Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi: Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali

Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi:
Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali

Answers


Kavungya
fig127620191115.png
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 08:16

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Akifisha kifungu hiki: Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika insha hii. (Solved)

    Akifisha kifungu hiki:
    Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika
    insha hii.

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite “kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
    Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite
    “kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa katika uzalishaji mimea
    na uvunani. Imesemekana ya kwamba, ghairi ya wivu na kijicho baina ya jamii
    mbalimbali ulimwenguni, aina hii ya sayanzi ina uwezo na kuangamiza kabisa janga la
    njaa katika sayari hii yetu. Kivipi? Rahisi kabisa. Ni kwamba mbegu moja tu ya aina
    yoyote ya mmea, baada ya kuneemeshwa vyumba vyake vidogo ambavyo ndivyo hasa
    msingi wa uhai vinaweza kunyunyiziwa dawa maalum ili vitawanyike mara hata
    mamilioni na kuwa mimea kamili…. Mamilioni!

    Sayansi hii tarari inatumiwa kukuza viazi na vyakula vingine. Hii ina maana ya kwamba
    mashamba makubwa si muhimu siku hizi, yaani vyakula vingi kabisa vinaweza kukuzwa
    mahali padogo sana. Kwa hivyo hivi karibuni tu, kutakuwa hakuna haja ya kupigania
    mashamba.

    Vyema. Hebu sasa tuangalie zilizokwishapigishwa hii sayansi ya “kutumbisha” na mahali
    binadamu alipofika kimaendeleo kwa sababu ya hatua hizo. Jambo la kwanza sayansi hii
    tayari imeshatumiwa kuzalishia wanyama wengi, wengi sana wadogo wadogo kwa lengo
    la kuendeleza mbele utafiti. Kufikia sasa, wanyama hawa waliotengenezwa na binadamu
    katika maabara yake bado wanahifadhiwa mumo humo walimotengenezwa. Hii ni hatua
    kubwa na binadamu anastakili pongezi kwa jinsi anayotumia akili yake kuvumbua ibura
    hizi zote.

    Hata hivyo imesemwa kwamba kuchamba kwingi ni kuondoa mavi. Binadamu kama
    ijulikanavyo, anajaribu sana jujitakasa kwa kujitenga mbali sana na asili yake ya unyama
    ili aufikie ubinadamu mkamilifu. Hapana ubaya hapo. Lakini tukirudi nyuma tunakuta ya
    kwamba binadamu sasa aneingia tama kubwa sana kuliko wakati wowote ule. Tamaa hii
    imeletwa na ujuzi wake katika sayansi hii ya “kutumbisha.” Sasa binadamu ana jua
    vizuri sana kwamba kwa vile ana ujuzi wa kutengeza panya na hata kondoo katika
    maabara basi hata ujuzi wa kutengeneza binadamu pia anao! Na hapo ndipo tatizo lilipo.
    Swali hi hili: Je, ujuzi huu utatufikisha wapi? Na kikomo chake kitakuwaje?

    Binadamu sasa ujuzi wake unamtia wasiwasi. Wataalam wa sayansi hii wamejiuliza mara
    nyingi nini kitakachotokea ujuzi huu utakapomilikiwa na mwenda wazimu mweledi.”
    Watu kadha wa kadha, miongoni mwao wakiwa wanasiasa wamejiuliza mara
    zisizohesabika swali hili: kama Hitler angekuwa na ujuzi huu, angekuwa na lazima gani
    ya kuwaulia mbali wayahudi milioni sita wasiokuwa na hitia isipokuwa na nywele
    nyeusi na hawakuwa weupe sana kama wazungu? Hitler aliamini ya kwamba “mtu
    mzuri” ni mwenye pua ya upanga (kama mzungu), macho ya buluu nywele rangi ya dhahabu na mwenye kimo cha futi sita au zaidi kidogo. Hivyo lengo lake lilikuwa ni
    kubuni taifa la watu wazuri pekee ambao mwisho watautawala ulimwengu na kuenea
    duniani kote. Katika mpango wake, watu weusi wote wangefaa kuangamizwa tu ili watoe
    nafasi kwa watu aliowaona yeye kuwa bora.

    Sasa baada ya sayansi hili ya “kutumbisha” kuvumbuliwa, wataalam wametishika sana.
    Wamewaza jinsi ambavyo Hitler angeweza kufanya kama angekuwa mjuzi wa taaluma
    hiyo.

    Kitisho hiki kimezidi kuwatwanga wataalam na wasiokuwa wataalam hivi majuzi tu
    ilipogunduliwa maiti ya msichana wa miaka kumi na mine huko milima ya Andes,
    Amerika ya kusini. Msichana huyo alikuwa ametolewa kafara miaka karne tano zilizo
    pita lakini hakuoza kwa sababu ya baridi kali ya barafu milimani.

    Kwa sababu ya dukuduku la uvumbuzi ambalo haliishi dhana za kiajabu ubongo wa
    binadamu, wataalamu wa “kuchezea” maumbile walipomwona msichana huyo maiti,
    upesi upesi wakampima. Walipofanya hivyo wakagundua ya kwamba mayai yake ni
    timamu kabisa wala hayajaharibiwa na mpito wa karne. Papo hapo wengine wakajiwa na
    wazo la kuyatoa mayai hayo na kuyahifadhi kwenye mabara. Tamaa ikazidi zaidi ya
    zaidi. Baadhi ya wataalamu wakajiwa na wazo la “kuyaneemesha” mayai hayo na mbegu
    za uzazui za wanaume. Kwa lengo gani? Kuunda watoto amabo mama yao alikufa
    zamani za kale ili waonekane watakuwa watu wa aina gani!

    Sasa fikiria mwenyewe! Watoto hawa wa maabara wakiwa weledi zaidi ya binadamu
    yeyote yeyote wa kisasa lakini watiifu kama mbwa na paka itakuwaje? Hakuna
    atakayefikiria “kutumbisha” ili tuwe na vijitumwa vyetu vipenzi majumbani mwetu
    vinavyofanana nasi badala ya paka na mbwa wasiovishwa nguo?

    (a) Andika kichwa kifaacho kwa nakala hii
    (b) Kutumia sayansi ya “kutumbisha” kunaweza kumsaidia binadamu kuangamiza
    mabaa gani mawili yanayomkabili sasa?
    (c) Unadhani ni kwa nini wanyama waliozalishwa kwa kutumia sayansi hii bado
    wamo maabarani?
    (d) Fafanua methali “kuchamba kwingi nikuondoka na mavi” kulingana na muktadha
    wa habari hii
    (e) Kuna ubaya gani kutumbisha watu?
    (f) Mwandishi anaonekana kutishwa sana na uwezekano wa sayansi ya kutumbisha
    kuishia mikononi mwa “wendawazimu weledi” kwani kuna hatari gani?
    (g) Eleza kwa ukamilifu matatizo yanayoweza kuukumba ulimwengu iwapo mayai ya
    msichana wa Andes yatatumbishwa

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Bila kunyambua, andika maneno mawili ambayo yanatokana na shina moja na neno: imani (Solved)

    Bila kunyambua, andika maneno mawili ambayo yanatokana na shina
    moja na neno: imani

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi ya neno moja ambayo ina visehemu vifuatavyo vya sarufi - Kiima - Wakati - Kirejeleo - Kiswahili kitendwa - Kitenzi (Solved)

    Tunga sentensi ya neno moja ambayo ina visehemu vifuatavyo vya
    sarufi
    - Kiima
    - Wakati
    - Kirejeleo
    - Kiswahili kitendwa
    - Kitenzi

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Mahali palipohamwa panaitwa? (Solved)

    Mahali palipohamwa panaitwa?

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana mbili mbili zinazotokana na sentensi zifuatazo (i) Mtoto alitimua mbio, kuona nyoka (ii) Juma alifagia chakula (iii) Sisikii vizuri (Solved)

    Eleza maana mbili mbili zinazotokana na sentensi zifuatazo
    (i) Mtoto alitimua mbio, kuona nyoka
    (ii) Juma alifagia chakula
    (iii) Sisikii vizuri

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Andika methali nyingine ambayo maana yake ni kinyume cha Riziki kama ajali huitambui ijapo (Solved)

    Andika methali nyingine ambayo maana yake ni kinyume cha
    Riziki kama ajali huitambui ijapo

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi moja moja Kuramba kisogo Kuzunguka mbuyu (Solved)

    Eleza maana ya misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi moja moja
    Kuramba kisogo
    Kuzunguka mbuyu

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Bila kubadilisha maana, andika sentensi zifuatazo ukitumia kirejeleo cha ngeli kifaacho (i) Nyumbu alishinda farasi kukimbia (ii) Milango yote yajifunga ovyo, nenda uakafunge (iii) Hamisi amekata nyasi vizuri... (Solved)

    Bila kubadilisha maana, andika sentensi zifuatazo ukitumia kirejeleo cha ngeli
    kifaacho
    (i) Nyumbu alishinda farasi kukimbia
    (ii) Milango yote yajifunga ovyo, nenda uakafunge
    (iii) Hamisi amekata nyasi vizuri
    (iv) Jiwe lile liliangukia matunda

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Andika katika kauli ya kutendesha (i) Nataka upike chakula hiki vizuri (ii) Toa ushuru wa forodhani (Solved)

    Andika katika kauli ya kutendesha
    (i) Nataka upike chakula hiki vizuri
    (ii) Toa ushuru wa forodhani

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto (Solved)

    Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo
    (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini
    (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama (Solved)

    Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii
    Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Kutokana na vitenzi tunaweza kuunda majina na pia kutokana na majina tunaweza kuunda vitenzi. Mfano Jina ... (Solved)

    Kutokana na vitenzi tunaweza kuunda majina na pia kutokana na majina
    tunaweza kuunda vitenzi. Mfano
    Jina Kitendo
    Mwuzaji Uza
    Mauzo Uza
    Wimbo Imba

    Sasa kamilisha:
    Jina Kitenzi
    (i) Mnanda
    (ii) Kikomo
    (iii) Ruhusa
    (iv) ashiki
    (v) husudu

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Tunasema: Mtoto huyu mzuri anapendeza Ukitumia majina yafuatayo kamilisha sentensi ukifuata mfano ulio hapo juu (i) Ngome (ii) Mitume (iii) Heshima (iv) Ng’ombe (v) Vilema (Solved)

    Tunasema: Mtoto huyu mzuri anapendeza
    Ukitumia majina yafuatayo kamilisha sentensi ukifuata mfano ulio hapo juu
    (i) Ngome
    (ii) Mitume
    (iii) Heshima
    (iv) Ng’ombe
    (v) Vilema

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza kazi ifanywayo na (i) Mhariri (ii) Jasusi (Solved)

    Eleza kazi ifanywayo na
    (i) Mhariri
    (ii) Jasusi

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Fafanua maana za misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi (i) Kula uyundo (ii) Kula uhondo (Solved)

    Fafanua maana za misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi
    (i) Kula uyundo
    (ii) Kula uhondo

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Andika sentensi zifuatazo ukitumia kinyume cha neno lililoandikwa kwa herufi za Mlazo (i) Usijaribu kupaaza sauti unapoimba (ii) Huyu ni mtu mwenye busara (iii) Binadamu hawezi kumuumbua mwenzake (Solved)

    Andika sentensi zifuatazo ukitumia kinyume cha neno lililoandikwa kwa herufi za
    Mlazo
    (i) Usijaribu kupaaza sauti unapoimba
    (ii) Huyu ni mtu mwenye busara
    (iii) Binadamu hawezi kumuumbua mwenzake

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya sentensi hizi (i) Mikono yao imeshikana (ii) Mikono yao imeshikamana (Solved)

    Eleza maana ya sentensi hizi
    (i) Mikono yao imeshikana
    (ii) Mikono yao imeshikamana

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Sahihisha makosa yaliyomo katika sentensi mbili zifuatazo (i) Bei za vitu zimepanda juu sana siku hizi (ii) Weka mizigo kwa gari (Solved)

    Sahihisha makosa yaliyomo katika sentensi mbili zifuatazo
    (i) Bei za vitu zimepanda juu sana siku hizi
    (ii) Weka mizigo kwa gari

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)

  • Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Mababu walituachia msemo maarufu kuwa “ Kuzaa sio kazi. Kazi kubwa ni kulea.” Busara iliyomo katika methali hii inatupambazukia peupe pindi... (Solved)

    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Mababu walituachia msemo maarufu kuwa “ Kuzaa sio kazi. Kazi kubwa ni kulea.”
    Busara iliyomo katika methali hii inatupambazukia peupe pindi tukianza kuchunguza
    maisha ya vijana wa siku hizi katika jamii zote, hasa zile za Afrika. Kwa upande
    mmoja, maisha ya vijana hawa yanaonyesha cheche ya matumaini kwa maisha ya siku
    za usoni kwa sifa zao za mori na kupenda kujaribu na kushika mambo upesi kama
    sumaku. Lakini kwa upande wa pili, tunashuhudia upotevu wa kimawazo na hulka
    ambayo ndiyo kipingamizi cha kuendelea kwao kama raia wa kutegemewa.

    Kuwanyeshea vijana lawama na kashifa za kila aina hakufai wala hakufui dafu katika
    juhudi za kuwaongoza na kuwalea. Kwa hili hatuna budi kusadiki, “mtoto umleavyo
    ndivyo akuavyo.” Basi hivyo badala ya kuwashambulia vijana wenyewe. Tutafanya
    hivyo kwa imani kuwa “mwiba uchomeako ndiko utokeako.” Kiini cha matatizo ya
    vijana wa leo ni namna ya mwongozo na vielezo wanavyopokea kutoka kwa wazazi,
    waalimu, viongozi wa kijamii wakiwemo pia wale wa medhehebu tofauti na hasa kutokana na vyombo tofauti vya habari: vitabu majarida, filamu, magazeti na
    kadhalika.

    Jamii ina haki gani kuwashtumu vijana iwapo mzazi, tangu utotoni mwao
    amewahubiria maji na huku mwenyewe anakunywa mvinyo? Kama fasihi na
    maandishi mengine wanayoyabugia vijana yamejazwa amali, picha, jazanda na taswira
    zinazohimidi ugeni na kutweza Uafrika, tutashangazwa na nini pale vijana
    watakapoanza kupania zile zile amali za ugenini? Iwapo jamii na mazingira
    wanamokulia vijana yanatukuza kitu kuliko utu. Hatupaswi kupepesa macho na
    kukonyeza tunapowaona vijana wakihalifu sheria zote kwa tamaa ya kujinufaisha binafsi.

    Ni hoja isiyopingika kuwa kulea sio tu kulisha na kuvisha au kumpeleka mtoto
    shuleni sharti itambulike wazi wazi kuwa sehemu kubwa ya elimu na mwongozo
    unaoathiri mienendo ya jijana na watoto haitokani na yale waambiwayo bali hasa yote
    wanaoyashuhudia kwa macho na hisia zao.

    (a) Katika aya ya kwanza, maisha ya vijana wa kisasa yameelezwaje?
    (b) Kwa nini vijana hawapaswi kulaumiwa kulingana na mwandishi
    Maneno 30 – 35
    (c) Eleza sifa za malezi bora
    (Maneno 20 – 25)

    Date posted: June 27, 2019 .    Answers (1)