Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Tanzu za lugha katika mawasiliano

  

Date Posted: 10/8/2017 1:12:18 AM

Posted By: SAW  Membership Level: Silver  Total Points: 122


Tanzu za lugha katika mawasiliano

Tanzu hurejelea mbinu au nyenzo za mawasiliano.kuna tanzu nne kuu ambazo kwazo binadamu hutimiza shughuli za mawasiliano.
1.maongezi
Binadamu maranyingi huwasiliana kwa njia ya maongezi au mazungumzo katika shughuli mbalimbali.mbinu hii hudhihirika katika
Majadiliano
Mazungumzo ya ana kwa ana
Mahojiano
Mikutano
Hotuba
Warsha
Muhimu katika maongezi ni matumizi yam domo na sauti.
Nyenzo hii huwa na manufaa mengi katika mawasiliano.
Umuhimu wa maongezi
Hutendeka moja kwa moja miongoni mwa washiriki na hudhihirisha sifa ya kuuliza na kujibiwa kwa maswali .
Mzungumzaji huweza kupata majibu ya papo hapo au maitikio ya moja kwa moja ilikuendeleza mkondo wa mawasiliano.
Kuna uwezekano wa kumtathmini ukweli wa ujumbe hasaa kwa kuangalia miondoko ya mwongezi.
Ni rahisi kujumlisha viziada lugha katika uwasilishi ilikuweka msisitizo kwenye hoja zinazowasilishwa
Ishara za uso mkondo na mkondo na miondoko nyingineyo inayo tumika katika maongezi huongeza msisitizo na hivyo basi huchangia upokezi ifaayo ya ujumbe .viziada lugha pia huchangia kuhusisha viwango vya sauti an namna sauti hiyo inavyopokelewa na msikilizaji, sauti ya juu huashiria uchungu au hasira.
Maongezi hufanikisha Zaidi ushawishi,hudhihirika waziwazi wakati hisia zinapandwa miongoni mwa wasikilizaji kuhusu jambo Fulani.maongezi kwa hivyo hutumia lugha yakiusanii kubadilisha na kupanda mawazo Fulani miongoni mwa watu.
Maongezi ni rahisi wala hayana gharama kubwa ikilinganishwa na mbinu nyinginezo
Ni rahisi kutambua athari wanazopata wasikilizaji katika maongezi maalum.
Maranyingi washiriki katika maongezi hutagusana katika mazingira maalum ana kwa ana hivyo ni rahisi kuamulia mkondo wa mazungumzo na

pia kujirekebisha unapokosea.
Dosari/udhaifu ya maongezi
Hayana hifadhi ya kudumu kuhusu yale yaliyozungumzwa kwa hivyo mzungumzaji anaweza kukana aliyoyasema.
Ni vigumu kudhibiti makundi makuu ya watu.
Kuna uwezekano wa kukatizana na kukosa mweleko wa kimazungumzo.
Maranyingi washiriki huathiriana kwani huonana uso kwa uso.
Ubishi huweza kuzuliwa hasa washiriki wanapokosa kuelewana kuhusu mada Fulani.
Kadri muda,mazingira na wahusika wanavyo badilika ndivyo kiini cha ujumbe kinaweza kupotea na kubadilika kabisa.
(2)maandishi
Maranyingi hutumiwa katika mawasiliano yenye urasmi ambapo hati maalum ya lugha hutumiwa kupitisha ujumbe.huweza kutumiwa katika ripoti,barua,kumbukumbu,taarifa na Makala mengineyo ya kifasihi.
Manufaa ya maandishi
Maandishiyana rekodi ya kudumu ya ujumbe unaowasilishwa na huweza kurejelewa baadaye.
Isipokuwa katika uchapisho mpya wa ujumbe na maandishi hubaki ule ule.
Msomaji huwa na muda wa kutosha kusoma,kuchambua na kutafsiri maandishi kadri ilivyokusudiwa na mwandishi.
Kuna ushahidi wa kutumia na kupokea ujumbe
Maandishi huweza kutolewa katika Makala mengine na kusambazwa kwa watu wengi ilikupata ujumbe huo huo kwa wakati mmoja.
Maandishi ni nyenzo rahisi na pia yenye uwazi wa kupitisha maswali nyeti.
Udhaifu wa maandishi
Ni vigumu kudhibitisha iwapo ujumbe uliotuma kimaanishi imesomwa na kueleweka kwa mpokezi.
Majibu na maitikio ya ujumbe hayawezi kufikia mwasilishwaji moja kwa moja
Maandishi yakiwa na kasoro ni vigumu sana kurekebisha hivyo basi kasoro hiyo inakuwa moja wapo ya ujumbe, hayawezi kufikia mwasilishwaji moja kwa moja.
Maandishi hayana nafasi ya mjadala au mashauriano kati ya mwandishi na mpokezi.
(3)Ishara
Ni zile alama na miondoko inayotumiwa kuwasilisha ujumbe pasipona kutumia lugha.hujumlisha ishara ishara uso,macho,kichwa,mikono,na viungo vinginevyo kupasha ujumbe.
Matumizi ya ishara hutegemea muktadha pamoja na kaida ya jamii.
Sperber anasema kwamba chochote unachokionyesha ama katika kukimya ni ishara ya mawasiliano.picha za hizi ishara sauti za kuarifu hujumlishwa katika mawasiliano ishara.

Udhaifu wa ishara
Isipokuwa ishara maalum ishara nyingi huhitaji maarifa kuhusu jamii husika ilikupata kuwasiliana
Ishara huweza kutafsiriwa visivyo hivyo kusababisha ugomvi.
Ishara zinazo tumiwa katika mawasiliano na watu wenye upungufu ya kuongea huhitaji ufunzaji iliueleweke.
Huhusika na muktadha pekee ya mazungumzo.



Next: Making our country self-sufficient food supply
Previous: Limitations of income per capita in measuring the standards of living in different countries

More Resources
Quick Links
Kenyaplex On Facebook


Kenyaplex Learning