Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Tunga sentensi mbili kuonyesha tofauti kati ya maneno haya. (i) shuka (ii) suka

      

Tunga sentensi mbili kuonyesha tofauti kati ya maneno haya.
(i) shuka
(ii) suka

  

Answers


Kavungya
(i) shuka – enda chini kutoka juu ya kitu
-pungua thamani
-shiti

(ii) suka – kutengeneza nywele
-Tikisa kitu
Kavungya answered the question on November 24, 2022 at 06:43


Next: Eleza maana ya misemo ifuatayo. (i) kupiga domo (ii) kupiga kijembe
Previous: Onyesha vivumishi vya sifa katika sentensi zifuatazo. (i) Anayetaka chakula kitamu ni nani? (ii) Kiatu kirefu kimeng’oka kikanyagio.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Eleza maana ya misemo ifuatayo. (i) kupiga domo (ii) kupiga kijembe(Solved)

    Eleza maana ya misemo ifuatayo.
    (i) kupiga domo
    (ii) kupiga kijembe

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Bainisha vitenzi halisi katika sentensi zifuatazo. (i) Nyanchama hakufika mkutanoni (ii) Horukut amerudi kutoka masoni(Solved)

    Bainisha vitenzi halisi katika sentensi zifuatazo.
    (i) Nyanchama hakufika mkutanoni
    (ii) Horukut amerudi kutoka masoni

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha nomino za jamii katika sentensi zifuatazo (i) Chuki baina ya jamii lazima ikomeshwe barani Afrika. (ii) Wageni watatumbuizwa na bengi ya kayamba Afrika.(Solved)

    Onyesha nomino za jamii katika sentensi zifuatazo
    (i) Chuki baina ya jamii lazima ikomeshwe barani Afrika.
    (ii) Wageni watatumbuizwa na bengi ya kayamba Afrika.

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Onyesha kundi nomino na kundi tenzi katika sentensi hii. Nyayo za wanyama hao zimeonekana hapa. (Solved)

    Onyesha kundi nomino na kundi tenzi katika sentensi hii.
    Nyayo za wanyama hao zimeonekana hapa.

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Eleza tofauti kati ya: (i) Mofimu huru (ii) Mofimu tegemezi (Solved)

    Eleza tofauti kati ya:
    (i) Mofimu huru
    (ii) Mofimu tegemezi

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Eleza tofauti kati ya sauti /z/ na /f/ (Solved)

    Eleza tofauti kati ya sauti /z/ na /f/

    Date posted: November 24, 2022.  Answers (1)

  • Soma taarifa hii kisha ujibu maswali Kuna wataalamu siku hizi wanaosema kuwa jela si pahala pa adhabu bali pa matibabu. Yaani madhumuni ya kumtia mhalifu jela isiwe...(Solved)

    Soma taarifa hii kisha ujibu maswali
    Kuna wataalamu siku hizi wanaosema kuwa jela si pahala pa adhabu bali pa matibabu. Yaani
    madhumuni ya kumtia mhalifu jela isiwe kumwadhibu kwa makosa aliyofanya bali iwe kumtibu na kujaribu
    kumrekebisha tabia yake ili awe raia mwema.
    Zamani wahalifu waliadhibiwa kwa mujibu wa makosa waliyoyafanya. Mhalifu aliyefanya makosa
    madogo madogo alifungwa lakini mtu aliyeua naye aliuawa. Sasa wataalamu wanatuambia kuwa mhalifu
    akiadhibiwa anapokuwa kifunguno,basi akitoka hurejea tena kufanya uhalifu. Madhumuni ya kumtia jela iwe si
    kumwadhibu bali kumfunza tabia njema. Wanatuambia kuwa makosa afanyayo mhalifu yanatokana na
    matatizo ya jamii kwa jumla,nayo ni matatizo kama ya umaskini, msongamano wa watu, kosa afanyalo mhalifu
    si kosa lake pekee bali ni kosa la jamii nzima.
    Jitu lilizoea kuua halioni kitu kumpiga mtarimbo au rungu la kichwa na kumyang’anya kila alicho
    nacho. Siku hizi,jitu kama hili baadhi ya wataalamu husema lisiuawe lifungwe maisha tu. Lakini ‘kifungo cha
    maisha’ ni kama tunavyokijua. Muuaji hufungwa pengine miaka kumi tu kisha husamehewa muda uliobaki.
    Hapo tena huwa huru ama kuifichua mali aliyoiiba na kuistarehea raha mustarehe au kurejea tena kufanya
    uhalifu.
    Haya ni kinyume kabisa na mambo yalivyokuwa zamani. Aliyeua aliuawa kwa hivyo watu waliogopa
    kuua. Raia na pia askari waliokuwa wakiwasaka wahalifu walinusurika vifo kwani wahalifu wengine
    walichukua silaha za hatari kama bastola na bunduki.
    Sasa wale wahalifu wabaya sana – mijizi, minyang’anyi na wauaji ndio wanaotukuzwa. Magazeti
    huwashawishi makatili hawa na kuwapa mapesa chungu nzima waeleze maisha yao ya kikatili. Magazeti haya
    sasa ndiyo yanayopata wasomaji wengi. Pia wachapishaji vitabu vya hadithi zinazohusikia na uhalifu, biashara
    zao zinazidi kustawi. Kadhalika sinema zinazoonyesha picha za ukatili; wizi na mauji hujaa watazamaji
    wanaoshangilia uhalifu ufanywao.
    Wahalifu kwa upande mmoja wanatukuzwa na masinema vitabu na magazeti na kwa upande mwingine
    “haki” zao zinapiganiwa na baadhi ya wataalamu. Watu wanaowalaani wahalifu ni wale waliohasirika tu na
    kuteswa na wahalifu . Baadhi yao hata kulaani hawawezi kwa sababu wameshauawa,hawana tena kauli.

    MASWALI
    (a) Fupisha aya ya kwanza hadi ya tatu kwa maneno 50.
    Matayarisho
    Nakala safi

    (b) Fupisha aya mbili za mwisho kwa maneno kati ya 45-50
    Matayarisho
    Nakala safi

    Date posted: November 23, 2022.  Answers (1)

  • Soma taarifa hii kisha ujibu maswali ifuatayo. UKANDAJI Je,unajua kuwa ukandaji wa mwili umetumika kama njia mojawapo ya matibabu toka jadi?(Solved)

    Soma taarifa hii kisha ujibu maswali ifuatayo.
    UKANDAJI
    Je,unajua kuwa ukandaji wa mwili umetumika kama njia mojawapo ya matibabu toka jadi? Watu
    wanaofahamika kutumia ukandaji kimatibabu toka jadi ni Wahindi,Wachina,Wagiriki,Warumi na Waafrika.
    Ukandaji unajulikana kuwa na manufaa makubwa kimatibabu. Mathalani,ukandaji hufungua vitundu
    vya ngozi. Ufunguzi huu huondoa sumu mwilini kupitia kwa utoaji jasho. Pili,ukandaji hupunguza mkazo wa
    misuli. Misuli ikiwa na mkazo zaidi kwa muda mrefu huleta urundikaji wa asidi. Ukandaji huondoa asidi
    hii,huufanya mwili kuwa mlegevu,humletea mtu uchangamfu na kuondoa uchovu.
    Halikadhalika,ukandaji huimarisha mzunguko wa damu mwilini kwa wepesi. Hali hii huhakikisha kuwa
    virutubishi vya mwili huweza kufikia viungo vyote vya mwili. Hili nalo huchangia kuzidisha uwezo wa mwili
    kujikinga na maradhi. Hewa safi ya oksijeni huweza pia kusambaa kote mwilini kupitia kwa uimarishaji wa
    mzunguko wa damu. Aidha,ukandaji wa taratibu na polepole hupunguza mkazo wa neva na kuziliwaza
    ukandaji wa kasi huchangamsha neva na kuimarisha utendaji kazi wake.
    Ukandaji unaweza kufanyiwa kiungo chochote mwili ni. Ukandaji huu huweza kuwa na matokeo
    mbalimbali mwilini.
    Mathalani,ukandaji wa njia ya chakula mwilini,hasa tumbo na utumbo,huimarisha usagaji wa chakula na
    kuchangia uondoaji wa uchafu na sumu mwilini. Nao ukandaji wa njia ya mkonjo hustawisha uondoaji wa
    chembechembe za sumu mwilini.
    Kwa kawaida,viganja vya mikono hutumika katika ukandaji. Viungo hivi vinapaswa kuwa na wororo.
    Wororo huu hupatikana kwa kutumia mafuta. Mafuta ambayo ni bora zaidi kwa shughuli za ukandaji ni ya
    ufuta au simsim. Matumizi ya kitu chochote kama ungaunga kinachoweza kuziba vitundu vya ngozi
    hayapendekezwi.
    Ukandaji wapaswa kutekelezwa kwa njia ifuatayo. Mtu aanzie mikono na miguu. Kisha aingie kukanda
    kifua,tumbo,mgongo na makalio. Hatimaye,akande uso na kichwa. Mtu anaweza kutumia kitambaa kukandia
    mgongo. Ni bora kutumia viganja vya mikono kukandia. Kwa njia hii,manufaa huwa maradufu.
    Kwanza,tutanufaika na ukandaji na wakati huo huo tutakuwa tukifanya mazoezi ya viungo. Wasioweza
    kujikanda,wanaweza kuomba msaada. Ni muhimu ukandaji ufuatiwe na kuoga kwa maji vuguvugu.
    Kwa walio na tatizo la shinikizo au mpumuko wa damu wanaweza kubadilisha utaratibu wa ukandaji.
    Waanzie kichwani,kisha waelekee usoni,kifuani,tumboni,mgongoni,makalioni,miguuni na kuhitimisha
    mikononi.
    Hata hivyo,ukandaji haupaswi kufanywa wakati mtu anaugua maradhi yoyote. Wanawake wajawazito
    nao wanatakiwa kuepuka ukandaji wa tumbo. Halikadhalika,ukandaji wa tumbo hauruhusiwi wakati mtu
    anaendesha,ana vidonda vya tumbo au uvimbe tumboni. Hatimaye,ukandaji haupendekezwi iwapo mtu ana
    maradhi ya ngozi.

    MASWALI
    (a) Ukandaji ni nini?
    (b) Eleza manufaa matatu ya ukandaji.
    (c) Ukandaji unatakiwa kutekelezwa kwa njia gani?
    (d) Ukandaji unatakiwa kutekelezwa na nani na kwa nini?
    (e) Onyesha ni lini ukandaji haupendekezwi.
    (f) Eleza maneno yafuatayo kama yalivyotumika:
    (i) ufunguzi
    (ii) auni
    (iii) maradufu
    (iv) maji vuguvugu
    (v) shinikizo la damu

    Date posted: November 23, 2022.  Answers (1)

  • Nani kuku....? Sosi poa leo .... Mate ndo! ndo! ndo!. Ukimanga hii hutaona daktari kwa miaka kumi..... Ng’ombe je? nani? ......nani!... Ni wewe.... poa basi naja...... a....(Solved)

    Nani kuku....? Sosi poa leo .... Mate ndo! ndo! ndo!. Ukimanga hii hutaona daktari kwa miaka
    kumi..... Ng’ombe je? nani? ......nani!... Ni wewe.... poa basi naja......
    a. Je, sajili hii inapatikana wapi?

    b. Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza sifa nne za sajili hii.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tumia kirejeshi amba- katika sentensi ifuatayo: Jembe lililonunuliwa limepotea.(Solved)

    Tumia kirejeshi amba- katika sentensi ifuatayo:
    Jembe lililonunuliwa limepotea.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika katika udogo: Mbwa amekanyagwa na gari.(Solved)

    Andika katika udogo: Mbwa amekanyagwa na gari.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Sahihisha sentensi ifuatayo. Ukienda mle pao atakuweko. (Solved)

    Sahihisha sentensi ifuatayo.
    Ukienda mle pao atakuweko.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya maneno haya: Paka na baka(Solved)

    Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya maneno haya:
    Paka na baka

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Akifisha sentensi ifuatayo: mwalimu kazungu alimuuliza mwanafunzi je unataka kunidanganya kuwa ulifika shuleni mapema(Solved)

    Akifisha sentensi ifuatayo:
    mwalimu kazungu alimuuliza mwanafunzi je unataka kunidanganya kuwa ulifika shuleni mapema

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Andika kinyume cha sentensi hii: Alipoinama nilifurahi.(Solved)

    Andika kinyume cha sentensi hii: Alipoinama nilifurahi.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tambua aina za maneno katika sentensi zifuatazo: Msichana mrembo amechora haraka sana. Yeye ataenda sokoni.(Solved)

    Tambua aina za maneno katika sentensi zifuatazo:
    Msichana mrembo amechora haraka sana.
    Yeye ataenda sokoni.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Tia shadda ili kutoa maana mbili tofauti ya neno ‘katakata’.(Solved)

    Tia shadda ili kutoa maana mbili tofauti ya neno ‘katakata’.

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza maana ya aina zifuatazo za silabi: Silabi funge Silabi wazi Silabi mwambatano(Solved)

    Huku ukitoa mifano mwafaka, eleza maana ya aina zifuatazo za silabi:
    Silabi funge
    Silabi wazi
    Silabi mwambatano

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Eleza sifa za sauti zifuatazo: /e/ /p/(Solved)

    Eleza sifa za sauti zifuatazo:
    /e/
    /p/

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)

  • Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali FADHILA ZA PUNDA Rita na Evelyn walikuwa marafiki wa chanda na pete kwa muda mrefu.(Solved)

    Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali
    FADHILA ZA PUNDA
    Rita na Evelyn walikuwa marafiki wa chanda na pete kwa muda mrefu. Waliishi katika mtaa wa Kibokoni
    jijini Mombasa. Evelyn alikuwa mwanafunzi wa masomo ya uhazili katika chuo kimoja pale mjini. Naye
    Rita alifanya kazi ya ukarani papo hapo mjini. Waliishi kidugu katika chumba kimoja walichopanga pale
    mtaani. Ingawa marafiki hawa walishirikiana kwa kila njia katika shughuli za upishi, kupiga deki, kufagia,
    kufua na kazi nyinginezo za nyumbani, aliyekuwa akitoa msaada mkubwa zaidi alikuwa ni Rita. Rita
    alikuwa na mazoea ya kutunza pesa zake vyema. Aidha alijua maana ya haba na haba hujaza kibaba.
    Alijua kuwa Evelyn, kama mwanafunzi, hakuwa na uwezo wa kuyakidhi baadhi ya mahitaji yake.
    Alijitolea sabili hata kumnunulia Evelyn nguo, viatu na vim vingine alivyohitaji. Mara nyingine ilibidi Rita
    kulipa kodi ya nyumba peke yake kwa vile mwenzake hangeweza kupata pesa kwa wakati. Hakuwahi
    hata siku moja kumkera wala kumtesa Evelyn kwa jinsi yoyote ile. Fauka ya hayo, hakuwahi
    kumsemesha vibaya wala kuonyesha dharau kwake. Aliamini kama wanavyosema watu kuwa dunia
    rangi rangile, huenda siku moja atahitaji kusaidiwa yeye pia. Siku kama hiyo atamtegemea Evelyn,
    mwandani wake. Evelyn alipomaliza masomo yake alikuwa na bahati ya mtende. Alipata kazi nzuri mara
    moja katika kampuni moja ya maffita papo hapo jijini. Lakini muda si muda, mambo ya ajabu yalianza
    kutokea. Baada ya kupata kazi yenye kipato kizuri, kichwa cha Evelyn kilianza kufura mfano wa kaimati.
    Badala ya kunisaidia mwenzake katika kazi za pale nyumbani pamoja na gharama za maisha, alifhatilia
    raha za jijini kwa kuamini ule msemo wa ponda raha kufa kwaja. Rita alipomwuliza alimjibu kwa ukali,
    “Nikusaidie nini? Sasa si kama wakati nilipokuwa mwanafunzi. Kila mtu ana pesa zake.Ala!” Rita
    hakumwelewa tena Evelyn.Isistoshe, alianza kumwibia Rita vitu vyake wakati alipokuwa hayupo
    nyubani. Mara kwa mara Rita aligundua kuwa pesa alizokuwa ameficha sehemu Fulani nyumbani
    zimedokolewa. Alipomwuliza, Evelyn alikujajuu, “Unafikiri mimi sina pesa? Unadhani ni wewe tu
    uliyeajiriwa?” Rita alizidi kushangaa, Muda wote alioishi na kumfadhili rafiki yake aliamini kuwa atamlipa
    mema. “Kumbe fadhila za punda ni mateke?” Alijiuliza Rita. Baada ya muda, urafiki wao ulivunjika na
    Evelyn akahamia mtaa wa Furaha alikoendelea na maisha yake ya starehe na ureda. Hata hivyo mambo
    yalianza kumwendea mrama Evelyn. Wakubwa wake kazini hawakupendezwa najinsi alivyoendesha
    shughuli zake pale ofisini. Mara nyingi alifika kazini akiwa amechelewa na kila wakati alitoa vijisababu
    mbalimbali ambavyo havikumridhisha yeyote. Aidha, alipokuwa ofisini hakufanya mengi isipokuwa
    kutembea kutoka ofisi hii hadi nyingine akiwasumbua watu kazini mwao. Mara kwa mara alionekana
    akisinzia wakati wenzake walipokuwa wakichapa kazi. Lakini lililowakera zaidi wakuu wa kampuni hiyo
    ya mafuta ni jambo fulani lililoanza kutendeka pale. Vitu vya watu vilianza kupoteapotea.Mara
    mfanyikazi huyu anapoteza saa yake, mara mwingine anapoteza pesa, mara hiki mara kile. Wakuu
    walipoyatupa mawazo yao nyuma wakagundua kuwa mambo haya yalianza kutendeka mara tu
    alipowasili Evelyn. Wakaamua kumwekea mtego. Evelyn alioshikwa kimasomaso akidokoa mkoba wa
    msichana mwenzake. Mkoba huo ulikuwa umeaehwa juu ya dawati kimakusudi ili kumvuta Evelyn.
    Evelyn alifutwa kazi papo hapo. Fauka ya hayo, alitiwa mikononi na kukabidhiwa poisi waliomtupa
    korokoroni. Kesho yake Evelyn alifikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa la wizi. Alitozwa faini ya
    shilingi elfu tano au kifungo cha miezi sita. Hakuwa na pesa zozote za kulipia faini hii. Akawekwa
    rumande. Hata rafiki mmoja hakuwa naye wa kumuauni katika wakati huo wa majaribu. Kwa bahati, Rita
    alisikia kuhusu kadhia hiyo.Hakupoteza muda. Akashika njia moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
    Mpango ukafanywa na akamlipia. Evelyn ile faini. Evelyn alipoachiliwa hum akashangaa. “Yaani
    nimesamehewa ama nini?”Aliuliza.“La. Hujasamehewa.Faini uliyotozwa imelipwa na msichana yule.”
    Evelyn akageuka na kumwona Rita. Alimtazama kwa muda bila kujua la kusema. Mwishowe alimsogea
    kisha wakakaribiana polepole na kukumbatiana. Machozi yakaanza kumdondoka Evelyn, nde! Nde! Nde!
    Akalia kilio cha uchungu na soni. Akamwomba Rita msamaha, “Nisamehe, sikujua nililokuwa
    nikifanya.Nilidhani kuwa baada ya kupata kazi sitahitaji tena urafiki wako. Haya yaliyonipata
    yamenifunza,” alisema kwa masikitiko. “Evelyn, kijengacho mtu ni uth na tabia,” alisema Rita.“Ni kweli
    rafiki yangu” alitamka Evelyn, Sasa nimejitia kwenye shida.Hata kazi yangu nzuri nimeipoteza.Sina
    mahali pa kuishi. Itabidi nirudi kijijini kwa baba na mama. Kwaheri rafiki yangu naasante kwa yote
    uliyofanya.”“La! Hutaondoka”. Rita alimwambia lcwa dhati, “Tutakwenda nawe nyumbani mwangu
    tukaishi pamoja kama zamani. Nitayagharamia mahitaji yako yote hadi utakapopata kazi”. Basi Rita na
    Evelyn wakaungana tena na kuishi vizuri katika nyumba ile ile mtaani Kibokoni. Kweli akufaaye kwa dhiki
    ndiye rafiki.

    MASWALI:
    1. Maisha ya Evelyn na Rita yalikuwaje kabla ya Evelyn kupata kazi?
    2. Kutokana na jinsi Rita alivyomtunza Evelyn, unafikiri yeye alikuwa ni mtu wa ama gani?
    3. Eleza baadhi ya mambo ambayo Rita alimtendea mwenzake.
    4. Baada ya kupata kazi Evelyn alikuwa mtu mkarimu. Je, unakubali?Eleza ilivyokuwa.
    5. Evelyn alipokuwa mwanafunzi hakuwa na tabia ya udokozi. Unafikiri ni kwa nini alianza tabia
    hiyo baada ya kuajiriwa?
    6. ‘Asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu.’ Methali hii inahusianaje na Evelyn?
    7. ‘Akufaaye ukiwa dhiki ndiye rafiki.’ Methali hii inahusianaje na Rita?
    8. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu: (alama 3)
    (a) marafiki wa chanda na pete
    (b) enda mrama
    (c) jitolea sabili

    Date posted: November 22, 2022.  Answers (1)