Yohana alisema “Njiani kulikuwa kumenyesha sana ndio sababu tumechelewa”
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 10:07
-
Taja vielezi vinavyopatikana katika sentensi hizi; kisha ueleze ni vielezi vya aina gani
(i) Aliamka alfajiri
(ii) Mtu huyu ni hodari sana
(Solved)
Taja vielezi vinavyopatikana katika sentensi hizi; kisha ueleze ni vielezi vya aina gani
(i) Aliamka alfajiri
(ii) Mtu huyu ni hodari sana
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Kamilisha jedwali ukifuatia mfano uliopewa
Wimbo Mwimbaji Uimbaji
Jengo ……………. ……….
Pendo ……………. ……….
(Solved)
Kamilisha jedwali ukifuatia mfano uliopewa
Wimbo Mwimbaji Uimbaji
Jengo ……………. ……….
Pendo ……………. ……….
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza tofauti iliyopo katika jozi hii ya sentensi.
Alimpatia soda ya chupa
Alimpatia soda kwa chupa.
(Solved)
Eleza tofauti iliyopo katika jozi hii ya sentensi.
Alimpatia soda ya chupa
Alimpatia soda kwa chupa.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Soma Makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Nchi nyingi za ulimwengu unaoendelea, au ule uliokuwa ukiitwa ulimwengu wa ta
zimegawika sehemu mbili mbili. Sehemu hizi zinazidi kutoshabihiana kila...
(Solved)
Soma Makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Nchi nyingi za ulimwengu unaoendelea, au ule uliokuwa ukiitwa ulimwengu wa ta
zimegawika sehemu mbili mbili. Sehemu hizi zinazidi kutoshabihiana kila uchao
zinatengana kiasi cha kukaribia kupigwa mfano wa masafa ya ardhi na mbingu. Seher
zenyewe ni mijini na mashabani. Sehemu hizi, hasa ukizitia katika mizani ya hali na jia
za watu za maisha, zimetofautiana mno. Kiasi cha tofauti hizi ni kikubwa hadi
kuonekana kama kwamba hazina uhusiano kamwe, mithili ya nchi mbili tofauti.
Hebu sasa tuzingatie yale yana yozifanya sehemu hizi kukosa kufanana. Hapa
tutawajibika kuzizingatia tofauti zilizo bayana baina ya watu wa shamba na wa mijini,
hasa kufungamana na jinsi wanavyoyaendesha maisha yao.
Jambo lililo wazi ni kwamba watu wa mashambani hawajapiga hatua ya maana kuhusu
jinsi wanavyuotakikana kuishi katika karne ya ishirini. Watu hawa bado wanaishi kama
walivyoishi mababu zao. Hawahisi halahala ya jambo lolote. Mategemeo yao ni shamba;
usubiriwe msimu mzuri wa mvua, watu walime, Mungu akineemeshe kilimo, wavune
mavuno mema, Chakula kikiwa tayari, wale, walale, siku nyingine warudie mkondo uo
huo wa kuendesha maisha yao.
Watu hawa maisha yao yamepangika mikondo mitatu tu: kuzaliwa, kuoa au kuolewa, na
kufa. Zaidi ya mikondo hii, maisha ya viumbe hawa hayana mabadiliko makubwa.
Mabadiliko haypendelewi sana huko mashambani. Huko, wanaume ni mabwana,
wanawake ni mfano wa vijakazi na watoto hawana tofauti kubea na watwana. Mwanume
akikohoa, mkewe akimbilie kulikokoholewa, na watoto watetemeke. Wanawake wa
shamba na watoto hawana haki hata ya kunena, wala hawajui haki ni nini.
Kwa upande mwingine, mijini kuna viwanda, kuna majumba, kuna magari na kuna
vyombo vingi sana vya maendeleo ya kisiku izi. Watu wa mijini ni watu wa ulimwengu
kote, wala si watu wa mji mmoja tu. Watu wa mji wowote ulimwenguni huweza
kuwasiliana na wenzao wa miji mingine kokote kule ulimwenguni kwa njia ya runinga.
Pia, kwa watu wa mjini, kuona kiumbe kidogo kabisa kisichoweza kuonekana kwa
macho si ibura hata. Kiumbe cha namna hiyo huonekana kupitia mangala. Na kwa wale
walioondokea kuwa wanajimu wa kisasa, kuziona sayari na thurea zilizoko mbali sana
nasi kupitia ningala ni jabo la kawaida sana.
Watu wa mjini huwa na mabadiliko mengi sana katika maisha yao, wala sio mikondo
aina tatu tu. Kwa mfano, wanawake wa mijini hawakubali tena kuonewa na wanaume.
Wanajua vyema sana maslahi yao na wameiweka menke yao mbele; yaani mahali pao
katika jamii, wakiwa wao ni wanawake. Kupigania haki sawa na wanaume bila kulegeza
kamba. Huku kupambana kimaisha kama wapambanavyo wanaume na kufanikiwa kufanya kazi za kusikika kam vile uwakili, udaktari, uhandisi, urubani na nyinginezo
zilizokuwa zikifanywa na wanaume tu. Wanawake wengine hata ni maprofesa! Kweli
watu wa mijini wameendelea.
a) Toa maelezo kuhusu tofauti zinazosemekana ni bayana baina ya maisha ya watu
wa shamba nay ale ya watu wa mijini.
b) Rejelea “Mungu” katika aya ya tatu na neon “viumbe” katika aya ya nne.
Bainisha uhusiano uliopo baina ya manen haya mawili, hasa ukizingatia jinsi
yavyotumiwa katika habari. Je matumizi haya yankupa hisia gani?
c) Unadhani mwandishi ana maana gani anaposema ya kwamba huko mashambani
“wanawake ni mfano wa vijakazi, na watoto hawana tofauti kubwa na watwana?”
d) Orodhesha vifaa vyovyote vitano vilivyotajwa katika taarifa hii, kisha ueleze
umuhimu wa kila kimoja wapo.
e) “Watu wa mijini ni watu wa ulimwengu kote” Hapa mwandishi anamaanisha
nini?
f) (i) Ni nini maana ya neon menke?
(ii) Mwandishi anamaliza taarifa yake kwa kusema “Kweli watu wa mijini
wameendelea.” Kwa muhtasari, ni tabia gani za wanamiji zilizomfanya
kukiri hivyo.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Kiambishi- U-hutambulisha majina yote ya ngeli ya U (umoja). Hata
hivyo baadhi majina hay huchukua viambishi tofauti tofauti katika wingi.
Orodhesha majina ma kama hayo, kisha uonyeshe...
(Solved)
Kiambishi- U-hutambulisha majina yote ya ngeli ya U (umoja). Hata
hivyo baadhi majina hay huchukua viambishi tofauti tofauti katika wingi.
Orodhesha majina ma kama hayo, kisha uonyeshe viambilshi hivyo tofauti
vya ngeli (Katika umoja na Wingi)
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maana mbili za sentensi:
Jua nisemalo ni muhimu kwetu.
(Solved)
Eleza maana mbili za sentensi:
Jua nisemalo ni muhimu kwetu.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Akifisha:
Sijaona kitabu kizuri kama hiki utaniazima siku ngapi bashiri alimuliza
sijaona.
(Solved)
Akifisha:
Sijaona kitabu kizuri kama hiki utaniazima siku ngapi bashiri alimuliza
sijaona.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Nyambua vitenzi vifuatavyo ili kupata majina (nomino) mawili mawili
tofauti:
(i) Kumbuka
ii)Cheka
(Solved)
Nyambua vitenzi vifuatavyo ili kupata majina (nomino) mawili mawili
tofauti:
(i) Kumbuka
ii)Cheka
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Andika kwa umoja
Tumewaondoleeni matatizo yenu, yafaa mtushukuru.
(Solved)
Andika kwa umoja
Tumewaondoleeni matatizo yenu, yafaa mtushukuru.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Mwanamke wa kisasa anazaliwa na kukulia katika mazingira yaliyobadilika mno.
Matazamio yake maishani ni tofauti na yale ya wanawake walioishi mapote...
(Solved)
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Mwanamke wa kisasa anazaliwa na kukulia katika mazingira yaliyobadilika mno.
Matazamio yake maishani ni tofauti na yale ya wanawake walioishi mapote mawili
yaliyopita; wanawake makamu ya nyanyake na mamaake-kuu.
Yeye hatarajii kuzaliwa, kukua, kuolewa, kuwa mke wa bwana, kumzalia watoto, na
daima dawamu kuwa ‘mwendani wa jikoni’ akawapikia watoto na bwanake chakula; na
akitoka jikoni aelekee shambani kulima, kichakani kuchanja kuni, mtoni kufua nguo na
kuteka maji ya kutumia nyumbani. Mwanamke wa kisasa huandamana na mwanamume.
Akanyangapo mume naye papo huutia wayo wake.
Mwanamke wa kisasa huenda shule na kujifunza yote yafunzwayo huko. Hushindana na
wanawake kwa wanaume na kuibuka mshindi si mara haba. Huibuka mshindi katika
masomo ya lugha, historia, jiografia, hesabu, sayansi na mengineyo, sawa na
mwanamume.
Mwanamke wa kisasa hutaka kufanya kazi za kibega, akazifanya. Akataka kuwa
mwalimu, akawa. Akataka kuwa daktari, akafanikiwa. Almuradi, siku hizi mwanamke
hufanya kazi yoyote ile afanyayo mwanamume. Kuna wanawake marubani wa ndege,
masonara, waashi, wahandishi, madereva wa magari, mawakili, mahakimu, mawaziri
wakuu na hata marais wa nchi. Hakuna kazi isiyofanywa na mwanamke siku hizi.
Mwanamke wa kisasa hateswi akafyata ulimi. Anapohiniwa yeye hupigania haki yake
kwa dhati na hamasa. Katu hakubali ‘mahali pake’ katika jamii alipotengewa na
wanaume wenye mawazo ya kihafidhina yaliyopitwa na wakati.
Siku hizi mwanamke huolewa tu wakati amepata kazi ya kumwezesha kujikimu maishani
au pale anapokuwa na hakika kwamba biashara yake, iwapo ni mfanyi biashara, imepiga
hatua ya kutomrudisha ukutani.
Mwanamke wa kisasa haamuliwi katika jambo lolote, bali hufanya maamuzi yake
mwenyewe. Kwa upande mwingine, mwanamume wa ‘kisasa’, ambaye bado amefungwa
pingu na taasubi za kiume, hapendezwi na mwanamke huyu. Huuma kidole akatamani ya
kale, lakini wapi! Analazimika kumkubali mwanamke huyu kama mshirika sawa
maishani, na kuishi naye, apende asipende. Shingo upande analazimika kukubali kwamba
mabadiliko haya sio mithili ya kiwingu kipitacho, bali ni ya aushi.
a) Msemo ‘mwendani wa vijungu jiko’ unadhihirisha hali gani ya
mwanamke katika jamii?
b) Jamii imemfanya mwanamke kuwa hayawani wa mizigo. Fafanua
c) Eleza maana ya ‘akanyagapo mume papo huutia wayo wake.’
d) Zungumzia maswala ya ndoa na elimu huku ukilinganisha mwanamke wa
kiasili na wa kisasa.
e) Mwanamume wa kisasa anamwonaje mwanamke wa kisasa?
f) Taja mifano minne ya ‘mawazo ya kihafidhina.
g) Eleza maana ya:
(i) Akafyata ulimu……………………………………………
(ii) Ukatani…………………………………………………….
(iii) Taasubi za kiume………………………………………….
(iv) Aushi…………………….………………………………..
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Andika upya sentensi ifuatayo ukitumia kirejeshi ( kihusiano) cha ngeli cha mwisho
Mwanafunzi anayefanikiwa maishani ni yule anayesoma kwa bidii na pia
anayetii wakuu wake
(Solved)
Andika upya sentensi ifuatayo ukitumia kirejeshi ( kihusiano) cha ngeli cha mwisho
Mwanafunzi anayefanikiwa maishani ni yule anayesoma kwa bidii na pia
anayetii wakuu wake
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Tumia semi hizi katika sentensi kuonyesha maana:
(i) Kuchokoachokoa maneno
(ii) Kumeza shubiri
(Solved)
Tumia semi hizi katika sentensi kuonyesha maana:
(i) Kuchokoachokoa maneno
(ii) Kumeza shubiri
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Tunatumia viashiria vya kuthibitisha kwa mfano kitabu kiki hiki. Sasa kamilisha
Ni mbwa …………………….. aliyekula chakula cha mtoto
(Solved)
Tunatumia viashiria vya kuthibitisha kwa mfano kitabu kiki hiki. Sasa kamilisha
Ni mbwa …………………….. aliyekula chakula cha mtoto
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza tofauti mbili muhimu za kimaumbile kati ya wanyama
(i) Kifaru
(ii) Nyati
(Solved)
Eleza tofauti mbili muhimu za kimaumbile kati ya wanyama
(i) Kifaru
(ii) Nyati
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Watu wafuatao wanafanya kazi gani
(i) Mhasibu
(ii) Mhazili
(Solved)
Watu wafuatao wanafanya kazi gani
(i) Mhasibu
(ii) Mhazili
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi:
(i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata
(ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike
(Solved)
Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi:
(i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata
(ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya
kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine
(Solved)
Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya
kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi:
Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali
(Solved)
Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi:
Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Akifisha kifungu hiki:
Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika
insha hii.
(Solved)
Akifisha kifungu hiki:
Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika
insha hii.
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)
-
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite
“kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa...
(Solved)
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite
“kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa katika uzalishaji mimea
na uvunani. Imesemekana ya kwamba, ghairi ya wivu na kijicho baina ya jamii
mbalimbali ulimwenguni, aina hii ya sayanzi ina uwezo na kuangamiza kabisa janga la
njaa katika sayari hii yetu. Kivipi? Rahisi kabisa. Ni kwamba mbegu moja tu ya aina
yoyote ya mmea, baada ya kuneemeshwa vyumba vyake vidogo ambavyo ndivyo hasa
msingi wa uhai vinaweza kunyunyiziwa dawa maalum ili vitawanyike mara hata
mamilioni na kuwa mimea kamili…. Mamilioni!
Sayansi hii tarari inatumiwa kukuza viazi na vyakula vingine. Hii ina maana ya kwamba
mashamba makubwa si muhimu siku hizi, yaani vyakula vingi kabisa vinaweza kukuzwa
mahali padogo sana. Kwa hivyo hivi karibuni tu, kutakuwa hakuna haja ya kupigania
mashamba.
Vyema. Hebu sasa tuangalie zilizokwishapigishwa hii sayansi ya “kutumbisha” na mahali
binadamu alipofika kimaendeleo kwa sababu ya hatua hizo. Jambo la kwanza sayansi hii
tayari imeshatumiwa kuzalishia wanyama wengi, wengi sana wadogo wadogo kwa lengo
la kuendeleza mbele utafiti. Kufikia sasa, wanyama hawa waliotengenezwa na binadamu
katika maabara yake bado wanahifadhiwa mumo humo walimotengenezwa. Hii ni hatua
kubwa na binadamu anastakili pongezi kwa jinsi anayotumia akili yake kuvumbua ibura
hizi zote.
Hata hivyo imesemwa kwamba kuchamba kwingi ni kuondoa mavi. Binadamu kama
ijulikanavyo, anajaribu sana jujitakasa kwa kujitenga mbali sana na asili yake ya unyama
ili aufikie ubinadamu mkamilifu. Hapana ubaya hapo. Lakini tukirudi nyuma tunakuta ya
kwamba binadamu sasa aneingia tama kubwa sana kuliko wakati wowote ule. Tamaa hii
imeletwa na ujuzi wake katika sayansi hii ya “kutumbisha.” Sasa binadamu ana jua
vizuri sana kwamba kwa vile ana ujuzi wa kutengeza panya na hata kondoo katika
maabara basi hata ujuzi wa kutengeneza binadamu pia anao! Na hapo ndipo tatizo lilipo.
Swali hi hili: Je, ujuzi huu utatufikisha wapi? Na kikomo chake kitakuwaje?
Binadamu sasa ujuzi wake unamtia wasiwasi. Wataalam wa sayansi hii wamejiuliza mara
nyingi nini kitakachotokea ujuzi huu utakapomilikiwa na mwenda wazimu mweledi.”
Watu kadha wa kadha, miongoni mwao wakiwa wanasiasa wamejiuliza mara
zisizohesabika swali hili: kama Hitler angekuwa na ujuzi huu, angekuwa na lazima gani
ya kuwaulia mbali wayahudi milioni sita wasiokuwa na hitia isipokuwa na nywele
nyeusi na hawakuwa weupe sana kama wazungu? Hitler aliamini ya kwamba “mtu
mzuri” ni mwenye pua ya upanga (kama mzungu), macho ya buluu nywele rangi ya dhahabu na mwenye kimo cha futi sita au zaidi kidogo. Hivyo lengo lake lilikuwa ni
kubuni taifa la watu wazuri pekee ambao mwisho watautawala ulimwengu na kuenea
duniani kote. Katika mpango wake, watu weusi wote wangefaa kuangamizwa tu ili watoe
nafasi kwa watu aliowaona yeye kuwa bora.
Sasa baada ya sayansi hili ya “kutumbisha” kuvumbuliwa, wataalam wametishika sana.
Wamewaza jinsi ambavyo Hitler angeweza kufanya kama angekuwa mjuzi wa taaluma
hiyo.
Kitisho hiki kimezidi kuwatwanga wataalam na wasiokuwa wataalam hivi majuzi tu
ilipogunduliwa maiti ya msichana wa miaka kumi na mine huko milima ya Andes,
Amerika ya kusini. Msichana huyo alikuwa ametolewa kafara miaka karne tano zilizo
pita lakini hakuoza kwa sababu ya baridi kali ya barafu milimani.
Kwa sababu ya dukuduku la uvumbuzi ambalo haliishi dhana za kiajabu ubongo wa
binadamu, wataalamu wa “kuchezea” maumbile walipomwona msichana huyo maiti,
upesi upesi wakampima. Walipofanya hivyo wakagundua ya kwamba mayai yake ni
timamu kabisa wala hayajaharibiwa na mpito wa karne. Papo hapo wengine wakajiwa na
wazo la kuyatoa mayai hayo na kuyahifadhi kwenye mabara. Tamaa ikazidi zaidi ya
zaidi. Baadhi ya wataalamu wakajiwa na wazo la “kuyaneemesha” mayai hayo na mbegu
za uzazui za wanaume. Kwa lengo gani? Kuunda watoto amabo mama yao alikufa
zamani za kale ili waonekane watakuwa watu wa aina gani!
Sasa fikiria mwenyewe! Watoto hawa wa maabara wakiwa weledi zaidi ya binadamu
yeyote yeyote wa kisasa lakini watiifu kama mbwa na paka itakuwaje? Hakuna
atakayefikiria “kutumbisha” ili tuwe na vijitumwa vyetu vipenzi majumbani mwetu
vinavyofanana nasi badala ya paka na mbwa wasiovishwa nguo?
(a) Andika kichwa kifaacho kwa nakala hii
(b) Kutumia sayansi ya “kutumbisha” kunaweza kumsaidia binadamu kuangamiza
mabaa gani mawili yanayomkabili sasa?
(c) Unadhani ni kwa nini wanyama waliozalishwa kwa kutumia sayansi hii bado
wamo maabarani?
(d) Fafanua methali “kuchamba kwingi nikuondoka na mavi” kulingana na muktadha
wa habari hii
(e) Kuna ubaya gani kutumbisha watu?
(f) Mwandishi anaonekana kutishwa sana na uwezekano wa sayansi ya kutumbisha
kuishia mikononi mwa “wendawazimu weledi” kwani kuna hatari gani?
(g) Eleza kwa ukamilifu matatizo yanayoweza kuukumba ulimwengu iwapo mayai ya
msichana wa Andes yatatumbishwa
Date posted:
June 27, 2019
.
Answers (1)