-
Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli ya kutendewa
i) cha …
ii) nywa
Date posted:
October 7, 2019
-
Tunga sentensi ukitumia kinyume cha kitenzi: ‘umba’
Date posted:
October 7, 2019
-
Unda nomino za/lm,k, dhahania kutokana na maneno yafuatayo :-
i) Kwea .
ii) Himarisha
Date posted:
October 7, 2019
-
Eleza maana mbili ya sentensi:-
Tumetengeneza barabara
Date posted:
October 7, 2019
-
Andika katika usemi wa taarifa:-
Tutaanza mashindano kesho, Mwalimu alimwambia mwanafunzi.
Date posted:
October 7, 2019
-
Huku ukitumia mifano mwafaka, eleza tofauti ya sentensi sahili na ambatano
Date posted:
October 7, 2019
-
Ainisha shamirisho /yambwa katika sentensi ifuatayo:-
Mchezaji alimpigia mwenzake mpira kwa mguu wa kushoto.
Date posted:
October 7, 2019
-
Onyesha tofauti ya vitate vifuatavyo kwa kuvitungia sentensi
(i) Dhamani
(ii) Thamani
Date posted:
October 7, 2019
-
Andika udogo wa sentensi:-
Ndama wa ng’ombe yule ameuzwa.
Date posted:
October 7, 2019
-
Tunga sentensi sahihi ukitumia –wa- katika kauli ya kutendeana
Date posted:
October 7, 2019
-
Onyesha matumizi mawili mawili ya alama zifuatazo:-
(a) Alama ya mshangao
(b) Mshazari
Date posted:
October 7, 2019
-
Tunga sentensi ya maneno manne ambayo ina sehemu zifuatazo. Kielezi cha namna,
kivumishi,kitenzi na jina
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza matumizi mawili ya kiambishi ‘ku’
Date posted:
October 5, 2019
-
Unda kitenzi kimoja kutokana na nomino ‘Mtubia”
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja moja kudhihirisha ngeli zifuatazo:-
(i) U-U
(ii) Pokomo /Pa-ku-mu
Date posted:
October 5, 2019
-
Andika sifa bainifu za sauti
(i) e:-
(ii) n:-
Date posted:
October 5, 2019
-
Andika kwa udogo:-
Gari la Mzee Maritu limegonga ng’ombe wa jirani wake
Date posted:
October 5, 2019
-
Geuza zentensi zifuatazo katika kauli kwenye mabano:-
(i) Fundi ameharibu saa (kutendea)
(ii) Umemwona mgeni? (kutendewa)
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi ukitumia mzizi – choyo kama :-
(i) nomino
(ii) Kivumishi
(iii) Kiwakilishi
Date posted:
October 5, 2019
-
Bainisha aina za nomino zilizopigiwa mistari katika sentensi hii:-
Uhodari wa wanariadha wa Kenya unahitajika kote duniani
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza maana ya ‘jinsi’ kama inavyojitokeza katika sentensi zifuatazo
(i) Naomba unionyeshe jinsi ya kuendesha gari
(ii) Wakenya hawapendezwi na jinsi viongozi wanavyoendeleza ufisadi
Date posted:
October 5, 2019
-
Eleza mambo matano yaliyochangia kuenea kwa Kiswahili nchini kabla na baada ya uhuru
Date posted:
October 5, 2019
-
Unganisha sentensi hizi ukitumia kiunganishi cha kinyume:
Wananchi walikabiliwa na hatari
Wananchi waliendelea kuwaokoa majeruhi
Date posted:
October 5, 2019
-
Unda nomino moja moja kwa kila kitenzi
Shuku
Vumilia
shona
lia
Date posted:
October 5, 2019
-
Ainisha vitenzi katika tungo lifuatalo:
Huyu alikuwa angali bwenini
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja kuonyesha tofauti ya maana kati ya ‘guna’ na ‘kuna’
Date posted:
October 5, 2019
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mishale/mistari:-
Watoto wote wameamka mapema na wazazi wanatayarisha staftahi
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi yenye kiigizi na kihusishi cha mahali
Date posted:
October 5, 2019
-
Bainisha shamirisho kipozi, kitondo na ala katika sentensi ifuatayo:-
Maksuudi alimjengea Tamima Kasri kwa matofali mazuri
Date posted:
October 5, 2019
-
Tunga sentensi moja ukitumia kinyume cha neno ‘lewa’.
Date posted:
October 5, 2019