Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza suala la nafasi ya ndoa katika kigogo

      

Eleza suala la nafasi ya ndoa katika kigogo

  

Answers


kennedy
ASASI YA NDOA

a)NDOA KATI NYA ASHUA NA SUDI.

Ni ndoa yenye mapenzi yanayoegemea upande mmoja.Sudi anampenda Ashua kwa dhati,anajitahidi kwa udi na uvumba ili kumkidhi Ashua.Kila kitu anachokipata humletea.

Sudi ni mwaminifu katika ndoa yake,hajamwenda Ashua kinyume hata Ashua anapotiwa ndani na Majoka.

Aidha, ndoa hii imejengwa katika misingi ya kutoaminiana.Ashua anamshuku mumewe kuwa ana mipango ya kimapenzi na Tunu.

Ashua amechoshwa na Sudi na anaswema kuwa ni afadhali alipo jelani. Anadai kuwa, mawazo ya Sudi,hisia zake, nafsi yake ma kila kitu chake kimesombwa na Tunu.

Ashua ametawalwa na tamaa ya mali na kumwambia Sudi kuwa amechoka kupendwa kimaskini, anabadilika akiwa ndani kwa Majoka, awali alimpenda mumewe kwa dhati lakini baadaye anaomba talaka.Anafurikwa na tamaa na ubinafsi.





b) NDOA KATI YA MAJOKA NA HUSDA.

Ni ndoa ambayo imejaa lawama,Majoka anamlaumu Husda kuwa hampendi bali aliolewa na mali yake.( uk 75)

Hakuna mapenzi ya dhati katika ndoa hii.Majoka hampendi Husda. Alimoa ili kutimiza wajibu wake katika jamii na kama kiongozi,alipaswa kuoa.Alilia usiku huo baada ya kumwoa Husda lakini moyo na nafsi yake viko kwa Ashua.(uk75)

Majoka anampenda Ashua zaidi ya kumpenda hata anaweza kumfia. Anapanga njama ili kumpata. Majoka anakiri kuwa Ashua anamuua moyoni kwa penzi. Anamkondesha na kumkosesha raha kwa kumkataa.Ashua kumkimbia Majoka alimwachia Majoka aibu na penzi lake kwa Ashua linamsongoa.(uk 76).

Asasi ya ndoa imo hatarini kwa kutawaliwa ma tamaa ya mali.Baadhi ya wanaume huoa ili kutimiza matakwa yao na wanawake huolewa kwa sababu ya tamaa ya mali na ubinafsi.

Wanaume wanapaswa kujidadisi na wakae na wake zao kwa heshima.Wanawake nao wanapaswa kujirudi vinginevyo asasi ya ndoa imo hatarini.(uk 77)
Uaminifu na mapenzi ya kweli ni kigezo muhimu ili ndoa idumu.


6965 answered the question on May 1, 2018 at 09:42


Next: What were the effects of long distance trade in Central Africa?
Previous: “Sources of law is that which may be pointed out as forming the basis of law.” In light of this, name and explain FIVE sources of law in Kenya

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions