Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

CHEMA HAKIDUMU Chema hakidumu, kingapendekeza, Saa ikitimu, kitakuteleza, Ukawa na hamu, kukingojeleza, Huwa ni vigumu,

      

CHEMA HAKIDUMU
Chema hakidumu, kingapendekeza,
Saa ikitimu, kitakuteleza,
Ukawa na hamu, kukingojeleza,
Huwa ni vigumu, kamwe hutaweza.

Chema sikiimbi, kwamba nakitweza,
Japo mara tumbi, kinshaniliza,
Na japo siombi, kipate n’ongeza,
Mtu haniambi, pa kujilimbikiza.

Chema mara ngapi, kinaniondoka,
Mwahanga yu wapi? Hakukaa mwaka,
Kwa muda mfupi, aliwatilika,
Ningefanya lipi, ela kumzika?

Chema wangu babu, kibwana Bashee,
Alojipa tabu, kwamba anilee, Na yakwe sababu, ni nitengenee,
Ilahi wahhabu, mara amtwee.

Chema wangu poni, kipenzi nyanyangu,
Hadi siku hini, Yu moyoni mwangu,
Yu moyoni ndani, hadi kufa kwangu,
Ningamtamani, hatarudi kwangu.

(a) Eleza dhamira ya mwandishi
(b) Fafanua umbo la shairi hili
(c) Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya nathari
(d) Taja na kutoa mfano mmoja wa tamathali yoyote ya lugha inayojitokeza katika shairi
(e) Taja mbinu nne za uhuru wa mshairi huku ukitolea kila mbinu mfano

(f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kulingana na vile yalivyotumika:-
(i) Nitengenee
(ii) Ningamtamani
(iii) Ikitimu

  

Answers


Maurice
(a) Dhamira ya mwandishi ni kuwa chema hakidumu.

(b) Shairi lina beti 5
-Kilau beti una mishoro 4 yenye vipande 2.
-kila mshororo una mizani 6, yaani (6 kwa 6) jumla mizani 12 kila mshororo.
-Shairi limetungwa kutumia bahari ya KIKAI na pia bahari ya UKARAGUNI.

c)Kitu chema hakidumu hata kama kinapendeza ,saa yake ikifika kwa kuponyoka ukawachwa
na hamu ya kukirejea lakini wapi.Ni vigumu kwani hauwezekani.

d)Mfano mmoja wowote wa tamathali uliojitokeza katika shairi ni ule wa Balagha/
Istiari/Uhaishaji

e)-Vina vina badilika badilika.
-Idadi ya mizani katika kila mishororo ya ubeti wa shairi hili imepunguzwa kutoka 8 hadi 6.
-Mshororo wa kwanza katika kila ubeti wa shairi hili ni kama kibwagizo au mkarara.
-Neno chema limetumiwa kubainisha maana tofauti.
-Aina ya tarbia lakini limetengeka kikai.

f) (i)Nitengenee, Niweadilifu / niwe mwema / niwe sawa.
(ii)Ningamtamani – Ningemthamini
(iii)Ikitimu – ikifika
maurice.mutuku answered the question on October 9, 2019 at 10:23


Next: State one factor that necessitated the exchange of trade items between the early communities.
Previous: Identify two weapons that were used in the First World War (1914-1918)

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • (1).Twamshukuru Mwenyezi. Kamwe wingi ukarimu Alo na kiti cha enzi, Mola wetu akramu Kutupa kitu azizi , lugha kutakalamu Lugha ni kitu kitamu, ujuwapo kutumia (2) Lugha mkuu mlezi...(Solved)

    (1).Twamshukuru Mwenyezi. Kamwe wingi ukarimu
    Alo na kiti cha enzi, Mola wetu akramu
    Kutupa kitu azizi , lugha kutakalamu
    Lugha ni kitu kitamu, ujuwapo kutumia

    (2) Lugha mkuu mlezi , aleaye binadamu
    Hata wanyama ja mbuzi, wema lugha wafahamu
    Hafuguwa simulizi, izaayo tabasamu
    Lugha huwa ni imamu, ujuwapo kutumia

    (3) Lugha hodari mkwezi, akweaye tata ngumu
    Huzifyeka pingamizi, zizushazo uhasama
    Ikazidisha mapenzi, wapendanao kudumu
    Lugha huyeyusha sumu, ujuwapo kutumia

    (4) Lugha ndiye mpagazi, mazito kuyahudumu
    Pia hupanga vizazi, pasi mbari kudhulumu
    Aidha hufanya kazi, ikawa mustakumu
    Lugha kwayo ni timamu, ujuwapo kutumia

    (5) Lugha ni mpelelezi, maovu kuwakasimu
    Huwatowa palo wazi, kashuhudia kaumu
    Yasifiwa na wajuzi, kuwa ni kitu adhimu
    Lugha mkuu hakimu, ujuwapo kutumia

    (6) Lugha huizuwa kazi, kutatiza mahakimu
    Huwaacha kanwa wazi, wakili kitakalamu
    Muhalifu na jambazi, wakaishinda hukumu
    Urongo huwa timamu, ujuwapo kutumia

    (7) Lugha iwe ni kiongozi, Kizungu au Kiamu
    Iwekapo waziwazi, silabi na tarakimu
    Huyakimu maongezi,yakasikizwa kwa hamu
    Lugha huwa ni muhimu, ujuwapo kutumia.

    (8) Lugha ni mapinduzi, wanyonge na wajukumu
    Kadhalika ni jahazi, ya nahodha muhitimu
    Kufa maji haiwezi, si vina si miizamu
    Lugha maji zam-zamu, ujuwapo kutumia

    (a) Eleza maudhui ya shairi hili
    (b) Eleza muundo wa shairi hili
    (c) Andika ubeti wa nne katika lugha ya nadhari/ nadharia
    (d) Taja huku ukitoa mifano, mbinu tatu za lugha alizotumia mshairi kuwasilisha ujumbe
    (e) Eleza maana ya msamiati kama ulivyotumika
    (i) Azizi
    (ii) Uhasimu
    (iii) Adimu.

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Msituni nikakuta, nyuki wamo mzingani, Kwa juhudi wanakita, mara nje mara ndani, Husuda wameikata, hata hawasengenyani, Nyuki ni wadudu duni, wanashinda kwa umoja Mchwa nao nikaona, wamejenga masikani, Wafanya bidii...(Solved)

    Msituni nikakuta, nyuki wamo mzingani,
    Kwa juhudi wanakita, mara nje mara ndani,
    Husuda wameikata, hata hawasengenyani,
    Nyuki ni wadudu duni, wanashinda kwa umoja

    Mchwa nao nikaona, wamejenga masikani,
    Wafanya bidii sana, uvivu hawatamani,
    Wao husaidiana, tena hawadanganyani,
    Mchwa wadudu wa chini, wanaishi kwa umoja

    Nalo jeshi la siafu, hutandawaa njiani,
    Laenda bila ya hofu, maana ajiamini,
    Silaha zao dhaifu, meno, tena hawaoni
    Wa kuwatadia nini ? Kwani wanao umoja.

    Nao chungu wachukuzi, nyama warima njiani,
    Masikini wapagazi, mizigo yao kichwani,
    Ingawa si wachokozi, wakali ukiwahini,
    Katu hawafarakani, wanadamu kwa umoja.

    Sisi ni wana Adamu, mbona hatusikizani,
    Tusitietie hamu, ukubwa kuutamani,
    Wachache wataalamu, tuwasadi kwa imani,
    Hii “Huyu awezani,” yatuvunjia umoja


    (a) Lipe shairi hili anwani mwafaka.
    (b) Ni sifa zipi nne zinazopewa wanaozungumza.
    (c) Onyesha jinsi mwandishi alivyotumia uhuru wake katika shairi hili.
    (d) Eleza muundo wa shairi hili.
    (e) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha nathari.
    (f) Taja mafunzo mawili unayopata kutokana na wahusika wanaozungumziwa.
    (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi hilo.
    (i) Chungu
    (ii) Tuwasadi

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Alipokwenda kwao, mamaye alimwambia, Nipa fedha au nguo, nataka kwenda tumia! Nikosapo hivi leo, nipa kisu tajitia ! Huzunguka akilia kwa maana ya uketo Ndipo mamaye kawaza, pamwe na...(Solved)

    Alipokwenda kwao, mamaye alimwambia,
    Nipa fedha au nguo, nataka kwenda tumia!
    Nikosapo hivi leo, nipa kisu tajitia !
    Huzunguka akilia kwa maana ya uketo

    Ndipo mamaye kawaza, pamwe na kuzingatia,
    Fedha zako umesoza, na leo zimekwisha,
    Kisu sikukukataza, twaa upate jitia!
    Mbele zangu n’ondokea! Wende na ukiwa wako!


    Ulipogeuka nondo, nguo ukazingilia,
    Kakaka kwa vishindo, usisaze hata moya,
    Leo wanuka uvundo, wambeja wakukimbia!
    Mbele zangu n’ondokea ! Wende na ukiwa wako!
    Ukijigeuza nyama, kama Simba ukilia,
    Watumwa ukawaegema, ukawla wote pia,
    Pasi kuona huruma, kutoa wahurumia,
    Mbona hukuzingatia? Wende na ukiwa wako!


    Si mimi naliokupa, ukata huo, sikia!
    Kwamba utakuja hapa, nipate kuondolea,
    Naapa thama, naapa, sina la kukutendea!
    Mbele zangu n’ondokea! Wende na ukiwa wako!

    Tamati, nalikomile, ni hayo nalokwambia,
    Hapahitaji kelele na kujirisha mabaya,
    Na kwamba yakutukie, sema yapate n’elea!
    Zidi radhi kuniwea ! Wende na ukiwa wako!


    (a) Lipe shairi hili anwani mwafaka
    (b) Ni maudhui gani yanayojitokeza katika shairi hili
    (c) Taja na ueleze tabia za mnenewa katika shairi hili
    (d) Mshairi ametumia uhuru wa utunzi. Taja sehemu mbili alikotumia uhuru huo
    (e) Eleza umbo la shairi hili
    (f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi :-
    (i) Uketo
    (ii) Ukata

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • KIACHE KINACHONG’AA Katu siwe na harara, wala moyo kukupapa, Usichukue hasira, na moyo kutapa-tapa, Utaharibu na sura, mwishowe uende kapa, Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara Mbeleye kina madhara, kile kinachokukukwepa, Mbele...(Solved)

    KIACHE KINACHONG’AA
    Katu siwe na harara, wala moyo kukupapa,
    Usichukue hasira, na moyo kutapa-tapa,
    Utaharibu na sura, mwishowe uende kapa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Mbeleye kina madhara, kile kinachokukukwepa,
    Mbele yake ni hasara, si chema kitakutupa,
    Hutaipata ijara, kuchuma ama kukopa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Hicho jangwa la Sahara, si mnofu ni mfupa,
    Hakina njema ishara, humtupa mwenye pupa,
    Kibovu kama tambara, hupasuka kama chupa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Kitaleta ufukura, si huko wala si hapa,
    Kina mengi mazingira, na mbele kitakuchapa,
    Sijitie usogora, ukavimbisha mishipa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara


    Si kazi yenye ujira, mshahara kukulipa,
    Ya cheo chenye kinara, na heshima wakikupa,
    Mbele haina imara, japo leo wajitapa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Japo kazi ya biashara, kutwa wauza makopa,
    Uwe mtu na kipara, Mwananchi ama Yuripa,
    Bora uwe na busara, fedha tajaza mapipa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Usione kinang’ara, huku chapiga marapa,
    Ukimbilie kupora, moyo wako kukuzipa,
    Kitakugeuza chura, mbele yake utaapa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara


    Usitupe sarara, nyuma kisogo kuipa,
    Ukaenda kwa papara, kiumbe mbele kitanepa,
    Kwanza tumia fikira, uchague njema chapa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Na sisemi masihara, hakika kweli nawapa
    Mlio pwani na bara, wa Mufindi na wa lupa
    Maneno haya kitara, muarifu na Wachepa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara

    Tamati niliyochora, ya shikeni si kuepa
    Kisha muwe na basira, na Mola kumuogopa,
    Kinachokwepa si nyara, ufunge ndani ya kwapa,
    Kiache kinachokwepa, mbeleye kina madhara


    (a) Eleza hii ni bahari gani ya shairi
    (b) Eleza dhamira ya mshairi
    (c) Fafanua hasara nne zinazoletwa na tamaa - vile ving’aavyo
    (d) Taja na ueleze mbinu mbili za kifasihi zilizotumika katika shairi
    (e) Andika ubeti wa tano katika lugha ya nathari
    (f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika shairi
    (i) Kuchuma
    (ii) Kisogo kuipa

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • 1. Namwona yu shambani, Na jembe mkononi, Analima, Mwanamama,(Solved)

    MWANAMKE
    1. Namwona yu shambani,
    Na jembe mkononi,
    Analima,
    Mwanamama,
    Mavuno si yake,
    Ni ya mume wake.

    2. Namwona viwandani,
    Pia maofisini,
    Yu kazini,
    Hamkani,
    Anabaguliwa,
    Na anaonewa.

    3. Namwona yu nyumbnai,
    Mpishi wa jikoni,
    Yaya yeye,
    Dobi yeye,
    Hakuna malipo,
    Likizo haipo.

    4. Namwona kitandani,
    Yu uchi maungoni.
    Ni mrembo
    Kama chombo,
    Chenye ushawishi,
    Mzima utashi.

    5. Namwona mkekani,
    Yuwamo uzazini,
    Apumua,
    Augua,
    Kilio cha kite,
    Cha mpiga pute.

    6. Kwa nini mwanamke,
    Ni yeye peke yake,
    Heshimaye,
    Haki anakosa,
    Kwa kweli ni kosa
    (Muhammed Seif Khatib)


    (a) “Shairi hili ni la kukatisha tamaa”. Fafanua dai hili kwa kutoa mifano minne
    (b) Eleza umbo la shairi hili
    (c) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari
    (d) Taja tamathali ya usemi iliyotawala katika shairi zima utoe mifano miwili ya jinsi
    ilivyotumika
    (e) Onyesha mifano miwili ya ubabedume inayojitokeza katika shairi hili
    (f) Eleza maana ya maneno yafuatayo jinsi yalivyotumiwa katika shairi:
    (i) mzima utashi
    (ii) maungoni

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • KIPI NIKITENDE? Tayari ni sarakani, niambie yote johara,Mosi nimpe shukrani, kanizaa bira zira,Wapo haiko hisani, ningefaa kwa uparara,Kipi takachokitenda, ni nene heko kwa mama?Miezi tisa...(Solved)

    KIPI NIKITENDE?
    Tayari ni sarakani, niambie yote johara,
    Mosi nimpe shukrani, kanizaa bira zira,
    Wapo haiko hisani, ningefaa kwa uparara,
    Kipi takachokitenda, ni nene heko kwa mama?


    Miezi tisa tumboni, yote nina kajinyima,
    Kanikopa uchunguni, safari ndefu kazima’
    Kama kinda kiotani, kiniasa huyu mama’
    Kipi takachokitenda, ninene heko mama ?

    Baba siku jana madadi, kawa vingaito mambo,
    Kaolewa na asadi, kachalazwa kwa wimbombo,
    Kaona – bali jadili, kuchao puani bombo,
    Kipi takachokitenda, ninene heko mama?


    Kila kuchao zarani, kupalilia kondeni,
    Kachanika mpinini, chungu povuka motoni,
    Kaviyariya fingani, kinijali jikoni,
    Kipi tukachokitenda , ninene heko mama?


    Wa siku hizi vijana, wakahujuru nyumbani,
    Wengine wao jagina, kawa lofa mutaani,
    Hali ukashiba nina, afikapo tu, “kongoni!”
    Kipi takachokitenda, ninene heko mama?


    Nawe bwana siwe maya, vita hasha kiwa kombo,
    Tena simfanye yaya, ya kikoa ndio mambo,
    Simtende ya hizaya, siwe mwao kila jambo,
    Kipi takachokitenda, ninene heko mama?


    Sasa jamvi nakuja, kisa nimesakarika,
    Naomba niliyotaja, tatia manani kaka,
    Nenayo yasiwe ngoja, ili nipokee baraka,
    Mema nitamtendea, apate futahi pia.



    (a) Eleza umbo la shairi hili
    (b) Kwa nini msanii amshukuru mamaye ?
    (c) Ni kina nani wanaokashifiwa na msanii ? Kwa nini ?
    (d) Onyesha tofauti katika ujumbe iliyoko katika beti nne za kwanza na mbili zinazofuata
    (e) Toa majina mengine yenye maana sawa na haya yaliyotumiwa katika shairi hili :
    (i) Mama
    (ii) Dawati
    (iii) Imara/thabiti
    (f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika kaika shairi:
    (i) Kawa vangaito mambo
    (ii) Wimbombo
    (iii) Kongoni

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • 1. Nitampa nani, sauti yangu ya dhati Kwa kipimo gani, ingawa kiwakatiti Amefanya nini, la kutetea umati Kipimo ni kipi? 2. Yupi wa maani, asosita katikati Alo na maoni, yasojua...(Solved)

    1. Nitampa nani, sauti yangu ya dhati
    Kwa kipimo gani, ingawa kiwakatiti
    Amefanya nini, la kutetea umati
    Kipimo ni kipi?

    2. Yupi wa maani, asosita katikati
    Alo na maoni, yasojua gatigati
    Atazame chini, kwa kile ule wakati
    Kipimo ni kipi?

    3. Alo mzalendo, atambuaye shuruti
    Asiye mafundo, asojua mangiriti
    Anoshika pendo, hata katika mauti
    Kipimo ni kipi?

    4. Kipimo ni kipi, changu mimi kudhibiti
    Utu uko wapi, ni wapi unapoketi
    Nje kwa mkwapi, au ndani kwa buheti
    Kipimo ni kipi?

    a) Eleza umbo la shairi hili
    b) Taja na ueleze jinsi mwandishi alivyotumia uhuru wa ushairi
    c) Eleza ujumbe unaowasilishwa na mshairi
    d) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari
    e) Taja bahari tatu zinazojitokeza katika shairi na utoe sababu
    f) Eleza msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi hili
    i) Katiti
    ii) Gatigati
    iii) Mangiriti

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • 1. Mke wangu wameshanipoka Ndugu zangu, wamedai ububu Wazazi kuzoea kunigombeza(Solved)

    HATIMA YANGU
    1. Mke wangu wameshanipoka
    Ndugu zangu, wamedai ububu
    Wazazi kuzoea kunigombeza

    2. Juzi mali lilimbikiza
    Furaha lilitanda
    Makanwa yalijaziwa
    Hoi hoi ikawa desturi

    3. Kilabu tulikwenda
    Nyama tulichoma
    Mahali tulizuru
    Tuliteremsha!

    4. Leo mambo yamenigeuka
    Wao masahibu siwaoni
    Matumbo yakaninguruma
    Kama radi ya mvua

    5. Nyumbani nimebaki pweke
    Mke amenitoroka
    Watoto wameparara
    Skuli kugharamia
    Imegeuka balaa belua

    6. Ndipo nimeamua
    Afadhali kitanzi badala ya balaa
    Kumbe kupanga ndiyo maana
    Maisha na waasia


    (a) Eleza mambo muhimu yanayoelezwa katika shairi hili
    (b) Fafanua sifa mbili za anayezungumza katika shairi
    (c) Dondoa na ufafanue mbinu zozote mbili za lugha katika shairi hili
    (d) Eleza maana ya:-
    (i) Ndugu zangu wamedai ububu
    (ii) Kumbe kupanga ndiyo maana

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • WAFULA KABILIANA NA KISU Ee mpwa wangu, Kwetu hakuna muoga, Uoga ukikufikia, huenda ni wa akina mamayo, Fahali tulichinja ili uwe mwanamme, Eewe mpwa wangu, kisu kikali ajabu ! Iwapo utatingiza...(Solved)

    WAFULA KABILIANA NA KISU
    Ee mpwa wangu,
    Kwetu hakuna muoga,
    Uoga ukikufikia, huenda ni wa akina mamayo,
    Fahali tulichinja ili uwe mwanamme,
    Eewe mpwa wangu, kisu kikali ajabu !
    Iwapo utatingiza kichwa,
    Uhamie kwa wasiotahiri.

    Wanaume wa mbari yetu,
    Si waoga wa kisu,
    Wao hukatwa kuanzia macheo hadi machweo,
    Wewe ndiye wa kwanza,
    Iwapo utashindwa,
    Wasichana wote,
    Watakucheka,
    Ubaki msununu,
    Simama jiwe liwe juu,
    Ndege zote ziangamie.

    Simu nimeipokea,
    Ngariba alilala jikoni,

    Visu ametia makali,
    Wewe ndiye wangojewa,
    Hadharani utasimama,
    Macho yote yawe kwako,
    Iwapo haustahimili kisu,
    Jiuzulu sasa mpwa wangu,
    Hakika sasa mpwa wangu,
    Hakika tutakusamehe, mwaka kesho unakuja.


    Asubuhi ndio hii,
    Mama mtoto aamushwe,
    Upweke ni uvundo,
    Iwapo utatikisa kichwa,
    Iwapo wewe ni mme,
    Kabiliana na kisu kikali,
    Hakika ni kikali!

    Kweli ni kikali!
    Wengi wasema ni kikali!
    Fika huko uone ukali!
    Mbuzi utapata,
    Na hata shamba la mahindi,
    Simama imara,
    Usiende kwa wasiotahiri


    (a) Hili ni shairi la aina gani ? Thibitisha
    (b) Ni nani anayeimba shairi hili na analiimba kwa nani ?
    (c) Toa ithibati kwenye shairi hili kuthibitisha kuwa msimulizi ana taasubi za kiume
    (d) Taja kwa kutolea mifano mbinu zozote nne za uandishi katika shairi hili
    (e) Taja shughuli zozote mbili za kiuchumi za jamii inayorejelewa katika shairi hili
    (f) Eleza kwa mifano, uhuru wa kishairi katika shairi hili
    (g) Msamiati ufuatao umetumika kwa maana gani katika shairi hili ?
    (i) Mbari
    (ii) Msununu
    (iii) Ngariba
    (iv) Uvundo

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Sinisumbuwe akili, nakusihi e mwandani.Afya yangu dhahili, mno nataka amaniNawe umenikabili, nenende sipitaliniSisi tokea azali, twende zetu mizumuniNifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?Mababu hawakujali, wajihisipo...(Solved)

    Sinisumbuwe akili, nakusihi e mwandani.
    Afya yangu dhahili, mno nataka amani
    Nawe umenikabili, nenende sipitalini
    Sisi tokea azali, twende zetu mizumuni
    Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?

    Mababu hawakujali, wajihisipo tabani
    Tuna dawa za asili, hupati sipitalini
    Kwa nguvu za kirijali, Mkuyati uamini
    Kaafuri pia kali, dawa ya ndwele fulani
    Nifuateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?

    Mtu akiwa hali, tumbo lina walakini,
    Dawa yake ni subili, au zongo huanoni
    Zabadili pia sahali, kwa maradhi yalo ndani
    Au kwenda wasaili, wenyewe walo pangani
    Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?

    Mtu kwenda sipitali, ni kutojuwa yakini
    Daktari k’ona mwili, tanena kensa tumboni
    Visu visitiwe makali, tayari kwa pirisheni
    Ukatwe kama fagili, tumbo nyangwe na maini
    Nifuateni sipitalini, na dawa ziko nyumbani?

    Japo maradhi dhalili, kutenguliwa tegoni
    Yakifika sipitali, huwa hayana kifani
    Wambiwa damu kaliti, ndugu msaidieni
    Watu wakitaamali, kumbe ndiyo bunani
    Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?

    Mizimu wakupa kweli, Wakueleze undani.
    Maradhiyo ni ajali, yataka vitu thamani
    Utete huku wawili, wa manjano na kijani
    Matunda pia asali, vitu vyae shamoni
    Nifuateni sipati, na dawa zi langoni?


    (a) Lipe shairi hili kichwa mwafaka
    (b) Mtunzi alikuwa na lengo gani alipotunga shairi hili
    (c) Mbona mshairi hataki kwenda hospitalini
    (d) Eleza umbo la shairi hili
    (e) Kwa nini mshairi alitumia ritifaa katika ushairi ?
    (f) Andika maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa kwenye shairi :-
    (i) Dhalili –
    (ii) Azali-
    (iii)Sahali-

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Umekata mti mtima Umeangukia nyumba yako Umeziba mto hasira ...................(Solved)

    SHAIRI ‘A’.
    Umekata mti mtima
    Umeangukia nyumba yako
    Umeziba mto hasira
    Nyumba yako sasa mafurikoni
    Na utahama
    Watoto Wakukimbia
    Mbuzi kumkaribia chui
    Alijigeuza Panya
    Akalia kulikuwa na pala
    Kichwani
    Mchawi kutaka sana kutisha
    Alijigeuza Simba
    Akalia na risasi kichwani
    Jongoo kutaka sana kukimbia
    Aliomba miguu elfu
    Akaachwa na nyoka
    Hadija wapi sasa yatakwenda
    Bwanako kumpa sumu ?
    Hadija umeshika nyoka kwa mkia
    Hadija umepitia nyuma ya punda


    SHAIRI ‘B’
    Piteni jamani, Piteni haraka
    Nendeni, nendeni huko mwendako
    Mimi haraka, haraka sina
    Mzigo wangu, mzigo mzito mno
    Na chini sitaki kuweka
    Vijana kwa nini hampiti ?
    Kwa nini mwanicheka kisogo ?
    Mzigo niliobeba haupo.
    Lakini umenipinda ngongo na
    Nendako
    Haya piteni ! Piteni haraka ! Heei !
    Mwafikiri mwaniacha nyuma !
    Njia ya maisha ni moja tu.
    Huko mwendako ndiko nilikotoka
    Na nilipofikia wengi wenu
    Hawatafika.
    Kula nimekula na sasa mwasema
    Niko nyuma ya wakati
    Lakini kama mungepita mbele
    Na uso wangu kutazama
    Ningewambia siri miaka
    Mingi.

    (a) Haya ni mashairi ya aina gani ? Toa saabu
    (b) Washairi hawa wawili wanalalamika. Yafafanue malalamishi yao
    (c) Onyesha jinsi kinaya kinavyojitokeza katika tungo hizi mbili
    (d) Ni vipi Hadija :-
    (i) Amekata mti mtima ?
    (ii) Amepita nyuma ya Punda
    (e) Toa mifano 2 ya uhuru wa mashairi kwa kurejelea mashairi haya
    (f) Kwa kurejelea shairi ‘B’ eleza maana ya:-
    (i) Mzigo
    (ii) Siri
    (iii) Kula nimekula
    (iv) Niko nyuma ya wakati

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Mzee Oluoch :....................................................................ni kweli hayo! Mzee Mwenda : Ndio. Huyu mtoto wangu nimemsomesha mpaka akahitimu chuo kikuu na anafanya kazi ya uhasibu. Mzee Oluoch : Na wangu...(Solved)

    Mzee Oluoch :....................................................................ni kweli hayo!

    Mzee Mwenda : Ndio. Huyu mtoto wangu nimemsomesha mpaka akahitimu chuo kikuu na anafanya kazi ya uhasibu.

    Mzee Oluoch : Na wangu amehitimu na sasa ana shahada ya uzamili. Yeye ni mhandisi
    mkuu. Chukua tu mbuzi hamsini na utukubalie kujenga uhusiano wa ukwe.

    Mzee Mwenda : Je, mbuzi hao ni wa ‘mfuko’ au ni .......?

    (a) Mazungumzo ya aina hii hutokea katika muktadha wa aina gani?
    (b) Eleza sifa nane za lugha inayotumika katika wa aina hii

    Mzee Oluoch : Kuna wa mfuko ......thelathini na hao wengine ishirini.

    Mzee Mwenda : Basi lete hao ulio nao. Wengine hamsini watabaki deni. Utakuwa
    ukinilipa polepole. Idhini yangu nimetoa ili mipango iendelee.

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • AZIZ : Ingia 46! Adams mbao Kenyatta, railways beba! 46 Adams mbao kenyatta, railways! SHIKU : Namba nane ngapi? AZIZ : Mbao ingia, blue. SHIKU : Nina hashuu. AZIZ...(Solved)

    AZIZ : Ingia 46! Adams mbao Kenyatta, railways beba! 46 Adams mbao kenyatta, railways!

    SHIKU : Namba nane ngapi?

    AZIZ : Mbao ingia, blue.

    SHIKU : Nina hashuu.

    AZIZ : Blue Auntie.

    SHIKU : Sina.

    AZIZ : Ingia. 46 Adams mbao, kenyatta railways gari bebabeba.

    AHENDERA : Mimi sinako shirini. Chukuako tu kumi.

    AZIZ : Dinga inakunywanga petrol mzee.

    AHENDERA: Kumi mingi.

    AZIZ : Haaya ingia twende. Driver imeshon twende.


    (i) Eleza muktadha wa mazungumzo haya
    (ii) Taja sifa sita za lugha iliyotumika katika mazungumzo haya

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Eleza juhudi tano zinazotumika kukiendeleza Kiswahili(Solved)

    Eleza juhudi tano zinazotumika kukiendeleza Kiswahili

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • Bw. Mosuka : Mheshimiwa spika, naichukua fursa hii kuipinga hoja iliyowasilishwa na mbunge wa Mahira, mheshimiwa Kochaberi kuhusu suala la kuavya.... (a) Hii ni sajili gani? (b) Eleza...(Solved)

    Bw. Mosuka : Mheshimiwa spika, naichukua fursa hii kuipinga hoja iliyowasilishwa na
    mbunge wa Mahira, mheshimiwa Kochaberi kuhusu suala la kuavya....
    (a) Hii ni sajili gani?
    (b) Eleza sifa za mazungumzo ya sajili hii

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • A : Ohh, dada NaomiB : Dada Ruth (anamsogea kwa bashasha wanakumbatiana). Ahh Mungu asifiwe!A: Asifiwe sanaB: Ehh dadangu, miezi ...mingi...sijakuonaA: dada wee...Nilitumwa huko kusini...(Solved)

    Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali :

    A : Ohh, dada Naomi
    B : Dada Ruth (anamsogea kwa bashasha wanakumbatiana). Ahh Mungu asifiwe!
    A: Asifiwe sana
    B: Ehh dadangu, miezi ...mingi...sijakuona
    A: dada wee...Nilitumwa huko kusini ...Kuwahubiria watu injili (mtuo mdogo)singeweza kukata...
    B: Ehh, usiwe kama Yona
    A: Habari ya siku nyingi?
    B; Nzuri Mungu bado ameendelea kunibariki
    A: Amen!
    B: Nimeendelea kuiona neema yake
    A: Amen! Asifiwe Bwana
    B: Halleluya
    A: Ni Mungu wa miujiza!
    B : Amen. Hata nami nimeona neema yake
    Bado niko imara katika wokovu katika siku hizi za mwisho
    A : Amen !
    B : Ni Mungu wa ajabu kweli !
    A : Nilikumbana na matatizo lakini nikategemea sala
    Kama Paulo na sila… Na nikashinda (anatua). Sikuweza kumpa shetani nafasi…maana
    ameshindwa
    B : Ameshindwa kabisa


    (i) Hii ni sajili ya wapi ? Fafanua
    (ii) Taja na ueleze sifa za sajili hii
    (iii) Taja na ueleze mambo mawili muhimu yaliyosaidia katika maenezi ya Kiswahili
    Afrika mashariki na kati

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • Niaje wasee! Ma-holiday ndizo hizo tena. Najua ma-mission ni mingi! Lakini jo, mambo imebadilika ! Ni kubaya maze. Usifikirie kila kitu unaona ni reality, ukadhani ni...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata:-

    Niaje wasee! Ma-holiday ndizo hizo tena. Najua ma-mission ni mingi! Lakini jo,
    mambo imebadilika ! Ni kubaya maze. Usifikirie kila kitu unaona ni reality, ukadhani ni gold !
    Hiyo siyo real life maze ! Round hii maze ni ‘‘Ku-chill!’’ Usipige ma-stunts zingine zitakuacha uki-regret later! NI POA KU- CHILL au aje maze?


    a) Bainisha rejista ya mazungumzo haya
    b) Kwa kurejelea kifungu andika sifa za rejista hii.
    c) Kwa nini watu hutumia lugha zaidi ya moja.
    d) Orodhesha hatua tatu zinazoweza kuchukuliwa kusuluhisha matatizo yanayokumba Kiswahili nchini.

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • Fafanua changamoto tano zinazozuia maenezi ya haraka ya lugha ya Kiswahili(Solved)

    Fafanua changamoto tano zinazozuia maenezi ya haraka ya lugha ya Kiswahili

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • Fafanua mikakati mitano inayoweza kuchapuza kukua na kuenea kwa kiswahili nchini Kenya(Solved)

    Fafanua mikakati mitano inayoweza kuchapuza kukua na kuenea kwa kiswahili nchini Kenya

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)

  • Uchunguzi uliofanywa umeonyesha kuwa anasumbuliwa na uto mwingi mwilini. Uto unaweza kudondoshwa kwa kufanya mazoezi, kupunguza ulaji wa vyakula vya wanga na hata protini. Protini...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata

    Uchunguzi uliofanywa umeonyesha kuwa anasumbuliwa na uto mwingi mwilini. Uto unaweza kudondoshwa kwa kufanya mazoezi, kupunguza ulaji wa vyakula vya wanga na hata protini. Protini iwapo nyingi mwilini hugeuzwa kuwa glukosi ambayo huhifadhiwa mwilini. Hii huwa msingi wa unene pia ambao unahatarisha afya. Jamaa yake aliyeaga dunia alikuwa mgonjwa wa bolisukari ambayo inaweza kurithishwa. Kimsingi, lazima awe na welewa bora kabisa wa lishe. Mwenzake naye aliathiriwa na aflatoxins zilikuwa kwenye chakula alichokula.
    (a) Sajili hii inapatikana wapi? Kwa nini?
    (b) Taja sifa zinazohusishwa na sajili yenyewe

    Date posted: October 8, 2019.  Answers (1)