Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

(a) Katika jamii huwa wakati mwingine kuna matumizi ya lugha isiyo ya kistaarabu.taja mifano mitano ya lugha ya sampuli hiyo. ( alama 5) (b) Taja mambo matano...

      

(a) Katika jamii huwa wakati mwingine kuna matumizi ya lugha isiyo ya kistaarabu.taja mifano mitano ya lugha ya sampuli hiyo. ( alama 5)

(b) Taja mambo matano yanayoathiri jinsi tunavyoweza kutumia lugha katika jamii(mtindo nafsi na mtu)
MAJIBU

  

Answers


ESTHER
1. (a) - Hutaja sehemu nyeti za mwili wa binadamu k.v za uzazi.
- Hutaja mada pale isisyofaa mf. Kutaja vifo,magonjwa , upimaji wa kinyesi , makamasin.k wakati wa kula.
- Wanataja vilema au walio na udhaifu mbalimbali wakiwepo. Mf. Zeruzeru , kipofu , kiziwi
- Hutumia maneno ya kimatusi k.v mjinga , pumbavu, mshezi. n.k.
- Hutumia lugha ya kulaani . KN Ninakuombea kifo cha haraka au ufutwe kazi. (5 x 1 = 5)
(b) - Hadhira mf. Wale anaowazugumzia kama ni watoto atatumia lugha yenye ucheshi.
- Utungo / matini - kama ni mashairi utatumia lugha yenye ukiushi.
- Tabaka mf. Tabaka la juu wamezoea kingereza hawapendi kwa mfano Kiswahili.
- Hali mf. Chokora wanatumia lugha ya kutisha, mtu akiwa mgonjwa ua mlevi lugha yake huwa tofauti.
- Mada - zile ngumu lugha huwa nyepesi.
- Matilaba - mf Mtu anapotaka wenzake wamuunge mkono atatumia lugha kwa namna ambayo itawavuta kwake.
- Umri - Kundi la kiumri husababisha vilugha mf. Vijana watakuwa na mtindo wao. (5 x 5 = 10)


ESTHER STEVE answered the question on April 30, 2018 at 19:53


Next: (a) Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii. i) Lafudhi ii) Lahaja iii) Rejesta Taja sifa nne za sajili ya wanasiasa (alama 4)
Previous: Tom: Vipi Tracey? Naona leo unalinga sana. Umenivaria miwani, mbona hivi? Is it because you are very smart today? Tracey: Niko poa! Hata hivyo naona una yako mengine wewe!...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions