Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Taja sababu ambazo wewe kama anayekusanya kazi ya fasihi zingechnagia kutotumia mahojiano

Taja sababu ambazo wewe kama anayekusanya kazi ya fasihi zingechnagia kutotumia mahojiano.

Answers


KELVIN
a) Mahojiano yanahitaji stadi za mawasiliano za kiwango cha juu ikiwa mtafiti hana hizi stadi huenda akaathiri majibu ya mhojiwa.
b) Urasmi unaotokana na vikao vya mahojiano huenda ukatatiza mawasiliano kati ya mhoji na mhojiwa.
c) Ukosefu wa muda wa kutosha wa mahojiano, mahojiano huchukua muda mrefu na huenda mtafiti akakosa kupata muda kumhoji huenda asimwamini mtafiti ahisi kuwa anapelelezwa na kukataa kutoa habari.
d) Kiwango cha elimu cha mtafiti huenda kikawahajisha na kuwatia wahojiwa hisia za unyonge na kuwafanya kutoa habari za zisizotegemewa.
e) Wahojiwa wengine huenda wakampa mtafiti habari za uongo ili kumfurahisha.
f) Matatizo ya kutafsiri, ikiwa data imeandikwa kwa lugha tofauti huenda yakaathiri mahojiano.
g) Mahojiano ni njia ghali ya kutafiti kutokana na gharama ya usafiri kwenda nyanjani.

kalvinspartan answered the question on August 5, 2018 at 12:53

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions