-
Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili.
Date posted:
October 1, 2019
-
Kidagaa kimemwozea
"Kwa nini mnaifunga mnyororo ile doggy mgonjwa? Mbona msiiwache free".
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Onyesha jinsi wahusika riwayani wamefungwa minyororo.
(c) Minyororo inayorejelewa katika (b) hapo juu ilifunguliwaje?
Date posted:
October 1, 2019
-
Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
(i) Kanda la usufi
(ii) Shaka ya mambo
(iii) Mwana wa darubini
(iv) Ndoa ya Samani.
Date posted:
October 1, 2019
-
Wafrika hupitia changamoto nyingi sana wakiwa masomoni ughaibuni. Thibitisha kauli hii ukirejelea hadithi "Damu nyeusi"
Date posted:
October 1, 2019
-
"Kero hizi na dharau zinamfanya kuthamini zaidi utu wake ....."Ukirejelea hadithi "Damu nyeusi" Eleza muktadha wa dondoo hili.
Date posted:
October 1, 2019
-
Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.
Date posted:
October 1, 2019
-
Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"
Date posted:
October 1, 2019
-
"Damu nyeusi na hadithi zingine"
"Sisi kama wazazi...........hukabiliana na mengi...........mara nyingi tabia zao hutupiga chenga........"
a) Weka dondoo hili katika muktadha wake
b) Dhihirisha mbinu NNE za lugha zinazojitokeza katika dondoo hili
c) Jadili yaliyomsibu mrejelewa.
Date posted:
October 1, 2019
-
Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano
Date posted:
October 1, 2019
-
kidagaa kimemwozea
"...........wanaume wangewastahi wanawake kidogo,.......dunia ingekuwa pahala pema zaidi pa kuishi.
a) Weka dondoo hili katika muktadha wake.
b) Kwa kurejelea wahusika wanne, onyesha jinsi Mtemi Nasaba Bora anavyochangia kumkandamiza mwanamke.
Date posted:
October 1, 2019
-
Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.
Date posted:
October 1, 2019
-
"Mstahiki Meya"
"Hadi sasa sijaelewa kwa nini hakujitokeza kueleza hali ilivyo........Huenda hii ni dalili za..........."
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Fafanua masuala matano yanayofaa kuelezewa kuhusu hali inayorejelewa.
c) Eleza umuhimu wa anayerejelewa
d) Bainisha matumizi ya tamathali moja katika dondoo
Date posted:
October 1, 2019
-
Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.
Date posted:
October 1, 2019
-
Eleza maana ya maapizo.
Date posted:
October 1, 2019
-
Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.
Date posted:
October 1, 2019
-
Soma wimbo ufuatao kisha ujibu maswali
Ewe mpwa wangu,
Kwetu hakuna mwoga, usiwe kama msichana.
Uoga ukikufika, huenda ni wa akina mamayo,
Fahali tulichinja ili uwe mwanamume
Iwapo utatingiza kichwa
Uhamie kwa wasiokatwa
Waume wa mbari yetu
Si waoga wa kisu
Wao hukatwa kuanzia macheo hadi machweo.
Simama jicho liwe juu
Ngariba alilala jikoni
Visu ametia makali
Kabiliana na kisu kikali
Wengi wasema ni kikali
Mbuzi utampata
Na hata shamba la mahindi
Usiende kwa wasiotahiri.
MASWALI
(a) Huu ni wimbo gani? Fafanua
(b) Eleza shughuli mbili za kiuchumi zinazodokezwa na wimbo huu.
(c) Onyesha taasubi ya kiume inavyojitokeza katika wimbo huu.
Date posted:
October 1, 2019
-
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.
Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu. Kila mara bibi akipigia mumewe simu, ilipokelewa na sauti nyororo "mteja wa nambari uliopiga hapatikani kwa sasa."Alifunga safari kumtembelea mume wake mjini na kukabiliana na huyu kisura.
MASWALI
a) Bainisha kipera cha utungo huu.
b) Onyesha sifa tano za kipera hiki.
c) Eleza manufaa tano ya kipera hiki.
Date posted:
October 1, 2019
-
Kanda la Usufi - (R. Nyaga)
(a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
Fafanua kwa kutolea mifano.
(b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.
Date posted:
October 1, 2019
-
Kidagaa Kimemwozea; Ken Walibora
Ningemweka hai afikishwe mahakamani kweli idhihiri na uongo ujitenge".
(a) Eleza muktadha wa dondoo.
(b) Fafanua kwa kutolea mifano ukweli wa kauli "kweli idhihiri".
(c) Eleza hulka ya mnenaji.
(d) Vitaje vitushi vyovyote vitatu vilivyomshangaza msemaji kulingana na muktadha wa dondoo.
Date posted:
October 1, 2019
-
Pauline Kea: Kigogo
'Hivi vishahada vyao wanavyovipata siku hizi vinawavimbisha vichwa!'
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Taja tamathali zozote mbili zinazojitokeza katika dondoo hili.
(c) Eleza changamoto zilizomkabili mrejelewa na wenzake.
Date posted:
September 24, 2019
-
Assumpta Matei: Chozi la Heri
Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmoja baada ya mwingine.
(a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.
(b) Eleza sifa tatu za anayerejelewa katika dondoo hili.
(c) Eleza tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.
(d) Fafanua masaibu yaliyomkumba mrejelewa.
(e) Huku ukitolea mifano riwayani, jadili matatizo yanayowakumba wanajamii katika ndoa.
Date posted:
September 24, 2019
-
Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba
'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Ndevu, Mame Bakari, Shibe Inatumaliza na Mtihani wa Maisha.
Date posted:
September 24, 2019
-
Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
-
Taja mifano ya taswira katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
-
Taja lugha za mahakama?
Date posted:
August 24, 2019
-
Taja vipera vya mazungumzo
Date posted:
August 24, 2019
-
RIWAYA
S.A MOHAMED: UTENGANO
“ Katu asingajitia kibuibui na kutanga na njia. Lo, kachoshwa na shimiri za baruti
anazoshindiliwa moyoni mwake.”
a) eleza muktadha wa dondoo hili.
b) taja na ufafunue tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili
c) Eleza umuhimu wa kisa kinachorejelewa na dondoo.
d) kwa kurejelea matukio mengine katika riwaya ya Utengano, fafanua maudhui
mawili yayoashiriwa na dondoo hili.
Date posted:
June 29, 2019
-
Bainisha maudhui yanayojitokeza katika riwaya ya chozi la heri
Date posted:
June 14, 2019
-
Damu Nyeusi
Jadili maudhui ya elimu kwa mujibu wa "Kanda la Usufi", "Shaka ya Mambo"
na "Tazama na Mauti"
Date posted:
May 7, 2019
-
Kidagaa Kimemwozea:
"Wasemao husema, atafutaye hachoki."
(a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
(b) Kauli hii ina tnaana gani kwa mujibu wa muktadha huu.
(c) Jadili umuhimu wa kinachotafutwa katika riwaya ya Kidagaa
Kimemwozea.
Date posted:
May 7, 2019