Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Kiswahili Revision Revisions. Question Paper

Kiswahili Revision Revisions. 

Course:Secondary Level

Institution: Kcse question papers

Exam Year:2011



SHINERS GIRLS HIGH SCHOOL
KISWAHILI

1. Andika sentensi zifuatazo upya ukizingatia maagizo yaliyo kwenye mabano.

a. Mazingira yamehifadhiwa. (Hali ya mazoea)

b. Mwalimu anasahihisha kitabu cha mwanafunzi. (Anza kwa: Kitabu)

c. Dhahabu itafuliwa kiwandani. (Wakati uliopita)

2. Eleza maana mbili zinazojitokeza katika sentensi hii:

Alimpigia mpira.

3. Tofautisha sentensi hizi kimaana:
Gari liliibwa.
Gari liliibiwa.

4. Kanusha sentensi hizi:

a. Alijitahidi masomoni.
b. Tuliimba tukivuna mahindi.
c. Maharagwe yalivunwa na kutiwa ghalani.

5. Pambanua sentensi hii kwa njia ya mstari.

Nchi iliyo na imani huvutia.

6. Tunga sentensi yenye sehemu hizi:

a. I + N + T + W
b. T + E

7. Andika maneno yenye sauti mwambatano zenye miundo hii:

a. KKI
b. KKKI
c. KKKKI

8. Tunga sentensi zenye miundo hii:
a. KT
b. KN + KT

9. Andika sentensi zifuatazo bila ya kutumia kirejeshi amba-
a. Fulana ambayo imefumwa ni nyekundu.

b. Matendegu ambayo yametengenezwa ni ya kitanda ambacho kilivunjika juzi.

10. Sentensi zinaweza kuwa katika hali tatu: Kwa kila sentensi andika hali zilizokosekana.

a. Goma lililotumiwa katika sherehe zile ni zuri.

b. Mwizi aliyeiba alipatikana amejificha kando ya mto.

11. Panga maneno haya vizuri ili yaunde sentensi sahihi.

a. Hodari yule mwanamuziki nchini amezuru nyingi Africa za.

b. Kompyuta kwa mpya mawasiliano mtandao imerahisisha rununu teknolojia na kupitia wavuti.

12. Tofautisha maneno haya kimaana kwa kuyatungia sentensi:

a. Fasiri, fasili
b. Tunza, tuza.

13. Tunga sentensi mbili kwa kila neno ulilopewa kubainisha maana.

a. Paa
b. Shuka.






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers