
Siasa ni itikadi inayofuatwa na kundi fulani au jamii fulani ambayo ni msingi wa kuendesha uchumi, utamaduni na mwenendo mzima wa maisha ya jamii.
Siasa ni mfumo unaohusisha zaidi ya uongozi wa watu kwa kufuata kanuni, sheria sera, uwajibikaji, uwazi na ugawaji wa rasilimali sawa kwa wanachi wake katika kuwaletea maendeleo.
Wananchi huchagua kikundi cha watu ambao wanaamini na kuwapa uwezo wa kuunda serikali ili waongoze kwa niaba yao.
Mwandishi ameeleza siasa kama mchezo mchafu. Inageuka mchezo mchafu pale serikali inaanza kwenda kinyume na utaratibu na kanuni sahihi na kutofuata maadili ya uongozi. Viongozi wanageuka waongo, wakatili, wanafiki, wenye uchu wa mali, wanyonyaji na wauaji. Wanafanya lolote ili kujitajirisha. Wanaongoza nchi kwa manufaa yao binafsi na sio kuwaletea wananchi maendeleo. Wanawajengea hofu na kuwasababishia maisha magumu.
Majoka anajua vilivyo kuucheza huu mchezo. Atafanya lolote lile kujitajirisha na anaonekana kutotosheka. Ana washauri wabaya kama vile Kenga. Kenga anamfundisha ile siasa ya kuuma na kuvuvia.
Sudi amekuwa akipinga uongozi mbaya wa Majoka. vile vile Majoka alitaka kuchongewa kinyago na Sudi lakini Sudi anakataa. Ili kulipiza kisasi, Majoka analifunga soko na kumtia ndani Ashua ; mkewe Sudi. Anashauriwa kufanya hivi na Kenga ili pia aweze kumshawishi Sudi kumchongea kinyago ili mkewe aachiliwe.
Majoka anaapa kuifunga runinga ya mzalendo kwa kupeperusha habari za maandamano moja kwa moja. Anaipenda runinga ya mashujaa inayotangaza habari nzuri kumhusu pekee.
Majoka anawaua wapinzani wake au kuwatumia wahuni. Akitumia Kenga, alimuua Jabali ; mpinzani wake wa kipindi kilichotangulia wa chama cha mwenge. Anatumia Ngurumo kumvamia Tunu. Alikuwa amesema auawe lakini bahati nzuri akanusurika. Majoka anapotambua kuwa njama yake imejulikana, anamuua Ngurumo. Hata bibiye ; Asiya alikuwa pia auawe akanusurika.
Maziara ya Jimbo yamejaa na Ngurumo hana nafasi ya kuzikwa. Majoka anajua kuwa hili litamharibia sifa iwapo litaangaziwa na vyombo vya habari. Anaicheza karata yake vizuri. Anapanga chatu auwawe. Anajua kuwa wakereketwa wa mazingira wataandamana kutetea haki za wanyama na kwa hivyo vyombo vya habari vitawaangazia wao wala si mazishi ya Ngurumo atakayezikwa juu ya mfu mwingine.
Kenga alitarajia watu wengi wangehudhuria sherehe za uhuru. Haiwi hivyo. Anajuta heri wangelikodisha mabasi yawalete vijana na akina mama wajaze uwanja. Hii ni mbinu watumiayo wanasiasa kuonyesha walivyo na umaarufu kumbe sivyo.
Mwandishi wa tamthilia hii hata hivyo ametaka kuonyesha kuwa wananchi wanachangia pakubwa katika kuamua watatawaliwa vipi na viongozi. Iwapo watazinduka, waache usaliti, wasiongozwe na tamaa na waache ubaraka, kwa kutumia uwezo wao wa kura, wanaweza kuwachagua viongozi wazuri. Tunu anawahimiza wananchi kutowachagua tena viongozi wanaokiuka haki zao na wasiowajibika.
ESTHER STEVE answered the question on April 30, 2018 at 20:27
-
Jadili kwa kina sifa zozote tano zinazokitambulisha Kiswahili kama lugha ya kibantu
(Solved)
Jadili kwa kina sifa zozote tano zinazokitambulisha Kiswahili kama lugha ya kibantu.
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Jadili juhudi za TUKI katika kuendeleza na kustawisha Kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki.
(Solved)
Jadili juhudi za TUKI katika kuendeleza na kustawisha Kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Eleza nafasi ya makundi yafuatayo katika ama kukua au kudhoofika kwa Kiswahili nchini Kenya kabla ya uhuru. (a) Watawala (b) Wamisheni (c) Walowezi
(Solved)
Eleza nafasi ya makundi yafuatayo katika ama kukua au kudhoofika kwa Kiswahili nchini Kenya kabla ya uhuru.
a) Watawala
b) Wamisheni
c) Walowezi
(alama 15)
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Jadili aina tatu za ‘maana’ huku ukizitolea mifano kutoka Kiswahili.
(Solved)
Jadili aina tatu za ‘maana’ huku ukizitolea mifano kutoka Kiswahili.
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Na ujenge nyumba yako, jingi jasho likuoshe,Ufyeke, upime na uweke nguzo,Kisha paa uweke na ukandike,Siku nyingi bila kuingiliwa na mgeni hutakaa.Wataanza kutalii mpaka mende usiku,Nje...
(Solved)
1. Na ujenge nyumba yako, jingi jasho likuoshe,
Ufyeke, upime na uweke nguzo,
Kisha paa uweke na ukandike,
Siku nyingi bila kuingiliwa na mgeni hutakaa.
Wataanza kutalii mpaka mende usiku,
Nje na ndani ya nyumba watazunguka,
Bila woga, bila ruhusa ulichonacho watakula,
Masalia yatakuwa yako, ijara ya kaziyo.
Na nyingi dawa uweke, nyumba nzima uihame,
Ukae nje nzima siku usubiri,
Wazima wamelala ukirudi usiku,
Vichwa vigumu hawafi mende rahisi.
Kifo cha mende sharti miguu juu
Kichwa ukikanyage kipasuke usikie,
Na kisha wengine usiku mchana uwasake.
Mpaka watakapokwisha. Usiseme nao.
Maswali
(a) (i) Hili ni shairi la aina gani? (alama 1)
(ii) Tetea jibu lako. (alama 3)
(b) Eleza jinsi mshairi alivyoutumia uhuru wake katika utunzi wa shairi hili. (alama 4)
(c) Taja mbinu mbili za lugha alizotumia mshairi na uzitolee mifano. (alama 4)
(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha nathari. (alama 4)
(e) Eleza ujumbe wa mshairi. (alama 2)
(f) Toa mfano mmoja wa mshata. (alama 1)
(g) Kichwa gani kinaliafiki shairi hili? (alama 1)
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
(a) Katika jamii huwa wakati mwingine kuna matumizi ya lugha isiyo ya kistaarabu.taja mifano mitano ya lugha ya sampuli hiyo. ( alama 5)
(b) Taja mambo matano...
(Solved)
(a) Katika jamii huwa wakati mwingine kuna matumizi ya lugha isiyo ya kistaarabu.taja mifano mitano ya lugha ya sampuli hiyo. ( alama 5)
(b) Taja mambo matano yanayoathiri jinsi tunavyoweza kutumia lugha katika jamii(mtindo nafsi na mtu)
MAJIBU
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
(a) Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii.
i) Lafudhi
ii) Lahaja
iii) Rejesta
Taja sifa nne za sajili ya wanasiasa (alama 4)
(Solved)
(a) Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii.
i) Lafudhi
ii) Lahaja
iii) Rejesta
Taja sifa nne za sajili ya wanasiasa (alama 4)
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Mifano miwili ya fomyula ya ufunguzi wa hadithi
(Solved)
Mifano miwili ya fomyula ya ufunguzi wa hadithi
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Eleza vigezo vya kutumia katika uchambuzi wa lugha
(Solved)
Eleza vigezo vya kutumia katika uchambuzi wa lugha
Date posted:
April 30, 2018
.
Answers (1)
-
Jadili ufaafu wa anwani "kigogo" katika tamthilia ya kigogo
(Solved)
Jadili ufaafu wa anwani "kigogo" katika tamthilia ya kigogo
Date posted:
April 29, 2018
.
Answers (1)
-
(a) Nini maana ya kufa kwa lugha. (b) Eleza sababu zozote tano zinazochangia kufa kwa lugha
(Solved)
(a) Nini maana ya kufa kwa lugha.
(b) Eleza sababu zozote tano zinazochangia kufa kwa lugha.
(c) Taja aina tatu za makosa ya lugha.
Date posted:
April 28, 2018
.
Answers (1)
-
1. Eleza maana ya istilahi hii: Usanifishaji 2. Eleza mambo manne yaliyochangia maenezi ya kiswahili kabla ya uhuru.
(Solved)
1. Eleza maana ya istilahi hii: Usanifishaji
2. Eleza mambo manne yaliyochangia maenezi ya kiswahili kabla ya uhuru.
Date posted:
April 28, 2018
.
Answers (1)
-
Tamaa inatawala katika Tamthilia ya Kigogo. Dhibitisha
(Solved)
Tamaa inatawala katika Tamthilia ya Kigogo. Dhibitisha
Date posted:
April 28, 2018
.
Answers (1)
-
Jadili maudhui ya utabaka katika tamthilia ya Kigogo
(Solved)
Jadili maudhui ya utabaka katika tamthilia ya Kigogo.
Date posted:
April 28, 2018
.
Answers (1)
-
Ichambue jalada ya tamthilia ya Kigogo
(Solved)
Ichambue jalada ya tamthilia ya Kigogo
Date posted:
April 28, 2018
.
Answers (1)
-
Eleza tofauti kati ya malumbano ya utani na mawaidha
(Solved)
Eleza tofauti kati ya malumbano ya utani na mawaidha
Date posted:
April 27, 2018
.
Answers (1)
-
Eleza umuhimu wa ngomezi.
(Solved)
Eleza umuhimu wa ngomezi
Date posted:
April 27, 2018
.
Answers (1)
-
(a) Eleza maana ya mivigo na inakotumika (b) Eleza sifa za miviga (c) Onyesha umuhimu wa miviga.
(Solved)
(a) Eleza maana ya mivigo na inakotumika
(b) Eleza sifa za miviga
(c) Onyesha umuhimu wa miviga.
Date posted:
April 27, 2018
.
Answers (1)
-
Fafanua sifa za mawaidha ukizingatia: hadhira, fanani, maudhui, fani
(Solved)
Fafanua sifa za mawaidha ukizingatia
hadhira
fanani
maudhui
fani
Date posted:
April 26, 2018
.
Answers (1)
-
Fafanua aina za nyimbo zifuatazo bembelezi, za sifa, za mapenzi
(Solved)
Fafanua aina za nyimbo zifuatazo bembelezi, za sifa, za mapenzi.
Date posted:
April 24, 2018
.
Answers (1)