Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.
Got a question or eager to learn? Discover limitless learning on WhatsApp now - Start Now!

Lswa 105:Historia Ya Kiswahili Question Paper

Lswa 105:Historia Ya Kiswahili 

Course:Elimu

Institution: Kenya Methodist University question papers

Exam Year:2011



FACULTY : EDUCATION & SOCIAL SCIENCES

DEPARTMENT : EDUCATION AND PRE-UNIVERSITY

TIME : 2 HOURS

MAAGIZO Jibu Swali la KWANZA kutoka Sehemu A na mengine MAWILI kutoka Sehemu B


Sehemu A

Swali 1

a) Jadili huku ukitoa mifano mwafaka nadharia tatu ambazo zinaeleza chimbuko la Kiswahili. (alama9)

b) Eleza dhana zifuatazo

i) pijini

ii) krioli

iii) lugha ya taifa

iv) lugha rasmi (alama8)

c) Fafanua fasiri tatu kuhusu dhana ya mswahili ni nani kama inavyoelezwa na wataalamu wa historia ya lugha. (alama3)


Sehemu B

Swali 2

a) Lugha ya Kiswahili haikuenea kwa mapana nchini Uganda kama nchini Tanzania na Kenya. Fafanua dai hili. (alama15)

b) Eleza sababu TANO zilizokwaza kuenea kwa Kiswahili nchini Kenya kabla ya uhuru.(alama5)


Swali 3

a) Eleza majukumu sita ya kamati ya usanifishaji wa lugha ya Kiswahili. (alama12)

b) Fafanua sababu zilizopelekea Kiunguja kuchaguliwa kama lahaja ya usanifishaji. (alama8)


Swali 4

Teknolojia ya kisasa ya mawasiliano inatumia Kiswahili. Thibitisha dai hili kwa kutoa mifano toshelevu. (alama20)


Swali 5

Jadili hali iliyopelekea Kiswahili kuenea zaidi nchini Tanzania kuliko nchi nyingine za Afrika mashariki. (alama20)






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers