-
Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata.
Angaza, mtazame mlimwengu
Bidii, nayo matokeo chungu
Wezesha, kuishi bila uchungu
Teknolojia maendeleo.
Angaza, zitazame barabara
Aenda, kwa kasi pia salama
Bidhaa, sokoni upesi fika
Teknolojia maendeleo.
Angaza, majokofu majumbani
Vyakula, na vinywaji hifadhika
Nafuu, zizima maji ridisha
Teknolojia maendeleo.
Angaza, leo pote madukani
Mikebe, vyakula vinywaji tiwa
Mimea, huwawirishwa haraka
Teknolojia maendeleo.
Angaza, nguo kwa mashine stimu
Upesi, runinga na simu juza
Angani, burudika eropleni
Teknolojia maendeleo.
Angaza, tarakilishi nguzoye
Mauzo, mawasiliano kwayo
tibani, ni mwenzi kwake tabibu
Teknolojia maendeleo.
Angaza, mja hajakoma katu
Shughuli, kila uchao shajara
Apate, tulia kwa ufanisi
Teknolojia maendeleo.
(a) Eleza dhamira ya msanii katika shairi hili.
(b) Onyesha mifano mitano ya maendeleo katika maisha ya binadamu.
(c) Eleza umbo la shairi hii.
(d) Andika ubeti wa nne katika lugha ya nathari.
(e) Eleza kwa kifupi mtazamo wa mshairi kuhusu teknolojia.
(f) Eleza maana ya maneno yafuatayo;
(i) Majokofu
(ii) Hunawirisha
(iii) Shajara
Date posted:
October 4, 2019
-
An experiment was set-up as shown below to investigate a certain plant process.
(a) What process was being investigated above?
(b) What observation was made if;
(i) The experiment was left in strong wind for one hour?
(ii) All the leaves were removed from the plant?
Date posted:
October 4, 2019
-
Kwa zaidi ya mwongo mmoja uliopita, ulimwengu mzima uliathiriwa na masaibu ya kifua kikuu kwa kiwango cha kuogofya kiasi kwamba katika mwaka wa 1993, shirika la afya duniani (WHO) lilitangaza ugonjwa huu kuwa swala dharura la kimataifa.
Ongezeko kubwa la visa vya kifua kikuu lililotokana na kuchipuka kwa viini vinavyosababisha maradhi hatari ya Ukimwi na magonjwa yaliyohusiana na punde baadaye ilibainika kuwa bara la Afrika lilikuwa ndilo lililoathiriwa zaidi na Ukimwi pamoja na maradhi ya kifua kikuu. Hii ndiyo hali inayotawala sasa ulimwenguni. Afrika likiwa bara linaloongoza kwa wagonjwa walioambukizwa viini vya Ukimwi lilikuwa likishuhudia visa vya maradhi ya kifua kikuu.
Viini vya Ukimwi vinapunguza uwezo wa mwili wa mgonjwa kupigana na vijidudu vya maambukizi. Swala linalowafanya wagonjwa hawa kutodhibiti maambukizi ya magonjwa mbalimbali. Katika hali ya kawaida mwili wa mtu kama huyo unaweza kujikinga dhidi ya viini kama hivyo. Maambukizi kama haya kawaida hujitokeza kukiwa na nafasi duni ya kinga mwilini. Katika baadhi ya mataifa kama vile Kenya, maambukizi ya kifua kikuu hufanyika mapema katika umri mchanga maishani.
Kwa kawaida, viini hivyo huwa havisababishi ugonjwa wenyewe. Badala yake, kinga katika mwili wa aliyeambukizwa unaweza kusitiri maambukizi hayo bila mhusika kuwa mgonjwa kutokana na sababu mbalimbali. Viini hivyo baadaye vinaweza kuwa hai tena na kumfanya mgonjwa kukumbwa na ugonjwa. Swala hili kwa kawaida hujitokeza wakati mgonjwa anapoambukizwa virusi vya Ukimwi. Virusi hivyo pia huongeza hatari ya ugonjwa kujitokeza baada ya maambukizi au pengine kujitokeza tena baada ya mgonjwa kupokea tiba ya kwanza.
Kulingana na utafiti, inakadiriwa kwamba mmoja kati ya wagonjwa wawili au watu wenye virusi vya Ukimwi watapata kifua kikuu wakati mmoja katika maisha yao. Inakadiriwa kwamba karibu asilimia 50 hadi 60 ya wagonjwa wenye maradhi ya kifua kikuu nchini Kenya pia wameambukizwa viini vya Ukimwi. Kwa upande mwingine, maradhi ya kifua kikuu hujitokeza kama kawaida kwa wagonjwa wenye virusi vya ukimwi. Kwa hivyo, wakati wa kushughulikia wagonjwa ni lazima pia wafanyiwe uchunguzi wa kubaini ikiwa wameambukizwa kifua kikuu.
(a) Ipe taarifa uliyoisoma kichwa mwafaka
(b) Ni nini hasa kilichochangia kuongezeka sana kwa maradhi ya kifua kikuu?
(c) Kwa kifupi, eleza ni kwa nini ugonjwa wa Ukimwi ni hatari mwilini
(d) Ukimwi na kifua kikuu una uhusiano mkubwa, eleza uhusiano huu kulingnana na
taarifa uliyoisoma
(e) Andika urefu wa neno ‘Ukimwi”
(f) Eleza mambo mawili ambayo yametokana na utafiti
(g) Ni jambo lipi ambalo ni la kushangaza kuhusiana na kifua kikuu
(h) Andika maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika kifungu hiki
(i) Kusitiri
(ii) Mwongo
(iii) Swala la dharura.
(iv)Viini
Date posted:
October 4, 2019
-
Give two examples for each of the following types of cost incurred in broiler production .
a)Variable cost
b)fixed cost
Date posted:
October 4, 2019
-
What is the destination of materials translocated in plants.
Date posted:
October 4, 2019
-
The diagram below shows a bone obtained from a mammal.
(a) Name the part of the skeleton from which the bone has been taken.
(b) Label the parts B and C.
(c) State the functions of part A.
Date posted:
October 4, 2019
-
Thibitisha kauli kuwa, "Mla naye huliwa zamu yake ifukapo". Ukirejelea riwaya ya Kidagaa Kimemwozea.
Date posted:
October 4, 2019
-
Study the dental formula of an organism below.
(a) (i) What is the total number of teeth this organism possess?
(ii) What is the mode of feeding of the organism?
(b) State two functions of mucus produced along the alimentary canal
Date posted:
October 4, 2019
-
Kidagaa kimemwozea
Elimu ya kajielewa sisi nani, na twatoka wapi, twaelekea wapi na utu tutaurejeshaje pahali pake....
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Taja mfano mmoja wa tamathali ya usemi kwenye dondoo.
(c) Dhihirisha jinsi utu ulivyotoka pahali pake, ukirejelea riwaya nzima.
Date posted:
October 4, 2019
-
Soma taarifa hii kisha ujibu maswali
Licha ya kuwa na historia ya kiasi, maisha ya binadamu ni kioja kikubwa. Hebu jiulize jinsi uhai wako wewe mwenyewe ulivyoanza sembuse unavyoweza kupumua na kuishi siku nenda siku rudi.
Dini zimefahamisha kuwa sisi binadamu tumeumbwa na Mwenyezi Muumba. Hata hivyo muumba hutumia mume na mke kutuanzishia maisha yetu humu humu duniani. Uhai wa hapa duniani huanzia katika tumbo la mwanamke muda mfupi tu baada ya mume na mke kushirikiana katika tendo la kujamiana. Katika ngono hii yenye ufanisi, mbegu moja ya manii kutoka kwa mwanamume, hudunga na kujiingiza katika yai la mwanamke huku ikilirutubisha. Tangu hapo mtu huwa na mama akawa mjamzito. Hatua ya kwanza ya uhai!
Wanasayansi wametuthibitishia kuwa mbegu katika shahawa kutoka kwa mwanamume ina kromosomu ishirini na tatu (23) nalo yai la mwanamke lina idadi iyo hiyo ya kromosomu. Basi katika hatua ya kwanza ya uhai wake, binadamu ana kromosomu arubaini na sita (46).
Kromosomu hizo zote ndizo humfanya mtu kuwa mkamilifu kwa kukadiria mambo mbalimbali adhimu. Kwa mfano, kukadiria kama kiumbe kitakuwa cha kike au cha kiume, mtu mweupe au mtu mweusi, mwerevu au wa wakia chache, mwenye nywele za singa au za kipilipili, atakuwa na damu ya namna gani, michoro ya vidole vyake itakuwa vipi na hata utu wake utakuwa wa namna gani katika siku za usoni.
Elimu yote anayopata mtu kutoka kwa jamii na mazingira huweza tu kujenga juu ya yaliyokwisha kuanzilishwa na kromosomu katika yai lililorutubishwa tumboni.
Haihalisi kabisa kufikiria kwamba huwa katika hali ya ukupe. La hasha! Yeye hujitegemea kwa vyovyote na ana upekee wake. Hatangamani na mama yake. Roho yake humdunda mwenyewe na damu yake ambayo huenda ikawa tofauti kabisa na ya mama yake, humtembea na kumpiga mishipani mwake. Isitoshe, yeye si mojawapo katika viungo vya mwili wa mama yake vinavyomdhibiti katika himaya yake ndogo.
Amini usiamini, hapana binadamu hata mmoja ambaye amewahi kuwa sawa kimaumbile na mwingine na wala hatakuweko. Hata watoto pacha kutoka yai moja la mama hawawi sawa, lazima watofautiane. Si nadra kusikia mtu amepata ajali akahitaji msaada wa damu, na pakakosekana kabisa mtu hata mmoja kutoka jamaa yake wa kimwauni. Basi ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni.
1. Ipe taarifa uliosoma anwani mwafaka
2. Mwandishi ana maana gani anaposema ‘ngono yenye ufanisi’?
3. Uchunguzi wa sayansi umekita mizizi imani gani ya kidini?
4. Taja majukumu yoyote matano yanayotekelezwa na kromosomu
5. Katika makala, elimu kutoka kwa jamii na mazingira yaelekea kuwa bure ghali. Kwa nini?
6. Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika makala:-
(i) huwa katika hali ya ukupe…
(ii) himaya
(iii) hatangamani na mama yake
Date posted:
October 4, 2019
-
a)List three forces that facilitate the transport of water and mineral salts up the stem.
b)Name the tissue that is removed when the bark of a dicotyledonous plant is ringed.
Date posted:
October 4, 2019
-
Simplify completely
Date posted:
October 4, 2019
-
Without using Logarithms tables or a calculator evaluate.
Date posted:
October 4, 2019
-
The diagram below shows an experiment that was carried out to measure how fast a were plant such as Elodea photosynthesizes
The shoot was exposed to different light intensities and the rate of photosynthesis estimated by counting the number of bubbles of gas leaving the shoot in a given time. the results are given below;
a) Plot these data on apiece of graph paper provided
b) At what light intensity did the shoot produce ;
i) 18 bubbles per minute
ii) 25 bubbles per minute
c) Give two better ways of measuring the rate of photosynthesis than counting bubbles
d) What is the role of light intensity in photosynthesis
e) Account for the expected results of doing this experience at the following temperature;
i) 4ºC
ii) 34ºC
iii) 60ºC
f) Other than light intensity and temperature, name other factors that affect the rate of
photosynthesis
Date posted:
October 4, 2019
-
Mtahiki Meya; Timothy Arege
"Siku moja kabla ya kufika kwa wageni. Meya ana mkutano na wawakilishi wa wafanyikazi ambao wameketi mkabala naye".
(a) Fafanua madai yaliyotolewa na wafanyakazi katika mkutano huu.
(b) Eleza jinsi Meya alivyojibu madai ya wawakilishi wa wafanyakazi.
Date posted:
October 4, 2019
-
Soma taarifa hii kisha ujibu maswali
Chamkosi alipiga goti huku machozi yakimdondoka njia nne nne. Mbele yake, palikuwa na makaburi mawili. Waliokuwa wamelala mle hawakuwa na habari juu ya kihoro na simanzi ya aliyepiga magoti pale. La kwanza, lilikuwa kongwe kiasi na lilikuwa limemea vichaka na magugu. La pili lilionyesha upya kwani shada za maua zilizowekwa na waombolezaji zilikuwa bado kukauka. La kwanza, ndimo babake mzazi alipolala. Nalo la pili, ndimo mamake alimolazwa kiasi cha siku mbili zilizopita.
Kwa Chamkosi, maisha hayakuwa na maana tena. Alikuwa mwanafunzi wa miaka kumi na miwili. Hakuwa amehitimu kujitegemea na kukimu mahitaji yake. Aliokuwa akiwategemea sasa wamemwacha akiwa yatima. Hakuna yeyote ambaye angejaza pengo la wazazi wake wawili kwa kipindi cha mwaka mmoja. Haya yalikuwa kama donda sugu lisilopona.
Kwa sasa, Chamkosi anayakumbuka mengi. Anakumbuka maisha ya babake. Alikuwa jibaba nene, zito lenye sura jamala na sifa nzuri. Baba mtu alikuwa na chake na alijiweza kiuchumi. Wengi pale mjini walimheshimu na kumstahi kutokana na uwezo wake wa kiuchumi.
Alitunza familia yake vizuri. Chamkosi hakumbuki siku moja aliyokosa chochote alichohitaji kutoka kwa babake. Alikuwa na bidii kazini mwake pia.
Walakini, kama mja asiyekamilika, baba mtu alikuwa na dosari moja. Aliyapenda maisha ya anasa na kufukuzia wasichana wadogo pale mtaani. Mamake Chamkosi aliyajua haya. Alijaribu kuzozana na mumewe ili aachane na tiabia hizi lakini kila akitaka ushauri, mama mtu alikemewa na kufokewa kuwa aache upuzi wa wanawake. Akafikia kufyata ulimi na kumwachia Mungu aongoze maisha ya bwanake.
Hata hivyo hakuna marefu yasiyo na kikomo. Baada ya kuponda raha na vimada si haba, baba mtu alianza kuugua. Maradhi yake yakawa ni msururu. Mara, alipata mafua yasiyopona, mara kuendesha, mara maradhi ya ngozi. Haya yalimtia wasiwasi. Baada ya kukaguliwa na daktari, alipatikana kuwa ameumwa na mbuzi. Hakuamini haya. Baba aliyekuwa bashasha na mcheshi aliingiwa na upweke na kutotaka kutangamana na yeyote hata jamaa zake.
Waliosema kuwa hakuna msiba usiokuwa na mwenzake, hawakukosea. Maradhi ya baba mtu yaliifilisi jamaa huku waking’ang’ania kumtafutia tiba. Wakaenda kwa waganga si haba. Waganga nao wakafaidi tamu.
Muda si mrefu, mama mtu naye akaanza kuugua. Baada ya uchunguzi, alipatikana kuwa na maradhi yayo hayo ya bwanake. Ikawa ni kama mji umelogwa. Baada ya muda mfupi baba mtu aliaga dunia, mama naye hakukawia. Naye akasalimu amri na kumfuata bwanake kaburini. Familia ikawa kama inaangamia. Chamkosi kijana mdogo akaachwa pweke.
Kama kawaida, mja hakosi neno. Wengi walisikika wakisema hili na lile kuhusu vifo hivi. Wengi walieneza uvumi. Lakini, Chamkosi alijua ukweli wa vifo vya wazazi wake.
Sasa hapa alipo aliyatambulia macho makaburi ya wazazi wake, anasononeka. Anaomboleza zaidi kifo cha mamake ambaye alimwona hana hatia na hakupaswa kufa kwa maradhi yale. Anaukumbuka vizuri wema wa mamake usio na kifani. anakumbuka alivyojitunza kama mke na mzazi.
Anakumbuka jinsi mamake alivyomshughulikia babake katika siku zake za mwisho licha ya baba mtu kuungama maisha yake maovu. Chamkosi alishindwa kujua kwa nini mamake akawa msamehevu kiasi hicho. Hakukosa kukumbuka wasia wa mama yake. Haya yalimfariji. Faraja hizi zilimpa nguvu mpya za kuyakabili maisha.
Chamkosi aliwaza juu ya maisha yake. Akaona kuwa, kama yatima atawategemea wafadhili miongoni mwa jamaa na marafiki wenye huruma iwapo wapo. Aliwaza jinsi anasa za babake zilivyowaathiri watu wengi.Alitambua kuwa Ukimwi haumwathiri aliyeupata tu, bali na wengine wengi. Kweli, mtego wa Panya huingia waliokuwemo na wasiokuwemo. Lakini akiwatazama watu, hakuelewa kwa nini walidhamiria kuishi ujingani. Aliwaona baadhi ya vimada wa babake wakishikana viuno na vijana wadogo. Akawasikitikia. Akabaki na swali kwa nini watu wengine wanafikiria kuwa virusi hivi haviwezi kuwapata. Kwani wanafikiria kuwa vinabagua na kuwa wao hawahatarishi maisha yao? Alishindwa kufahamu watu watabadili vipi mienendo yao miovu na waweze kukabili janga hili lini?
Kwa wakati huu, Chamkosi alikata shauri kusomea Taaluma ya Uelekezi na Ushauri kutokana na vifo vya wazazi wake. Alitaka kupata ujuzi utakaomwezesha kuwashauri na kuwaelekeza vijana wenzake ambao wanahatarisha maisha yao. Kama mshauri, alinuia kuhamasisha na kuzindua jamii juu ya hatari za Ukimwi.
Alitaka kuhakikisha kuwa hatua zimechukuliwa na kila mtu katika jamii kukabili janga hili n kuliangamiza
Chamkosi aliomba dua fupi. Akainuka na kuondoka huku akiwa na faraja na matumaini moyoni kutokana na azimio lake lile.
(a) Toa kichwa mwafaka kwa makala haya
(b) Eleza madhara mawili ya ugonjwa sugu uliotajwa katika makala haya
(c) Taja mifano ya tabia zinazoweza kumfanya mtu aathiriwe na ugonjwa wa Ukimwi
(d) Tofautisha tabia za baba na mama wa Chamkosi
(e) Chamkosi baada ya kufikwa na madhila hayo yote aliamua kufanya nini? Toa maoni
(f) Eleza maana ya:
(i) Tumbulia macho
(ii) Ameumwa na mbuzi
Date posted:
October 4, 2019
-
Damu nyeusi na hadithi zingine
"Leo ndio mtanitambua. Mama gani anayemtazama mwana akigeuka afriti?"
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Tambua "mwana aliyegeuka afriti‘na ueleze hulka zake nne.
(c) Jadili maudhui yoyote matano yanayojitokeza katika hadithi husika.
Date posted:
October 4, 2019
-
The table below shows the results of an experiment carried out to determine the rate of photosynthesis at different light intensities and varying Carbon (IV) oxide concentrations. The rate was determined by counting the number of bubbles per minute. The temperature was kept constant.
a) On a graph paper provided, draw a graph for each of the light intensities. All the three graphs should be plotted on the same axis (rate of photosynthesis on vertical axis and carbon (IV) oxide concentration on horizontal axis
b) What is the effect of an increase in carbon (IV) oxide concentrations and light intensities
c) Briefly explain how aquatic green plants meet light intensities and carbon (IV) oxide
requirement
d) Using the data provided in the table state two factors required by the green plants for food
production
Date posted:
October 4, 2019
-
Eleza sifa tano za sajili ya magazeti.
Date posted:
October 4, 2019
-
A student was culturing E. coli (a bacterium) in a Petri-dish. He placed the Petri-dish in an incubator at 30oC.He removed it from the incubator the following day and found that five colonies of bacteria had grown. He decided to return it into the incubator to give it more time. When he removed it fourteen days later, he could not observe any colony.
a) Why was there no colony on the fourteenth day?
b) Explain how bacteria cause spoilage of stored food in warm moist conditions.
c) Name other organisms which also cause food spoilage.
d) State their economic importance to nature.
Date posted:
October 4, 2019
-
Andika maana ya msemo.
Kuwa na mihayara.
Date posted:
October 4, 2019
-
Andika kinyume.
Ukipitia kwao utalaaniwa.
Date posted:
October 4, 2019
-
Mwanafunzi aliadhibiwa kwa uongo wake.
(Anza kwa .......Uongo)
Date posted:
October 4, 2019
-
Form one students from Inungo school arranged their apparatus as shown below, to investigate a certain phenomenon. The set up was placed in light.
(a) State the likely aim of the set up
(b) State the role of the syringe in the set-up above
(c)
(i) Name gas X
(ii) Write an equation to show how gas X was formed in the set-up
(d) State three factors that increase the rate of enzyme activity
(e) Give a reason why the test tube is immersed in a beaker of water
Date posted:
October 4, 2019
-
Complete the following diagram on the classification of man made textile fibre.
(Indicate what the number given stands for)
Date posted:
October 4, 2019
-
Andika maana mbili za neno "mlango".
Date posted:
October 4, 2019
-
Giving reasons in each case, explain three changes that take place in a dough during the frying of mandazi.
Date posted:
October 4, 2019
-
Describe how mammalian small intestine is adapted to its function.
Date posted:
October 4, 2019
-
Jibu kulingana na maagizo.
(i) Ufisadi (unda kitenzi)
(ii) - pya (unda nomino)
Date posted:
October 4, 2019
-
Kanusha sentensi hii katika hali ya "a"
Kibofu hupaa angani.
Date posted:
October 4, 2019