Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Questions and answers: Ushairi

Q&A Categories


Do you have Q&A pairs? Post them here

62 Questions  View: All | Solved | Unsolved



Search Results...
  • Nini umuhimu wa ushairi katika jamii?(Solved)

    Nini umuhimu wa ushairi katika jamii?

    Date posted: February 6, 2023.  

  • Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata. WASAKATONGE 1. Wasakatonge na juakali Wabeba zege ya maroshani, Ni msukuma mikokoteni, Pia makuli bandarini, Ni wachimbaji wa migodini, Lakini...(Solved)

    Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata. WASAKATONGE 1. Wasakatonge na juakali Wabeba zege ya maroshani, Ni msukuma mikokoteni, Pia makuli bandarini, Ni wachimbaji wa migodini, Lakini maisha yao chini 2. Juakali na wasakatonge Wao ni manamba mashambani, Ni wachapa kazi viwandani, Mayaya na madobi wa nyumbani, Ni matopasi wa majaani, Lakini bado ni masikini. 3. Wasakatonge na juakali Wao huweka serikalini, Wanasiasa madarakani, Dola ikawa mikononi, Wachaguliwa na ikuluni, Lakini wachaguaji duni 4. Juakali na wasakatonge Wao ni wengi ulimwenguni, Tabaka lisilo ahueni. Siku zote wako matesoni, Ziada ya pato hawaoni, Lakini watakomboka lini? (Mohammed Seif Khatib) (a) “Shairi hili ni la kukatisha tamaa”. Fafanua rai hii kwa kutoa mifano minne. (b) Taja tamathali ya usemi iliyotawala katika shairi zima na uonyeshe mifano miwili ya jinsi iiivyotumika. (c) Eleza umbo la shairi hili. (d) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari. (e) Onyesha mifano miwili ya maadiii yanayojitokeza katika shairi hili. (f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi. (i) Manamba (ii) Tabaka lisilo ahueni

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata: Kila Mchimba Kisima Musa Mzenga 1. Tenda utendapo tendo, tenda tendo kwa hekima, Lindamane mwenendo, sawa na yakio kalmia, Kalmia yenye upendo, kufurahisha...(Solved)

    Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata: Kila Mchimba Kisima Musa Mzenga 1. Tenda utendapo tendo, tenda tendo kwa hekima, Lindamane mwenendo, sawa na yakio kalmia, Kalmia yenye upendo, kufurahisha mtima, Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 2. Utendapo la faraja, tendo ni yako salama, Ya kukupa kila tija, na ushindi wa daima, Upate njema daraja, duniani na kiyama, Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 3. Utendapo la miuja, tendo ni yako nakama Ya kukutia harija, hasara kukuandama, Usione afuwaja, mwanza ajue heshima, Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe 4. Nakwambia uelewe, pulika ninayosema, Si ari ya mwenginewe, kumuonya kwa lazima, Mtu hufunza mwanawe, Kwanza ajue heshima, Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 5. Nisipokwambia wewe, kukufunza kila jema, Kusudi nikuongowe, uepukwe na tujuma, Matusi ndimi nipawe, ila na kila lawama, Kila mchimba kisima, bundi hungia mwenyewe 6. Hii si heri ujuwe, matusi kuigandama, Hadhi usiniuzuwe, hamithilishwa na nyama, Fikiri moyo utuwe, nikupapo taaluma Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 7. shika tena utambuwe, wasia huu ni mwema Matendo usipunguwe, mazuri kutenda hima, Yatende ubarikiwe, upawe na taadhima Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 8. Yakupasa uchunguwe, kila jambo kulipima Upime ufafanuwe, mambo yote kwa alama La kuwaka ulijuwe, pia lipi la kuzima, Kila mchimba kisima hungia mwenyewe. a) Eleza maudhui ya shairi hili. b) Ujumbe unaowasilishwa katika shairi hili una hadhira lengwa tatu. Zitaje na utoe mifano. c) Eleza umuhimu wa kipokeo kinachotumiwa katika shairi hili

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi kisha ujibu maswali yanayofuata: KIBARUWA: Abdilatif Abdalla Kwenye shamba hilo kubwa asilani hakunyi mvuwa! Ni kwa mitilizi ya jasho langu ndiyo hunweshezewa Kwenye shamba hilo kubwa sasa...(Solved)

    Soma shairi kisha ujibu maswali yanayofuata: KIBARUWA: Abdilatif Abdalla Kwenye shamba hilo kubwa asilani hakunyi mvuwa! Ni kwa mitilizi ya jasho langu ndiyo hunweshezewa Kwenye shamba hilo kubwa sasa imeshaiva kahawa Na bunize ni matone ya damu yangu niliyotowa Ndipo mte ukatipuza! Buni hiyo itakaangwa buni hiyo itapondwapondwa Buni hiyo itasagwa na buni hiyo itafyondwafyondwa Bali itabaki nyeusi kama ngozi yangu Kibaruwa Waulize ndege kwa nyimbo nyanana watutumbuizao Iulize na mito kwa furaha maji itiririkao Uulize na upepo mkali kwa ghadhabu uvumao-. Viulize: Ni nani araukaye na mapema kuzitema mbuga na kuzilaza? Viulize: Ni nani akweaye minazi tangu kuchapo hadi lingiapo giza? Viulize: Ni nani abebeshwaye mizigo hadi maungo yakageuka shaza? Halfuye hana faida moja apatay wala malipo yanayotoshelezaIsipokuwa kusundugwa na kutupiwa matambara na vyakula viliyooza? Viulize: Ni nani huyo ni nani! Viulize: Ni nani aliyemaye mashamba na kuyapoliliya? Na mimea kochokocho ikajaa kwa uzito ikajinamiya? Hatimaye nani atajirikaye mali yakammiminikiya Akatoa na kitambi kama mja mzito wa miezi tisiya Na akaongeza magari na wanawake kutoka na kuingiya? Viulize: Ni nani huyo nani1 Na hao ndege kwa nyimbo nyanana watutumbuizao Nayo hiyo mito kwa furaha maji itirikao Na huo upepo mkali wenye ghadhabu uvumao Vyote hivyo vitatu vitakujibu kawa umoja wao “Ni Kibaruwa Manamba ndiye mtendaji hayo!” a) Eleza dhamira ya shairi hili. b) Kwa kutoa mifano, eleza aina mbili za idhini ya kishairi alizotumia mshairi c) kwa kurejelea ubeti wa tatu taja na ueleze tamathali ya usemi na mbinu ya kimuundo mshairi d) Huku ukitoa mifano, eleza kwa kifupi mwelekeo wa mshairi kuhusu vibarua. e) Andika ubeti wa tano katika lugha ya nathari f) Onyesha utata wa maana katika matumizi ya Kibaruwa Manamba

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata. Dhamiri yangu Dhamiri imenifunga shingoni. Nami kama mbuzi nimefungwa Kwenye mti wa utu. Kamba ni fupi Na nimekwishachora duara. Majani niwezayo kufikia yote nimekula. Ninaona...(Solved)

    Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata. Dhamiri yangu Dhamiri imenifunga shingoni. Nami kama mbuzi nimefungwa Kwenye mti wa utu. Kamba ni fupi Na nimekwishachora duara. Majani niwezayo kufikia yote nimekula. Ninaona majani mengi mbele yangu Lakini siwezi kuyafikia: kamba, kamba. Oh! Nimefungwa kama mbwa. Nami kwa mbaya bahati, katika Uhuru kupigania, sahani ya mbingu Nimeipiga teke na niigusapo kwa mdomo Mbali zaidi inakwenda na siwezi tena Kuifikia na hapa nilipofungwa Nimekwishapachafua na kuhama siwezi. Kamba isiyoonekana haikatiki. Nami sasa sitaki ikatike, maana, Mbuzi wa kamba alipofunguliwa, mashamba Aliharibu na mbwa aliuma watu. Ninamshukuru aliyenifunga hapa Lakini lazima nitamke kwa nguvu “Hapa nilipo sina uhuru!” (E. Kezilahabi) (a) Taja mambo manne ambayo mshairi analalamikia. (b) Kwa nini mshairi haoni haja ya yeye kuwa huru? (c) Eleza rnaana ya mshororo ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi. “Kamba isiyoonekana haikatiki.” (d) Taja na utoe mifano ya aina mbili za tamathali zilizotumika katika shairi hili. (e) Kwa kutoa mifano miwili, eleza jinsi matumizi ya mishata yanavyojitokeza katika shairi hili. (f) Andika ubeti wa pili kwa lugha nathari.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • HAKI 1. Haki watutisha, tusikuandame, kwa matendo yetu, Watukorofisha, tusikuandame, kila penye kitu, Mbona watugwisha, miba ituchome kwenye huu mwitu, Tutokwe na utu! 2. Hatutakufanya, mwana kwa...(Solved)

    HAKI 1. Haki watutisha, tusikuandame, kwa matendo yetu, Watukorofisha, tusikuandame, kila penye kitu, Mbona watugwisha, miba ituchome kwenye huu mwitu, Tutokwe na utu! 2. Hatutakufanya, mwana kwa mvyele; aliyemzaa, Haki watunyima, machumi ya mbele, na nyingi hadaa, Tuchumayo nyanya, uchungu umbele, hatuna wasaa, Haki twashangaa! 3. Na kambi nzima, kunaiyenea, hasa hapa petu, Tunakutazama, kwa kuulizia, kuweza thubutu, Na kwenye milima, ilotueka, kupandia watu, Usifanyekatu! 4. Sio hao mabwana, waloteuliwa, kupata mwangaza, Haki wakubana, lilotarajiwa, kwenye hichi kiza, Ndevu kuchomana, wengine kuliwa, tukijiingiza, Kambi yatuviza! 5. Haki buna njia, kizuizi mali, ndio njia panda, Tukiifatia, hatufiki mbali, wengi tunaganda, Sio yetu nia, lakini akili, mali ishapenda, Haki yatuponza! 6. Wala hutasemwa, sababu ni nyoyo, kwisha haribika, Ya mali kuchumwa, vyovyote iwavyo, itavyopatika, Wakati mtumwa, ushatumwa ndivyo, na ushatufika, Kwetu nimashaka! 7. Haki hufanyiki, papitapo mambo, na vikubwa visa, Watu hawataki, kutenda kijambo, tunu yao pesa, Sisi kwetu dhiki, yatunisha tumbo, wao hata hisa, Nandio ya sasa! 8. Haki husimami, kwa viumbe sisi, tuvyojaaliwa, Na huna ulimi, kuweza tukisi, tukageukiwa, Zama za uchumi, zishashika kasi, nguvu zishapewa, Haki wauliwa! 9. Iwe hivi haki, hakuna mmoja, akukumbukae, Hatuna ashiki,kuvutalahaja,haki ituvae, Mbona hatutaki, twalia na tija, haki iambae, Haki tamati! (Suleiman A. Ali) Malenga Wapya (a) Eleza dhamira ya shairi hili. (b) Huku ukitoa mfano, eleza aina ya shairi hili. (c) Taja na ufafanue tamathali ya usemi inayotawala katika shairi hili. (d) Kwa kutoa mfano mmoja mmoja, onyesha aina tatu za idhini ya kishairi katika shairi hili. (e) Andika ubeti wa saba kwa lugha ya nathari. (f) Mshairi ana maana gani kwa kusema: (i) Kambi yatuviza (ii) Kuweza tukisi.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Capture.JPG (a) Mtunzi wa shairi hili ana dhamira gani? (b) Shairi hili ni la aina gani? Toa...(Solved)

    Capture.JPG (a) Mtunzi wa shairi hili ana dhamira gani? (b) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu moja. (c) Eleza mambo matatu ambayo mshairi anashauri nchi ifanye ili kujitegemea. (d) Taja aina moja ya idhini ya kishairi iliyojitokeza kwa wingi zaidi katika shairi na utoe mifano mitano ya matumizi yake. (e) Andika ubeti wa pili kwa lugha ya nathari. (f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi: (i) Ghaibu (ii) Tukamshabihi.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali 1. Huno wakati mufti, vijana nawausia, Msije juta laity, mkamba sikuwambia, Si hayatti si mamati, vijana hino dunia, Uonapo vyang’aria,...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali 1. Huno wakati mufti, vijana nawausia, Msije juta laity, mkamba sikuwambia, Si hayatti si mamati, vijana hino dunia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 2. Japo aula kushufu, na machoni vyavutia, Dunia wana dhaifu, waugua nisikia, Vijana nawasarifu, falau mkisikia, Ukiona vyang’aria, tahadhari vitakula. 3. Jepusheni na zinaa, mlale penye sheria, Msije andama baa, makaa kujipalia, Jepusheni na zinaa, madhara kukadiria, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 4. Ngawa waone wazuri, nadhifu kukuvalia, Wajimwaie uturin na mapoda kumichia, Si mlango nyumba nzuri, ngia ndani shuhudia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 5. Wawapi leo madume, anasa walopapia? Wamepita ja umeme, leo yao sitoria, Shime enyi wana shime, bora kumcha Jalia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 6. Nambie faida gani, nambie ipi fidi? Upatayo hatimani, waja wakikufukia, Ilakufa kama nyani, kasoroyako mkia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 7. Kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia, Ujifanye kama kwamba, u jiwe huna hisia, Wakwambe watalokwamba, kwa lolote vumilia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 8. Vyatiririka tiriri, vina vyanikubalia, Alo bora mshairi,pa tamu humalizia, Nahitimisha shairi, dua ninawapigia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. 9. Ewe Mola mtukuka, si shaka wanisikia, Wakinge wanarika, na anasa za dunia, Amina wangu Rabuka, dua yangu naishia, Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. (Mwalaa M.Nyanje) (a) Eleza ujumbe wa shairi hili. (b) Fafanua kwa kutoa mifano, mbinu nne alizotumia mshairi kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika shairi hili. (c) Nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili inasema na pande mbili. Zieleze pande hizo. (d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili. (e) Bainisha toni ya shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana, Nikaiga rika langu, kwa vileo, na mbio za wsichana, Kiwa ni riziki yangu,...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana, Nikaiga rika langu, kwa vileo, na mbio za wsichana, Kiwa ni riziki yangu, mapokeo, kuoa na kuona, Ni wakati utanena. Nashukuru kwa ugumba, wenye ndimi, wanipazao nao, Wapitao wakiimba, eti mimi, ningapenda hali zao, Haupandiki mgomba, wana nyemi, fisadi wa hadhi zao, Eti ni kwa raha zao. Ni lipi lenye kukera, kwa Muumbi, marufuku kwenye misa, Ni mtu kuwa hawara, wa vitimbi, ama alozawa tasa? Ugumba na ukapera, sio dhambi, wala haujawa kosa, Waama sina makosa Bora tungeni vitabu, magazeti, mutangaze kwa rediyo, Muwaite watribu, kina Siti, watuzwa ilimu hiyo, Na zaidi muhutubu, kwa umati, muwambe ambayo siyo, Kwalo sichafuki moyo Hidhuru yote ni bure, sio kitu, kudhiki asodhikika, Siwi nikaona ghere, lailatu, nyota njema itafika, Kwa shangwe na njerejere, kila mtu, mdomo utafumuka, Akiri amejibika. (Mwalaa M. Nyanje) (a) Eleza jambo ambalo mzungumzaji (nafsineni) katika shairi hili anasingiziwa. (b) Fafanua mambo matano ambayo mzungumzaji (nafsineni) anapinga katika shairi hili. (c) Eleza umuhimu wa viishio vya beti za shairi hili. (d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari. (e) Eleza muundo wa shairi hili. (f) Bainisha matumizi mawili ya tafsida katika shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Watafuta Riziki 1. Watafuta riziki, watatokwa jasho vijijini Wakulima shakiki, wakuza chai na mibuni Vyakula washakiki, visipungue vinyuani. 2. Watafuta riziki, wahaingaikao...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Watafuta Riziki 1. Watafuta riziki, watatokwa jasho vijijini Wakulima shakiki, wakuza chai na mibuni Vyakula washakiki, visipungue vinyuani. 2. Watafuta riziki, wahaingaikao mijini Kutwa kile na hiki, kama watanga na mipini Japo hawasikii, hawakosi kujiamini 3. Watafuta riziki, wazalendo wa nchi hii Kamwe hawajidhiki, tama za moyo kutii Bali huafiki, kupingana na ulaghai 4. Watafuta riziki, pato ambalo la halali Ndoto haizimiki, ya kesho kuwa njema hali Wiki baada wiki, la haramu jasho hawali (a) Fafanua sifa tano za watu wanaozungumziwa katika shairi hili. (b) Bainisha umuhimu wa tamathali tatu za usemi zilizotumiwa katika shairi hili. (c) Eleza kwa kutoa mifano, mbinu tatu ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi. (d) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo: (i) idadi ya mishororo katika beti. (ii) mpangilio wa vina (iii) mpangilio wa maneno

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Amiri A. S. Andanenga: Sauti ya Kiza 1 Ngakua na mato, ya kuonea Ngalisana kito,cha kuchezea Kilicho kizito, cha kuelea Kikamuenea,...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Amiri A. S. Andanenga: Sauti ya Kiza 1 Ngakua na mato, ya kuonea Ngalisana kito,cha kuchezea Kilicho kizito, cha kuelea Kikamuenea, akivae. 2 Makusudi yangu,ngaliandaa Ngafinyanga chungu, cha mduwaa Ngatia vitangu,vinavong’aa Ili ziwe taa, kwa apikae. 3 Mkungu wa tano, wa mduwara Ulo bora mno, kisha imara Ulo na maono, kuwa ni dira Kwenye barabara, itindiae. 4 Ngaomba Baraka, kwake Rabana Punje za nafaka, kila aina Chunguni kuweka, kwa kulingana Hajaangu suna, yule alae. 5 Ngafanya bidii, kwenda mwituni Sio kutalii, kukata kuni Ya miti mitii, huko jikoni Isio na kani,ni iwakae. 6 Kwa yangu mabega, nikathubutu Ngabeba mafiga, yalo matatu Bila hata woga, kwenye misitu Simba tembo chatu, sinitishie. 7 Miti yenye pindi,na jema umbo Ngajenga ulindi, mwema wimbombo Fundi aso fundi, penye kiwambo Moyo wenye tambo, apekechae. 8 Singaajiri, ngachimba mimi Kisima kizuri, cha chemchemi Maji ya fahari, ya uzizimi Jua la ukami, siyaishae 9 Tamati nafunga, kwa kuishia Mato ndo malenga, kanikimbia Nahofu kutunga, mabeti mia Asije chukia, ayasomae. (a) Eleza ujumbe wa shairi hili. (b) Kwa kurejelea ubeti wa pili, eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa kishairi aliotumia mshairi. (c) Andika ubeti wa saba kwa lugha ya nathari. (d) Eleza toni ya shairi hili. (e) Fafanua aina tatu za urudiaji zilizotumiwa katika shairi hili. (f) Bainisha nafsi neni katika shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Mwili Leo kitaka nifike, natamani, ila wauma mwili Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili. Vitisho kamwe...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. T. Arege: Mwili Leo kitaka nifike, natamani, ila wauma mwili Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili. Vitisho kamwe kelele, ninavicha, kwa nafsi na mwili Ila ugonjwa utimile, umechacha, na kuudhili mwili Msikose simile, magalacha, si gurudumu mwili. Vingekuwepo viraka, kuutia, ngeushuruti mwili Kifundi kivipachika, kuingia, hata kuridhi mwili Upya ukaungilika, kuvutia, roho na wake mwili. Lakini kamwe haiwi, kuvipata, vipande vyake mwili Sihofu kupata mawi, sitajuta, kupigania mwili Hata kufutwa sikawi, nitakita, kidete nao mwili. Kazi ninaithamini, ni hakika, akilini na mwili Ila kamwe siamini, kusagika, damu, jasho na mwili Uwele hususani, kioneka, nguvu hitishi mwili. a) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili. b) Fafanua mbinu nne za lugha zilizotumiwa katika shairi hili. c) Eleza toni ya shairi hili. d) Ni nani anayezungumziwa na nafsineni katika shairi hili? e) Eleza bahari ya shairi hili kwa kurejelea vipande. f) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha ya nathari.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Daima alfajiri na mapema Hunipitia na jembe na kotama Katika njia iendayo kondeni Kama walivyofanya babuze zamani; Nimuonapo huwa anatabasamu Kama mtu aliye na kubwa...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. Daima alfajiri na mapema Hunipitia na jembe na kotama Katika njia iendayo kondeni Kama walivyofanya babuze zamani; Nimuonapo huwa anatabasamu Kama mtu aliye na kubwa hamu Kushika mpini na kutokwa jasho Ili kujikimu kupata malisho. Anapotembea anasikiliza Videge vya anga vinavyotumbuiza Utadhani huwa vimemngojea Kwa usiku kucha kuja kumwimbia; Pia pepo baridi kumpepea Rihi za maua zikimletea Nao umande kumbusu miguu; Na miti yote hujipinda migongo kumpapasa,kumtoa matongo; Na yeye kuendelea kwa furaha kuliko yeyote ninayemjua Akichekelea ha ha ha ha ha ha … Na mimi kubaki kujiuliza Kuna siri gani inayomliwaza? Au ni kujua au kutojua? Furaha ya mtu ni furaha gani katika dunia inayomhini? Ukali wa jua wamnyima zao Soko la dunia lamkaba koo; Dini za kudhani zamsonga roho Ayalimia matumbo ya waroho; Kuna jambo gani linamridhisha? Kama si kujua ni kutokujua Laiti angalijua, laiti angalijua! (T. Arege) Maswali a) Eleza hali ya mzungumziwa katika shairi hili. b) Huku ukitoa mifano, onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili. c) Fafanua aina tatu za taswira ukirejelea ubeti wa pili. d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili. e) Bainisha vipengele vifuatavyo vya kimtindo katika shairi hili: i. tashhisi ii. kinaya iii. tashbihi f) Eleza toni ya shairi hili. g) Bainisha nafsineni katika shairi hili. h) Changanua muundo wa shairi hili.

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali T. Arege: Barabara Barabara bado ni ndefu Nami tayari nimechoka tiki Natamani kuketi Ninyooshe misuli Nituliza akili Lakini Azma yanisukuma Mbele ikinihimiza kuendelea Baada ya miinuko na kuruba Sasa naona...(Solved)

    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali T. Arege: Barabara Barabara bado ni ndefu Nami tayari nimechoka tiki Natamani kuketi Ninyooshe misuli Nituliza akili Lakini Azma yanisukuma Mbele ikinihimiza kuendelea Baada ya miinuko na kuruba Sasa naona unyoofu wake Unyoofu ambao unatisha zaidi Punde natumbukia katika shimo Nahitaji siha zaidi ili kupanda tena Ghafla nakumbuka ilivyosema Ile sauti zamani kidogo “Kuwa tayari kupanda na kushuka.” Ingawa nimechoka Jambo moja li dhahiri Lazima nifuate barabara Ingawa machweo yaingia Nizame na kuibuka Nipande na kushuka Jambo moja nakukumbukia: Mungu Je, nimwombe tena? Hadi lini? Labda amechoshwa na ombaomba zangu Nashangaa tena! Kitu kimoja nakiamini Lazima niendelee kujitahidi kwa kila hatua mpya Nijikokote kuiandama hii barabara yenye ukungu Nikinaswa na kujinasua Yumkini nitafika mwisho wake Ingawa wangu mwisho haitauwahi kabla. (a) Eleza toni ya shairi hili. (b) Tambua nafsineni katika shairi hili. (c) Mshairi ana maana gani anaposema “Kuwa tayari kupanda na kushuka” katika ubeti wa tatu? (d) Fafanua tamathali tano za usemi zilizotumiwa katika shairi hili ukizitolea mifano mwafaka. (e) Eleza ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa tano wa shairi hili. (f) Eleza maana ya: (i) kuruba (ii) barabara yenye ukungu

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Kilio cha Lugha Ni wimbo najiimbia,nijiliwaze Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi Lugha ya mtu mweusi, Kiswahili chalilia Wataalamu ni nani, mulipo mwaninyanyasa Hamna nami...(Solved)

    Kilio cha Lugha Ni wimbo najiimbia,nijiliwaze Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi Lugha ya mtu mweusi, Kiswahili chalilia Wataalamu ni nani, mulipo mwaninyanyasa Hamna nami imani, wala kupanga siasa Mwasema sayansini, siku ningalitosa Mwanambia nikotosa, kuiva sijafika Ela muelewe sana, Maamuma na Imamu Mulipokuwa vijana, kwenu nilikuwa timamu Sasa mumesoma sana, mwaniona ni haramu Mujue kuwa dawamu, utumwa mwauridhia. Mzaliwapo mwalia, ‘maa’, maneno ya kwanza Lugha munayokulia, ya mama zetu ya kwanza Wa lugha muwedoria, muweze na kuikuza Sio kujipendekeza, uzungu kuigiza. Majira ya ukoloni, ukombozi kusambaza Lugha mulithamini, Kiswahili kufukiza Hata kule risavuni, kizungu hanikuwaza Sasa mbona mwanibeza, mbali mwanitupilia? Sayansi sio asili, msamiatiwe sinao Sayansi yataka mbali, msamiati ni wa hao Nitakuwa Kiswahili, kiomba majina yao Lugha kujikuza kwao, huomba linalofaa. Enyi viongozi wetu, ipangeni nadharia Kujenga siasa yetu, tuzidi kuwa huria Lugha hata ‘mbusha watu, tuche kuriaria Sifa ni kwa chake mtu, cha mwenzi hutoringia Utajiri wangu hasa, nikiwatajia wote Msamiati huwa, ni wa Afrika yote Na methali za kuasa, nahau na ngeli zote Na nisemwapo popote, ujumbe hukamilika. Afrika ndipo petu, pa wabantu halisi Baba na mama ni Bantu, shina la wangu ukwasi Warabu na wengi wetu, sio wangu Adinasi Kwao ‘meomba kiasi, ili kujizidisha Mfumo mpya hongera, wa elimu humu Kenya Lugha takuwa imara, ukabila tutafinya Kiswahili ni ibara, kila mtu kiimanya Methali imetuonya, mtumwa si mwasilia. Tamati lugha yalia, yabaguliwa bayana Kukua imeridhia, msamiati kufana Wengine wataijulia, kwa marefu na mapana Lugha yetu ya maana, mwaipuuza yalia. Maswali (a) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu (b) Kwa kutoa hoja nne, eleza kwa nini shairi hililikaitwa kilio cha lugha. (c) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari. (d) Eleza toni ya shairi hili. (e) Tambua uhuru wa kishairi uliotumiwa kwa kurejelea mifano mitatu. (f) Bainisha nafsineni katika shairi. (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa mujibu wa shairi. i. nasongwa ii. kuriaria iii. adinasi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Lau dunia nanena, tuseme si ati ati, Mauti kawa hakuna, katika wote wakati, Vipi tungelisongana, tunaoishi tiati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Dunia ingetatana, na kizazi katikati, Huku kwazaliwa bwana,...(Solved)

    Lau dunia nanena, tuseme si ati ati, Mauti kawa hakuna, katika wote wakati, Vipi tungelisongana, tunaoishi tiati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Dunia ingetatana, na kizazi katikati, Huku kwazaliwa bwana, kule kwazawa binti, Vipi tungelioana, na kuzaa hatuwati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Lau mauti hakuna, tungesongana sharuti, Kwa viumbe kukazana, wanadamu na manyati, Vipi tungelijazana, kwa kusitawi umati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Walakini Subuhana, kapanga sisi na miti, Ili tusizidi sana, si wengi na si katiti Maisha ya kupishana, yule ende yule keti, Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Ndipo dunia kufana, ikawa kama yakuti, Kwa uwezowe Rabana, kaipanga madhubuti, Maisha kugawiana, kayagawa kwa mauti, Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Njia ingekuwa hapana, pembeni na katikati, Sote tungeambatana, kama ukosi na shati, Na njaa ingetutafuna, pa kulima hatupati, Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Peleleza utaona, hayataki utafiti, Kama tungelikongana, ingekuwa ni bahati, Vipi tungesukumana, katika hiyo hayati? Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? Mbele sitokwenda tena, hapa mwisho nasukuti, Yaoleni waungwana, shauri yake Jabaruti, Yote tuloelezana, katenda bila senti, Lau hakuna mauti, vipi tungelisongana? (Abdalla Said Kizere) Maswali a) Pendekeza anwani mwafaka la shairi hili. b) Je, hili ni shairi la bahari gani? Eleza c) Eleza vile mwandishi alivyotumia uhuru wa kishairi. d) Eleza umbo la shairi hili. e) Fafanua ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa tano. f) Andika majina mawili ya Mungu kwa mujibu wa shairi. g) Kwa kutolea mifano, eleza mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi hili

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Eleza mambo yanayozingatiwa katika uhuru wa kishairi (Solved)

    Eleza mambo yanayozingatiwa katika uhuru wa kishairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja baadhi ya masuala muhimu katika uchambuzi wa mashairi(Solved)

    Taja baadhi ya masuala muhimu katika uchambuzi wa mashairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja aina mbalimbali za takriri katika ushairi(Solved)

    Taja aina mbalimbali za takriri katika ushairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Katika ikisiri yake, Joseph Nyehita anaangazia kuwa matumizi ya methali yanapozingatiwa, ushairi wa Kiswahili unaweza kuainishwa zaidi kwa kuzingatia kutumiwa au kutotumiwa kwa methali. Anasema...(Solved)

    Katika ikisiri yake, Joseph Nyehita anaangazia kuwa matumizi ya methali yanapozingatiwa, ushairi wa Kiswahili unaweza kuainishwa zaidi kwa kuzingatia kutumiwa au kutotumiwa kwa methali. Anasema kuwa kila kikundi cha ushairi kinaweza kupendekezewa jina mahususi kuwa kitambulisho chake. Taja majina yanayopendekezwa

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja huku ukitoa mfano, aina kadha za taswira katika ushairi(Solved)

    Taja huku ukitoa mfano, aina kadha za taswira katika ushairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja na ueleze tamathali tofauti za usemi(Solved)

    Taja na ueleze tamathali tofauti za usemi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja mambo ya kuzingatia katika kueleza muundo wa shairi(Solved)

    Taja mambo ya kuzingatia katika kueleza muundo wa shairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja na ueleze mambo muhimu yanayozingatiwa katika uchambuzi wa mashairi(Solved)

    Taja na ueleze mambo muhimu yanayozingatiwa katika uchambuzi wa mashairi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Eleza aina za bahari za ushairi zifuatazo: a) Sakarani b) Ngonjera c) Malumbano d) Masivina e) Taabili f) Mandhuma g) Kisarambe h) Mavue i) Sabilia j) Togoo k) Kumbukizi(Solved)

    Eleza aina za bahari za ushairi zifuatazo: a) Sakarani b) Ngonjera c) Malumbano d) Masivina e) Taabili f) Mandhuma g) Kisarambe h) Mavue i) Sabilia j) Togoo k) Kumbukizi

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja na ueleze aina za mashairi kulingana na mizani(Solved)

    Taja na ueleze aina za mashairi kulingana na mizani

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Eleza aina ya mashairi kulingana na mpangilio wa maneno(Solved)

    Eleza aina ya mashairi kulingana na mpangilio wa maneno

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Eleza aina za mashairi kulingana na vina(Solved)

    Eleza aina za mashairi kulingana na vina

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Eleza aina za mashairi kulingana na idadi ya vipande katika mshororo(Solved)

    Eleza aina za mashairi kulingana na idadi ya vipande katika mshororo

    Date posted: February 1, 2023.  

  • Taja aina ya mashairi kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti (Solved)

    Taja aina ya mashairi kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti

    Date posted: February 1, 2023.  

    1        2        3        Next