Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Mtambaji bora anafaa kuwa na sifa zipi?

Mtambaji bora anafaa kuwa na sifa zipi?

Answers


KELVIN
a)Asiwe mwoga ili kuweza kuzungumza hadharani.
b)Asiwe na haya ili kuweza kuzungumzia mambo ya aibu inapobidi.
c)Awe na uelewa wa mazingira na masuala ibuka katika jamii ili kuweza kuwasilisha dhana zisizopatikana katika mazingira yake k.m. kutumia rais kuelezea dhana ya mfalme.
d)Awe na ufahamu mpana wa lugha ili aweze kuitumia kwa uhodari na kuwasilisha kwa wepesi.
e)Awe mchanganfu na mcheshi ili kunasa makini ya hadhira na kuzuia isikinai.
f)Awe na ufahamu mpana wa utamaduni husika ili kuzuia kutumia maneno na ishara zinazoweza kuwaudhi au kupingana na imani za hadhira.
g)Awe na uwezo wa kushirikisha hadhira k.v. kuimba, maswali ya balagha ili isikinai, n.k.

kalvinspartan answered the question on October 21, 2017 at 10:01

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions