili ufaafu wa anwani kwa kurejelea mnenaji.
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi ukitumia mzizi – choyo kama :-
(i) nomino
(ii) Kivumishi
(iii) Kiwakilishi
Date posted:
October 5, 2019
-
Vile lelo walalama, kwa yale ulotendewa,
Huyakumbuki ya nyuma, pindi ulipochachawa,
Ulipotenda unyama, uliona ndiyo sawa,
Mtenda akitendewa, hulalama kaonewa!
Ulizusha uhasama, leo wewe wapagawa,
Walia bila kukoma, tungadhani umefiwa,
Sasa huna usalama, huwezi kujiopowa
Mtenda akitendewa, hulalama kaonewa!
Tenda mambo kwa kupima, usiruke huna mbawa,
Una macho kutazama, na akili umepewa,
Matendo hurudi nyuma, atendaye hurudiwa,
Mtenda akitendewa, hulalama kaonewa!
Dunia haishi njama, sijione umepewa,
Ukadhani usalama, binadamu kuwagawa,
Ukahisi ni wanyama, waso hali kama ngawa,
Mtenda akitendewa, hulalama kaonewa!
Unapotenda zahama, siku yako itakuwa,
Ambapo utaungama, useme umechachiwa,
Na uanze kutetema, ulie umeonewa,
Mtenda akitendewa, hulalama kaonewa.
Maswali
a) Lipe shairi hili kichwa mwafaka.
b) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu.
c) Eleza muundo wa ubeti wa pili.
d) Ni kaida zipi za utunzi zilizozingatiwa na mshairi?
e) Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya mjazo.
f) Toa mifano miwili ya idhini ya mshairi.
g) Kwa nini msemewa hafai kulalamika ?
h) Eleza maana ya maneno yafuatayo.
i) Uhasama
ii) Umepowa
Date posted:
October 5, 2019
-
Bainisha aina za nomino zilizopigiwa mistari katika sentensi hii:-
Uhodari wa wanariadha wa Kenya unahitajika kote duniani
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza maana ya ‘jinsi’ kama inavyojitokeza katika sentensi zifuatazo
(i) Naomba unionyeshe jinsi ya kuendesha gari
(ii) Wakenya hawapendezwi na jinsi viongozi wanavyoendeleza ufisadi
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza mambo matano yaliyochangia kuenea kwa Kiswahili nchini kabla na baada ya uhuru
Date posted:
October 5, 2019
-
Unganisha sentensi hizi ukitumia kiunganishi cha kinyume:
Wananchi walikabiliwa na hatari
Wananchi waliendelea kuwaokoa majeruhi
Date posted:
October 5, 2019
-
Unda nomino moja moja kwa kila kitenzi
Shuku
Vumilia
shona
lia
Date posted:
October 5, 2019
-
Ainisha vitenzi katika tungo lifuatalo:
Huyu alikuwa angali bwenini
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja kuonyesha tofauti ya maana kati ya ‘guna’ na ‘kuna’
Date posted:
October 5, 2019
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mishale/mistari:-
Watoto wote wameamka mapema na wazazi wanatayarisha staftahi
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi yenye kiigizi na kihusishi cha mahali
Date posted:
October 5, 2019
-
Bainisha shamirisho kipozi, kitondo na ala katika sentensi ifuatayo:-
Maksuudi alimjengea Tamima Kasri kwa matofali mazuri
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja ukitumia kinyume cha neno ‘lewa’.
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza matumizi ya ‘ji’ katika sentensi hii:
Mwimbaji amejikata jidole lake kwa jiwe
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi ukitumia kitenzi ‘pwa’ katika kauli ya kutendea
Date posted:
October 5, 2019
-
Onyesha kiima, chagizo na yambwa tendewa katika sentensi hii:
Mkulima alimfungia mwajiri ng’ombe kondeni
Date posted:
October 5, 2019
-
Jibu kulingana na maagizo kwenye mabano:-
(i) Hatujui ambako alitorokea (tumia ‘O’ rejeshi)
(ii) Angekuwa na pete, angekupatia (ibadilishe katika wingi kisha uikanishe)
Date posted:
October 5, 2019
-
Yakinisha sentensi hii katika umoja:
Msipohama hapa hamtapewa makazi mapya
Date posted:
October 5, 2019