Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza dhima ya fasihi simulizi

      

Eleza dhima ya fasihi simulizi.

  

Answers


Mitch
1. Huburudisha, huliwaza na kufurahisha Jamii Kama vile nyimbo Za kazi huimbwa kuwaondolea watu uchovu wakati wa kazi.
2. Huhifadhi historia ya Jamii kwa vile hupokezwa kwa mdomo kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
3. Hukuza uwezo wa kufikiri na kudadisi hasa katika tanzu Kama mafumbo,vitendawili na methali.
4. Hukuza lugha kupitia vipera Kama vile ulumbi,malumbano ya utani na misimu na utambaji wa hadithi.
5. Fasihi simulizi huadilisha kwa vile katika hadithi matendo mabaya hukashifiwa.
6. Hutambulisha jamii na utamaduni wake kupitia tanzu Kama vile visasili, miviga na nyimbo.
7. Fasihi simulizi ni nguzo ya kuunganisha watu kwa vile uwasilishaji wa fasihi simulizi huhitaji uhusika wa watu hivyo umoja hujengeka.
8. Hukuza uzalendo kwa vile watu wanaposhiriki katika miviga ya jando, harusi na matambiko,wao hujitambulisha na kuionea fahari jamii yao .
Mitch_254 answered the question on April 12, 2018 at 07:20


Next: State the characteristics of alpha radiation
Previous: State the characteristics of beta radiation

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions