Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.

Educ 331:Mbinu Za Kufundisha Kiswahili Question Paper

Educ 331:Mbinu Za Kufundisha Kiswahili 

Course:Elimu

Institution: Kenya Methodist University question papers

Exam Year:2012



CHUO KIKUU CHA KIMETHODISTI, KENYA

MTIHANI WA MWISHO WA TREMESTA YA PILI, 2012
KITIVO : ELIMU NA SAYANSI YA JAMII
IDARA : ELIMU
KODI : EDUC 331
ANWANI : MBINU ZA KUFUNDISHA KISWAHILI
MUDA : SAA MBILI




MAAGIZO:

Swali la Kwanza

Baadhi ya makosa ambayo wanafunzi hufanya katika kuongea na kuandika kwa lugha ya Kiswahili hutokana na maingiliano kati ya Kiswahili na lugha za kwanza. Jadili.

(al. 12)

Eleza stadi nne za kufunzia lugha ya Kiswahili kwa kuzitolea mifano mwafaka.

(al. 8)

Swali la Pili

Eleza shida ambazo huwakumba sana wanafunzi wanaposoma Kiswahili kwa sauti.

(al. 10)

Ni hatua gani anazoweza kuchukua mwalimu kupunguza shida hizo?


(al. 10)

Swali la Tatu
Huku ukitoa mifano mwafaka eleza jinsi teknolojia ya kisasa inavyoweza kutumiwa katika ufunzaji wa lugha ya kiswahili. (al. 20)

Swali la Nne

Taja na ufafanue mambo yoyote matano yanayoweza kutatiza ufahamu sikizi.

(al. 10)

Thibitisha jinsi mafunzo ya sarufi yanavyofaa mwanafunzi.

(al. 10)

Swali la Tano

Mwalimu Rea hatayarishi azimio la kazi; Je katika ufunzaji wake atatatizika vipi?

(al. 10)

Matumizi ya vifaa yana umuhimu gani katika ufunzaji wa somo la lugha ya Kiswahili.

(al. 5)

Kabla mkufunzi kwenda kufunza lugha ya Kiswahili nyanjani katika mazoezi ya kufudisha, anafaa kujiandaa vipi?

(al. 5)






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers