Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.

Lswa 400:Nadharia Ya Uhakiki Wa Fasihi Na Sanaa Za Maonyesho Question Paper

Lswa 400:Nadharia Ya Uhakiki Wa Fasihi Na Sanaa Za Maonyesho 

Course:Elimu

Institution: Kenya Methodist University question papers

Exam Year:2013



CHUO KIKUU CHA KIMETHODISTI, KENYA

MTIHANI WA MWISHO WA TREMESTA YA KWANZA, 2013
KITIVO : ELIMU NA SAYANSI YA JAMII
IDARA : ELIMU
KODI : LSWA 400
ANWANI : NADHARIA ZA UHAKIKI WA FASIHI
MUDA : SAA MBILI




Maagizo: Jibu Maswali Matatu

Swali la Kwanza

Eleza maana ya nadharia kisha ufafa111aaanue umuhimu na nadharia katika kuhakiki kazi za fasihi.

(Alama 6)


Mchango wa Aristotle na Plato kuhusiana na sheria za utunzi wa kazi za fasihi umechangia pakubwa katika uundaji wa sheria mwafaka. Jadili mawazo yao kuhusiana na swala hili.

(Alama 4)

Swali la Pili

Nadharia nzuri huwa na sifa kadha. Fafanua sifa hizo.

(Alama 10)

Uchambuzi wa kazi za fasihi hujikita katika vipengele mbalimbali. Fafanua vipengele ambavyo uhakiki wake unaweza kuzingatia nadharia mbalimbali.

(Alama 10)

Swali la Tatu
Nadharia ya umaksi ni ya kimapinduzi. Jadili kauli hii ukirejelea milimili yake muhimu na mifano katika fasihi ya Kiswahili. (Alama 20)

Swali la Nne

Onyesha jinsi ushairi wa Kiswahili unaweza kuhakikiwa kwa mjibu wa matapo yafuatayo:

Urasmi

(Alama 10)

Ulimbwende

(Alama 10)

Swali la Tano

Tapo la uhalisia limetawala pakubwa uandishi na uhakiki wa kazi za fasihi. Jadili kauli hii ukirejelea mifano ya kazi za kihalisia katika fasihi ya Kiswahili.
(Alama 20)






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers