Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Jadili mbinu ya kinaya katika kigogo

      

Jadili mbinu ya kinaya katika kigogo

  

Answers


Noah
Kinaya(irony)-ni hali ya mambo katika riwaya ama hadithi kuwa kinyume na matarajio.
(i)Habari zinazotolewa na mjumbe katika rununu ni za kinaya,kuwa wanasagamoyo wasirudishe maendeleo nyuma bali wafurahie ufanisi ambao umepatikana katika kipindi cha miaka tisini baada ya uhuru.Ujumbe huu ni kinaya kwa vile Sagamoyo hakuna maendeleo wala ufanisi.
(ii)Boza anadai kuwa kulipa kodi na kujenga nchi ni kujitegemea,kauli hii ni kinaya kwa vile kodi wanayolipa wanasagamoyo haitumiki kujenga nchi kwa vyovyote vile.
(iii)Sudi anasema kuwa katika kipindi cha mwezi mzima wa uhuru wale mali walizochuna kwa miaka sitini.Ni kinaya kwa kuwa hakuna walichovuna,Viongozi hujilimbikizia mali.
(iv)Boza anamwambia Sudi kuwa wanatia doa kwa kila jambo nzuri.Ni kinaya kwa vile hakuna mambo Mazuri ambayo Majoka amefanya Sagamoyo.
(v)Wanasagamoyo kusheherekea miaka sitini ya uhuru ni kinaya kwani hakuna cha muhimu kusheherekewa.
Boza anadai kuwa Kinyango chake chapendeza na kufanana na shujaa Marara Bin Ngao,ni kinaya kwani kinyango hicho hakifanani na shujaa huyo.
(vi)Mzee Majoka kudai kuwa anamheshimu Sudi ni Kinaya kwani Majoka hana heshima kwa raia wake,nia yake ni kutaka Sudi amchongee kinyango.


Kibet Koina answered the question on January 5, 2019 at 18:35


Next: "Sitaacha kula mkate kwa kuchelea kiungulia"eleza muktadha wa dondoo hili katika tamthilia ya kigogo
Previous: Discuss the class alliance and colonial political power in Kenya

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions